Je, Wajua Waraka wa TEC Sio Neno la Mungu? Ili Kuepuka Kuchanganya Dini na Siasa, Kuna Haja Waumini Tuambiwe Ukweli Waraka wa TEC Sio Neno la Mungu?

Ndugu yangu biblia ni neno la ufunuo. Halisomwi ovyo ovyo tu.

Hebu soma hapa:-

Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
Mithali 11:14

Huyo aliesema hivyo ni muhenga wa walioleta kitabu kwa meli ambae ni ‘mtakatifu’.



Wewe muhenga wako ambae ni ‘mzimu’ alisema hivi; Miluzi mingi humpoteza mbwa njia.
 
Ndugu yangu Pascal unakosa kitu cha msingi katika imani yako. Huelewi maana ya neno la Mungu, na umepungukiwa na mengi.

Nitakupeleka taratibu ili uweze kuelewa. Katika maisha yetu ya kila siku, Biblia ni sawa na sheria, baada ya sheria kuna kanuni na miongozo.

Makanisa huunda kanuni na taratibu namna ya kutekeleza maagizo ya Mungu. Makanisa yote yanatumia biblia, yanatofautiana kwenye taratibu na kanuni ya kutekeleza yaliyomo kwenye biblia.

Biblia ambalo ni neno la Mungu, inaagiza kuwa ni wajibu wa viongozi wa dini na kwa mkristo yeyote kupigania haki.

Jeremiah 22:3-17

This is what the LORD says: Do what is just and right. Rescue from the hand of the oppressor the one who has been robbed. Do no wrong or violence to the foreigner, the fatherless or the widow, and do not shed innocent blood in this place.

Yaani

3. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Tendeni mambo ya haki na uadilifu. Mwokoeni mikononi mwa mdhalimu mtu yeyote aliyenyanganywa mali zake. Msiwatendee vibaya au ukatili wageni, yatima na wajane wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia mahali hapa.

Hivyo kwa maaskofu kutetea mali zilizo hatarini kuporwa ni kutekeleza agizo la Mungu linamtaka kila mwenye uwezo kupigania mali za mnyonge zisiporwe na mwenye nguvu.

Katika kulitekeleza neno la Mungu linalotutaka kupigania haki ya wanaoonewa, Kanisa Katoliki la Tanzania kupitia TEC, wamejiwekea kanuni ya kutoa waraka kila kunapotokea jambo lililo kinyume na mapenzi ya Mungu.

Kuunga mkono uporwaji wa bandari iliyo mali ya watu wote wa Tanzania wa sasa na wa siku zijazo ni kubariki dhuluma, kubariki dhuluma ni kumtumikia shetani ambaye ni bwana wa dhuluma.

Ni halali sana waraka wa maaskofu unaopinga dhuluma ya rasilimali ya watu wasio na sauti kusomwa madhabahuni ili kumdhihirishia Mungu kuwa kamwe Kanusa Katoliki halikuwahi kushikamana na wale wenye kupalilia dhuluma.
 
Hawezi akaelewa kazi ya Altar na Lactern.
 
Wakristo Wakatoliki wanadhani waraka huo wa Maaskofu Katoliki Tanzania, ni sehemu ya ibada na ni neno la Mungu!.
Hata hilo baraza halijasema kuwa huo waraka ni Neno la Mungu. Pale altare huwa kuna matangazo(taarifa) nyingi ambazo sio Neno la Mungu hutolewa kila siku ya ibada ili kuwaweka sawa waumini.

Kwa mfano matangazo ya ya kuzima simu sio Neno la Mungu ila hutolewa madhabahuni.

Sio tatizo kwa huo waraka kusomwa madhabahuni
 
Huu ni ushauri au agizo ?
 
Paskali sijui kama watakuelewa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao na nia ovu ya dhamira zao


