Je Zitto Amepoteza Uhalali wa kuwa Kiongozi?

Je Zitto Amepoteza Uhalali wa kuwa Kiongozi?

Unataka kubadili historia au wewe ndiye unataka Zitto akaongelee chumbani kwa Chadema? Zitto kaflip flop, kajichanganya, karopoka na zaidi ya yote, kaonyesha mapenzi yake yako mbali na chama chake.


Yaani unataka watu wasubiri kagonjwa haka ka mafua kageuke kuwa Kansa kama katika CCM ndio tuanze kuwa wazi na kumuona mganga atutibie?

Guys, CHADEMA has to be more than just another CCM in the making....We need credable alternative not just available alternative....Open self criticisms kama hizi ambazo inawezekana zimekuja kwa wakati na style isiyo muafaka ni muhimu kwa ujenzi wa upinzani makini utaaokuwa na tija kwa watanzania wote....

omarilyas
 
Yaani unataka watu wasubiri kagonjwa haka ka mafua kageuke kuwa Kansa kama katika CCM ndio tuanze kuwa wazi na kumuona mganga atutibie?

Guys, CHADEMA has to be more than just another CCM in the making....We need credable alternative not just available alternative....Open self criticisms kama hizi ambazo inawezekana zimekuja kwa wakati na style isiyo muafaka ni muhimu kwa ujenzi wa upinzani makini utaaokuwa na tija kwa watanzania wote....

omarilyas

Omar,

You well know how this flu got started. It doesnt take a yard to find a virus
 
Huyu mama ni mweupe sana, lazima mchaga tena mkibosho!

yeleuuuwiii
 
Zitto alitangaza kugombea na kisha akachomoa (sioni connection yoyote ya kukemea maovu ya Chadema).

What if kugombea nafasi ya uenyekiti ilikuwa hatua ya kwanza ambayo akalazimika kurudi nyuma kutokana na "busara za wazee" na kulazimika kuchukua hatua ya pili kwa style tofauti ili kushughulikia kitu hicho hicho

Kabla ya hapo, Zitto alifanya yafuatayo-

1. Alijiunga na kamati ya madeni ya Kikwete (akipingana na wenzake)
2. Aliungana na mafisadi kwenye issue ya Dowans
3. Hakujulikana msimamo wake kwenye bajeti ya serikali iliyopita.
Kupingana na wenzake kunahusiana gani na kukosa msimamo. Ama una maananisha kuwa kutokubali kuburuzwa kimtizamo ndio kukosa msimamo?

Kuhus dowans, tatizo lilikuwa the so called kuungana na mafisadi ama kupingana na MASIHA feki wenu ambao kutokana na ugoigoi wa kuuliza mswali maswali magumu mmeamua kuwakumbatia huku wakipiga bao la kisigino katika nia yao ya kulinda uhalali wa mfumo fisadi....



Hayo mengine ya uchaga na chadema nadhani unarudi kule kule kwenye ukabila na chuki zisizofaa ndani ya nchi na hivyo kukufanya wewe kuwa mtu mwenye chuki mbaya sana za kikabila na unayefaa kuogopwa kama ukoma.
Kujenga alliances zinazothamini ukabila na udini kunafaa, kuhoji na kukosoa matendo kama hayo ndio hakufai? Ukabila, Udini, ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kijinsia, ufisadi yote haya ni matatizo yaliyopo katika jamii yetu na sasa yanaota mizizi....ni lazima yaongelewe kwa uwazi ili kuyashughulikia ipaswavyo....

Kama CUF wanavyokosolewa kwa udini, CCM kwa ufisadi na Chadema kwa ukabila....mnachopaswa ni kuyashughulikia kwa kuepuka kufanya mambo ama maamuzi yanayotoa taswira hasi hizo na sio kuwajengea uadui wale wanaohoji ama kukosoa.....

omarilyas
 
Hapa umenena mkuu.Na hilo jina la first lady nani amempa?

na naona huko CHADEMA chama kimekuwa family business sasa not ve sonn utasikia mamake zitto ni mwenyekiti wa wanawake chadema!

Chadema ni family party ? Haya CCM hakuna ama umeamua kusema tu ?Hebu rudi tena kwenye CCM tuanze na JK , Makamba , na wengine wengi ambao wako CCM na ndugu zao wana madaraka .Kuna ubaya Mama kumsema mwanae ? Kuna Ubaya Mama na mwanae kuwa Chama kimoja ?Kua ubaya familia nzima kuimba nyimbo za CCM leo wakiimba Chadema mnasema chama cha familia ?

Shame shame na spinning za kitoto
 
Ha ha ha ha,

Labda mama yake Zitto naye ni mchaga maana sasa hivi wachaga wamejaa kila sehemu hapo Tanzania hadi inakuwa kazi kuwatambua.


