Je, wapinzani ni wakombozi?

Je, wapinzani ni wakombozi?

...alikuwa katoka kula Magibi, si unajua tena malala nje yote ya jamii ya mizizi ni dawa ya usingizi!!! aibu kweli, kubwa zima linauchapa usingizi bungeni....Chakechake, hamna mbunge hapo, mpeni "chubwiii" cycle inayokuja.

Be eazy babu...unajua tena kupambana na mafisadi is not kid's play.....Lol
 
Be eazy babu...unajua tena kupambana na mafisadi is not kid's play.....Lol

bottomline ni kuwa kalala bungeni, inatosha kumpa-fire!!! lakini ktk Tanzania yangu mmmmmmmmmmmmmh.......ndio kwanza wakina Mwiba wanakuja na theories za kwamba picha ni ya kutengenezwa!!! Ushabiki na ufisadi vinaimaliza Tanzania.

shame on you Magimbi bint Muhogo kwa kulala bungeni tena mchana kweupeee. Shame on you Mwiba kwa kuja na vistory vyako vya kishabikishabiki dizaini ya whodunnit....jamaa hawapo sophiscated kihivyo, kwahiyo usituletee mambo ya kwenye movie hapa.
 
Mama wa watu kachoka kusikiliza kauli za Pinda na za akina Marmo zinanzojichanganya changanya na zisizoeleweka, inachosha akili.

Mtu wa kawaida lazma uchoke akili na mwili kama leo hii unadanganywa hadharani kwamba Meremeta ni ya Jeshi, wakati wamiliki ni waingereza, akili lazma ichoke tu.
 
Mama wa watu kachoka kusikiliza kauli za Pinda na za akina Marmo zinanzojichanganya changanya na zisizoeleweka, inachosha akili.

Mtu wa kawaida lazma uchoke akili na mwili kama leo hii unadanganywa hadharani kwamba Meremeta ni ya Jeshi, wakati wamiliki ni waingereza, akili lazma ichoke tu.

..bora angechukua udhuru na kurudi hoteli au popote anapoishi hapo dodoma badala ya kuuchapa usingizi!! hii ishu si ndogo bwana, huwezi kulala kazini.....
 
She Has Done The Wrong Thing At Wrong Place......!

Yes sir...alikuwa na kila sababu na jinsi za kufanya asikamatwe ktk picha hii!! huyu mama ni pathetic kabisa na hafai kuendelea kuwa mbunge. Hafai....kulala kazini tena wakati kazi zikiendelea pia nao ni UFISADI.
 
Wacheni Kumzushia Mama Wa Watu Hiyo Picha Imekuwa Edited Na Ndo Maana Unaona Mleta Mada Ameweka Kapicha Kadogo...... Kwa Wale Wote Waliosoma Majira Ya Leo Angalie Ukurasa Wa Mbele Kabisa Kuna Picha Ya Huyu Mama Angalieni Kama Amelala Au Yupo Macho.......... Tutoleeni Uzushi Usio Na Msingi
 
Hivi ule unga unga (wa kisukuma) uliokwenda kwa Mkemia Mkuu, ulifagiliwa wote? Maana usikute kuna chembe chembe zilibaki na sasa unaendelea kuwatesa wabunge wetu!
 
bottomline ni kuwa kalala bungeni, inatosha kumpa-fire!!! lakini ktk Tanzania yangu mmmmmmmmmmmmmh.......ndio kwanza wakina Mwiba wanakuja na theories za kwamba picha ni ya kutengenezwa!!! Ushabiki na ufisadi vinaimaliza Tanzania.

