Je, Watanzania tumeridhika kabisa na Dharau, Kejeli na Matusi anayotufanyia sasa Tapeli wa Kiimani 'Kiboko ya Wachawi' akitokea huko Kwao Congo DR?

Je, Watanzania tumeridhika kabisa na Dharau, Kejeli na Matusi anayotufanyia sasa Tapeli wa Kiimani 'Kiboko ya Wachawi' akitokea huko Kwao Congo DR?

Kwa Mwamposa Yesu yupo pale, kwanza halazimishi mtu kufika Kawe hata kwenye tv unapokea mibaraka, Matomaso ndio wanasafiri mpaka wafike live Kawe.

Ni makosa kumuweka Mwamposa kwenye kundi la kina Kiboko ya Wachawi, ukifuatilia mahubiri yao ni rahisi tu kumtambuwa yupi ni Apostle wa kweli.
Aisee... hii safari ndiyo kwanza inaanza.
Gari ni moja, wanaobalika ni madereva tu...
Sijui tutaendeshwa hadi lini...?
Inabidi JESUS arudi haraka aje aone waumini tulivyogeuzwa mazuzu.
 
Mi Kuna mdogo wangu aliniazima gari lake pale kwenye dash board kuna mafuta ya mwamposa, roho ikawa inaniambia yatupe nje, akiuliza utamwambia ulepeleka carwash madogo wameyapoteza labda
Mwisho wa siku nikayaacha tu.
Ni roho ya ibilisi hiyo, ikiona mafuta ya upako inateseka.
 
Ni roho ya ibilisi hiyo, ikiona mafuta ya upako inateseka.
Hakuna kitu kama hicho hivi mafuta ya upako ndio nini? Nyie ndio mnaibiwa yaan mafuta ya upako uyanunue uweke kwenye gari, nyumbani, ofisini, chumbani kwamba ndio utakuwa safe😀😀😀
 
Kubaini na kukubali udhaifu ndio hatua ya kwanza ya kutatua changamoto yoyote duniani wazungu wanaita ownership of the problem. Kuna matukio kama hayo yalishatokea na yanaendelea kutokea, hivi sasa wakati natoa comment hii Kuna watu wanapigwa lakini hatujifunzi, kwa nini. ?
Kwa hiyo Ili tutatue hili tatizo kwanza bado sisi Watanzania LAZIMA TUKUBALI wengi wetu ni WAJINGA
Angalia yaliyowahusu au yanaowahusu watu hawa

Babu wa Loliondo
Mchungaji Mwingira
Mzee wa Upako
Mchungaji Kakobe
Mtume/Nabii Mwamposya
Sharifu Majini
Kibwetele
Mr. Kuku, Zanzibar
DECI Mabibo
Gwajima
Na wengine

Hao mtaji wao mkubwa ni ujinga wetu. Hawana jinsi wanaweza ku survive ikiwa sisi tutakuwa werevu

Baada ya kukubali sisi ni WAJINGA, then tunafanya nini kutoka ktk ujinga huu ?

Serikali
Inaonekana haina shida na hawa watu na ndio maana wanaendelea ku survive. Kumbuka tukio la Moshi (Mwamposya)baada ya watu kadhaa kufa tulitarajia serikali ingechukua hatua lakini hicho hakikutokea na bado Mshua anatamba kwenye Majukwaa. Tunajiuliza
Kuna udhaifu ktk kusajili haya Makanisa/ Taasisi ?
Kuna rushwa ?
Kuna maslahi ya kisiasa wakuu wetu wanayapata kushindwa kuwachukulia hatua ?
Kuna udhaifu wa Kisheria ambao wanautumia kama uchochoro kiasi inakuwa ngumu kuwawajibisha ?
Ukiangalia tukio la Moshi baada ya kutokea tu. Waziri wa Home Affairs+ RPC wa Kilimanjaro, walikuwa wako tayari kuchukua hatua. lakini walivyomsoma boss wao JPM alionekana Hana shida na Mshua, hivyo jamaa (RPC + Waziri) wakapotezea hii issue
Yale makumi ya watu waliokufa kwenye lile tukio ikaonekana kama kifo cha panya tu
Na hii love affair haikuwa tu kwa Mshua wa Kawe bali ilikuwa kwa Gwajiboy + Mzee wa Upako

Jamii

Bado jamii yetu Iko nyuma ktk masuala ya kuwasiliana/kufunguka juu ya changamoto tunazokutana nazo
Kwa mfano hata humu JF kungekuwa na platform ya watu walioumizwa na matapeli wa aina hii
Motivational speakers kama Nanauka tulitarajia aje na vitu vya kutahadharisha wananchi wa kawaida na mada kwa mfano "UTAJUAJE KANISA/MCHUNGAJI NI MPIGAJI"
Katika suala hili nampa big up Mchungaji Hananja

Media

Kwanza nilipopata tu taarifa za huyo jamaa Kiboko ya Wachawi nikajiuliza media ambayo ilikuwa Ina host vipindi vyake hawa kuwa wanatathmini maudhui yake. ?
Kwa muda gani amekuwa akiendesha vipindi ?
Hapa sasa ndio naamini kwa kiasi kikubwa sana Mauaji ya kimbari ya Rwanda yalichochewa na media especially Radio

Education System

Kwenye mfumo wetu wa elimu za dini yaani EDK(Elimu ya Dini ya Kiislamu) + Divinity zitiwe mada maalum jinsi ya kung'amua Matapeli waliojificha kwenye kichaka cha dini
Lakini pia inaweza ikawekwa hata kwenye Civics/General Studies

Wakatabahu
Kuna vitu umeandika lakini huvielewi vizuri nitakujuza vichache tu.

