Je, Wajua Waraka wa TEC Sio Neno la Mungu? Ili Kuepuka Kuchanganya Dini na Siasa, Kuna Haja Waumini Tuambiwe Ukweli Waraka wa TEC Sio Neno la Mungu?

How did you know that? What does he need a presidential appointment for? And what do you need, if I may ask?
 
Yoooooote ni sawa lakini hoja yako ni "kuchanganya dini na siasa".

Maswali:

1. Siasa ni nini kwani? Na dini ni kitu gani? Na baada ya kuelewa hayo mawili, then unaweza kutueleza huku kuchanganya dini na siasa ndiyo kukoje hasa?

2. Na kwa kadiri mimi ninavyoelewa, siasa ni huduma bora za maji, usafiri, usafirishaji, uchumi, afya, elimu amani, usalama wa watu na mali zao, makazi na mavazi ya watu, haki na wajibu na ustawi na maendeleo ya ya watu kwa ujumla...

3. Sasa ndugu Pascal Mayalla hebu tuambie wewe unafikiri dini inahusika na nini kama siyo juu ya ustawi na maendeleo ya watu pia? Na unafikiri siasa na wanasiasa wapo huko ili wafanye nini kwa watu? Wapigiwe kura tu kisha waachwe wafanye watakalo na watakavyo huku wakitweza utu wa watu??

4. Na labda pia tueleze, hivi ni wakati gani mtu anaweza kuwa amevuka mstari toka kwenye siasa na kuanza kuelekea kwenye dini au kutoka kwenye dini na kuanza kuingia kwenye siasa? Kwa lugha nyingine mstari wa hii kitu unachorewa wapi?

3. Na kuhusu tamko la TEC; Kwanza hakuna cha kuchanganya dini na siasa au siasa na dini. Kanisa Katoliki kupitia kwa Baraza lao la maskofu (TEC) wametenda wajibu wao mtakatifu.

By the way, wewe Pascal Mayalla na wenzako mbona mnakimbilia kwenye kujadili TEC kwa kigezo cha kuchanganya na dini na siasa badala ya kujadili hoja zao zinazopinga mkataba wa bandari? Hii wewe unaionaje? Iko sawa kweli?
 
Kardinali Pengo alijibu haya maswali yako yote
 
Nimeumizwa na Uzi huu!
Wewe kama msomi ulitakiwa uuchambue sio unatuletea hisia zako,chefuzi kama hizi.

Viongozi wetu waliisha toa maoni Yao dhidi ya mkataba ule mbele ya raisi kwenye kikao cha pamoja na viongozi serikali.
Wameona maoni Yao yanapuuzwa wakajifungia wakaomba wakaja na maoni ambayo pia Kwa sehemu Mwenyezi Mungu amewagusa wayatoe wewe unawapinga hivi wewe mkatoliki Aina ya Tomaso,dunia ya Leo Una nafasi gani wewe?
Pascally uliyegombea ubunge kipindi cha utawala WA dhambi WA mwendazake Una nini la kutwanbia Sisi?

Wewe ungekuwa mkristu mwema usingekubali kugombea ubunge kipindi cha mwendazake.
 
Neno la Mungu halikushuka kama mvua bali ni yale mema unayonena,unapokemea baya unanena yale ya kimungu.Biblia inakemea umasikini,ufisadi,uzembe na unyonyaji.Waraka ni kemeo la kimungu ndio maana watu tunasali ili Mungu awafunue viongozi wafikie maamuzi yatakayompendekeza Mungu.
 
Ndugu Comte, sina comment na maneno ya Cardinal Pengo kama kweli ni yake. Siyo watu wote uwa na mtizamo wa aina moja ktk kila jambo.
Ila kuhusu hili la ndugu yangu Paschal Mayalla kwa kweli imebidi nimshangae maana kama yeye ni Mkatoliki ilibidi yeye ndiyo awe mstari wa mbele kuwaelimisha wasiyo wakatoriki taratibu za kanisa. Anaingia ktk mtego uleule wa kuchanganya siasa na dini.
 
How did you know that? What does he need a presidential appointment for? And what do you need, if I may ask?
I know him.He is a common pressman who live from hand to mouth.Wewe pengine ni masikini mwenzake.Hakuna mtangazaji tajiri bali matajiri ni wamiliki wa vyombo vya habari.Huyu kijana anatafuta uteuzi.shenzi kabisa.
 
Maaskofu wa Kanisa Katoliki wanateuliwa na kutenguliwa na Vatikani, sawa na balozi wa Marekani au India
Sasa iweje wawakilishi wa serikali ya Vatican waingilie sera ya nchi yetu na kuwaagiza wananchi wetu kuhusu sera zetu? Mabalozi wa kigeni wakifanya hivyo tungekubali? Naomba ufafanuzi
 
I know him.He is a common pressman who live from hand to mouth.Wewe pengine ni masikini mwenzake.Hakuna mtangazaji tajiri bali matajiri ni wamiliki wa vyombo vya habari.Huyu kijana anatafuta uteuzi.shenzi kabisa.
Huu utajiri au umasikini wa Paskali unaingiaje katika maoni yake? Yaani kila unapotofautiana na mtu maana yake ni yu masikini? be serious
 
Huu utajiri au umasikini wa Paskali unaingiaje katika maoni yake? Yaani kila unapotofautiana na mtu maana yake ni yu masikini? be serious
Kwanza rudi shuleni ukasome sarufi ya kiingereza maana kiingereza chako kinaonyesha umesoma juzijuzi elimu ikiwa imeharibika ukasoma tujifunze lugha yetu kibanga ampiga mkoloni very far away from like of us who went through cambridge tutorial papers.
 
Mapadre (wakiwemo maaskofu) wamepewa mamlaka hayo:

Mathayo 18:18
Amin, nawaambieni: yoyote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni, na yoyote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.
 
Mayala sidhani kama utaaminiwa na ujumbe huo kutolewa eneo upendekezalo.
Lakini je,wayaamini haya :

"Esta 4
7 Naye Mordekai akamweleza yote yaliyompata, na hesabu ya fedha Hamani aliyoahidi kulipa katika hazina ya mfalme, ili Wayahudi waangamizwe.

14 Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; walakini ni nani ajuaye kama wewe hukuujia ufalme kwa ajili ya wakati kama huo?"
 
Wananchi kila mahala, kila kijiwe wanaona IGA haifai na imejaa ufisadi.
 
Hamisi yuko sahihi. Mwenye nyumba ahojiwi, analalamikiwa.


Na kwa mujibu wa Katiba ya JMT, iko wazi ni nani Mwenye Nyumba.
Kuhoji ni kuuliza jambo na kutaka litolewe ufafanuzi, watanzania wana haki ya kumhoji Rais hata kama ni in direct lkn ujumbe ufike na hujavunja sheria!! Nadhan ungeiweka sawa context yako kua ... Wanaccm hawapasw kumhoji mwenyekiti wao na sio wananchi!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…