Je Zitto Amepoteza Uhalali wa kuwa Kiongozi?

Je Zitto Amepoteza Uhalali wa kuwa Kiongozi?

Hakuna mwenye chuki na uchaga na wala hakuna anaechukia wachaga lakini hupaswi kuwa nu miwani ya darubini kuona yote hayo.au unataka kunimbia ni kipi cha uongo nilichoandika...nawapenda wachaga na hata mke wangu pia ni mchaga na huwa ananitania kuwa sisi wamakonde tuko primitive lakini bado anakubaliana na mimi kuw kuna kingdom ya wachaga ambayo ni hatari sana kwa mustakhbali wetu

Wewe umeonyesha chuki kubwa kabisa kwa Kwayu kwa kutaja uchaga wake bila sababu yoyote ile (na wala bila kuulizwa). Wachaga wamekukosea nini?

Na pia, nani kakuuliza (au kataka kujua) kabila lako au la mke wako?
 
Lakini kumbuka kuwa, kamati ya madini ni kitu tofauti. Kabla ya hii kamati ya Zitto, kulikuwa na kamati na tume kibao zimeundwa kuchunguza na kutoa ushauri kuhusu masuala ya madini. Kabla hayo mapendekezo ya kamati na tume zilizopita hayajafanyiwa kazi, kamati nyingine ikiundwa ni upotevu na uharibifu wa muda na pesa za watanzania.

Zitto alilijua hili, aliambiwa na wenzake kuhusu hili lakini bado tu alijiunga na Kikwete kuwapotezea muda na pesa watanzania. Je ile kamati ya Zitto imeleta nini tofauti na kile kilicholetwa kabla?

Je issue ya Buzwagi ambayo ndiyo ilianzisha yote haya ilishughulikiwa? Kuna wakati chama kilicho madarakani.

BTW ... kuita watu kuwa hamnazo hakujengi hoja yako zaidi ya kukuonesha vile ulivyo. Mtu mwenye chuki za ajabu (ohh nimekumbuka, kuwa ulipondea wachaga somewhere hapo juu) za kikabila.

wewe tueleze mabaya aliyofanya Zitto alipokuwa kwenye hiyo kamati badala ya kuja na conspiracy theories ambazo nashindwa kuona vichwa chake. Haya mambo ya kuhesabu kamati na mafanikio yake hayahusiani na mada inayoonyesha kwamba Zitto hana sifa za uongozi.

Tafadhali, tupe kosa au ufisadi (kama upo) alioufanya Zitto akiwa kwenye hiyo kamati.
 
Ikumbukwe kwamba kazi kubwa ya upinzani ni kuweka checks and balance dhidi ya serikali, ushiriki wa Zitto kwenye kamati ile ulikuwa wa haki na ndio maana Chadema hawakuthubutu kumwadhibu kwa kushiriki kwake.

Kutomwadhibu Zitto (at least hadharani) haimaanishi kuwa Chadema walikubaliana na alichofanya Zitto. Zitto aliwauza watanzania na chama chake kwa kuingia kwenye kamati feki iliyoundwa kula pesa za wananchi ili kuzuia uchunguzi halali na unaojitegemea ambao ungefanyika na kulipatia ufumbuzi suala la Buzwagi na migodi mingine.

Zitto analijua hilo na ndio maana yuko kimya kabisa kuhusu Buzwagi ingawa anajua kabisa kuwa hakuna kilichobadilika.
 
wewe tueleze mabaya aliyofanya Zitto alipokuwa kwenye hiyo kamati badala ya kuja na conspiracy theories ambazo nashindwa kuona vichwa chake. Haya mambo ya kuhesabu kamati na mafanikio yake hayahusiani na mada inayoonyesha kwamba Zitto hana sifa za uongozi.

Tafadhali, tupe kosa au ufisadi (kama upo) alioufanya Zitto akiwa kwenye hiyo kamati.

Kwa kuanzia tu, ni kile ambacho Zitto hakufanya (au kamati haikufanya) kuhusiana na mkataba wa Buzwagi. Una jibu katika hilo?
 
