Je, wajua? Pesa iliyotoa Qatar kuandaa Kombe la Dunia ni pato la Taifa Tanzania kwa miaka 3.5

Je, wajua? Pesa iliyotoa Qatar kuandaa Kombe la Dunia ni pato la Taifa Tanzania kwa miaka 3.5

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Qatar nchi yenye km za mraba 11,000 na watu wapatao milioni 3 imeandaa Kombe la Dunia lililotumia gharama zaidi tangu Dunia iumbwe.

Zaidi ya dola bilioni 220 zimetumika kwenye maandalizi mpaka kufanikisha Kombe la Dunia huku mapato ya kiuchumi yakitarajiwa dola bilioni 7.5 pekee mpaka kuisha kwake. Vimejengwa mpaka viwanja na makazi yatakayobomolewa baada ya mashindano. Pato la Tanzania ni $ Bilioni 62 kwa mwaka.

Nini Tanzania inaweza kufanya na $ bilioni 220;
  1. Ingejenga bandari ya Bagamoyo($ Bil 10) na kuepuka kuingizwa mjini na Mchina.
  2. LNG plant($ Bil 30) na kutumia gesi kila sehemu kuondokana na utumwa wa kulipa mafuta nje.
  3. SGR($ Bil 14) tungeifikisha Mwanza na Kigoma, kwa jeuri tugemjengea na Congo, akitoa mzigo wake Bagamoyo kituo cha kwanza Lubumbashi.
  4. Deni la Taifa($ Bil 28) tungelipa lote na bungeni tufocus kwenye kuongelea maendeleo maana mjadala wa deni la taifa huwa unapoteza muda wakati tunaendelea kukopa.
  5. Madarasa($ Bil 2), tungeacha kwenda kumpigia goti Mzungu eti kujenga vyumba vya madarasa.
  6. BRT($ Bil 2), tungejenga mwendokasi Dar nzima na kuwaonjesha Mwanza ikiwa na mabasi ya kutosha kama yale mekundu ya waingereza na kuachana na haya ya bluu tena 'Level seat' yakiendeshwa na gesi ya bei nafuu.
  7. Ile 'smelter' aliyokuwa anaiota Magufuli kila akilala, tungejenga japo bei yake siijui tungemudu 😉. Tungeachana na kugombana kuhusu mchanga na makinikia, tungeuza madini yaliyokamilika.
  8. Gridi ya taifa ya mfumo wa maji safi maana ukame mdogo tu vilio kila kona.
  9. Tungemaliza tantalila zisizoisha kuhusu chanzo cha umeme nchini.
  10. Inabakia kama nusu, $ Bil 20 tungewapa kabisa mafisadi wagawane wasituharibie miradi yetu.
  11. $ Bil 5 tungewaita Mo, Bakhresa, Rostam na watoto wa Mengi wawekeze zaidi walichowekeza sasa na waajiri kina siye maana hizo pesa zinazidi walichonacho. Serikali wakifanya wao, miaka 5 mingi kila kitu juu ya mawe.
  12. Zilizobaki tunaziweka kwenye akauti tukisubiri mambo yaende mrama kama Tanzania tulivyozoea.
Kumbe kumekucha, ngoja niwahi kibaruani, taifa la watu milioni 60, eneo la mraba 900,000km, rasilimali kila kona tumeshindwa kuubadili uchumi wetu achilia mbali kuandaa Kombe la Afrika.
 
Usiamini kila stori za waarabu. Gharama walizotumia haziwezi kuvuka dola bilioni 15.
 
Qatar nchi yenye km za mraba 11,000 na watu wapatao milioni 3 imeandaa kombe la dunia lililotumia gharama zaidi tangu dunia iumbwe. Zaidi ya dola bilioni 220 zimetumika kwenye maandalizi mpaka kufanikisha kombe la dunia huku mapato ya kiuchumi yakitarajiwa dola bilioni 7.5 pekee mpaka kuisha kwake. Vimejengwa mpaka viwanja na makazi yatakayobomolewa baada ya mashindano. Pato la Tanzania ni $ Bilioni 62 kwa mwaka.