Haya matusi nadhani kwenye forum kama hii we above this nonsense za uchaga na ukabila
 
Huyu mama ni mweupe sana, lazima mchaga tena mkibosho!

yeleuuuwiii

yaani hapa imebidi nishikilie mbavu tu maana haya mambo muda mwingine yanauma hadi yanatisha.

Hiyo yeleuuuwiii imenimaliza kabisa hadi nikakumbuka miaka ile ...... kibosho
 
Namba nitamke wazi kuwa huu sasa ni upupu na majaribio ya wazi ya kumchafua Mh Zitto Kabwe.....kwanza nataka kuweka wazi kuwa si lazima kila kinachotokea kwenye vikao ni lazima viwekwe hewani kwa wananchi,pili mleta habari ni mshabiki wa kundi mojawapo na ndio maana kaleta sehemu tu ya hotuba ya Slaa,kama unataka kotoa hoja ni lazima kusiwepo na ushabiki wowote na badala yake ueleze kilichojiri....unaeleza majibu ya slaa kanakwamba wewe ni tarishi wake.....naomba thread hii ifutwe...tumtukane Zitto lakini tumuheshimu yeye na familia yake.
 
What if kugombea nafasi ya uenyekiti ilikuwa hatua ya kwanza ambayo akalazimika kurudi nyuma kutokana na "busara za wazee" na kulazimika kuchukua hatua ya pili kwa style tofauti ili kushughulikia kitu hicho hicho

Sidhani kama hiki ndicho alichofanya alipoanza kupondea wamachame na wachaga.

Kupingana na wenzake kunahusiana gani na kukosa msimamo. Ama una maananisha kuwa kutokubali kuburuzwa kimtizamo ndio kukosa msimamo?

Kukosa msimamo ndiko Zitto ameonesha hapa kwenye swala la kugombea na huku ni zaidi ya kupingana na wenzake.

Kuhus dowans, tatizo lilikuwa the so called kuungana na mafisadi ama kupingana na MASIHA feki wenu ambao kutokana na ugoigoi wa kuuliza mswali maswali magumu mmeamua kuwakumbatia huku wakipiga bao la kisigino katika nia yao ya kulinda uhalali wa mfumo fisadi....

Zitto alijiunga na mafisadi kutaka kununua mitambo ya Dowans. Hapa sio tu alikuwa anauza nchi, alijionyesha jinsi asivyokuwa na principles.

Kujenga alliances zinazothamini ukabila na udini kunafaa, kuhoji na kukosoa matendo kama hayo ndio hakufai? Ukabila, Udini, ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kijinsia, ufisadi yote haya ni matatizo yaliyopo katika jamii yetu na sasa yanaota mizizi....ni lazima yaongelewe kwa uwazi ili kuyashughulikia ipaswavyo....

Kama CUF wanavyokosolewa kwa udini, CCM kwa ufisadi na Chadema kwa ukabila....mnachopaswa ni kuyashughulikia kwa kuepuka kufanya mambo ama maamuzi yanayotoa taswira hasi hizo na sio kuwajengea uadui wale wanaohoji ama kukosoa.....

omarilyas

Omar ... huwezi kulinganisha ufisadi wa ccm (IPTL, buzwagi, EPA, richmond, meremeta, tangold, ndege, rada, wizi wa pesa za kodi) na mengine mengi na madai ya kijinga kuwa CUF ni chama cha kidini au chadema ni chama cha kikabila.

Hivi ni vitu viwili tofauti - kimoja ni upuuzi (kudai kuwa CUF au CHADEMA ni vyama vya kidini na kikabila) na kingine ni fact (ccm ni chama cha kifisadi).
 
Omar,

Nilikuuliza jana kama unamsemea Zitto au unasema kwa niaba yako. Zitto alidai kuwa anaandamwa na wamachame (na wachaga?) lakini baadaye akaonekana kuback down.

Naona wewe leo umekuja full ... kudai kuwa Zitto anaandamwa na watu wa dini na kabila tofauti na Zitto.

Unaamini kuwa wanaompinga Zitto hapa na kwingine wanafanya kwa vile wao sio kabila au dini moja na Zitto! are you serious?

Hivi wewe kichwa yako mbona iko shallow hivyo halafu unadhani unaweza kazi ya spining?

Huoni kuwa hapo nilikuwa namchokoza huyo alioleta masuala ya kuwa ni magazeti ya serkali na chama ndio yanamuongelea Zitto tofauti na mnavyotaka aache kuulizwa maswali mepesi kama hayo ya udini na ukabila...

samahani kama technique yangu inakukwaza....

kwa kuwa namjua che naamini anapata ujumbe ninaomtumia vizuri zaidi yako

omarilyas
 
Hivi wewe kichwa yako mbona iko shallow hivyo halafu unadhani unaweza kazi ya spining?

