Je, wapinzani hawapotoshi kuhusu vitambulisho vya ujasiliamali?

Je, wapinzani hawapotoshi kuhusu vitambulisho vya ujasiliamali?

Kenge hawasikii mpaka damu ziwatoke masikioni,chadema ninkuachana nao tuu nakuwaona malofa na mafala.

Kiumbe kenge kwa mara ya kwanza kwenye bandiko lako linatoka kuelekezwa CDM.

Jiridhishe mara ngapi limetumika kuwamaanisha wale mboga mboga.

Hili copyright.

Ulikolileta si kwenyewe.
 
[

Mkuu kwani kweli huoni unafuu wowote kati ya 20,000/= vs 180,000/=? Hakuna taifa linaloendeshwa bila Taxes and levies, mimi naona serikali iliwaza vyema na imeweza kutanua vyanzo vya mapato.

unataka kuniambia bodaboda anakosa (20,000/360=55.55/=) Yaani ashindwe kulipa shillingi 56/= kila siku ambayo kwa mwaka ndio hiyo 20,000/=.

Hapana kwakweli hata Chadema mwaka 2100 itakapo kamata dola lazima itatoza kodi.

Nakubali kuelimishwa Mkuu
hiyo elfu 20,000 ni kodi au ushuru? unazijiua principles za government revenue & expenditure?, hiyo 20,000 inaenda kusapoti bajeti ipi, nani anafanya monitoring ya makusanyo na matumizi yake?, vile vitambulisho havina picha na havijawa linked na NIDA, kundi linalotozwa 20,000 tayari sheria ilitamka kuwa income yao ni exempt, sasa kama income yao ni exempt unapata wapi guts za kuitetea ili itozwe, makada muwe mnaenda shule kutafuta maarifa na sio kutafuta uteuzi
 
Wakuu habari zenu,

Katika muendelezo wa kampeni za uchaguzi huu limejitokeza hili suala la vitambulisho vya ujasiriamali,nami nikasema si vibaya nikilileta hapa jukwaani tuweze kujiuliza yafuatayo:-

- Kama kusingekuwa na hivi vitambulisho je hawa wajasiriamali wangelipa tozo za biashara kiasi gani?

Ilikuwa kawaida kwenye masoko kuwa na ushuru wa biashara usiopungua TZS 500/=, sasa kwa mahesabu ya kawaida huyu mtu kama atafanya biashara kwa mwaka mzima bila kukosa

maana yake (500x30x12=180,000).

Hii maana yake si huyu mjasiriamali angelipa 180,000/= kwa mwaka, lakini kwa sababu ya vitambulisho hivi atalipa 20,000/= tu ?

Sasa najiuliza jambo lipi ni jema kati ya haya mawili kulipa 20,000/= au kulipa 180,000/= kwa mwaka?

Nafikiria tungekuwa wakweli wa nafsi zetu nakuacha kuwadanganya au kuwayumbisha wananchi wenzetu.

Ni hayo tu nakaribisha kuelemishwa na pia povu ni ruksaa.

JPM 2020 - 2025

CCM 5 Tenaa
120031639_10158385745613930_446542250276946638_o.jpg


Mnaucheza mziki wa Mnyaturu huyu
 
Mimi ni miongoni wa wanaounga mkono hivi vitambulisho viwepo ili Machinga wabaki salama. Nakumbuka niliwahi kukuta Lori la Manispaa wanasomba bidhaa za Watu wakati ule niliumia sana.

Ingawa siungi mkono walivyokaa kiholela na kuharibu kabisa sura za miji...nilidhani Maofisa wa Mipango miji walioajiriwa na kulipwa na serikali wanapaswa kutafuta namna ya kuwapanga Watu hawa badala ya kila Mtu kukaa pembeni na kusema "tuwaache maana bwana Mkubwa kawaruhusu"
 
hiyo elfu 20,000 ni kodi au ushuru? unazijiua principles za government revenue & expenditure?, hiyo 20,000 inaenda kusapoti bajeti ipi, nani anafanya monitoring ya makusanyo na matumizi yake?, vile vitambulisho havina picha na havijawa linked na NIDA, kundi linalotozwa 20,000 tayari sheria ilitamka kuwa income yao ni exempt, sasa kama income yao ni exempt unapata wapi guts za kuitetea ili itozwe, makada muwe mnaenda shule kutafuta maarifa na sio kutafuta uteuzi
Iitwe kodi au ushuru lakini ni bora kuliko kuachwa hali iwe kama ilivyokuwa awali.