Sociologists who do research on religion analyze the relationship between society and religion and study the role that religion plays in people’s lives. They do not try to prove that one religion is better than another. Nor is it their goal to verify or disprove anyone’s faith. As was mentioned in Chapter 1, sociologists have no tools for deciding that one course of action is more moral than another, much less for determining that one religion is the “correct” one. Religion is a matter of faith—and sociologists deal with empirical matters, things they can observe or measure. When it comes to religion, then, sociologists study the effects of religious beliefs and practices on people’s lives.
They also analyze how religion is related to stratification systems. Unlike theologians, however, sociologists do not try to evaluate the truth of a religion’s teachings. Emile Durkheim was highly interested in religion, probably because he was reared in a mixed-religion family, by a Protestant mother and a Jewish father. Durkheim decided to find out what all religions have in common. After surveying religions around the world, in 1912 he published his findings in The Elementary Forms of the Religious Life.
Here are Durkheim’s three main findings. The first is that the world’s religions are so varied that they have no specific belief or practice in common. The second is that all religions develop a community centering on their beliefs and practices. The third is that all religions separate the sacred from the profane. By sacred, Durkheim referred to aspects of life having to do with the supernatural that inspire awe, reverence, deep respect, even fear. By profane, he meant aspects of life that are not concerned with religion but, instead, are part of ordinary, everyday life.
Durkheim (1912/1965) summarized his conclusions by saying:
A religion is a unified system of beliefs and practices relative to sacred things, that is to say, things set apart and forbidden—beliefs and practices which unite into one single moral community called a Church, all those who adhere to them.
 
Kawaida hawezi kuhalalisha kosa- mbona hutulii ekaristi takatifu pale sisi waumini?
 
Mkuu samahani, kama wewe ni mkatoliki kweli, matangazo ndani Kanisa bila kujali aina ya hayo matangazo, siku zote ufanyikia wapi? Kwenye hili la bandari leo unataka wabadilishe utaratibu?

Ni Askofu, Paroko au Padri yupi ameshatangazia umma kuwa tamko lao la TEC kuhusu mkaba wa kampuni ya DPW na Serikali ya Tanzania ni "neno toka kwa Mungu"? Waraka wenyewe unasomeka "waraka wa baraza la maaskofu........." Hayo ya maneno ya "waraka toka kwa Mungu"" umeyatoa wapi? Unataka waumini waambiwe nini kisichoeleweka hapo? Una lengo la kuwaaminisha nini jamii hasa ya wasio wakatoliki?
 

Mimi nilifikiri ni bibulia
 
Wewe ni mkatoliki kwa jina tu ila hujui mafundisho ya kanisa lako. Ungekuwa unajua maandiko matakatifu ungejua kuwa hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu wakati wowote ila Mungu huwasiliana na watu kupitia wateule wake wenye uwezo wa decode lugha ya Mungu na kuiweka katika maneno ya kibinadamu. Kumbuka pia mitume, wamepewa uwezo wa kufunga na kufungua duniani na kuwa hivyo mbinguni. Niishie hapo kwani inaonekana uelewa wako katika mambo hayo ni mdogo sana
 
Yaani we mayalla na wewe unakuwaga wa ajabu sana. Give up brother, it's not adviced lakini kwa hapo ulipofikia hakuna cha maana utapata serikalini kwa kujikomba komba hivyo. Kama ni wa kuonekana ungekuwa ushaonekana. Don't fall in line of stupid group of people who badly discredit waraka so as waonekane na watawala.
 
unamshambulia bure mwenzako, hebusoma hii kutoka kwa Kalidinali Pengo

Kadinali Pengo ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana.


“Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazungumzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:-
“Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji…mimi nimeipokea, baadhi yenu mmeshaipokea.
” Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu…naamini na baadhi ya maaskofu lakini mimi mwenyewe hata nilikuwa sijaiona, hata nilikuwa sijaambiwa kuna kitu cha namna hiyo kinakuja.
“Tuelewane vizuri, ninaposema hivi sitaki kusema ile barua ni mbaya. Moja tu ni kwamba barua nzima imechanganya vitu viwili; Mwalimu angekuwepo angepiga kelele Maaskofu msichanganye Dini na Siasa.
“Angepiga kelele sana kuhusu waraka huu katika nyakati zake. Na hilo nawambia sina hofu, muende mkamwambie mtu yeyote nimesema hivi. Ndio wala msione aibu, najua labda hata wengine mmekunja nyuso, kunjeni tu lakini huo ndio msimamo wangu.
“Zipo sehemu katika waraka huo zinazochanganya Dini na Siasa na si kazi ya maaskofu ni kazi yenu wanasiasa mkiwa ni wa CHADEMA, mkiwa ni wa CCM lakini haiwezi kuwa kazi yangu mimi.
“Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa?
 
TEC ya Kitima CHADEMA wamekurupuka wamechanganya dini na siasa FULL STOP.
“Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa?(PENGO, 2015)

sasa wewe jifanye mkatoliki kuliko Papa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…