Jenista Joakim Mhagama

Jenista Joakim Mhagama

Nimekuuliza swali moja je hao ni waalimu wa msingi au sekondari? Umeshindwa kujibu?

Kwa kuwa elimu yao ni darasa la saba basi ni waalimu wa shule za msingi. Na kama ni waalimu wa shule za msingi basi masuala yao ya ajira yanamalizwa na halmashauri za wilaya.

Na kama sheria inasema kuwa darasa la saba hana ajira, kwanini uyaite majibu ya waziri ni rahisi? Watu hawana sifa za kupewa ajira? Na kama wanasifa wapeleke nondo zao.

Mkuu naona labda ulipitwa vile vielelezo alivo vitoa Mhagama, wengine wamemaliza hadi kidato cha sita, na hao wengine kulingana na sheria aliyo inukuu Mhagama kwamba kama wamepitia kozi mbali mbali na experience sheria ina ruhusu kuwaajiri. Hata hivo myaka yote hiyo alishindwa nini kutoa ufafanuzi mpaka asubili kibano? Huwezi ona bado kwamba kuna sehemu hakuwajibika hivyo ni halali alivyo kumbushwa kama ilivyo ada?
 
Mkuu naona labda ulipitwa vile vielelezo alivo vitoa Mhagama, wengine wamemaliza hadi kidato cha sita, na hao wengine kulingana na sheria aliyo inukuu Mhagama kwamba kama wamepitia kozi mbali mbali na experience sheria ina ruhusu kuwaajiri. Hata hivo myaka yote hiyo alishindwa nini kutoa ufafanuzi mpaka asubili kibano? Huwezi ona bado kwamba kuna sehemu hakuwajibika hivyo ni halali alivyo kumbushwa kama ilivyo ada?

There you go. Je ni wajibu wa waziri kuuliza qualifications za watu au ni wajibu wa watu kuakikisha kuwa qualifications zao zinatambulika?

Vilevile unaruka swali langu la kuhusu shule wanazaofundisha?
 
Last edited:
Presha inapanda na kushuka kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi mkuu, Mwakani
 
...na alipompa orodha ya walimu wenye matatizo, alijibiwa, "nimepokea siwezi kuwa na majibu hapa, ngoja niagize huko mikoani wanipe maelezo nitakupatia, sasa subiri baada ya kumaliza bajeti nitakuwa na majibu"...

Je, lengo ni kulipua, ama kupata ufumbuzi wa tatizo? Je, huo ndio utaratibu wa zimamoto? kama yeye alikaa na hayo majina kwa miezi mitatu bila kupata majibu, imekuaje amtake mwenzake awe na majibu ya vijiji vya Songea papo kwa papo?

Kwa maoni yangu, huu sasa ni mchezo wa kukata tamaa na kutafuta wachawi kwa matatizo ya wabunge wetu ambao wameshindwa kazi majimboni. ... kama mtu ulishindwa kwa miaka minne kufanya kazi jimboni, huwezi kupiga kelele bungeni kipindi kilichobaki ukafanikiwa. Waende majimboni kufanya kazi na wananchi na si kupiga kelele

Waziri kaandikiwa barua time and again, hadi Pinda nae kamkumbusha lakini wapi. Yaani azidi kuongezewa muda upi, kumbuka lile halikuwa swali la nyongeza issue inaonekana ya siku nyingi! Madai ya Ghasia kuwa wizara hiyo wamepita mawaziri wengi ni lame excuse. Kwa hiyo watumishi wa umma wawe wanatoa majibu kama hayo wanapo-deal na issue zilizotokea wakati hawajazaliwa au kuanza kazi? Unafika sehemu unamkuta mtumishi wa umma anakwambia "hilo swala lako kwa nini hukulishughulikia zamani, kwanza mimi ni mgeni hapa kazini" TUTAFIKA?.

Pinda nae kudai hayo yanatokana na presha ya uchaguzi kapinda. Hakumbuki yeye naye alipata u-PM sababu ya shinikizo/ukali wa wabunge kumtimua Lowassa? Je wakati huo kulikuwa na uchaguzi gani? Nadhani hii defense ya homa ya uchaguzi inawanufaisha/inawafurahisha mawaziri sana.

Eti wabunge waende majimboni wakafanye kazi na wananchi! Na jengo la bunge litumike kufanyia kazi gani??? Nadhani kufanya kazi na wananchi haitakuwa na maana kama kero zao hazitafikishwa bungeni-ndio platform pekee!

Jamani tuangalie uzito/ukweli wa hoja na si zinatolewa muda gani. Vinginevyo wabunge wakiwa wakali baada ya bunge kuapishwa mtasema "wamekasilika kukosa uwaziri". Wakiwa wakali ktkt ya miaka 5 mtasema "chuki binafsi". Wakiwa wakali karibu na uchaguzi mtasema, "joto la uchaguzi". HATUFIKI.

Na haya maisha binafsi ya mtu hadi kwenye sherehe yanamnufaisha nani hapa? Na kwa nini yasemwe baada ya kuwa mkali bungeni? Personally, napendelea hoja ya mtu na si background yake.