shame on you Magimbi bint Muhogo kwa kulala bungeni tena mchana kweupeee. Shame on you Mwiba kwa kuja na vistory vyako vya kishabikishabiki dizaini ya whodunnit....jamaa hawapo sophiscated kihivyo, kwahiyo usituletee mambo ya kwenye movie hapa.
Inaonyesha unaongelea Tanzania ya Miaka 15 nyuma ,watu katika mambo ya video na picture editing wako mbele sana kwa kiasi chao na kwa kilichofanywa basi ni kitu kidogo tu ,ila subiri tumsikie huyo mama nae akiharakia kudai kulipwa feza kwa kuzalilishwa kwa wapiga kura wake ,akizalilishwa kwa WaTanzania ,ila huenda akawa ana uwezo wa kuchuja kati ya sense na none sense na kupambambanua na kumsanifu muandishi na kumueka katika kundi la kutaka kufurahisha watu na kuvutia gazeti lake.Ila akicharuka na kuona akitinga mahakamani ataondoka na kitita basi tusicheze mbali ,halafu wapiga picha wanaruhusiwa kuingia Bungeni wakati wa vikao ?
 
Binafsi nina hakika kuwa huyu Mama hakuwa ktk Kikao cha Bunge kama alivyodai mwandishi..Nadhani ilikuwa kabla ama baada ya bunge kuanza/kwisha..
Kwanza yaonyesha wazi kuwa hapakuwepo na mtu mwingine zaidi yake na mpiga picha ambaye wanatazamana (eye contact). Huyu Mama kapigwa picha akijipumzisha, kisha imetumiwa kumpakazia..
Ni maoni yangu!...
 
Anakandamiza kizenji, bonyeeeeeee!!!! Ila msinung'unike sana ndugu zangu, huyu mama kama mbunge mwingine yoyote mwenye mume- akitoka hapo lazima akapige 'night shift' kwa mumewe kulinda ndoa, kwahiyo rukhsa tu!
 
Huyu mama ana ugomvi na Nyaulawa pamoja na Karamagi. Ile picha hajalala kabisa, tazameni macho chini ya miwani mtaona yako wazi. Hivi kuna watu wanalala macho wazi? Mwenye gazeti la majira atazame vizuri badala ya kumsingizia

PM
 
Huyo ni mzenji na kiitikadi anajua kinachojadiliwa hapo hakisaidii wala hakipunguzi zaidi ni kujadili mambo ambayo mwisho wake hupitishwa japo hayafai ,hivi ni mambo mangapi yalipelekwa bungeni na hayakupitishwa tokea lianze Bunge hili ?
Yaani ukisema ndio ,ndio hilo hilo na ukisema hapana ,inakuwa hapana ila hilo hilo.
 
MMK mambo uliyoandika katika makala yako ni mazuri kwa upande mmoja na kwa upande mwingine hayaeleweki. Nina maana gani? Namaanisha kuwa ni kweli katika mfumo tulionao sasa wa CCM haiwezekani akaingina mpinzani akaweza kuleta maendeleo kama ulivyoyataja hila watu kwa kuchoka lazima wafikilie kuwa kikitoka CCM kikaingia kingine kutakuwa na hafadhali.

Kwa upande wangu naona mfumo mzima inabidi ubadilike turudi kule kwa mwanzo kwani sasa hivi hata kama serikali nzima ni nzuri lakini mfumo wenyewe umeoza maana hata watoto wadogo sikuizi wanajua rushwa kuwa ukipokea mambo yana kuwa fresh. Mmesikia mara nyingi mtu akiwa mfuatiliaji wanasema hiyo NGUVU ya soda. Lakini nani katuleta mpaka hapa ni hao CCM kwani hakuna mjinga ambaye atakuwa kwenye nafasi wenzake waine yeye apitishe ni ngumu utakuta au aingie kwenye mkondo au utupwe nje hiyo inabidi uchague mwenyewe.

Hivyo Tanzania inaweza kubadilika na ikawa nchi nzuri lakini inabidi jamaa kwanza watoke harafu hao watakao ingia waingia na sera za nchi si vyama. Maana hatuna sera nzuri kwani zote ni vyama lazima tuwe na vipaumbele vya TAIFA ambavyo hata kiwe chama gani lazima kwanza kifuate vipaumbele.