Ni Tanzania inaweza kufanya na $ bilioni 220
  1. Ingejenga bandari ya Bagamoyo($ Bil 10) na kuepuka kuingizwa mjini na Mchina
  2. LNG plant($ Bil 30) na kutumia gesi kila sehemu kuondokana na utumwa wa kulipa mafuta nje
  3. SGR($ 14) tungeifikisha Mwanza na Kigoma, kwa jeuri tugemjengea na Congo, akitoa mzigo wake Bagamoyo kituo cha kwanza Lubumbashi
  4. Deni la Taifa($ Bil 28) Tungelipa lote na bungeni tufocus kwenye kuongelea maendeleo maana mjadala wa deni la Taifa huwa unapoteza muda
  5. Madarasa($ Bil 2) Tungeacha kwenda kumpigia goti mzungu,
  6. BRT($ Bil 2) Tungejenga mwendokasi Dar nzima na kuwaonjesha Mwanza ikiwa na mabasi ya kutosha kama yale mekundu ya waingereza na kuachana na haya ya bluu(Level seat) yakiendeshwa na gesi ya bei nafuu
  7. Ile smelter aliyokuwa anaiota Magufuli kila akilala, tungejenga japo bei yake siijui tungemudu 😉 Tuangachana na kugambana kuhusu mchanga na makinikia, tungeuza madini yaliyokamilika
  8. Gridi ya Taifa ya mfumo wa maji safi maana ukame mdogo tu vilio kila kona
  9. Tungemaliza tantalila zisizoisha kuhusu chanzo cha umeme nchini
  10. Inabakia kama nusu, $ Bil 20 tungewapa kabisa mafisadi wagawane wasituharibie miradi yetu
  11. $ Bil 5 tungewaita Mo, Bakhresa, Rostam na watoto wa Mengi. Wawekeze zaidi walichowekeza sasa na waajiri kina sie maana hizo pesa zinazidi walichonacho. Serikali wakifanya wao, miaka 5 mingi kila kitu juu ya mawe
  12. Zilizobaki tunaziweka kwenye akauti tukisubiri mambo yaende mrama kama Tanzania tulivyozoea
Kumbe kumekucha, ngoja niwahi kibaruani, Taifa la watu milioni 60, eneo la mraba 900,000km, rasilimali kila kona tumeshindwa kuubadili uchumi wetu achilia mbali kuandaa kombe la Afrika.
UNAWEZA KUWA SAHIHI

How Much It Cost to Host Fifa World Cup: Look Back At Previous World Cups as Qatar’s Investment Rise To $220 Billion For 2022 Tournament​

 
Kujenga viwanja nane na hotel pamoja na hostel haziwezi kuvuka dola bilioni 15.

Uwanja mmoja ni kama dola milioni 500 kwahiyo vinane ni kama dola bilioni 4.

Sasa hapo nini kingine chenye gharama kubwa kuliko viwanja? Maana hoteli nyingi tayari zilikuwepo.
Kuna air conditioning system ya uhakika pale Qatar kwa kukwepa lawama za kuandaa mashindano kipindi cha joto. Hata hivyo sijaona hiyo $220 billion imefikaje mwenyewe nilijiuliza sana pamoja na kwamba ile ni nchi ya watu wachache haijajengwa kupokea watu wengi kwa pamoja kukaa mwezi mzima. Wangekuwa ni wale wapigaji wa Qatar Airways accomodation ingetosha. Wanetumia gharama kubwa ila imepitiliza, mwanzo nilidhani watacheza kwenye $30. South Africa ile 2010 walitumia $3.5 billion tu
 
Kujenga viwanja nane na hotel pamoja na hostel haziwezi kuvuka dola bilioni 15.

Uwanja mmoja ni kama dola milioni 500 kwahiyo vinane ni kama dola bilioni 4.

Sasa hapo nini kingine chenye gharama kubwa kuliko viwanja? Maana hoteli nyingi tayari zilikuwepo.
Miundo mbinu mingi mipya ilijengwaa kumbuka ile ni nchi ndogo kwaiyo ilijenga miundombinu mipya ili kubeba watu wengi vile nchi nyingi ambazoo ziliandaa michezoo hii nyuma zilikuwa zimeshaendelea kabisaa miundo mbinu mingi ilishajengwaa tofauti na quter wengi mnakataa gharama izi mtasema mlipewa mchanuo halisi

Sent from my Infinix X571 using JamiiForums mobile app
 
Wewe ni masikini wa fikra na unateseka sana,utakufa masikini na chuki zako za hovyo,
Ingia hata google ujue utajiri wa Qatar.
Wapi nimesema qatar sio matajiri? Hapa tunaongelea gharama za kuandaa kombe la dunia pamoja na uhalisia wake.
 
