ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,154
- 4,184
Habri za wakati huu;
Nimekuwa nikifuatilia kwa kina mitazamo ya wananchi hasa vijana wa umri kati ya miaka 18 hadi 45 ambao wengi wao ndio wapiga kura watakaoshiriki katika kuamua nani awe rais mwaka huu wa 2020.Kwa fikra na mtazamo wao kwa hakika wanatafuta sana alternative candidate/Mbadala wa Magufuli.
Wanawatazama watu kama kina Zitto Kabwe,John Mnyika,Freeman Mbowe na vijana wengine katika siasa za taifa letu na kutoka kuona kama watapata Mbadala wa hakika wa Magufuli.Wengi wao sio kwamba wanataka kumpigia kura Magufuli bali wanatafuta mbadala wa Magufuli.
Wanataka mtu ambaye atasimama kama anti establishment ambaye atasimama nao katika matatizo yao ya siku kwa siku na kuwasaidaia kushughulikia matataizo yao.Wanataka wanasiasa ambao wataachana na siasa za kutafuta political mileage na badala yake wakae nao,wazungumze nao na kushirikiana nao katika kutatua matatizo kama vile ya ajira,biashara,uchumi,afya,elimu,na changamoto nyingine za kimaisha na kimaendeleo.Wanataka kiongozi ambaye watamuona kwamba ametokana na wao na sio mwenye uchu w madaraka.
Je kiongozi huyo yupo?Kama hayupo je nani atapewa kura zao?Kuna uwezekano kwamba wengi wao wasipige kura.Ndio.Wengi wa vijana wa kundi hili wanaweza wasishiriki katika kupiga kura kwa sababu ya kutokuona umuhimu wa kufanya hivyo.Ni muhimu sasa viongozi wakajipambanua na jamii kwa kushirikiana nao ili kujenga jamii mpya na kujenga hamasa ya maendeleo
Nimekuwa nikifuatilia kwa kina mitazamo ya wananchi hasa vijana wa umri kati ya miaka 18 hadi 45 ambao wengi wao ndio wapiga kura watakaoshiriki katika kuamua nani awe rais mwaka huu wa 2020.Kwa fikra na mtazamo wao kwa hakika wanatafuta sana alternative candidate/Mbadala wa Magufuli.
Wanawatazama watu kama kina Zitto Kabwe,John Mnyika,Freeman Mbowe na vijana wengine katika siasa za taifa letu na kutoka kuona kama watapata Mbadala wa hakika wa Magufuli.Wengi wao sio kwamba wanataka kumpigia kura Magufuli bali wanatafuta mbadala wa Magufuli.
Wanataka mtu ambaye atasimama kama anti establishment ambaye atasimama nao katika matatizo yao ya siku kwa siku na kuwasaidaia kushughulikia matataizo yao.Wanataka wanasiasa ambao wataachana na siasa za kutafuta political mileage na badala yake wakae nao,wazungumze nao na kushirikiana nao katika kutatua matatizo kama vile ya ajira,biashara,uchumi,afya,elimu,na changamoto nyingine za kimaisha na kimaendeleo.Wanataka kiongozi ambaye watamuona kwamba ametokana na wao na sio mwenye uchu w madaraka.
Je kiongozi huyo yupo?Kama hayupo je nani atapewa kura zao?Kuna uwezekano kwamba wengi wao wasipige kura.Ndio.Wengi wa vijana wa kundi hili wanaweza wasishiriki katika kupiga kura kwa sababu ya kutokuona umuhimu wa kufanya hivyo.Ni muhimu sasa viongozi wakajipambanua na jamii kwa kushirikiana nao ili kujenga jamii mpya na kujenga hamasa ya maendeleo