Upande mwingine ambao sikukuelewa ni kuwa siasa zetu huwa kuna watu ni wajanja wanakuwa hawaelewe wamesimamia wapi! Makala yako mojakwamoja lakini kwanini sasa useme kuwa hawa wapinzani wahaidi kuwa watarekebisha hayo yote? Je hao ambao wamekaa miaka 44 wamelifanyia nini TAIFA maana hata hivyo vilivyokuwepo tulinyang'anya kutoka kwa wakoloni na sasa tumewarudishia japo vipo baadhi tulivyoanzisha wenyewe. Unata tubaki na CCM kwasababu ya hulka za kibinadamu kuwa huwa tu wabinafsi hivyo hata hao wakiingia ni ngumu wote kuwa wasafi? Huoni kuwa waliokuwepo kwa muda mrefu inabidi watoke waingie wengine ili angalau vitu kama EPA, MIKATABA MIBOVU NA MENGINEYO VIFANYIWE KAZI? Lazima tujaribu kupeana moyo ili angalau tuweze kusonga mbele vinginevyo hata hicho kidogo tutakikosa.

Shukrani.
 
Wapinzani Tanzania wanakatisha tamaa
Barnabas Maro
Daily News; Monday,November 03, 2008 @20:20

wapinzani.JPG

Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia (kulia) na Mwenyekiti wa TLP, Agustino Mrema wakizungumzia mustakabali wa vyama vya upinzani.

BAADA ya kuona udhaifu katika vyama vya upinzani, Mwalimu Julius Nyerere alipata kusema kuwa ‘Upinzani imara utatoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi.' Tangu Serikali ya Tanzania iliporuhusu upinzani, vyama hivyo vimelegalega, kutokana na viongozi wake kuwa na mitazamo tofauti.

Baadhi yao hutumia nafasi zao kujinufaisha. Kwa hakika ni watu wenye kuangalia masilahi yao zaidi, kuliko haki au uhalali wa mambo wanayoyapigania, yaani maendeleo ya wananchi. Kwa lugha ya Kiingereza naomba niwaite opportunists.

Ukiangalia mwenendo mzima wa upinzani nchini, utadhani wananchi wanaelezwa kikamilifu haki zao za kiraia na wanachotakiwa kufanya ili kukubali upinzani. Badala yake baadhi ya viongozi wa vyama hivyo, wamekuwa watu wa kubangaiza maisha tu.

Hawa ni wale wanaohesabu vyama, wakitoka kimoja kwenda kingine na kubadili vyama mara tatu au nne. Kiongozi wa aina hiyo anapokuwa katika chama A husema mabaya mengi ya chama C.

Lakini kesho na kesho kutwa anaporudi kwenye chama kile kile alichokikosoa na kuanika 'madhambi' yake, hula matapishi yake mwenyewe, kwa kusema mazuri ya chama chake cha zamani na kukisema vibaya chama alichokikimbia.

Inashangaza kwa sababu haiwezekani jana kwa leo tu kile alichosema hakifai kwa kuwa kimeoza, ghafla kimekuwa kizuri na kile alichokiona kizuri kwa miaka kadhaa, leo hakifai hata chembe.

Mbali ya tamaa za vyeo na ulaji, kuna baadhi yao huwa mamluki wanaotumwa kwenda kuchunguza mambo katika vyama vingine.

Mamluki hawa wanapokamilisha kazi zao hurejea kwa waliowatuma na kutoa shutuma kadhaa, kwamba huko walikokuwa, viongozi wao ni wababaishaji wasiokuwa na mwelekeo unaofahamika.

Tumeona viongozi mbalimbali wakihama kutoka chama kimoja kwenda kingine. Baadhi yao wamefanikiwa kupewa nafasi kubwa katika vyama wanavyohamia na wengine kubahatika kuwa madiwani, wabunge na hata mawaziri serikalini.

Matokeo yake ni wananchi kuyumbishwa wasijue pa kushika. Je, huu ndio upinzani uliohitajika?

Maana upinzani si uadui, bali ni kioo cha kukisaidia chama kilicho madarakani kutojisahau na kukizindua pale kinaposinzia au kukosea. Tatizo sugu kwa viongozi wa upinzani ni kutoaminiana, kunakosababisha wasiwe na umoja wenye nguvu. Hapana shaka kwamba kila chama humu nchini, kuna maeneo yanakopendwa zaidi ya vyama vingine.