Wabunge endeleeni kuwa-blast mawaziri hadi genge lao walivunje tena kama 2008.

Naomba kutoa hoja!
 
Last edited:
Wakati mwingine watu huwa tunashindwa kuelewa hawa Watawala wetu na jinsi mambo yao wanayofanya
 
Kumbe nyie wote hamjui.... Subirini kuna mtu atakuk hapa na kuwaelezea kuwa kabla ya kikao cha Bunge huwa wanakaa na mazungumzo yanakua hivi 'mwenyekiti' "sasa wewe Jenista tunakaribia uchaguzi na hata hujasikika ukistua bungeni.Sasa tukifika pale we Mletee Da' Ghasia kelele ambazo kila gazeti litaweka habari yako ukurasa wa mbele....halafu we Hawa jidai kama umekasirika hata kuongea huwezi..hata ikiwezekana na Machozi yakutoke. Halafu kesho itakua zamu ya nani aah nani huyu ...huyu nanii bwana!" Mwisho wa kunukuu... Bora nijisomee zangu Hadi thi za "mashimo ya mfalme Suleiman" kuliko kuangalia this boring movie called Bunge
 
Kwa kifupi ngalangala au mbofu mbofu bure ya ghali!

Still dont get it?

Hizi tabia zote unazompa mbunge wetu mhagama na sikia na mama yako anazo na ndiyo maana unazijua sana! Tuwe wastaarabu jamani na tueshimu kila mtu. Tunaweza kumpinga mtu ila haina haja ya kuanza matusi ya nguoni
 
Waziri kaandikiwa barua time and again, hadi Pinda nae kamkumbusha lakini wapi. Yaani azidi kuongezewa muda upi, kumbuka lile halikuwa swali la nyongeza issue inaonekana ya siku nyingi! Madai ya Ghasia kuwa wizara hiyo wamepita mawaziri wengi ni lame excuse. Kwa hiyo watumishi wa umma wawe wanatoa majibu kama hayo wanapo-deal na issue zilizotokea wakati hawajazaliwa au kuanza kazi? Unafika sehemu unamkuta mtumishi wa umma anakwambia "hilo swala lako kwa nini hukulishughulikia zamani, kwanza mimi ni mgeni hapa kazini" TUTAFIKA?.

Pinda nae kudai hayo yanatokana na presha ya uchaguzi kapinda. Hakumbuki yeye naye aliingia bungeni sababu ya shinikizo/ukali wa wabunge kumtimua Lowassa? Je wakati huo kulikuwa na uchaguzi gani? Nadhani hii defense ya homa ya uchaguzi inawanufaisha/inawafurahisha mawaziri sana.

Eti wabunge waende majimboni wakafanye kazi na wananchi! Na jengo la bunge litumike kufanyia kazi gani??? Nadhani kufanya kazi na wananchi haitakuwa na maana kama kero zao hazitafikishwa bungeni-ndio platform pekee!

Jamani tuangalie uzito/ukweli wa hoja na si zinatolewa muda gani. Vinginevyo wabunge wakiwa wakali baada ya bunge kuapishwa mtasema "wamekasilika kukosa uwaziri". Wakiwa wakali ktkt ya miaka 5 mtasema "chuki binafsi". Wakiwa wakali karibu na uchaguzi mtasema, "joto la uchaguzi". HATUFIKI.

Na haya maisha binafsi ya mtu hadi kwenye sherehe yanamnufaisha nani hapa? Na kwa nini yasemwe baada ya kuwa mkali bungeni? Personally, napendelea hoja ya mtu na si background yake.

Wabunge endeleeni kuwa-blast mawaziri hadi genge lao walivunje tena kama 2008.

Naomba kutoa hoja!

Uzito/ukweli hupo wapi sasa? Mbunge anamtaka waziri kushughulikia waalimu wa Songea vijijini, wakati ajira na mambo yote kuhusiana na waalimu yanafanyika wilayani kwenye halmashauri za wilaya.

Kama watanzania hamfanyi kazi huko wilayani na mikoani mnategemea nini kutoka kwa waziri.

Kuna uwezekano mkubwa hata afisa elimu wa wilaya alikuwa anamshangilia mbunge Mhagama wakati yeye ndio point of contact.
 
Hizi tabia zote unazompa mbunge wetu mhagama na sikia na mama yako anazo na ndiyo maana unazijua sana! Tuwe wastaarabu jamani na tueshimu kila mtu. Tunaweza kumpinga mtu ila haina haja ya kuanza matusi ya nguoni

Uzalendo umekushinda.
 