Kuna air conditioning system ya uhakika pale Qatar kwa kukwepa lawama za kuandaa mashindano kipindi cha joto. Hata hivyo sijaona hiyo $220 billion imefikaje mwenyewe nilijiuliza sana pamoja na kwamba ile ni nchi ya watu wachache haijajengwa kupokea watu wengi kwa pamoja kukaa mwezi mzima. Wangekuwa ni wale wapigaji wa Qatar Airways accomodation ingetosha. Wanetumia gharama kubwa ila imepitiliza, mwanzo nilidhani watacheza kwenye $30. South Africa ile 2010 walitumia $3.5 billion tu
Air conditioning system zipo miaka yote kwenye hizo nchi. Walichofanya ni kuziongeza kwenye viwanja,, hosteli na hoteli mpya. Lakini bado sioni gharama ziwe hizo wanazizitaja.
 
Miundo mbinu mingi mipya ilijengwaa kumbuka ile ni nchi ndogo kwaiyo ilijenga miundombinu mipya ili kubeba watu wengi vile nchi nyingi ambazoo ziliandaa michezoo hii nyuma zilikuwa zimeshaendelea kabisaa miundo mbinu mingi ilishajengwaa tofauti na quter wengi mnakataa gharama izi mtasema mlipewa mchanuo halisi

Sent from my Infinix X571 using JamiiForums mobile app
Qatar ni nchi ya utalii hivyo hoteli za maana zipo. Wameongeza nyingine pamoja na kujenga hosteli. Viwanja pia vimekula hela ila bado sioni gharama za kuvuka $15B.
 
Qatar nchi yenye km za mraba 11,000 na watu wapatao milioni 3 imeandaa kombe la dunia lililotumia gharama zaidi tangu dunia iumbwe. Zaidi ya dola bilioni 220 zimetumika kwenye maandalizi mpaka kufanikisha kombe la dunia huku mapato ya kiuchumi yakitarajiwa dola bilioni 7.5 pekee mpaka kuisha kwake. Vimejengwa mpaka viwanja na makazi yatakayobomolewa baada ya mashindano. Pato la Tanzania ni $ Bilioni 62 kwa mwaka.

Ni Tanzania inaweza kufanya na $ bilioni 220
  1. Ingejenga bandari ya Bagamoyo($ Bil 10) na kuepuka kuingizwa mjini na Mchina
  2. LNG plant($ Bil 30) na kutumia gesi kila sehemu kuondokana na utumwa wa kulipa mafuta nje
  3. SGR($ Bil 14) tungeifikisha Mwanza na Kigoma, kwa jeuri tugemjengea na Congo, akitoa mzigo wake Bagamoyo kituo cha kwanza Lubumbashi
  4. Deni la Taifa($ Bil 28) Tungelipa lote na bungeni tufocus kwenye kuongelea maendeleo maana mjadala wa deni la Taifa huwa unapoteza muda wakati tunaendela kukopa
  5. Madarasa($ Bil 2) Tungeacha kwenda kumpigia goti mzungu,
  6. BRT($ Bil 2) Tungejenga mwendokasi Dar nzima na kuwaonjesha Mwanza ikiwa na mabasi ya kutosha kama yale mekundu ya waingereza na kuachana na haya ya bluu tena Level seat yakiendeshwa na gesi ya bei nafuu
  7. Ile smelter aliyokuwa anaiota Magufuli kila akilala, tungejenga japo bei yake siijui tungemudu 😉 Tuangachana na kugombana kuhusu mchanga na makinikia, tungeuza madini yaliyokamilika
  8. Gridi ya Taifa ya mfumo wa maji safi maana ukame mdogo tu vilio kila kona
  9. Tungemaliza tantalila zisizoisha kuhusu chanzo cha umeme nchini
  10. Inabakia kama nusu, $ Bil 20 tungewapa kabisa mafisadi wagawane wasituharibie miradi yetu
  11. $ Bil 5 tungewaita Mo, Bakhresa, Rostam na watoto wa Mengi. Wawekeze zaidi walichowekeza sasa na waajiri kina sie maana hizo pesa zinazidi walichonacho. Serikali wakifanya wao, miaka 5 mingi kila kitu juu ya mawe
  12. Zilizobaki tunaziweka kwenye akauti tukisubiri mambo yaende mrama kama Tanzania tulivyozoea
Kumbe kumekucha, ngoja niwahi kibaruani, Taifa la watu milioni 60, eneo la mraba 900,000km, rasilimali kila kona tumeshindwa kuubadili uchumi wetu achilia mbali kuandaa kombe la Afrika.
Dah...umenifikirisha sana mambo haya tukiamua yanawezekana ...na mpaka sasa sijajua nani alituloga
 
Back
Top Bottom