Lakini kwa mshangao, wakati wa uchaguzi wowote, kila chama husimamisha mgombea hata kama hakijulikani!


Kama mara mbili au tatu hivi, wapinzani walijaribu kuwa na umoja, lakini ulisambaratika, lilipokuja suala la kiongozi gani asimamishwe kuviwakilisha vyama vyote vya upinzani katika kiti cha urais wa Tanzania.

Hapo viongozi husisitiza umuhimu wa kila chama kusimamisha mgombea wake. Kwa kufanya hivyo, udhaifu na tamaa za viongozi wa vyama hivyo, huwachanganya wafuasi wao.


Matokeo yake ni kuzigawa kura na wao kubakia kuwa wasindikizaji tu, kwa faida ya chama chenye nguvu. Hii inahalalisha ule usemi kwamba vita vya panzi furaha ya kunguru.

Maana yake ni kwamba watu wamoja, kama marafiki au jamaa, wakigombana huwa ni furaha kwa mpinzani wao, kwani huweza kuwanyang'anya mali yao au kuwapiga mmoja mmoja.

Ndivyo inavyokuwa rahisi kwa CCM kupata ushindi katika chaguzi mbalimbali. Hii inathibitishwa na wingi wa wabunge wake dhidi ya wale wa upinzani wakijumuishwa pamoja.

Ni kuingia gharama zisizokuwa za lazima, kwa mfano, kwa chama kingine chochote kusimamisha wagombea kwenye uchaguzi wa uwakilishi kisiwani Pemba kukabiliana na wagombea wa CUF au kumsimamisha mgombea wa chama kingine dhidi ya aliyesimamishwa na CCM kule Zanzibar. Vivyo hivyo kumsimamisha mgombea wa chama kingine sehemu iliyo ngome ya chama tofauti.

Viongozi wanapaswa kuondoa tofauti na tamaa zao. Wafike mahali waaminiane kwa dhati ili waachiane maeneo wanayojua. Hawawezi kushinda endapo kila chama kitasimamisha mgombea wake. Eneo ambalo chama A kinapendwa zaidi ya vingine, vyama vilivyosalia viunganishe nguvu zao na kumpigia debe mgombea wa chama A.

Kama wangezinduka tangu mapema, hivi leo tungekuwa na wabunge wengi zaidi wa upinzani kuliko wachache waliopo sasa.
Tangu zamani, Chama Cha Mapinduzi kimekuwa na utaratibu mzuri sana wa utawala.

Chama hicho kimejikita kuanzia ngazi za chini kabisa. Mashina, Serikali za Mitaa, kata, tarafa, wilaya, mikoa mpaka taifa kuanzia vijijini hadi mijini. Ndio maana CCM imekuwa na utaratibu mzuri wa kujua wanachama wake, kupanga mikutano na chaguzi mbalimbali.

Kwa maana hii, hata vijiji vya ndani kabisa yasikofika magari, utaona bendera za CCM zikipepea. Sivyo ilivyo kwa wapinzani. Wao wamebaki Dar es Salaam wakitumia ukumbi wa Maelezo kuwafikia wanachama wao walioko vijijini.

Vingi ya vyama hivi sidhani kama vina ofisi vijijini na mara nyingi wananchi huvisikia wakati wa chaguzi za udiwani na ubunge. Haishangazi basi kwa upinzani kukosa nguvu vijijini kwa sababu wananchi hawavielewi.

Wapinzani wanapaswa kuondoka Dar es Salaam na kuwafuata wananchi vijijini, wakajitambulishe na kueleza sera zao na kwamba wakipata ridhaa yao watawafanyia nini.

Wakati wanapojinadi wawe makini kwa kila wanachoahidi, kwani mara nyingi wanasiasa huwa wepesi kuahidi mambo yasiyotekelezeka, mradi tu wawafurahishe wapiga kura ili wachaguliwe katika nafasi wanazogombea!