Nishawahi kusema kuwa Zitto sasa alikuwa amejaa kiburi sana na pengine kujiona kuwa ni yeye ndio Pekee katika CHADEMA. Kuna watu wengi sana katika CHADEMA kuwa lakini sio Active katika Politics za Tanzania. Lakini Zitto alikuwa ana jaribu hata timing yake ilikuwa Mbovu sana. Nilikasilika sana kuona anasema na kumwaga mambo haya hapa JF. Zitto sasa alishapoteza Dira yake Siku nyingi sana

Unajua kama wangeshindanishwa na Zitto akashindwa ndipo hii hoja ya iming kuwa mbovu ingekuwa na mshiko....lakini kitendo cha kuogopa ushindani kinatoa taswira tofauti....

Na hili la watu wengi sana CHADEMA lakini sio active katika politics ndio tatizo kiasi cha kupelekea kujengeka kwa muono kuwa katika chama kizima MBOWE ndio kimbilio. Sasa kama mngeacha kuwa timid and opportunists kama asemavyo Mbowe ni wazi CHADEMA wangekuwa mbali zaidi ya walipo sasa ambako wanalazimiko kuridhika with the least they can get.....

omarilyas
 
Mgonjwaukimwi,
Mkuu hapa nitatofautiana na wewe. Unataka kusema katiba ya Chadema inapiga marufuku kwa wanachama wake kufanya kazi serikalini? Mbona sikuelewi.
Hapana mkuu wangu kuna tofauti kubwa kati ya wawakilishi wetu (wabunge) na waajiriwa wa serikali kama vile tofauti ya Waziri wa wizara na Mkurugenzi wa wizara.. nikiwa na maana mkurugenzi wa wizara anaweza kutokuwa namwanachama wachama chochote cha siasa na akafanya kazi..lakini hai apply kwa waziri.

Sidhani kama JK anaweza kumchagua mtu toka toka Chadema awe waziri wa wizara fulani na ikakubalika ikiwa JK hakubaliani na sera wala mpango wowote wa chama ktk uendeshaji wa wizara hiyo. Pia haiwezekani mbunge wa Chadema, CUF au chama kingine kwenda kuwa waziri wa serikali ya Kikwete wakati hakubaliani na mrengo, sera za JK.. sijui atakuwa anajaribu kufanya kitu gani kama sii kuwa mtumwa na mgungwa wa utawala uliopo. Ingekuwa rahisi hivyo watu wasingekuwa na vyama vingi (demokrasia) au kuhama vyama ya nini ikiwa tunachohitaji ni vichwa vya watu kutunga Policy..
 
Kujenga alliances zinazothamini ukabila na udini kunafaa, kuhoji na kukosoa matendo kama hayo ndio hakufai? Ukabila, Udini, ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kijinsia, ufisadi yote haya ni matatizo yaliyopo katika jamii yetu na sasa yanaota mizizi....ni lazima yaongelewe kwa uwazi ili kuyashughulikia ipaswavyo....


omarilyas

Maneno mazito haya, naona sasa Chadema inajikaanga kwa jasho lake
 
Unajua kama wangeshindanishwa na Zitto akashindwa ndipo hii hoja ya iming kuwa mbovu ingekuwa na mshiko....lakini kitendo cha kuogopa ushindani kinatoa taswira tofauti....

Na hili la watu wengi sana CHADEMA lakini sio active katika politics ndio tatizo kiasi cha kupelekea kujengeka kwa muono kuwa katika chama kizima MBOWE ndio kimbilio. Sasa kama mngeacha kuwa timid and opportunists kama asemavyo Mbowe ni wazi CHADEMA wangekuwa mbali zaidi ya walipo sasa ambako wanalazimiko kuridhika with the least they can get.....

omarilyas

Ndiyo maana jana nilimshauri Zitto kuwa ajiunge na Swahiba wake (kikwete) kule CCM kwa mafisadi wenzake wa Dowans.
 
Mwafrika wa kike nadhani wewe ni kati ya wale wanawake wanaomburudishaga kaka Mbowe kwenye helcopter ili wapewe ubunge.....

Hili la kuita members wengine wa JF hapa wasiohusika na unachokiongelea na kuwatolea lugha ya upuuzi na utoto kama hii sidhani kama ina nafasi yake hapa JF.

jitahidi kuna nafasi moja ya wazi ya ubunge ya Muhonga ili safu ya wachaga na babab mkwe Mtei itimie

Mkuu, wachaga wataendelea kuwepo tu hapa Tanzania iwe unapenda au hupendi.
 
