Je, Wanajeshi watalazimisha kuchukua nguo za kijeshi hata kwa wanaomiliki kwaajili kufanya kazi za sanaa wakati sheria haijazuia?

Je, Wanajeshi watalazimisha kuchukua nguo za kijeshi hata kwa wanaomiliki kwaajili kufanya kazi za sanaa wakati sheria haijazuia?

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
mavazi polisi.jpg


Sheria ya Makosa ya Adhabu namba 16 na Kanuni zake haimzuii mtu kumiliki wala kuvaa mavazi rasmi ya Jeshi ikiwa vazi hilo rasmi litavaliwa kwaajili ya matamasha au maigizo yanayowakilisha Jeshi lolote la Polisi kwa "Nia Njema"

Kifungu cha 178 kifungu kidogo 1, 2 na 3 cha Sheria hii pamoja na kanuni zake (Kanuni msambamba ya 178) vinazuia uvaaji wa mavazi rasmi ya Jeshi lolote la Polisi kwa mtu yoyote ambae hatumikii Jeshi lolote la Polisi bila ya ruhusa ya Rais.

Screenshot 2023-09-07 152517.png

Pia inazuia uvaaji wa sare hizo kwa njia inayodhalilisha Jeshi la Polisi. Zaidi ya hapo, Sheria hii inazuia mtu yoyote ambaye hayupo katika utumishi wa Jeshi kuingiza, kuuza au kumiliki kwaajili ya kuuza bila ruhusa ya maandishi kutoka kwa Mkuu wa Polisi.

Screenshot 2023-09-07 152535.png


Sheria hii haizuii umiliki wala uvaaji wa mavazi hayo katika matamasha, kumbi za muziki au michezo kama sarakasi nk, au mahali popote pale michezo hiyo inaporuhusiwa kuchezwa hadharani katika kuliwakilisha Jeshi "Kwa Nia Njema".

Screenshot 2023-09-07 152544.png


Screenshot 2023-09-07 152550.png

Hii inamanisha kwamba mahali pekee ambapo Polisi wanaweza kwenda kuchukua sare hizo ni kwenye maduka au mahali popote zinapouzwa au kuhifadhiwa kwaajili ya kuuza na sio kwa watu binafsi au majumbani ambapo hazitundikwi/kuoneshwa au kuhifadhiwa kwaajili ya kuuzwa.
 
But msemaji wa jeshi alisema waz kwa wasanii kuna taratibu zao za kufuata ili wavae kwaajil ya shughuli za kisanii!
 
Achaneni na nguo za Jeshi au zinazofanana na na Jeshi. Wenyewe hawataki muvae, msipoteze muda kutafuta logic. Mambo ya Jeshi hayaulizwi hata bungeni wala Mahakamani.

Jaribuni kufanya ubunifu wa vitenge au Batiki lakini hizo za wajeda wenyewe HAWATAKI.
 
But msemaji wa jeshi alisema waz kwa wasanii kuna taratibu zao za kufuata ili wavae kwaajil ya shughuli za kisanii!
Sheria imesema unaruhusiwa kutumia sare hizo kwenye matamasha/kuiguiza ukiliwakilisha jeshi vizuri bila kutaja vibali kupata ruhusa ya kuzitumia... hapa bado unahitajika kuwa na kibali?
 
Achaneni na nguo za Jeshi au zinazofanana na na Jeshi. Wenyewe hawataki muvae, msipoteze muda kutafuta logic. Mambo ya Jeshi hayaulizwi hata bungeni wala Mahakamani.

Jaribuni kufanya ubunifu wa vitenge au Batiki lakini hizo za wajeda wenyewe HAWATAKI.
Ukitengeneza batik yenye rangi zao nazo zinaingia kwenye nguo zinazofanan na zao
 
Wapige marufuku zinapouzwa jana k.koo ma sweta yana mabaka kama yote yanauzwa kule boma ndo usiseme mtumbani kuna pensi kali mno kwahiyo waanze nao hao watoe taarifa wakiona nguo za jeshi kwenye mabalo yao waziwasilishe kituoni na wale kariakoo wasichue mzigo wa mabaka.
 
Jeshi limeanza kufanya uanamitindo. Linalinda brand ya vazi. Pathetic!

Hivi jeshi hili halioni kazi nzuri inayofanywa na majeshi ya Niger, Mali, Burkina Faso na Gabon?
Hawana kazi za kufanya ndio maana wanakomalia vitu vya kipuuzii!!yaani hilo nalo limekuwa inshu kubwaa!!!
 
Polisi lini wamesema wanasaka hizo nguo?

Au mleta mada hujui kutofautisha haya majeshi?

Mi najua JW lina msemaji wake na PT wanaye msemaji wao.Hili sakata lipo kwa JW ambao nadhani walitoa siku 7,ambazo zimeisha.
 
Sheria imesema unaruhusiwa kutumia sare hizo kwenye matamasha/kuiguiza ukiliwakilisha jeshi vizuri bila kutaja vibali kupata ruhusa ya kuzitumia... hapa bado unahitajika kuwa na kibali?
Msemaji wa jwtz alisema cku wanatoa siku saba!! So sometimes katiba iliyopo haizingatiwagi maeneo mengi!!
 
Polisi tena!

Tangazo ni JWTZ hao polisi(Raia) wametoka wapi tena?

JW wanakamata popote na yeyote asiyestahili kuzivaa
 
Hao wanaojiita wasanii ndio hovyo kabisa wanadhalilisha majeshi na mafunzo ya kijeshi. Wanavaa nguo za kijeshi na kukata mauno huku wakivaa tofauti.

Kuna linguine lilivaa nguo za Jeshi likaingia na kamba uwanja wa Taifa kwa kuiga mafunzo wafanyayo wanajeshi ilikuwa bado kidogo liache kiuno uwanyani.

Vitu kama hivi picha zikirekodiwa nchi nyingine wanaweza kudhani kuwa ni mwanajeshi kweli kumbe ni limtu hata mgambo halijachezs
 
Nahisi kama jeshi wanatuandaa kisaikolojia muda si mrefu watafanya kama Gabon
 
Back
Top Bottom