Je, wameondoa vibao vya mwendokasi kuzidi?

Je, wameondoa vibao vya mwendokasi kuzidi?

RRONDO

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2010
Posts
55,727
Reaction score
123,094
Je, ushawahi kupigwa tochi ambayo huielewi? Yaani umefuata vibao vyote vizuri kabisa lakini unafika mbele unaoneshwa picha kwenye 50kph zone imepita na 85kph au zaidi?

Twende pamoja. Kawaida ukifika eneo linalokutaka uende mwendokasi fulani kuna kibao(50kph mfano) na ukimaliza eneo hilo kipo kinachokuonesha kikomo 50kph kimeisha.

Mara nyingi Kama sio mara zote ukiona kibao cha kukuamuru uende 50kph upande wa pili wanaokuja wana kibao kinachowaruhusu waende zaidi ya 50kph.

Baada ya kuelewana kwenye hivi vibao twende kwenye mada. Wale jamaa zetu baada ya kuona tumekuwa watiifu wa 50kph na mapato yamepungua 'wameamua kutoa' vibao vinavyokuonesha isizidi 50kph au tuseme wezi wameviiba. Sasa wewe ukija hujui kuwa umeingia 50kph zone hivyo unaingia na speed zako kama zote. Ndio unapigwa tochi ambayo utabaki unajiuliza hiki kibao kiko wapi ambapo sijakiona?

Nimejuaje kama kibao kimetolewa/limetoka/hakipo? Ni hivi tochi hii utapigwa kwa mbele wakati unaingia hio zone na aliekupiga tochi atahakikisha kibao cha opposite direction kinachoruhusu 50kph kinaoneka! Yaani wewe unaenda upande ambao 50kph hairuhusiwi na ushahidi wake ni hiko cha opposite kinachoruhusu zaidi ya 50kph(kumbuka hivi vipo pamoja kulia na kushoto).

Huyu anaekupiga tochi anajua cha kukataza hakipo ndio maana kaja mbele ili akuoneshe cha kuruhusu mwenzio anaekuja opposite direction. Ukielewa ninalosema utaweza kujitetea ingawa utapotezewa muda sana.

Tufanyaje kuepuka hili? Hakikisha ukiona kibao upande wowote wa barabara unakisoma. Ukiona cha kuruhusu upande kinzani jua upande wako cha kuzuia wamekitoa vinginevyo utapigwa tochi na kubaki unajiuliza hii ni wapi!
 
Yaani tunaishi kwa kuviziana balaa. Ukiona taasisi inayotakiwa kusimamia sheria ndio inakuwa ya kwanz kukandamiza watu ujue kuna shida kubwa mahali

Akili za kindugai kabisa hizi hawa polisi wetu
 
Mara nyingi kwenye 50 ni maeneo ya vijiji, makazi, miji iliyopo pembezoni mwa highways.

Sasa ukikaribia mji ni vyema ukapunguza mwendo na kama huoni kibao upande wako, check upande wa pili.

Vibao vya kuanza au kumaliza 50 kawaida huwa ni vya duara...
 
Kuna eneo moja nadhani ni Chimala, Mbeya ile.

Kuna wazee wa favor wanatega mingo kwenye zebra crossing, ukifika pale unatakiwa usimame as if unataka kuruhusu watu/mtu avuke

Sasa wewe pita pale hata kama upo 50kph ambao ndio mwendo unaoruhusiwa kupita, unakutana na mkono wa weka pembeni...
 
Kuna eneo moja nadhani ni Chimala, Mbeya ile...

Kuna wazee wa favor wanatega mingo kwenye zebra crossing, ukifika pale unatakiwa usimame as if unataka kuruhusu watu/mtu avuke

Sasa wewe pita pale hata kama upo 50kph ambao ndio mwendo unaoruhusiwa kupita, unakutana na mkono wa weka pembeni...
Sheria haikulazimshi kusimama kwenye zebra kama hakuna mvukaji.
 
Sheria haikulazimshi kusimama kwenye zebra kama hakuna mvukaji.
Sasa jamaa wanafanya kama sheria za mbele, kwamba kwenye zebra au stop sign, lazima usimame kwa sekunde kadhaa (walau mbili hadi tano) then ndipo uendelee na sadari
 
Sasa jamaa wanafanya kama sheria za mbele, kwamba kwenye zebra au stop sign, lazima usimame kwa sekunde kadhaa (walau mbili hadi tano) then ndipo uendelee na sadari
Ukiwakomalia hawakufanyi kitu. Walileta huu ujinga Dar mkubwa wao akasema hakuna kitu kama hicho.
 
Nilishawahi kutana na jambo kama hilo.

Siku hiyo nimetoka arusha kama saa 4 asubuhi, nimefuata vibao vyote toka arusha mjini mpaka njia panda ya himo.

Nimefika Uchira mida ya saa 7 mchana, sijaona kibao cha 50kph, nimeshaanza kuchochea nasimamishwa na polisi, naoneshwa nimezidisha speed.

Nikawaomba wanioneshe hiko kibao kilipo, wakasema nisubiri pembeni badae watanipeleka. (Hapo wanajua unaenda mbali, kwahiyo ni obvious utajiongeza).

Kilichoniokoa sikuwa na leseni, nilikuwa na ile karatasi ya ku-renew leseni. Hawakuweza nipiga fina na sikuwapa kitu. Ila walinipotezea kama dk 30 hivi.

Wakiona wewe unaenda mbali, wanajua utajiongeza tu. Ila hapo njia panda mpaka moshi mjini hapaeleweki. Unaweza ukadhani umeshamaliza kibao kumbe bado kabisa. Kuna vibao nina uhakika wamevitoa.
 
Back
Top Bottom