Mgonjwaukimwi,

Hapana mkuu wangu kuna tofauti kubwa kati ya wawakilishi wetu (wabunge) na waajiriwa wa serikali kama vile tofauti ya Waziri wa wizara na Mkurugenzi wa wizara.. nikiwa na maana mkurugenzi wa wizara anaweza kutokuwa namwanachama wachama chochote cha siasa na akafanya kazi..lakini hai apply kwa waziri.

Sidhani kama JK anaweza kumchagua mtu toka toka Chadema awe waziri wa wizara fulani na ikakubalika ikiwa JK hakubaliani na sera wala mpango wowote wa chama ktk uendeshaji wa wizara hiyo. Pia haiwezekani mbunge wa Chadema, CUF au chama kingine kwenda kuwa waziri wa serikali ya Kikwete wakati hakubaliani na mrengo, sera za JK.. sijui atakuwa anajaribu kufanya kitu gani kama sii kuwa mtumwa na mgungwa wa utawala uliopo. Ingekuwa rahisi hivyo watu wasingekuwa na vyama vingi (demokrasia) au kuhama vyama ya nini ikiwa tunachohitaji ni vichwa vya watu kutunga Policy..

Mkandara,

Namba za JK kumpa Zitto nafasi ya uwaziri zimezidi kupanda hasa baada ya hili saga Zitto alilofanikiwa kulileta Chadema.

Itafikia wakati tu Kikwete alipe fadhila (na huo wakati unakaribia sana).
 
Mkandara,

Namba za JK kumpa Zitto nafasi ya uwaziri zimezidi kupanda hasa baada ya hili saga Zitto alilofanikiwa kulileta Chadema.

Itafikia wakati tu Kikwete alipe fadhila (na huo wakati unakaribia sana).
Hapana JK hana sababu wala haja ya kulipa Fadhila.. Zitto alifungashiwa kanyaboya akalikoroga na kulinywa mwenyewe kwa gharama ya Chadema.. madini yetu bado yanaibiwa, Kina Karamagi ndio imetoka tena basi nasikia Buzwagi barricks tayari wameisha anza ujenzi yaani mwaka wa hasara ni hasara tu..
Kifupi ningependa sana kumskikliza Zitto ni mabadiliko gani ya sera au hata policy za JK imebadilishwa kutokana na kuingia kwake ktk kamati hiyo. Ila sikupata nafasi hiyo kwani toka saga la Dowans mkuu amekuwa adimu hapa Kijiweni.
 
Nah,

Huyo Omar alishadai kuwa si mwanachadema. Nadhani hapa ni outsiders wanajaribu kuikaanga Chadema - na wamechemsha.

Wakati mnalamba mafuta ya Mengi na wengine wanopita kuimba ngonjera za nina imani na Kikwete hamkuona kuwa hao ni outsiders na wala hamkuuliza uswahiba wao?

Hao mnaowaita wachangiaji wenu kiuchumi ambao mnadai kuna umuhimu wa kumuacha Mbowe ili waendelee kukichangia chama chenu mbona hamhoji iweje wawachangine ninyi asilimia kuni na tisini wakizipeleka CCM?

Hivi kati ya Mbowe, Slaa, Mtei na Zitto ni nani mwenye historia ya kuwa CCM?

Achenu kutafuta mchawi kwa jirani wakati wachawi ninyi wenyewe.....

Kubaka na kudumaza demokrasia mfanye wenyewe halafu muanze kusingizia furaha ya CCM. Mlitaka wanune wakati mnajikaanga wenyewe...

omarilyas
 
Wakati mnalamba mafuta ya Mengi na wengine wanopita kuimba ngonjera za nina imani na Kikwete hamkuona kuwa hao ni outsiders na wala hamkuuliza uswahiba wao?

Hapa nitasubiria waliolamba mafuta ya Mengi na kuimba ngonjera za Kikwete wakupe jibu.

Hao mnaowaita wachangiaji wenu kiuchumi ambao mnadai kuna umuhimu wa kumuacha Mbowe ili waendelee kukichangia chama chenu mbona hamhoji iweje wawachangine ninyi asilimia kuni na tisini wakizipeleka CCM?

Haya ni mawazo yako binafsi kwa hiyo nitayachukuliwa kama ni udaku tu.

