Je, wezi wa Wizara ya fedha wameshafahamu aina ya Rais tuliyenaye?

Je, wezi wa Wizara ya fedha wameshafahamu aina ya Rais tuliyenaye?

Patriot

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2008
Posts
5,705
Reaction score
4,703
Kwa wakulima wa mahindi na mpunga, tunaelewa uharibifu wa nyani na tumbili na ndege. Huwa tunaanza kuweka matambala na kichwa cha bandia ili wanyama hawa waamini huyo ni mlinzi.

Wanyama polepole huanza kuzoea na kugundua kwamba hayo ni matambala na hakuna kichwa, ni chungu cheusi. Hapo sasa mazao huanza kuliwa.

Tumeanza kuona wizi na ulaji wa hovyo. Tena ndani ya wizara mama yenye kushikilia hazina ya taifa na nchi. Wizara ya Fedha wanaanza kuikomba nchi kweupeee! Hisia yangu hawa ni nyani waliogundua kwamba hatuna tena mlinzi wa fedha ya umma. Rais wetu utajua mwenyewe! Kama nawe una maneno yale ya kusema nchi hii utaiacha kama alivyoiacha Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Magufuli. Aliyesema simtaji.

 
Maza apige 15 hata kama tutaibiwa lakini tuna amani hakuna mauji wala kesi za uhujumu uchumi za kipumbavu, kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake.
Tumewashtukia tumbili, kama hatutawaua kwa bunduki basi kwa sumu.

Mnapigia kelele mkisifu haiba ya mama kumbe mna malengo yenu.

Sent from my INE-LX1r using JamiiForums mobile app
 
Hii ofisi nayo kama iko kisiasa zaidi huwa inamfavor yule aliyemweka madarakani na mara nyingi sio wakweli!
na katika hili hata Professor Assad aliingia mtego huu wakati wa Kikwete hakuzungumza mabaya awamu ya tano akayaona mabaya.
huyu mwingine woga wa kukosa kazi na tamaduni za kujikombakomba zinafanya pia aponde kila kitu.
njaa bado ni tatizo kwa taaluma zetu!
VOTE ya ikulu ni kichaka haikaguliwi mzee, huko ndiyo wanakopigia pesa
 
Kwa wakulima wa mahindi na mpunga, tunaelewa uharibifu wa nyani na tumbili na ndege. Huwa tunaanza kuweka matambala na kichwa cha bandia ili wanyama hawa waamini huyo ni mlinzi. Wanyama polepole huanza kuzoea na kugundua kwamba hayo ni matambala na hakuna kichwa, ni chungu cheusi. Hapo sasa mazao huanza kuliwa.

Tumeanza kuona wizi na ulaji wa hovyo. Tena ndani ya wizara mama yenye kushikilia hazina ya taifa na nchi. Wizara ya Fedha wanaanza kuiokomba nchi kweupeee! Hisia yangu hawa ni nyani waliogundua kwamba hatuna tena mlinzi wa fedha ya umma. Rais wetu utajua mwenyewe! Kama nawe una maneno yale ya kusema nchi hii utaiacha kama alivyoiacha Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Magufuli. Aliyesema simtaji.

View attachment 1800357
Hii typicaly ndiyo yalikuwa maisha kipindi cha utawala wa Kikwete. Maofisini watu walikuwa wanatafuta visingizio vya kulipana posho. Mheshimiwa Samia asipokuwa makini na mkali hali inaweza kuwa mbaya hata zaidi ya kipindi cha Kikwete.
 
Wana haki ya kuishi kama miungu watu
 
Hii typicaly ndiyo yalikuwa maisha kipindi cha utawala wa Kikwete.
Yeye mwenyewe kasafiri kwenda USA kupasua tezi dume imagine matibabu ambayo angepata Nairobi kama aliona shida kuoneka nyumbani kwake
 
Back
Top Bottom