Kumbe nyie wote hamjui.... Subirini kuna mtu atakuk hapa na kuwaelezea kuwa kabla ya kikao cha Bunge huwa wanakaa na mazungumzo yanakua hivi 'mwenyekiti' "sasa wewe Jenista tunakaribia uchaguzi na hata hujasikika ukistua bungeni.Sasa tukifika pale we Mletee Da' Ghasia kelele ambazo kila gazeti litaweka habari yako ukurasa wa mbele....halafu we Hawa jidai kama umekasirika hata kuongea huwezi..hata ikiwezekana na Machozi yakutoke. Halafu kesho itakua zamu ya nani aah nani huyu ...huyu nanii bwana!" Mwisho wa kunukuu... Bora nijisomee zangu Hadi thi za "mashimo ya mfalme Suleiman" kuliko kuangalia this boring movie called Bunge

Tatizo lingine litakaloendelea kutukosesha maendeleo ni (kutoaminiana) kutoamini chochote kinachofanywa na Mtanzania kwa kudhani kila kitu kinapikwa.
 
Uzalendo umekushinda.

Siyo hivyo nilitaka kufikisha ujumbe kwamba kabla ya kumtupia kashfa mama wa mwenzio chunguza kwanza mama yako, dada zako na ndugu zako wengine usije ukawa unawatukana na wao
 
Idara za serikali nazo huwa zinatumia muda mrefu sana kutatua matatizo ya watumishi wake kwasababu ya urasimu!! Matatizo mengine haya yanatengenezwa na watu wanaokwenda na mwendo wa kinyonga kutimiza yale wanayotakiwa kutimiza.Kwa mfano kuna mtu namfahamu huu ni mwezi wa nne toka ameajiriwa na halmashauri fulani bila kulipwa mshahara eti jina lako bado halijapelekwa Tamisemi. Sasa hilo jina linapelekwa na mtu kwa miguu? Acha Mhagama awakumbushe kidogo wajibu wao.Wengi wamejisahau kabisa kuwa ni watumishi wa watu na sio mabwana wa kutumikiwa
 
Mbona wabunge hawajawahi cheleweshewa posho zao?
 
Sijajua huyu mamam amefanya nini jamani??

ametetea watumishi wa umma wanaonyanyaswa na Serikali huko jimboni kwake. Alipeleka malalamiko kwa Waziri (Hawa Ghasia) miaka mitatu iliyopita lakini Waziri hajashughulikia hadi leo. Amefuatilia sana alifika hadi ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI nao wakamwandikia barua Waziri hata hivyo hakuna kilichofanyika.

Kwa kuona hivyo alitaka kunyima shilingi ya bajeti ya Waziri mhusika (kifungu ya fedha za ziara ya Waziri mikoani) kwa madai kuwa hata matatizo anayopelekewa mezani hashughulikii, hivyo hakuna haja ya kumpatia pesa za kwenda mikoani.

Sasa ktk hoja hii (thread) Tina amemponda huyu mama kwa kigezo kwamba amemkoma nyani mchana kweupe tena mbele ya spika. Kwakuwa Waziri mtuhumiwa ni mwanamke, Tina anaona kama Jenister anawasaliti wanawake. So, anataka tumuunge mkoni kumkemea Jenister. Je? tutafika?
 
ametetea watumishi wa umma wanaonyanyaswa na Serikali huko jimboni kwake. Alipeleka malalamiko kwa Waziri (Hawa Ghasia) miaka mitatu iliyopita lakini Waziri hajashughulikia hadi leo. Amefuatilia sana alifika hadi ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI nao wakamwandikia barua Waziri hata hivyo hakuna kilichofanyika.

Kwa kuona hivyo alitaka kunyima shilingi ya bajeti ya Waziri mhusika (kifungu ya fedha za ziara ya Waziri mikoani) kwa madai kuwa hata matatizo anayopelekewa mezani hashughulikii, hivyo hakuna haja ya kumpatia pesa za kwenda mikoani.

Sasa ktk hoja hii (thread) Tina amemponda huyu mama kwa kigezo kwamba amemkoma nyani mchana kweupe tena mbele ya spika. Kwakuwa Waziri mtuhumiwa ni mwanamke, Tina anaona kama Jenister anawasaliti wanawake. So, anataka tumuunge mkoni kumkemea Jenister. Je? tutafika?

Pamoja na Tina kuonekana kutaka wanawake wasiumizane, alikuwa akionyesha kwamba kulikuwa na 'nia mbaya' katika kuuliza hoja husika, na kwa kweli ndani ya Bunge yeyote atakayefanya jambo kwa nia mbaya na si kwa nia ya kusaidia jamii, atakuwa amewakosea Watanzania. Pia kama alivyoeleza Pasco, kuna tatizo la kumbukumbu za walimu waliomaliza darasa la saba ambao walijiendeleza lakini takwimu zao hazijafika mahali husika. Jenista na Ghasia wangeshirikiana kuwasaidia walimu husika wapate haki zao, kazi ambayo isingeweza kuchukua saa chache. Pamoja na kuwa tunapenda watu wawashe moto bungeni, ni vyema pia tukazingatia kutenda haki na kufanya mambo yatakayosaidia zaidi watu wetu wa chini na si kutaka kulinda nafasi zetu. Haki na uadilifu iwe msingi mkuu.
 
Back
Top Bottom