Hivi kati ya Mbowe, Slaa, Mtei na Zitto ni nani mwenye historia ya kuwa CCM?

Achenu kutafuta mchawi kwa jirani wakati wachawi ninyi wenyewe.....

Kubaka na kudumaza demokrasia mfanye wenyewe halafu muanze kusingizia furaha ya CCM. Mlitaka wanune wakati mnajikaanga wenyewe...

omarilyas

Wote hao walishakuwa CCM ila sasa Zitto yeye anataka kurudi CCM kwa kasi na mbwembe zote.
 
Hapana JK hana sababu wala haja ya kulipa Fadhila.. Zitto alifungashiwa kanyaboya akalikoroga na kulinywa mwenyewe kwa gharama ya Chadema.. madini yetu bado yanaibiwa, Kina Karamagi ndio imetoka tena basi nasikia Buzwagi barricks tayari wameisha anza ujenzi yaani mwaka wa hasara ni hasara tu..
Kifupi ningependa sana kumskikliza Zitto ni mabadiliko gani ya sera au hata policy za JK imebadilishwa kutokana na kuingia kwake ktk kamati hiyo. Ila sikupata nafasi hiyo kwani toka saga la Dowans mkuu amekuwa adimu hapa Kijiweni.

Mkuu Mkandara,

Issue ya Dowans ilikuwa si mchezo kwani ilimmamliza kabisa kijana wetu. Ni muda tu labda atakuja kuelezea ukweli kilichomtokea kwenye kamati hizo za Kikwete alizokuwa anahudhuria.
 
Kifupi ningependa sana kumskikliza Zitto ni mabadiliko gani ya sera au hata policy za JK imebadilishwa kutokana na kuingia kwake ktk kamati hiyo. Ila sikupata nafasi hiyo kwani toka saga la Dowans mkuu amekuwa adimu hapa Kijiweni.

Naungana mkono nawe kuhusu yeye kuelezea mabadiliko yaliyopatikana na nini ulikuwa mchango wake huko kama alivyofanya kule jimboni ambako tayari hao wanaodai ni maswahiba wake walikuwa kazini wakimwaga sumu...

Kuhusu saga la dowans kaka unategemea nini kama ukija unakutana na hoja kiduchu majungu bwelele. Na ukijibu kama wanavyopaswa kujibiwa unajikuta umefungwa minyororo ya haki ya kusema kama ilivyo....Yaani humu wamejaa watu wanaotaka useme kama watakavyo wao na sio vinginevyo. Watanzania tunapenda viongozi wanafiki wa kututongotongoza kama hao tulio nao sasa na wakitokea wenye style tofauti basi tunachokijua ni majungu, mipasho na visasi..


omarilyas

omarilyas

omarilyas
 
.....Haya...hebu tupate Tangazo la biashara kidogo.....
[ame]http://www.youtube.com/watch?v=dBV6sh4cr2c[/ame]
 
Naungana mkono nawe kuhusu yeye kuelezea mabadiliko yaliyopatikana na nini ulikuwa mchango wake huko kama alivyofanya kule jimboni ambako tayari hao wanaodai ni maswahiba wake walikuwa kazini wakimwaga sumu...

Kuhusu saga la dowans kaka unategemea nini kama ukija unakutana na hoja kiduchu majungu bwelele. Na ukijibu kama wanavyopaswa kujibiwa unajikuta umefungwa minyororo ya haki ya kusema kama ilivyo....Yaani humu wamejaa watu wanaotaka useme kama watakavyo wao na sio vinginevyo. Watanzania tunapenda viongozi wanafiki wa kututongotongoza kama hao tulio nao sasa na wakitokea wenye style tofauti basi tunachokijua ni majungu, mipasho na visasi..


omarilyas

omarilyas

omarilyas

Omar,

Acha jaziba na kashfa kwa wanachama wa jamvi hili. Kuna watu makini na wengi wamekuwa wanampa Zitto nafasi ili aeleze kilichomtokea kwenye kamati hizo au kwenye issue ya Dowans.

Huwezi kulazimisha watu kukubaliana nawe. Ukiwa na mpango wa kuwa mwanasiasa, inabidi ujenge ngozi yako ili iwe ngumu kiasi cha kuhimili hoja za watu (wakiwemo wana JF).
 
