Jenga Greenhouse kwa gharama nafuu

Jenga Greenhouse kwa gharama nafuu

Dawasco bili yake sio mchezo, na vile ulisema angalau kwa siku zisipungue lita 200 (Ndoo kubwa 10).

Labda option ya kuvuna maji ya mvua, ambayo sasa wasiwasi wangu hii sio ya mwaka mzima kutokana na majira ya mvua, hivyo hata return itakua ndogo kwa kutolima mwaka mzima!!

Tunajadili tu, but otherwise nikishasafisha shamba lazima nikuone!!

Ni kweli bili ya dawasco itakugharimu lakini maji ya aina yoyote ile hayapatikani bure. Kisima kinahitaji pump hivyo kuhitaji umeme either wa Tanesco, Solar au Generator, na zote hizo ni gharama japo si kubwa.
Unaweza kuvuna lita elf 50 za maji kwa mvua za wiki moja tu.
Mfano mzuri ni jana usiku. Mvua iliyonyesha jana dar kwa mtu ambaye tayari ana tank la kuhifadho maji ingetosha kabisa kujaza maji ya matumizi ya mwaka mzima au miezi kama 9. Hata kama mvua si za kila mwezi lakini sidhani kama inaweza kupita miezi 9 bila mvua kunyesha.
Karibu sana.
 
Umejaribu Bobby,

Lakini ushajiuliza hayo maji ya dawasco yanapatikana wapi? Labda tufanye umeunganishwa kwenye bili je inaruhusiwa kumwagilia mboga maji ya kawaida ya kwenye mabomba?

Na kama hairuhusiwi au haifai means utahitajika kuyanunua, je ushajiuliza utayanunua kwa Tshs ngapi?

Tuseme 200lita = Ndoo kubwa 10, pengine @ Tshs 500/Ndoo 1, hivyo = Tshs 5,000/= kwa umwagiliaji kwa siku. Labda isiwe nyingi sana but ushajiuliza hayo maji utayanunulia wapi?

Na ushajiuliza huko atakapoyatoa yatakua ni yaleyale uliyoyapima mwanzo?

Nilifikiri chanzo cha mto au kisima yanakua ni hayohayo always, Pengine dawasco ni bora zaidi but sidhani kama inaruhusiwa, nimefikiri tu, sina uhakika Bobby!!

Aisee maji ndoo moja sh 500 !!!! kwa mpango huu dawasco hawatofaa kwa anayenunua maji kwa style hii. Nilisuggest dawasco kwa wale wanaopata maji japo kila jumatano usiku nk... yaani una bomba la dawasco nyumbani kwako na maji yanatoka japo kwa mgao...
 
Last edited by a moderator:
mm nipo dar kwa ss na eneo kakufanya shughuli hyo ipo lakini mwanza na kama ilivyo mwanza ni sehem ya miinuka kwa kiasi kilimo hicho cha greenhouse kita faa kweli

Inategemea Na muinuko ukoje? kama ni zaidi ya degrees 30 (kipenyo) basi halitofaa mpaka lisawazishwe au lijengewe msingi na kisha udongo kujazwa. Au kama si mkali sana basi panasawazishwa na kulimwa bila shida. cha muhimu ni kutengeneza njia za maji ya mvua kupita ili yasije kusumbua structure ya greenhouse
 
Inategemea Na muinuko ukoje? kama ni zaidi ya degrees 30 (kipenyo) basi halitofaa mpaka lisawazishwe au lijengewe msingi na kisha udongo kujazwa. Au kama si mkali sana basi panasawazishwa na kulimwa bila shida. cha muhimu ni kutengeneza njia za maji ya mvua kupita ili yasije kusumbua structure ya greenhouse

Asante kwa jibu zuri mamaNA. naomba kuuliza pia natakiwa kua na mtaji wa kiasi gani ili niweze kuanzisha kilimo hiki. yani kwa level ya chini kabisa. nitashukuru nikipata jibu itanisaidia kubadili maisha yangu pia
 
Ni kweli bili ya dawasco itakugharimu lakini maji ya aina yoyote ile hayapatikani bure. Kisima kinahitaji pump hivyo kuhitaji umeme either wa Tanesco, Solar au Generator, na zote hizo ni gharama japo si kubwa.
Unaweza kuvuna lita elf 50 za maji kwa mvua za wiki moja tu.
Mfano mzuri ni jana usiku. Mvua iliyonyesha jana dar kwa mtu ambaye tayari ana tank la kuhifadho maji ingetosha kabisa kujaza maji ya matumizi ya mwaka mzima au miezi kama 9. Hata kama mvua si za kila mwezi lakini sidhani kama inaweza kupita miezi 9 bila mvua kunyesha.
Karibu sana.