Yamefika hapa tena?

Huoni kuwa hapo nilikuwa namchokoza huyo alioleta masuala ya kuwa ni magazeti ya serkali na chama ndio yanamuongelea Zitto tofauti na mnavyotaka aache kuulizwa maswali mepesi kama hayo ya udini na ukabila...

Hii haikupi sababu ya wewe kujaribu kueneza chuki za kikabila na kidini hapa hata kama unayepingana naye kafanya hivyo.

samahani kama technique yangu inakukwaza....

kwa kuwa namjua che naamini anapata ujumbe ninaomtumia vizuri zaidi yako

omarilyas

Sidhani kama ulikuwa unamtumia ujumbe Che peke yake maana la sivyo ungemtumia ujumbe privately.

Ninaelewa kuwa hii issue imewachanganya sana maana mambo ambayo Zitto kayasema na kuyafanya ndani ya siku chache zilizopita na ambayo wewe rafiki yake mkubwa umeendelea kuyafanya hapa yanaonyesha kuwa hii issue imechukua toll kubwa kwako.

Katika hili, nitakupa breki kidogo upumue maana kazi uliyonayo ya kusafisha kambi yenu na hili doa la ukabila na udini mliloanza ni kubwa kweli.
 
Hapa nashuhudi uvivu wa hali ya juu wa kufikili,kama maneno haya yote yanasemwa kwa kuwa tu Zito ametaka kugombea basi nini na safari ya demokrasia ni ndefu sana..............tanzania mambo mengi yanajengewa uhalali na magazeti,mbaya kwa rafiki yangu Zitto hakujua kuwa leading gazeti lenye circulation kubwa ni Nipashe ambapo Mengi tayari alikuwa anampinga,acha mbali kibaraka wa Mbowe Jesse Kwayu ambaye ni mchaga na editor wa gazeti ambaye ndie aliandika makala ya Gazeti la Mwanahalisi....la pili ni Mwananchi ambaye Msaki mchaga ndie news editor pale nae akimpinga na la tatu ndio tanzania daima ambalo ndio la mbowe mwenyewe.................Zitto hiii ndio dunia.
 
Namba nitamke wazi kuwa huu sasa ni upupu na majaribio ya wazi ya kumchafua Mh Zitto Kabwe.....kwanza nataka kuweka wazi kuwa si lazima kila kinachotokea kwenye vikao ni lazima viwekwe hewani kwa wananchi,pili mleta habari ni mshabiki wa kundi mojawapo na ndio maana kaleta sehemu tu ya hotuba ya Slaa,kama unataka kotoa hoja ni lazima kusiwepo na ushabiki wowote na badala yake ueleze kilichojiri....unaeleza majibu ya slaa kanakwamba wewe ni tarishi wake.....naomba thread hii ifutwe...tumtukane Zitto lakini tumuheshimu yeye na familia yake.


Nakubaliana nawe thread hii ifutwe
watu wanageuza JF mahala pa kuleta kila upuuzi .Mbowe ukisha chukua uenyekiti uache masihala lazima upanguwe Chadema makao makuu bila ya aibu .Ondoa vijiwe kwenye Chama ndiyo watoto wanakimbilia huku na chuki zao .
 
Hapa nashuhudi uvivu wa hali ya juu wa kufikili,kama maneno haya yote yanasemwa kwa kuwa tu Zito ametaka kugombea basi nini na safari ya demokrasia ni ndefu sana..............tanzania mambo mengi yanajengewa uhalali na magazeti,mbaya kwa rafiki yangu Zitto hakujua kuwa leading gazeti lenye circulation kubwa ni Nipashe ambapo Mengi tayari alikuwa anampinga,acha mbali kibaraka wa Mbowe Jesse Kwayu ambaye ni mchaga na editor wa gazeti ambaye ndie aliandika makala ya Gazeti la Mwanahalisi....la pili ni Mwananchi ambaye Msaki mchaga ndie news editor pale nae akimpinga na la tatu ndio tanzania daima ambalo ndio la mbowe mwenyewe.................Zitto hiii ndio dunia.

Akimaliza mmoja, anafuata mwingine mwenye chuki za ajabu dhidi ya wachaga. Hizi chuki zenu zipelekeni huko chaga-haterslandville na wala sio hapa JF.

SteveD yuko wapi anisaidie kuweka ile toilet paper kwenye hiyo post hapo juu.
 
