Jemedari: Camara na Diarra waondoke Tanzania

Jemedari: Camara na Diarra waondoke Tanzania

Shida ni kuwa,wachezaji wetu hawajitumi. hili la kuwa na wachezaji wengi wa kigeni limekuja hivi karibuni,na tumeona faida zake,1.imeongeza thamani ya league yetu 2. wachezaji wazawa wameanza kujituma ie fei,mzize,baka,kapombe,nk 3. zamani sisi mashindano ya kimataifa tulikuwa wasindikizaji,lakn sasa tunatisha. 4. hata ktk team ya taifa kuna mafanikio kutokana na ongezeko la wachezaji wa kigeni,kwa sababu hawa wazawa kupata namba mpaka apambane hasa akipambana ktk klabu yake sisi huku tff tunamchukua kwa ajiri ya taifa. 5. kuwepo kwa wachezaji wa kigeni wengi,kumesababisha burudani kwa wapenda soka nchini.

NI HAYO TU by HOLOHOLO a man from TABORA..
 
Kila jambo unalofanya wakati fulani huwa na faida au hasara. Kuongezeka kwa idadi ya wachezaji wa kigeni kumesaidia kuongeza ushindani baina ya vilabu, na pia ubora wa baadhi ya vilabu kwenye mashindano ya Kimataifa umeongezeka maradufu!

Ila ukija kwenye timu ya Taifa (ambayo haijawahi kuwa na maajabu yoyote yale hata pale idadi ya wachezaji wa nje ilipokuwa ndogo!), hali imeendelea kubakia palepale.

Nini cha kufanya!!! Mimi nashauri TFF na serikali watengeneze mpango mkakati wa kupeleka nje vijana wenye vipaji vikubwa vya soka ili kuwajengea uwezo wa kupata nafasi ya kusajiliwa na vilabu vikubwa duniani.

Lakini pia serikali ifikie wakati sasa iruhusu uraia pacha, ili wachezaji wenye asili ya nchi yetu waliopo kwenye baadhi ya nchi zilizoendelea kisoka, wapatate nafasi ya kuja kuichezea timu yetu ya Taifa huku wakibakia na uraia wa nchi zao.

Al in all, huyo Jemedari Said aache kumtafuta mchawi, huku ukweli ukijulikana ya kwamba sisi Wabongo mpira siyo kipaji! Sisi tunaweza kufanya ngono, kupiga majungu, umbea, uchawa, rushwa, wizi, ufisadi, uchawi, nk.
 
Huyo Jemedari nae ameflop.
Kwani wakina Dickson Job/Bacca etc.. nani kawahi kuwaweka benchi kwenye nafasi zao? Wapandishe viwango vyao wenyewe tena mkiwatoa wakina Camara ndo tutarudi kwenye ulimbombo na ulindi mana hakutakua na ushindani wowote yani ndo wata relax haswaa! Ikibidi waongezwe wawe 15! Hao Kilimanjaro wao wenyewe wamejikaanga wakina Idi Nado wanacheza kama Bonanza mara 100 Crispin Ngushi
 
Kila jambo unalofanya wakati fulani huwa na faida au hasara. Kuongezeka kwa idadi ya wachezaji wa kigeni kumesaidia kuongeza ushindani baina ya vilabu, na pia ubora wa baadhi ya vilabu kwenye mashindano ya Kimataifa umeongezeka maradufu!

Ila ukija kwenye timu ya Taifa (ambayo haijawahi kuwa na maajabu yoyote yale hata pale idadi ya wachezaji wa nje ilipokuwa ndogo!), hali imeendelea kubakia palepale.

Nini cha kufanya!!! Mimi nashauri TFF na serikali watengeneze mpango mkakati wa kupeleka nje vijana wenye vipaji vikubwa vya soka ili kuwajengea uwezo wa kupata nafasi ya kusajiliwa na vilabu vikubwa duniani.

Lakini pia serikali ifikie wakati sasa iruhusu uraia pacha, ili wachezaji wenye asili ya nchi yetu waliopo kwenye baadhi ya nchi zilizoendelea kisoka, wapatate nafasi ya kuja kuichezea timu yetu ya Taifa huku wakibakia na uraia wa nchi zao.