Hapa umenigusa sana mkuu nisikuharibie uzi tutaongea mengi sana kwenye hili la uvunaji wa maji kwa matumizi ya Muda mrefu nikija Kukuona
 
Ni kweli bili ya dawasco itakugharimu lakini maji ya aina yoyote ile hayapatikani bure. Kisima kinahitaji pump hivyo kuhitaji umeme either wa Tanesco, Solar au Generator, na zote hizo ni gharama japo si kubwa.
Unaweza kuvuna lita elf 50 za maji kwa mvua za wiki moja tu.
Mfano mzuri ni jana usiku. Mvua iliyonyesha jana dar kwa mtu ambaye tayari ana tank la kuhifadho maji ingetosha kabisa kujaza maji ya matumizi ya mwaka mzima au miezi kama 9. Hata kama mvua si za kila mwezi lakini sidhani kama inaweza kupita miezi 9 bila mvua kunyesha.
Karibu sana.

Kunaweza kupatikana Tank lenye kutosha labda lita 50, au nijenge bwawa chini jirani?

Maana kweli kama mtu unalima hiki kilimo, hii mvua sio ya kuiacha iende
bure!!
 
Do I really need to comment here??
Sehemu nilizohighlight zinaonyesha kabisa hujasoma Uzi mzima. Soma uelimike kwanza, Maswali yako yote yapo kwenye hii hii thread.
NB: Kwanini Unadhani mimi ni MKENYA?? And If i was, Whats wrong with it? Waliokuja kuongea nami, waliopiga simu, waliocomment kwenye hii thread watakushangaa sana.

DONT BE JUDGMENTAL.
Jibu swali, tomatoes zinahitaji jua ama hazihitaji jua????

Kuhusu jua, umesema greenhouse kazi yake kuzuia jua, halafu ukasema tusijenge greenhouse sehemu ambayo ina miti ya kuzuia jua! Which means tutafute sehemu yenye jua! Then we don't need the greenhouse!!!!

Nimejuaje wewe Mkenya? Kwa sababu zamani miaka ya sabini na themanini ndio tulikuwa tunakuwa wowed na bidhaa za Kenya, leo hii ukitangaza biashara unasema eti kinatoka Kenya kama ndio selling point yako unaonekana ni lazima uwe wa kuja kutoka Kenya. I mean, of all the places, Kenya?
 
Kunaweza kupatikana Tank lenye kutosha labda lita 50, au nijenge bwawa chini jirani?

Maana kweli kama mtu unalima hiki kilimo, hii mvua sio ya kuiacha iende
bure!!

Matank ya lita elf50 nayaona sana kwenye building sites kwahiyo naassume yapo na yatakuwa yanauzwa na simtank au polytank. Wakulima wengi walio maeneo ambayo kuchimba kisima ni gharama sana kuwa wanatumia option ya kujenga kisima kinachofanana na septic tank na juu wanafunika na zege kama vile mashimo ya vyoo yanavyojengwa kisha ili kuzuia cement isiharibu PH huwa wanaweka dam liners kwenye kuta za shimo hilo na wanavuna maji kama kawaida.
Hii option ni nafuu sana kuliko kuchimba kisima kwa anayeanza uzalishaji au kilimo. Akishakaa vizuri kimapato anaweza kuafford kuchimba kisima kwa gharama inayostahili. Kujenga kwa style hii hakupaswi kuzidi mil2-2.5... Na hii ni nafuu sana kwani kama shamba liko mbali sana na barabara wachimba visima huquote bei kubwa sana kwasababu ya gharama zao za kusafirisha materials zinavyopanda.
 
Asante kwa jibu zuri mamaNA. naomba kuuliza pia natakiwa kua na mtaji wa kiasi gani ili niweze kuanzisha kilimo hiki. yani kwa level ya chini kabisa. nitashukuru nikipata jibu itanisaidia kubadili maisha yangu pia
Mtaji wa mil4.5 utakusimamisha pazuri sana mpaka kwenye kuvuna, then gharama ndogo ndogo za hapa na pale zitafuata bila formula, mf unapoona kuna dalili ya ugonjwa basi utanitafuta au kutafuta agronomist aliye karibu nawe kisha tukushauri ufanyeje, hapo utanunua dawa tu za kupambana na magonjwa yaliyojitokeza, au gharama za kufata mbolea za asili kwa ajili ya kutop dress nk.
Ukipitia post namba 164, page 9 ya uzi huu utaona mchanganuo mzima wa bei nimeuorodhesha hapo.

Karibu sana.
 
Jibu swali, tomatoes zinahitaji jua ama hazihitaji jua????

Kuhusu jua, umesema greenhouse kazi yake kuzuia jua, halafu ukasema tusijenge greenhouse sehemu ambayo ina miti ya kuzuia jua! Which means tutafute sehemu yenye jua! Then we don't need the greenhouse!!!!