Zitto alijiunga na mafisadi kutaka kununua mitambo ya Dowans. Hapa sio tu alikuwa anauza nchi, alijionyesha jinsi asivyokuwa na principles.

Which principles? Kuacha kuungana na MASIHA feki katika kamchezo kao ka-kupersonalize ufisadi kana kwamba hilo sio tatizo la kimfumo ambalo wao ni wahunzi, watetezi na walinzi wake? Umeshau nahau za Pengo?


Omar ... huwezi kulinganisha ufisadi wa ccm (IPTL, buzwagi, EPA, richmond, meremeta, tangold, ndege, rada, wizi wa pesa za kodi) na mengine mengi na madai ya kijinga kuwa CUF ni chama cha kidini au chadema ni chama cha kikabila.
Hivi ni vitu viwili tofauti - kimoja ni upuuzi (kudai kuwa CUF au CHADEMA ni vyama vya kidini na kikabila) na kingine ni fact (ccm ni chama cha kifisadi).

Yanakuwa ya kijinga yanapolengwa kwenu tu. Mkuki kwa guruwe kwa binadamu mchungu enhh

omarilyas
 
Sasa ikiwa serikali yetu haina hisa ndani ya mashirika hayo, hakuna sera wala kifungu cha mtazamo wa chama chake (Chadema) umekubalika na serikali kuu kutumiwa ili kuboresha sekta ya madini. Zitto hakutakiwa kufanya kazi huko kwa sababu ni Kinyume cha katiba ya chama chake.

Mkuu hapa nitatofautiana na wewe. Unataka kusema katiba ya Chadema inapiga marufuku kwa wanachama wake kufanya kazi serikalini? Mbona sikuelewi.

Serikali na chama ni vitu viwili tofauti ingawa chama ndio kinachozaa serikali. Kamati ya JK ilikuwa ni ya serikali sio ya CCM na hivyo Zitto hakufanya kosa lolote kushirikiana na serikali, angefanya kosa endapo angeshirikiana na chama (CCM).

Ikumbukwe kwamba kazi kubwa ya upinzani ni kuweka checks and balance dhidi ya serikali, ushiriki wa Zitto kwenye kamati ile ulikuwa wa haki na ndio maana Chadema hawakuthubutu kumwadhibu kwa kushiriki kwake.
 
Akimaliza mmoja, anafuata mwingine mwenye chuki za ajabu dhidi ya wachaga. Hizi chuki zenu zipelekeni huko chaga-haterslandville na wala sio hapa JF.

SteveD yuko wapi anisaidie kuweka ile toilet paper kwenye hiyo post hapo juu.
Hakuna mwenye chuki na uchaga na wala hakuna anaechukia wachaga lakini hupaswi kuwa nu miwani ya darubini kuona yote hayo.au unataka kunimbia ni kipi cha uongo nilichoandika...nawapenda wachaga na hata mke wangu pia ni mchaga na huwa ananitania kuwa sisi wamakonde tuko primitive lakini bado anakubaliana na mimi kuw kuna kingdom ya wachaga ambayo ni hatari sana kwa mustakhbali wetu
 
Which principles? Kuacha kuungana na MASIHA feki katika kamchezo kao ka-kupersonalize ufisadi kana kwamba hilo sio tatizo la kimfumo ambalo wao ni wahunzi, watetezi na walinzi wake? Umeshau nahau za Pengo?

Principle kwamba,

Huwezi kulala kitanda kimoja na mafisadi na ukategemea kuwa utatoka ukiwa msafi. Kuungana na mafisadi katika issue ya Dowans ilikuwa ni kujivika shuka lao la kifisadi kwa mategemeo kuwa angewabadili.

Matokeo yake Zitto anayajua na natumaini na wewe unayajua. Hakuna namna ambayo Zitto ataikwepa hii issue ya Dowans iwe ni kutokana na kutomfuata "masiha" au "shetwani". Katika hili, Zitto alithibitisha kile ambacho kilikuwa kinasemwa kumhusu kwa muda mrefu kuanzia azime ile momentum ya wapinzani kwenye Buzwagi kwa kuingia kwenye kamati ya madini ya Kikwete - kuwa anakubaliana na mafisadi.

Yanakuwa ya kijinga yanapolengwa kwenu tu. Mkuki kwa guruwe kwa binadamu mchungu enhh

omarilyas

Kwetu na nani? Nilikukumbusha kuwa unachodhania kuhusu mimi kiko very misguided. Itakuchukua muda kunikumbuka ingawa umeshahitimisha kuwa mimi ni mmoja wa hitmen wa kimachame(kichaga) na kikristo ambao wako hapa kummaliza Zitto.

Chukua muda utagundua unapokosea kuhusu mimi.
 
Back
Top Bottom