Wananchi wa vijijini hawajui maana ya upinzani, ndio maana ni rahisi kudanganyika kuwa wakikubali wapinzani wachukue madaraka, kutatokea machafuko, mapigano na mauaji, kama ilivyo katika baadhi ya nchi zinazotuzunguka!

Ni wakati sasa kwa wapinzani kuandaa sera zao na kuwapelekea watu wa vijijini wakiikosoa serikali kwa dhati, kuhusu mambo mengi ya maendeleo, badala ya porojo zisizokuwa na manufaa kwa wananchi.

Wakati wa mikutano ya kampeni, wagombea wajihadhari kutumia lugha za matusi na kupakana matope. Wananchi hawataki kusikia mambo hayo. Wanachongojea kusikia kutoka kwa wagombea na vyama vyao ni sera, yaani jinsi watakavyoshughulikia matatizo ya wananchi.

Kwamba mgombea wa chama fulani alikopa fedha hajalipa au alihusika na kashfa fulani itawasaidia nini wananchi? Uchaguzi uliomalizika hivi karibuni kule Tarime, uwe chachu na fundisho kwa wapinzani.

Baadhi ya vyama vya upinzani vilivyosimamisha wagombea, kwa kweli viliingia gharama za bure na kupoteza muda. Ukweli ni kwamba ulikuwa mpambano wa vyama viwili vyenye wafuasi wengi eneo lile -- Chadema ilitetea viti vyake vya udiwani na ubunge, na CCM ilijaribu, bila mafanikio, kuvitwaa viti vile.

Kwa upande mwingine, CCM wanapaswa kutambua kuwa wananchi wa leo ni tofauti na walivyokuwa zamani. Sasa watu wanajua kupokea maneno kisha wakayachambua kujua mbivu na mbovu.

Kadhalika watambue kuwa kila siku ina jina lake na kwamba jana haiwezi kuwa leo, kama jinsi leo isivyoweza kuwa jana. Wananchi nao waondokane na tabia ya kutojiorodhesha kwenye Daftari la Wapiga Kura.

Kupiga kura ni haki ya msingi ya raia yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 18 na mwenye akili timamu. Hata wanapojiorodhesha, ni muhimu pia kujiandikisha na kupiga kura bila kukosa.

Imedhihirika kuwa wengi hudharau kujiorodhesha na hata wale wanaojiorodhesha, hukataa kwa makusudi kwenda kupiga kura. Hawa ni wale wanaouza haki zao kwa kukubali kununuliwa wakitoa shahada zao za kupigia kura kwa kupewa vijisenti, nguo, vyakula na pombe!

Watu wa aina hii huwa mstari wa mbele kulalamika kuwa hao waliochaguliwa, hawatekelezi ahadi zao na kwamba walikuwa wanatafuta 'kula' badala ya kura. Je, kama hukwenda kupiga kura, unategemea nini?

Au kama unakubali kuuza haki yako kwa kupewa vijisenti na vishawishi vingine, hujui unajidhuru mwenyewe? Kura yako moja yaweza kabisa kubadili mwelekeo. Uchaguzi wa Tarime ni changamoto kwa wote.

Wapinzani waseme 'ah, kumbe inawezekana?' CCM nao waseme 'tukaze buti kwani ngoma ikivuma sana hupasuka!' Mwalimu Nyerere alisema ‘Upinzani imara utatoka ndani ya CCM'. Tunasubiri kuona unabii huo!.

Mwandishi ni mchangiaji makala wa gazeti hili.
 
Wapinzani Tanzania wanakatisha tamaa
Barnabas Maro
Daily News; Monday,November 03, 2008 @20:20

wapinzani.JPG

Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia (kulia) na Mwenyekiti wa TLP, Agustino Mrema wakizungumzia mustakabali wa vyama vya upinzani.




Maana upinzani si uadui, bali ni kioo cha kukisaidia chama kilicho madarakani kutojisahau na kukizindua pale kinaposinzia au kukosea. Tatizo sugu kwa viongozi wa upinzani ni kutoaminiana, kunakosababisha wasiwe na umoja wenye nguvu. Hapana shaka kwamba kila chama humu nchini, kuna maeneo yanakopendwa zaidi ya vyama vingine.