Nimejuaje wewe Mkenya? Kwa sababu zamani miaka ya sabini na themanini ndio tulikuwa tunakuwa wowed na bidhaa za Kenya, leo hii ukitangaza biashara unasema eti kinatoka Kenya kama ndio selling point yako unaonekana ni lazima uwe wa kuja kutoka Kenya. I mean, of all the places, Kenya?

Just read the whole thread and get educated. Ubishi haukusaidii, We just go on doing business with like minded people.
 
Mtaji wa mil4.5 utakusimamisha pazuri sana mpaka kwenye kuvuna, then gharama ndogo ndogo za hapa na pale zitafuata bila formula, mf unapoona kuna dalili ya ugonjwa basi utanitafuta au kutafuta agronomist aliye karibu nawe kisha tukushauri ufanyeje, hapo utanunua dawa tu za kupambana na magonjwa yaliyojitokeza, au gharama za kufata mbolea za asili kwa ajili ya kutop dress nk.
Ukipitia post namba 164, page 9 ya uzi huu utaona mchanganuo mzima wa bei nimeuorodhesha hapo.

Karibu sana.

thankx mamaNa
 
Habari nzuri sana hii. Intertek International Tanzania wako pale kurasini nyma ya chuo cha Diplomasia kuna barabara ya rami inakwenda Uhamiaji kama mita 100 kushoto mkabala na Kanisa la RC wana maabara pale na wamekuja na product moja inaitwa Precision Farming. wanatest Soil kwa dolla $ 7 tu kwa kila sample ni kama Tsh 11200/= kwa rate ya 1600 per dola... jaribu kuwatembelea pia.
 
Habari nzuri sana hii. Intertek International Tanzania wako pale kurasini nyma ya chuo cha Diplomasia kuna barabara ya rami inakwenda Uhamiaji kama mita 100 kushoto mkabala na Kanisa la RC wana maabara pale na wamekuja na product moja inaitwa Precision Farming. wanatest Soil kwa dolla $ 7 tu kwa kila sample ni kama Tsh 11200/= kwa rate ya 1600 per dola... jaribu kuwatembelea pia.

Wanatest udongo tu ndio Product Farming, au wana zaidi ya hiyo ya kutest Udongo?
 
Nimekuelewa sana ndugu, kwa mkulima ninaeanza kilimo kwa capital ya kuchangisha kwa mjomba Na binam,itabidi nisubiri kidogo!, but hyo source ya fund itabidi nikuombe unipe maelezo kidogo kwani itanisaidia sana kupanua kilimo changu hiki kdogo!, asante..
 
Please do the same to rabiahhassan88@yahoo.com

Cost analysis should also indicates price of all other required materials for construction of this greenhouse including wooden poles, suggested simtank-wall/dam, Water pump, water pipes, seeds, e.t.c please.

Thanks

Lady Ra,
Samahani sitoweza kukupa cost analysis ya mtindo huo kwani kila eneo linatofautiana bei za hizo poles, tank, water pipes nk. Mfano bei za poles mbezi beach ni tofauti na Kimara, bei za singida ni tofauti na Simiyu nk... Hivyo itakuwa ngumu kuestimate kwani naweza kukupa figure tofauti ikakutatiza baadae.
NB: Je unataka kujua kitu gani exactly kwa location ipi ili niweze kukushauri vizuri. na je unatarajia kujenga mwenyewe au Nitakujengea? Kama Nakujengea huna sababu ya kujua hizo cost zote kwani nitafanya hiyo husstle. Na kama unajenga mwenyewe naomba uniPM ili tuzungumze vizuri.
NB: Nimeshakuemail
 
Habari nzuri sana hii. Intertek International Tanzania wako pale kurasini nyma ya chuo cha Diplomasia kuna barabara ya rami inakwenda Uhamiaji kama mita 100 kushoto mkabala na Kanisa la RC wana maabara pale na wamekuja na product moja inaitwa Precision Farming. wanatest Soil kwa dolla $ 7 tu kwa kila sample ni kama Tsh 11200/= kwa rate ya 1600 per dola... jaribu kuwatembelea pia.

Asante sana kwa taarifa, Nimelifanyia kazi hili na kuwasiliana nao kwa simu. majibu niliyopata ni kwamba, Unapeleka Sample kwao, kisha wanaibadilisha na kuwa solution (yaani maji) Kisha wanaituma South Africa ikapimwe halaf majibu yakitoka ndio wanakuletea. Niliyeongea naye kwa simu hakuweza kunipa gharama za upimaji moja kwa moja kwani aliniambia mpaka aone sample ni ya kilo ngapi na wao watatoa solution ngapi kutokana na sample uliyopeleka hivyo ni mpaka niende na sample ya udongo ofisini kwao. Lakini alinihakikisha gharama sio kubwa sana ila tu ndio muda wa majibu hauko constant.
Ntawajaribu na sample mbili tatu ili nione efficiency yao kwani itawapunguzia sana gharama wateja wangu kama wako accurate.

Shukran sana.
 
Back
Top Bottom