Jebra, Mtobesya na Wanasheria wengine, fungueni kesi dhidi ya Mkataba wa DP World

Jebra, Mtobesya na Wanasheria wengine, fungueni kesi dhidi ya Mkataba wa DP World

Huihui2

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
7,021
Reaction score
11,475
Ni wazi Serikali ya Samia haina mpango wa kusikiliza maoni ya wananchi zaidi ya kufanya spinning na wasanii na wanasiasa.

Kabla hatujaingia barabarani kama wananchi wa Sri Lanka, nashauri tufungue kesi ya kikatiba dhidi ya huo mkataba.

Kuna wanasheria manguli kama Mtobesya, Jebra Kambole, Halima Mdee, Mwabukusi, Tundu Lissu etc. Fungueni kesi ya kupinga huo mkataba wa DP WORLD sisi wananchi TUTAWACHANGIA FEDHA
 
Huo wanaoita mkataba uishie kuwa MoU au makubaliano ambayo na yenyewe ni kuwasaidia tu wasizidi kuumbuka, hakuna mkataba hapo.
 
Tuna wafanyakazi hewa wengi tu aisee.
 
Ni wazi Serikali ya Samia haina mpango wa kusikiliza maoni ya wananchi zaidi ya kufanya spinning na wasanii na wanasiasa.

Kabla hatujaingia barabarani kama wananchi wa Sri Lanka, nashauri tufungue kesi ya kikatiba dhidi ya huo mkataba.

Kuna wanasheria manguli kama Mtobesya, Jebra Kambole, Halima Mdee, Mwabukusi, Tundu Lissu etc. Fungueni kesi ya kupinga huo mkataba wa DP WORLD sisi wananchi TUTAWACHANGIA FEDHA
Ni vigumu kwani akina Magufuli na Samia walishajiondoa kutoka ile mahakama ya Africa pale Arusha ili kukwepa kesi kama hizi.
 
Waache familia zao wawe wanashinda mahakamani huku wewe unafanya tu mapenzi na mkeo? mnatakiwa kuchangia
 
nashauri tufungue kesi ya kikatiba dhidi ya huo mkataba.

Na pia wananchi wawe na utashi wa juu wa kisiasa ( political will) ya kulichukua jambo hili kuwa ni lao na kuingia katika maandamano ya kuchagiza serikali

Hatuwezi kutegemea watu wachache kina Freeman Mbowe Mtobesya, Jebra Kambole, Halima Mdee, Mwabukusi, Tundu Lissu huku sisi tunabaki nyuma ya senyenge zenye usalama wa uwoga huku tukiongopa kuzivuka na kuwa kundi kubwa nyuma ya hao uliowataja ambao wamejitoa na kuobesha njia.
 
Mbeya, Tanzania

Wakili Mwabukusi - Ni sawa na nchi kuvamiwa na kukaliwa



Haki za watanganyika, historia, mali zilindwe na vivyo hivyo kwa Zanzibar

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haliwezi kugawa ardhi ya Tanganyika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mlinzi tu wa ardhi na siyo mmiliki wa ardhi ya Tanganyika

Bunge haliwezi kutoa masaa 24 waTanganyika kujadili pande la ardhi ya Tanganyika na hata lile tangazo la Bunge kuita wananchi na wadau watoe maoni ni utani mtupu ... na kukebehi waTanganyika

Endelea kusikiliza kitu hiki sensitive kikichambuliwa kwa kina makosa yake makubwa yasiyokubalika hata haufahi kutambulika kutokana na nia pia kusudio la mkataba huu yaani letter of intent ... ambao nadhani haujapita ktk interministerial technical Committee kutoa ushauri, hivyo document hii haikupita kwa washauri wabobezi waliopo serikalini ...

A letter of intent is a document outlining the understanding between two or more parties which they intend to formalize in a legally binding agreement. The concept is similar to a heads of agreement, term sheet or memorandum of understanding

Waandishi wa habari wamuenzi mwandishi Stan Katabalo ambaye aliona mambo haya miaka 30 iliyopita na kutaandika kwa kina kama habari za kiuchunguzi tofauti na waandishi wa habari wa kizazi cha sasa ambao hata kuhoji wabobezi wa sheria wanashindwa anauliza wakili msomi Boniface Mwabukusi

Wakili anaendelea hili la poor negotiation katika mkataba huu hata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa digrii ya sheria chuo kikuu hawezi kukubali kuuridhia na kuusaini ...

Tujiulize ndugu zetu wa Zanzibar hawatamani mamilioni ya dollar ya DP World, kwanini mkataba hauku husisha Zanzibar au kwa vile rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hana nguvu za kuwa mwangalizi wa ardhi / pande la ardhi Zanzibar kutokana na sheria pia katiba ya Zanzibar haimpi mamlaka rais wa Jamhuri ya Muungano kujinyakulia pande la ardhi Zanzibar lakini kwa upande wa Tanganyika rais wa Jamhuri ya Muungano na bunge la Muungano wanahisi wana mamlaka hayo kumega ardhi ya Tanganyika ..

Jambo ambalo wananchi wanatakiwa kufahamu ni kuwa Dubai imepewa kuwa nchi ndani ya Tanganyika huku heshima sovereignty ya Tanganyika imenajisiwa pia sheria inaipendelea Dubai wakati sheria haiwezi kutungwa

Idi Amini alituvamia kwa bunduki, mizinga na vifaru wakati Dubai imetuvamia kwa mkataba lakini katika haya yote inabaki kuwa nchi imevamiwa ..

Ushauri ni kuwa serikali iandae white paper mpya majadiliano mapya kuhusu jambo hili kisha kupelekwa Bungeni na mkataba huu wa DP World ukataliwe, uondolewe na kutupiliwa mbali ili usukwe upya..

Wakili Boniface Mwabukusi anasema bado ana mashaka kama walioshiriki katika mkataba huu pengine walikuwa na uwezo mdogo wa kufikiri na siyo hongo wala nia mbaya hivyo serikali ifanye jambo sahihi kuukataa mkataba huu baada ya wananchi na wadau kuonesha mapungufu yake makubwa ya kutisha na Mali za taifa kukabidhiwa bure kwa Dubai ...
 
Back
Top Bottom