Museven ndio Kibwetere halisi, achana na propaganda. Fuatilia Joseph Kony anatokea wapi na ana uhusiano gani na Kibwetere marehemu.

Pili tukio la Moshi ni hujuma za wazi dhidi ya huduma ya Mwamposa usidhani vyombo vya dola havipo au havipati taarifa, Mwamposa ni tishio kwa makanisa makongwe.

Halafu pia uelewe dini ndio siasa kongwe kabisa duniani, wanasiasa wa leo hawana watu, bali watu wa dini ndio wana watu, kiongozi wa serikali hawezi kucheza na kiongozi wa dini mwenye watu, labda kiongozi huyo awe na ajenda ya kupinduwa serikali hapo ndio partneship yao inaweza kuvunjika.

Unaona kuna ile kamati ya amani ya viongozi wa dini kina sheikh Alhad Musa na wenzake, kile ni chombo tu cha kuwapumbaza Watanzania na hao viongozi wa dini wanalipwa marupurupu yao na serikali.

Kwahiyo viongozi wa dini na serikali ni damdam kasoro wachache ambao wamesimama wahesabiwe wameikataa hii batwili hapo kuna Sheikh Ponda, Askofu Bagoza na Askofu Emaus Mwamakula hao ni mfano kwa uchache wamekataa kutumia majoho yao kuwa machawa wa serikali.
 
Hakuna kitu kama hicho hivi mafuta ya upako ndio nini? Nyie ndio mnaibiwa yaan mafuta ya upako uyanunue uweke kwenye gari, nyumbani, ofisini, chumbani kwamba ndio utakuwa safe😀😀😀
Nina uhakika nakuzidi ufahamu wa mambo mengi ya dunia hii utakuja kuyajuwa baadaye sana.

Mimi nimeukataa utapeli wa ccm unaamini naweza kutapeliwa na watu wa dini?

Kwa taarifa yako mimi ni muumini wa kanisa la Roman katoliki mpaka leo, ila namuelewa vizuri Mwamposa, Yesu yupo pale.

Halafu wengi hamjui chochote zaidi ya kufuata mkumbo wa chuki.

Mwamposa hana kanisa, wala Mwamposa haubiri dini, bali Mwamposa ana huduma (ministry) na siyo Kanisa ( church)

Hizo rituals za mafuta na maji ya upako unaweza kufanya hata ukiwa nyumbani kwako ukanunuwa chupa ya maji na ukajiconnect na madhabau yake kwenye tv, ukishangaa hili washangae wanaoswali kuelekea kibra.
 
Dogo anapiga kazi sana yule namkubali anajitambua kiuchumi wacha awanyolose.
 
Si ametimuliwa Bongo huyu jamaa!? Acha aongee unafikir ni vzr kunyang'anywa tonge mdomoni!? Hana nguvu yyte ya MUNGU ni mlaghai tu hvo apuuzwe yeye na waumini wake.
 
Kwa Mwamposa Yesu yupo pale, kwanza halazimishi mtu kufika Kawe hata kwenye tv unapokea mibaraka, Matomaso ndio wanasafiri mpaka wafike live Kawe.

Ni makosa kumuweka Mwamposa kwenye kundi la kina Kiboko ya Wachawi, ukifuatilia mahubiri yao ni rahisi tu kumtambuwa yupi ni Apostle wa kweli.
Huyo nae ni tapeli kama matapeli wengine over
 
Sisi hatunaga utaifa,tuna uccm na uchadema na ufisadi unaolindwa na Dola Kwa kivuli Cha katiba mbovu!

Utaifa ulishakufa siku nyingi sana!!

Umebaki hayo!
 
Huyo nae ni tapeli kama matapeli wengine over
Na ndiyo maana Kamtapeli hadi Akili zake na sasa kabakia tu kuwa Juha (Fool) hapa Jamvini hadi kusema kuwa miaka ya 70 aliyokuweko Yeye Tanzania na Mkoani Dar es Salaam kulikuwa hakuna Hospitali ya Agha Khan na kwamba zilizokuwepo ni yake ya Walala Hoi aliyozaliwa ya Ocean Road na Muhimbili. Nilishalidharau hilo Jamaa Kitambo tu na nashangaa sijui kwanini huwa linapenda pia Kushobokea Mada zangu wakati Kutwa linasema halinipendi.
 
Mbona uliambiwa uhamie uhamishoni Burundi kutoka kwenye nchi yako hukuona dharau
 
Sasa ni rasmi Watanzania wachache waliokuwa Wakimuamini wametuponza mno Watanzania wote kwa anayotufanyia.
Na anajua kweli kutu nanga na kutukejeli maana kaja kuchuma huku anawekeza kwao huku alikuwa shambani kujivunia ma pesa.
 
Back
Top Bottom