Haiwezekani wakaachwa wakae kati kati ya mji bila kulipa chochote...itakuwa ni vurugu badala ya biashara, ndio yale ya Mtu kubeba soksi mbili na kuzurura kwa kisingizio cha umachinga.
 
Iitwe kodi au ushuru lakini ni bora kuliko kuachwa hali iwe kama ilivyokuwa awali.

Haiwezekani wakaachwa wakae kati kati ya mji bila kulipa chochote...itakuwa ni vurugu badala ya biashara, ndio yale ya Mtu kubeba soksi mbili na kuzurura kwa kisingizio cha umachinga.
inabidi bunge litunge utaratibu maalum, 20,000 base yake ilikuwa nini? ililenga nini
 
Una maanisha nini unaposema pesa zinakwenda wapi?

Hauoni maendeleo ya miundo mbinu na maboresho ya huduma za kijamii?

Hii nchi ina wataalamu na watu wenye weledi katika kuweka mipango ya maendeleo, mbona Lissu anawachangisha wanachi hao hao maskini wakati walishalipa kodi zao na mkalipwa ruzuku.

Tuache ufitini.

..michango ni hiyari.

..pia ni kiwango kilicho ndani ya uwezo wako.

..Je, hivi vitambulisho aliyesema uwezo wake ni buku 2 alipewa?

..Au mmachinga aliyekuwa hana uwezo alisaidiwa kupewa hicho kitambulisho?
 
Iitwe kodi au ushuru lakini ni bora kuliko kuachwa hali iwe kama ilivyokuwa awali.

Haiwezekani wakaachwa wakae kati kati ya mji bila kulipa chochote...itakuwa ni vurugu badala ya biashara, ndio yale ya Mtu kubeba soksi mbili na kuzurura kwa kisingizio cha umachinga.

..wapeni ajira VIWANDANI.

..Jiwe aliahidi Tanzania ya viwanda.
 
Ingekuwa hivyo, watu wasingewekewa malengo ya kugawa vitambulisho, na visingetolewa kwa lazima kama ilivyo. Wafanyabiashara wenyewe wangevikimbilia.

Tangu lini uliona mfanyabiashara analazimishwa kupunguza gharama za kuendesha biashara yake mwenyewe?
Kwahiyo wewe unataka kutuambiaje?!
 
[

Mkuu kwani kweli huoni unafuu wowote kati ya 20,000/= vs 180,000/=? Hakuna taifa linaloendeshwa bila Taxes and levies, mimi naona serikali iliwaza vyema na imeweza kutanua vyanzo vya mapato.

unataka kuniambia bodaboda anakosa (20,000/360=55.55/=) Yaani ashindwe kulipa shillingi 56/= kila siku ambayo kwa mwaka ndio hiyo 20,000/=.

Hapana kwakweli hata Chadema mwaka 2100 itakapo kamata dola lazima itatoza kodi.

Nakubali kuelimishwa Mkuu
Ukienda sokoni kununua tenga la nyanya ujue limelipiwa ushuru. Ukienda kununua bidhaa dukani ujue ina vat. Pamoja na kitambulisho.
Watu walivichukia kwa sababu maafisa wa kata walilazimishwa kuviuza na wakuu wao. Yaana kulikuwa na utata. Utaratibu ungekuwa mzuri labda

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
..michango ni hiyari.

..pia ni kiwango kilicho ndani ya uwezo wako.

..Je, hivi vitambulisho aliyesema uwezo wake ni buku 2 alipewa?

..Au mmachinga aliyekuwa hana uwezo alisaidiwa kupewa hicho kitambulisho?
Serikali isiyokusanya Taxes and levies ni CORRUPT..
 
Mkuu hapa issue sio kulipa kiasi gani, hoja ni kuwa hicho ni kitambulisho hivyo kuna ubaya gani kikitolewa bure kwa mjasiriamali mdogo?

Mfano bodaboda kabla hakuwa analipia tozo yoyote, sasa hivi anatakiwa kulipa hiyo elfu 20 je naye umemuondolea mzigo au umemuongezea?

Hawa wajasiriamali wadogo ambao wanatafuta fedha ya kujikimu wanahitaji kusaidiwa na sio kukamuliwa hela kama Meko anavyofanya sasa.