Al in all, huyo Jemedari Said aache kumtafuta mchawi, huku ukweli ukijulikana ya kwamba sisi Wabongo mpira siyo kipaji! Sisi tunaweza kufanya ngono, kupiga majungu, umbea, uchawa, rushwa, wizi, ufisadi, uchawi, nk.
Fikiria kama Akina Pacome wakina Ahoua wakipewa uraia pacha mama makwao wamejaa mnatengeneza first eleven kabisa ya ivory coast tiwe kama France
 
Hii ni kwa mtu mpumbavu tu.
Kwani nchi hii kuna timu ngapi hazina wachezaji wa nje?
Kama hao wachezaji wazuri wapo mbona hawachezi prisons au jkt?Je ni lazima wacheze Simba na Yanga?
Nakubaliana na wewe ndugu Cashman. Pointi yako ni ya msingi sana kuizingatia. Vilabu vya soka nchii vipo vya kutosha kuanzia ligi kuu hadi ligi za mchangani. Ikiwa wenye vipaji wapo, wataonekana tu huko. Si lazima wacheze au waanzie Simba na Yanga.
 
Hakuna kitu. Hiyo ilishawahi kujaribiwa bado ikashindwa. Jiulize kuna Kenya,Uganda, Rwanda n.k hawana wachezaji wengi wa kigeni,lakini vipi mataifa yao yamefika wapi?. Tena nasisitiza bora hivi Tanzania tuna wachezaji wengi wa kigeni wameleta mabadiriko makubwa hata kwa Taifa stars. Unaionaje Taifa stars ya sasa?. Imechangamka. Hivi sasa imeanza kuwa kawaida kufuzu mataifa ya Africa
 
Yale yale ili tukuze Shirika la ndege Tanzania basi tuwafungia Fastjet.

Mbona hakuna mgeni anayechukua namba ya Mohammed Hussein? Namba inapambaniwa.
 
Itawapa nafasi? Kwa nini unataka wapewe nafasi kama zawadi? Si wanatakiwa wazipambanie. Mbona Kagoma anamuweka bench Mavambo. Mbona Zimbwe anamuweka bench Nouma?
Mbona Mzize yupo pale na sio Baleke?
 
Huyo jemedari aache umalaya wake, mbona tulipokuwa na wachezaji wachache wa kigeni taifa Star haikufanya vizuri, angalau sasa hivi wanajitahidi pamoja na kuwa idadi ya wachezaji wa kigeni imeongezeka.

Nifah mshauri huyo mchambuzi mwenzako.
 
Haya machezaji ya Kibongo yanayoendekeza uchawi (kurogana) ni ya kuyatetea namna hii? Hawa akina AISHI MANULA na KIBWANA SHOMARI na wengine wanaopiga misumari wenzao ili wapate namba pasipo kuweka jitihada kwenye pitch ni wa kuwatetea?

Unapambania Wachezaji wazembe dizaini ya IBRAHIM AJIB? Acha waendelee kufundishwa kujituma na wageni.
 
Wachambuzi pia wamekua wengi wapunguzwe,wanatuchanganya tu,anapongeza leo baada ya muda anaponda alichowahi kupongeza,wengi wa wachambuzi walipongeza kuongezwa kwa wachezaji wa nje wakisema wamekuza ligi yetu,mara ligi imechangamka,mara ligi inafatiliwa zaidi Afrika,ligi namba 6 kwa ubora...
Angekuja na alternatives zaidi nn kifanyike ili kuwa na timu Bora ya wazawa..
 
Akili za kifukara hizi! Baada ya kiwahimiza wapambane kuinua viwango vya either view Sawa na wageni au zaidi yeye anatafuta huruma...uchawi sio lazima Ubebe matunguli! By the way furaha ya wapenda soka nchini iko Simba na Yanga na sio Taifa stars
 
"Naendelea kusisitiza sitaki makipa wa nje na wachezaji wa nje wapunguzwe kutoka 12 hadi wabakie 5. Kilichoitokea Kilimanjaro Stars kule Zanzibar ndio uhalisia wa soka letu".

JEMEDARI SAID, Mchambuzi CROWN FM

My intake:

Mbona ukiwaza nje ya box kama Kuna ukweli mkubwa

1. Itasaidia kuwapa nafasi wachezaji wa ndani ( scouts watazunguka kuanzia mtaa,Kijiji, kata,tarafa kusaka vipaji halisi

2. Kujengwa timu ya taifa ( kutakuwa na option kibao ya wachezaji kuitwa timu ya taifa kwenye Kila nafasi uwanjani )

3. Itapunguza upigaji kwenye usajili wa wachezaji kwa hivi vilabu vyetu pendwa, mpaka mchezaji asajiliwe ni lazima awe mchezaji kweli na sio wa kuokota au wa mkopo

4. Academy zitaongezeka maana soko la soka kwa wachezaji wazawa litaongezeka
Nk. Nk.

Hayo ni maoni yangu, Nini maoni Yako??

Karibuni
Naungana na wewe, wapunguzwe wageni ili vipaji vya ndani viinuke.
 
Back
Top Bottom