Je, wewe ni Mzaliwa wa Kigoma? Fanya haya ili uraia wako usitiliwe shaka yoyote na wabaya wako

Rudi kwenu mkapambane nae,haiwezekani mtu mmoja awasumbue maelfu tena wasomi.
 
Cha kushangaza katika kasumba hii ya uraia huwakuti Wajaluo, Wamasai, na watu wa Kusini. Kwanini muda wote Kigoma na marachache Kagera. Kwanini wahamiaji haramu wa mkoa wa Kigoma na Kagera wanaogopwa sana, tofauti na Mara, Arusha, Ruvuma na Mtwara?.
Sababu iko wazi: wahaamiaji kutoka Burundi na Rwanda walioko katika mikoa ya jirani na nchi zao waliacha maadui kule walikotoka. Uadui wao unaendelea kwa kufanyiana kampeni chafu duniani kote. Baadhi ya kamepeni chafu dhidi yao hufanywa na viongozi wa nchi walikotoka na matajiri wakubwa. Mmasai wa Tz na Kny ni ndugu, mkulya wa Tz na Kny ni ndugu vile vile wajaruo
 

Ni kutokana na watanzania walichokishuhudia kipindi cha uhai wao!

Kama hujui ubaguzi huunganishwa na matukio fulani hauji tu kama kwamba wanabaguliwa no!

Watusi/wahutu ——mauji ya kimbari/M23/Machafuko
Wasomali—-ugaidi
waarabu——ubaguzi/ugaidi

Usihangaike kulalamika jua kila kitu kinachanzo!! Ubaya unaishi
 
Mbeya, Songwe, Mara na Kilimanjaro nazo zimepakana na nchi jirani na kuoa na kuolewa ni jambo la kawaida sn, mbona hakuna usumbufu wowote?

we netanyahu jina au kiazi??

Uwe unasoma comment zangu utoe uvundo kichwani.

Ubaya unaishi!! Yaliyotokea kwene hizo nchi ndio yanayosababishwa watu wawe na hofu au kinachoendelea Kongo!! Ni hilo lililoganda kichwan mwa watanzania si kua wanahangaika na mipaka yote ushaona wanasumbua mipaka ya kenya ,zambia au malawi??
 
Unasahau Rwanda Burundi na Tanganyika zilikuwa nchi moja koloni la mjerumani?

[mention]jay-millions [/mention] wewe n mrundi au mtusi??
Huwezi ng’ang’ania hawa watu wakat intelligencia ya nchi imeona kuna shida ya usalama!!

Kama wana kwao warudi
mbona sisi tulipokea wasomali wabantu walioishi miaka zaidi ya 200 somalia??
 
Ndugu watu wameishi vizazi na vizazi hawajafanya baya lolote leo unawafananisha na hamasi? Hii chuki imepitiliza sasa
Nimeona comments za mtu somewhere nikafumbuka macho: anasema kuwa huenda kuna agenda ambayo serikali inataka kutusahaulisha, anasema kuwa haoni sababu kwanini hili lisemwe sasa na lisemwe na mamlaka makubwa kwenye forum kubwa kama ile. Nimeona pia mtu akitoa orodha ndefu ya watu waliotajwa kuwa wanaasili ya nchi jirani. mtoa maoni kataja Julius Nyerere, KInana, Moses Mnauye, Iddi Simba , apson Mwangonda etc
 

kwaiyo we ni chotara??
 
Unafikiri kujaza nchi ubaguzi na chuki ndo kutaleta nafuu ya maisha? Tukimaliza kubagua hao who next? Waarabu, wahindi, wasomali au wazenji? Ubaguzi ukiulea hautaishia hapo bali mwishowe utabagua hata watoto wako mwenyewe wa kuwazaa

we bana rudi kwenu!!

Kongo had sasa watu milion 12 wamekufa!!

Kosa ni kupokea wageni?? bora kufa kwa ubaguzi kuliko siku mgeni akuue
 
Mm ni mtanzania.Lakin pale Uganda kuna, kabira yetu wengi sana. Haya Mambo Nyerere, aliyakataa. Nyerere mwenyewe alitokea Rwanda na kuja Musoma. Wajita wakawaita vijanaki. Yaan waliokuja na nn. Leo tunaanzisha debate za Kipumbavu.

we nchi yako yenyewe inatwaliwa na nyankole watusi wa uganda.

Tangu waingie madarakani hawajatoka hadi leo
 
Sikiliza dada angu unatakiwa usome historia, hawajaanza kusumbuliwa leo ni muda mrefu tangu enzi ya Mwl, nadhani kuna shida zaidi tunatakiwa kufanya utafiti mkuu.
 
Kagera wanachukiwa kwa sababu ya nguvu zao kiuchumi, elimu, nk, pia kwa vile kuna propaganda kuwa Rwanda(ya, Kagame) ni adui yetu, na wana kagera/karagwe/ngara, wana fanana Sana na watu wa huko Rwanda, Burundi, Uganda,
Ukiwa jamii ya mpkani, huwezi kuzuia kuwa na ndugu upande wa pili, hii mipaka aliyeiweka, hakuangslia jamii, akatenga jamii moja pande mbili,
Nina binamu zangu tumesoma shule za msingi Zambia, tunaongea kiwemba, chuo mi nikarudi bongo, wenzangu, wakazamia Zambia, wameoa huko, wanamiriki ma kampuni huko, wanapiga mpaka kura huko, harafu wakija bongo, kuna kenge uhamiaji, aliyepata ajira kwa kubebwa na D zake,anasema sio raia.
 
Rudini makwenu tu Nchi za Watu ni Za watu Na kwanin mlazimishe Urai kwenye Nchi za Watu apo mlipo utakuta Mnalima kwenye Ardhi yetu bure kabisa kana kwamba iyo Ardhi ni ya Mababu zenu Wakati Ardhi Yenu ipo ila Mnaogopa Kurudi
 
Me mw hata sikuwazaga ilo sana mpk rafiki yangu aliyezaliwa Kagera akasumbuliwa kupata passport ndo akaniambia watu wa ukanda la ziwa wanafanyiwaga ivi coz wapo kw boda nkaona ajabu coz mw nimezaliwa Mbeya.
 
Mbona sijaishi Kigoma na naona waha wanasumbuliwa hata huku kwetu? akionekana tu anaitwa Ndikumana anaitwa uhamiaji, hata mimi kwetu ni mpakani sn lakini hakuna usumbufu wowote na tuna vuka na kurudi salama

Weee ni muhaya na sio mtanzania ndio maana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…