Lakini kwa mshangao, wakati wa uchaguzi wowote, kila chama husimamisha mgombea hata kama hakijulikani!

Kama mara mbili au tatu hivi, wapinzani walijaribu kuwa na umoja, lakini ulisambaratika, lilipokuja suala la kiongozi gani asimamishwe kuviwakilisha vyama vyote vya upinzani katika kiti cha urais wa Tanzania.

Hapo viongozi husisitiza umuhimu wa kila chama kusimamisha mgombea wake. Kwa kufanya hivyo, udhaifu na tamaa za viongozi wa vyama hivyo, huwachanganya wafuasi wao.


Mwandishi ni mchangiaji makala wa gazeti hili.



Oh, thank God! Nilidhani huyu ni mwandishi wa Daily News.
Nilitarajia mwandishi afafanue ni kwa vipi kukosekana kwa umoja baina ya wapinzani kumesababishwa na kutokuaminiana. No research, no right to speak!

Kikwete naye akihutubia bunge mwaka huu alikatumia vibaya haka ka neno "kutoaminiana". Alisema muafaka wa Zanzibar umekwama kwa sababu ya kutokuaminiana baina ya CUF na CCM. I was so mad hearing that from Mr. Politician. Kwa kauli zake kama vile anawahutubia punguani, JK atakumbana na aibu kubwa sana muda si mrefu.




.
 
Ni bahati mbaya kwamba sijapata nafasi ya kupita hapa kwenye jarida letu tangu jana. Pamoja na michango katika mada zilizokuwepo, nimekutana na hii thread mpya ya Mh. Mzee Mwanakijiji. Niliamua kuanza kuisoma hii maana huwa namumini sana huyu mheshimiwa katika kuibua mambo kwa lugha nyepesi hadi kwa lugha ya mbwembwe ya mazingaombwe na ushairi! Lakini nasikitika kwamba huyu mheshimiwa sijui kitu gani kimetokea hapa maana katika siku za karibuni kweli amebadilika; sio Mwanakijiji niliyemjua. Naanza kujiuliza hivi ni yeye au kuna mtu amevamia jina lake. Maadamu hajakanusha kwamba sio yeye itabidi niendelee kuamini tu kuwa ni yeye. Labda tu ameokoka. Basi ngoja nami nikabiliana na huyu mlokole wetu mpya.

Kwanza, hakuna hata sehemu moja popote pale katika jarida hili, kwenye vyombo vya habari, katika sera au katika mikutano ya hadhara ambapo wapinzani wamewahi kusema kuwa wao wakiingia madarakani basi matatizo yote yatakuwa yamekwisha. Ndio nasema huyu mheshimiwa labda ameokoka kwa sababu sio kawaida yake ku-make sweeping statements namna hii.

Wanachosema wapinzani ni kuwa CCM imeirudisha nchi nyuma sana. Hatupigi hatua, hasa katika kipindi hiki cha JK. Mifano ipo wazi kabisa kuonesha kuwa hatuendi mbele kuanzia kwenye vigezo vya takwimu za kiuchumi za kitaalamu (macroeconomic indicators) kama vile kukua kwa pato la taifa, thamani ya shilingi, n.k. hadi kwenye maisha ya kila siku ya mtanzania. Kwa mfano takwimu za leo zinaonesha kuwa ukuaji wa uchumi wa Taifa umeshuka katika kipindi cha mwaka mmoja cha JK. Thamani ya shilingi imeshuka kuliko maelezo tangu hao wasanii waingie madarakani. Katika maisha ya kawaida, karibu kila bidhaa muhimu imepanda zaidi ya mara 100 katika kipindi cha mwaka mmoja cha ndugu yetu JK. Kwa mfano sukari ilikuwa inauzwa katika ya sh. 800-1200 hadi Mkapa anaondoka; sasa hivi inauzwa kati ya sh. 2400-3600! Hivi ni baadhi ya viashirio kuwa CCM wanaendesha serikali vibaya.

