Je waweza kupenda pasipo kumwona?

Je waweza kupenda pasipo kumwona?

Hii ni habari ya kweli kabisa,Rafiki yangu wa damu walitengana au tuseme waliachana na mkewe miaka mingi iliyopita.

Mkewe huyo akaolewa na kuzaa watoto kadhaa. Sasa rafiki yangu huyu kaniambia nimtafutie mchumba nikamsimulia kuhusu shemeji yangu mmoja yuko upcountry nikampa namba ya simu wakaweza kuwasiliana.

Cha kushangaza ni kuwa rafiki yangu huyu amefikia hatua ya kufanya maamuzi ya kumuoa yule shemeji yangu, hawajakutana hawajuani hata picha yake kila mmoja hamjui mwenzake zaidi ya mawasiliano kwenye simu tuu!!!

Ni mwezi wa tatu sasa unaenda wako kwenye mapenzi moto moto, ila kutokana na wingi wa kazi kila mmoja hapati mwanya wa kwenda kuonana na hasa hasa umbali uliopo kati yao.

Naomba kusikia kutoka kwenu wadau.


Kiroroma jibu unalo kwanini unatusumbua watu mkuu ? wk end ishaanza kaka, tunataka kuanza kuchapa maji !!!

Point ni kwamba anaamini maelezo yako..!! Ulisha msimulia kuhusu shemejio..!! Labda uulize kwamba kwanini Rafiki yako ameamua kukuamini wewe katika jambo la kumtafutia mchumba !! Na si kwanini kaamini mwanamke uliyo mtafutia! Kwaheri na wk njema !!!!
 
Very interesting case!


Mkuu nadhani jamaa hataki kuaminiwa na Rafiki yake..!!! Marafiki hujuana tabia ( interest , hobbies ) na mambo mengine .
Itakapofikia mahala pa kutafutiana wachumba ina maana wanajuana na kuaminiana vizuri..Sasa kesha pewa mkoba wa dawa anatuuliza sisi kwanini kapewa wakate kaonekana yeye tunguli ya mapenzi !!!!
 
Kiroroma jibu unalo kwanini unatusumbua watu mkuu ? wk end ishaanza kaka, tunataka kuanza kuchapa maji !!!

Point ni kwamba anaamini maelezo yako..!! Ulisha msimulia kuhusu shemejio..!! Labda uulize kwamba kwanini Rafiki yako ameamua kukuamini wewe katika jambo la kumtafutia mchumba !! Na si kwanini kaamini mwanamke uliyo mtafutia! Kwaheri na wk njema !!!!

Labda sikueleza ni kwa kiasi gani huyu rafiki yangu ananiamini,Tunaaminiana vizuri ,Ila hili la mchumba amelifanya kwa kasi kubwa ya mwanga wa jua kinyume kabisa na ushauri na matarajio yangu.Ukweli nilitarajia kuwa angevuta subira wapate kukutana,kujuana,na kufikia ahadi za kuoana.Pia siyo kwamba nilimsimulia nikiwa na nia ya kupiga debe kwamba ndiye huyo anafaa kuwa mchumba LA HASHA! Hata baada ya kung'amua kuwa wako kwenye advanced stage nilimshauri ajitahidi waonane kwanza lakini kaniwekea pamba masikioni, hasikii langu tena.Ndo maana nikatinga hapa jamvini kupata ushauri wa wadau wengine.Nawasilisha Mkuu.ASANTE
 
hicho ki2 mbona kipo2 lakin ingekua vizuri wakatumiana hata picha ili kila mmoja aka clear dought alizonazo akilini kuhusu mwenzake siku hiz kuna njia nyingi2 za kusend PIX kama MMS hi ni simple sana kwa sabab wote wana cm na garama ya MMS ni Tsh 80.
 
Nimesikia wema sepetu yuko kijijini.
Mhhhhh...
 
6149b7abd06d9c3ebe4808d75defffac.jpg
 
Hii ni habari ya kweli kabisa,Rafiki yangu wa damu walitengana au tuseme waliachana na mkewe miaka mingi iliyopita.

Mkewe huyo akaolewa na kuzaa watoto kadhaa. Sasa rafiki yangu huyu kaniambia nimtafutie mchumba nikamsimulia kuhusu shemeji yangu mmoja yuko upcountry nikampa namba ya simu wakaweza kuwasiliana.

Cha kushangaza ni kuwa rafiki yangu huyu amefikia hatua ya kufanya maamuzi ya kumuoa yule shemeji yangu, hawajakutana hawajuani hata picha yake kila mmoja hamjui mwenzake zaidi ya mawasiliano kwenye simu tuu!!!

Ni mwezi wa tatu sasa unaenda wako kwenye mapenzi moto moto, ila kutokana na wingi wa kazi kila mmoja hapati mwanya wa kwenda kuonana na hasa hasa umbali uliopo kati yao.

Naomba kusikia kutoka kwenu wadau.

...yawezekana sana tu, jaribu kujiweka kwenye nafasi ya 'wenye ulemavu wa macho' na ndoa zao.
 
Nduguhilo linawezekana kabisa.Kwani hujawahi kuwasikia boys to men na wimbo wao I knew iloved you before i met you.
 
Back
Top Bottom