Wanahitaji kuwekewa utaratibu mzuri ambao baadae utawawezesha kuwa walipaji wa kodi na watengeneze ajira kwa wengine sio kuwalipisha elfu 20 kisha kuwaacha wazurure hovyo na kuishia kuwa machinga maisha yao yote.

Mbali na hayo, hii fedha inayo kusanywa haijulikani ni kiasi gani kimepatikana na wala inaenda kufanya kazi gani.

Yote kwa yote, unaye jaribu kumtetea 'kashalegea' na kasema kulipia vitambulisho sio lazima kwa hiyo hata wasipolipa hakuna shida.View attachment 1578005
Utawala wa Lissu kila kitu kitakuwa bure! Vitambulisho vya machinga bure, bima ya afya bure, leseni za biashara bure, na hapatakuwepo na kodi ya aina yoyote!
Najua swali lako ni lile alilo uliza Dr Magufuli - kwamba hela ya kuendesha serikali itapatikanaje? Ni kwamba mali zetu (kama madini, misitu, fukwe etc) zitawekwa rehani kwa mataifa yalioendelea, na tupate hela tule bata.
Mambo ya hapa kazi tu ni ya utumwa! Lazima watu wawe na uhuru wachague wanayotaka! Hakutakuwa na Polisi maana kila mtu atafanya atakavyo.
Sasa kama CHADEMA/Lissu hawatafafanua vizuri, watu wengi wanafikiria itakuwa hivyo!
 
Utawala wa Lissu kila kitu kitakuwa bure! Vitambulisho vya machinga bure, bima ya afya bure, leseni za biashara bure, na hapatakuwepo na kodi ya aina yoyote!
Najua swali lako ni lile alilo uliza Dr Magufuli - kwamba hela ya kuendesha serikali itapatikanaje? Ni kwamba mali zetu (kama madini, misitu, fukwe etc) zitawekwa rehani kwa mataifa yalioendelea, na tupate hela tule bata.
Mambo ya hapa kazi tu ni ya utumwa! Lazima watu wawe na uhuru wachague wanayotaka! Hakutakuwa na Polisi maana kila mtu atafanya atakavyo.
Sasa kama CHADEMA/Lissu hawatafafanua vizuri, watu wengi wanafikiria itakuwa hivyo!
Kama unafatilia kampeni za Lissu anafafanua vema sana kila anapopita.

Anaposema UHURU anamaanisha watu wawe huru kufanya shughuli zao za kujiletea maendeleo bila kuonewa na serikali kama ilivyo sasa ambapo wakulima wanahangaika kutafuta mbegu na pembejeo wenyewe ila wakivuna serikali inawajazia ushuru wa mazao kila kona na inawalazimisha kuuzia mazao yao hapa nchini au kwa serikali kwa bei za hasara tena huku wakikopwa. Wafanya biashara wamekuwa wakibambikwa kodi zisizolipika na kusababisha wafunge biashara zao kwa kufilisika.

Anaposema HAKI anamaanisha watu wasitendewe unyama na wala unyanyasaji na serikali ama watendaji wake.

Watu wasibambikwe makesi ya uchochezi na uhujumu uchumi ili tu kuwafilisi mali zao kwa hila ama kuwanyamazisha wasiikosoe serikali. Watumishi wapande madaraja na mishahara kama inavyosema sheria ya kazi, sio kuwaburuza na kuwaonea kwa kigezo cha kufanya maendeleo.

Kutopeleka maendeleo baadhi ya maeneo ambayo yamechagua upinzani huku serikali ikikusanya kodi za watu hao. Kujiamulia matumizi ya fedha zetu bila idhini ya bunge kama vile kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa Chato unao gharimu zaidi ya bilioni 39 kusipo na tija yoyote.

Anaposema MAENDELEO YA WATU anamaanisha, tutumie rasilimali/mapato/mikopo tunayopata kwa kuzingatia vipaumbele vyetu kama taifa.

Haya masuala ya kujenga madaraja/SGR/ Mabwawa na kununua Ndege wakati wananchi wanashindia mlo mmoja, ukienda hospitali hakuna madawa ya kutosha, wauguzi na Madaktari hawatoshi, hakuna vifaa tiba. Huduma duni za maji na mizigo ya kodi inayopandisha gharama za maisha kwa mwananchi.

Serikali haitoi ajira kwa kigezo cha kufanya miradi mikubwa ambayo hata hivyo haijafata taratibu za kisheria na wala haifanyiwi ukaguzi kujua kama ina tija kwa taifa.
 
Back
Top Bottom