Sitaki kurudia mambo ya mikataba ya umeme. madini, rushwa, n.k. Haya hata wewe umekiri katika mawasilisho yako japo kwa kebehi. Sijui kwamba kama ni tatizo au la, hiyo nakuachia mwenyewe.


Kikubwa zaidi ambacho tunapigia kelele serikali hii ya chama cha majambazi ni uongo. Kwa kipindi cha chini ya mwaka mmoja serikali ya JK imeongopa zaidi ya mara tano. Mbili kati ya hizi ni muhimu kuzitaja:

i)Rais mzima alidanganya wananchi kuhusu umeme wa Richmond kuwa ungeanza Octoba. Hii ilikuwa ni mara ya kwanza Rais kusema uongo bila aibu katika historia ya nchi yetu. Yaani hata hakuwahi kujutia
ii) Serikali ya CCM wamedanganya mara tatu kuhusu mradi wa mabasi yaendayo kasi. Kwanza walisema ungeanza Agosti 2006; halafu wakasema utaanza January 2007. Sasa leo wamesema utaanza March 2009 karibu na uchaguzi mkuu wa 2010!


Sasa katika mambo yote haya unataka wapinzani wasisema. kazi ya nini basi? Kwa hivyo wanachosema wapinzani ni kuwa nchi haiendi mbele kimaendeleo. Hi ni kwa sababu alipoiachia Nyerere, Mwinyi akaja akaturudisha nyuma, akaja Mkapa akaturidisha nyuma kutoka pale alipotuachia Mwinyi. Huyu kaka yangu JK ndo inaonekana anaturudisha nyuma tena kwa kasi mpya ya ajabu. Ndiyo, tutasemaje kama ameweza kuongeza deni la nje kwa $385milion chini ya mwaka mmoja katika kipindi chake cha uongozi? Halafu unataka tumpigie makofi, kwa yepi hasa?

Katika matatizo haya, wapinzani hatusemi eti tutayamaliza kama ukungu. Tunachosema ni kuwa: 1) Hatutakuwa wanafika kwa kuwapa wananchi ahadi za ghiliba ili watupigie makofi. Tutasema kile ambacho tunataka kukifanya na ambacho tuna uwezo nacho. 2) Tutaweka misingi imara ya demokrasia ili kwamba wananchi wawe na uwezo wa kuwajibisha viongozi. Na hapa ndipo palipo na matatizo. Viongozi wa CCM wanajua wapo juu ya sheria; wanachosema wao basi kinatosha. Ndio maaana mikataba ya maana wanasaini kisirisiri lakini Taifa zima linaumia. Mambo muhimu yanayotakiwa kwenye katiba hawataki kuyaweka maana hawataki kujifunga. Sasa nchi zozote zisiongozwa kidemokrasia lazima ziishie ilipoishia CCM. Ni ghiliba mtindo mmoja; hata mtu akiteuliwa UN wanachukua sifa wao. Mtu akipata scholarship ya kusoma nje wanasema ni kazi ya CCM. Watu wanahangaika na msongamano hakuna barabara Dar, wao wanasema eti kwa kuwa wameleta maendeleo kwa kasi mpya hadi magari yamejaa barabara hazitoshi! Yaani ni usanii tna ghiliba tu ndo kinachoendelea. Kwa mtindo tusifie kitu gani hasa?

Kwa kifupi, hakuna njia ya mkato katika kuiletea nchi yetu maendeleo maana uharibifu uliofanyika ni mkubwa. Lakini tunahitaji kupiga hatua, na tuonekana kwamba tunapiga hatua. Sasa hivi hatupigi hatua, na ushahidi upo kedekede. Tukisema tusionekana kwamba eti sisi tunafikiri tutamaliza matatizo kama ukungu.

Usiwalishe wapinzani maneno. I believe you are not playing part of CCM gimmicks and manipulations!

Duna kuna watu wanaona mbali sana jamani
 
well.. swali bado linahitaji majibu na hadi sasa the answer is in the negative..
 
Back
Top Bottom