Mkuu kuhusu Zitto kuingia kamati ya madini kuna kasoro moja kubwa sana. Zitto anawakilisha sera za Chadema ambazo zinahitaji nchi yetu kuwa na hisa katika amshirika ya madini. Sasa ikiwa serikali yetu haina hisa ndani ya mashirika hayo, hakuna sera wala kifungu cha mtazamo wa chama chake (Chadema) umekubalika na serikali kuu kutumiwa ili kuboresha sekta ya madini. Zitto hakutakiwa kufanya kazi huko kwa sababu ni Kinyume cha katiba ya chama chake.

Kaka nakushauri upitie ripoti yao na uone kama hilo halikushauriwa ama la. Na jee una taarifa yoyote ya mabadiliko yanayoendelea katika STAMICO? Na si kweli kuwa serikali haina hisa atika makampuni yote ya madini. Huo ndio ilikuwa mwelekeo hapo mwanzo kabala ya kamati ya Bomani lakini sasa wameanza kurudi katika masuala ya umiliki wa hisa na hata NDC inajirekebisha ili kuendeleza mfumo uo kama ilivyo katika mradi wa Mchuchuma.....


Siku zote wabunge wanashirikiana na serikali kuu ikiwa tu serikali kuu itakubali kubadilisha baadhi na sera zake na kufuata mkondo wa kati kaisi kwamba hata Wapinzani wanakuwa na mchango wa sera zao.. Lakini sii mtu kuingia kamati ambayo malengo yake ni kinyume kabisa chga mtazamo wa chama chako..
Una maana maelngo ya kisiasa ama malengo yaliyokuwemo katika TORS za utendaji wa kamati hizo? Jaribu kupitia TORs za kamati ya bomani halafu ndio ufikie conclusion kama ilikuwa makosa kuingia huko? Hivi sio CHADEMA hao hao waliokuwa wakidai kuwa Tundu Lissu ndio aingie katika kamati hiyo. mmesahau maneno ya Slaa na Chacha Wangwe? Ama huo ulkuwa msimamo wao binafsi na sio wa chama chao?

Anyway haya yalikwisha pita.. Zitto alichemsha, akachemsha na anaendelea kuchemsha kutokana na tatizo kubwa na siasa nchini. Yaani vyama vyote vya siasa havina mrengo, Zitto ni Conservative na anahusudu mrengo huo wakati Bongo kila mtu ana dini yake lakini unaambiwa nchi haina dini..hivyo hivyo principal hiyo ipo ktk Mrengo..
Si kweli mkandara. Inawezekana vyama hivi vinashindwa kutengeneza na kuzisimamia sera zinazoendana na mirengo yao lakini wanayo. CUF wao ni waliberali ingawa ni mabingwa wa siasa za chuki na kukosa uvumilivu. Chadema walikuwa mabwanyeye na sasa wamepunguza makali na kuwa mabepari ingawa ukiangalia sera na misimamo na kauli mbiu zao zimejaa fikira za kijamaa. CCM wao ni wajamaa ingawa sera zao ni za kibepari.


Zitto hajawahi kuwa conservative. nimemjua Zitto kama mjamaa ingawa kuwepo kwake CHADEMA kumemfanya aanze ku-accomodate sera za kibepari. Na ni wao ndio waliokuwa wakipush CHADEMA kuelekea kushoto lakini mwisho wa siku 'busara za wazee" zikawalazimu wakubali kushindwa kwa kusogea kutoka kwenye ubwanyenye hadi ubepari. No wonder unawaona kina Kitila, Baregu na hata Mnyika wapo humo ilhali hawana asili ya ubepari wala ubwanyenye. Inawzekana wanaamini ku-camouflage kwa sasa hadi hapo baadae "wakati takaporuhusu"

Na tunapokuja katika mantiki ya Conservatism, mtizamo wangu ni kuwa ubepari wala ubwanyenye hauwezi kuwa conservatism kwa mantiki ya historia na fundamentals za Utanzania....Kwetu hapa ma-conservatives ni wale wanaokataa kukubali kushindwa na kufakamia ubepari. Consevatism kwa Tanzania imejikita katika misingi ya ujamaa na kujitegema kwani hiyo ndiyo iliyounda nchi na jamii ya Tanzania...

omarilyas
 
Back
Top Bottom