Jeshi la Kongo DRC sasa linaweza kuidhibiti M23 na majirani wabaya

Jeshi la Kongo DRC sasa linaweza kuidhibiti M23 na majirani wabaya

Mafanikio makubwa Sana haya kwa Fardc, wajitahidi kukomboa maeneo yanayoshikiliwa na hao wavamizi na mamluki wa nchi jirani.
@mtu chake @zitto junior @Moronight walker @Bukyanagandi
Hawa uliowaita wanauhusianao na CHIGALI??????????????????
 
Jeshi la nchi ya Congo DR limeonyesha uborekaji wa hali ya juu kwasasa . tangu waasi wa M23 wafanikiwe kutwaa mjii wa mpaka wa Bunagana nimekua nikifuatilia kwakaribu sana mapigano ya kila siku ya vita hii.

Mwazoni ni kama Jeshi lilishitukizwa na mashambulio lakini baada ya wiki mbilijeshi limeweza kusimamisha jitihada za waasi kusonga mbele

Kubwa zaidi ambalo FARDC wameonesha tofauti ni kuweza kuwachambua viongozi wa M23 na kuwashambulia mahususi kupoteza cordination ya waasi.

Juzi ililipotia kifo cha kamanda wa pili wa juu ya M23 (col Yusuph Mboneza) alishambuliwa katika mapigano na kuuwawa, aidha juzi hiyo hiyo ikalipotia kamanda mkuu wa M23Bw Bri Gen Sultan Makenga ameshambulia na kujeruhiwa vibaya.

Leo tarehe 29 june 2022 imeripotiwa tena kuwa asikari wa Rwanda waliokua ndani ya kikoasi cha m23 wameuwawa kwa wingi na mmoja wao akiwa asikari wa cheo cha juu cha luteni kanali akiiwa Col Davidi Kiiza.

Huko Rutchuru wameuawa asikari wengi wa M23 wakiwa na Uniform za Rwanda



Aisee dunia simama huyu Kiiza ninamfaham personal
 
Wanajeshi wa Rwanda wanauwawa kwa wingi wengine xnx na kukimbia wanaacha vifaa vya jeshi vyenye log ya jeshi lao. Sasa hakuna utata tena kua M23 ni RDF
IMG_20220701_164656.jpg
IMG_20220701_165107.jpg
IMG_20220701_164532.jpg
 
Safi sama Kongo kama hii habar ina ukweli. Ila kwa sisi ambao ni wakongwe humu ndani tuliowahi kufatilia hii vita, huyu Sultan Makenga kuhusishwa na kifo sio mara moja, mara nyingi tu lakini baada ya muda bado anarudi.
 
[emoji1][emoji1][emoji1] eti Jeshi la Congo Ni la 8 kwa ubora wa Africa,linaweza kupigwa hata na jeshi la sungusungu wa kitaa.
Jeshi la kijinga sana, hawatambui nafasi yao ni ipi ndani ya Taifa. Kuna clip ilirushwa humu kuna kanali wa Kongo alipata jeraha dogo mguuni, eti ameshikwa mabegani kulia na kushoto anasaidiwa kutembea. Tena anajiburuza huku anatabasamu kabisa.
 
Wakaze Waache Upuuzi
linchi lina Kila kitu linateswa na Rwanda Upuuzi mtupu
drc ni wapuuzi kabisa. wana raia zaidi ya 80mil, rwanda in 6mil na ni kubwa kama mkoa wa Tanga (26,000sqkm). wangeacha kuconcentrate na kujibizana na M23 wakajigawa kundi kubwa likaanzisha vita ya nguvu ya kushtukiza rwanda na wasisikilize cha mmarekani wala UN wala AU wala ye yote..
 
Tusubiri tuone kikosi cha EAC kitaleta jipya gani huko Kivu.
Hakuna jipya zaidi ya waasi kuondoka.

Kipindi cha JK, hawa M23 walikuwa kama 600 kwa idadi ila walileta balaa zito. M23 wala sio wengi sana sababu Rwanda sio nchi tajiri kuweza kuwagharamia.

M23 ina silaha nzuri kwa sehemu sababu zinatoka Rwanda, ukijumrisha na mafunzo walopokea jeshini Rwanda ndo ikawa fimbo kwa Congo. Jeshi la Congo nidhamu hakuna kabisa, hata JKT ya kwetu ikipewa silaha inainyoosha vizuri tu Congo.

Kwahiyo Idadi yao kuwa chache, silaha pia walikuwa nazo kwa sehemu, ikapelekea SADC kuunda kikosi kipana zaidi kuelekea vita ile. SADC ikatoa Brigade moja, askari wasiopungua 3,000 wakipewa baraka zote na UN pia, wakaenda Goma. M23 hawakuweza kutumia silaha kali zaidi kwani ingezidi kudhihirisha wanapewa msaada na Kagame na kumbuka kipindi hiko Kagame ndo alikuwa mshukiwa namba 1 kufadhili genge hilo, mpaka UN ikamtaja Kagame ndio anawafadhili jamaa hao.

Sasa hapo endapo EAC ikaunda majeshi yake kwa idadi kubwa kama ya kwanza na silaha pia. M23 watakimbia kama walivyokimbia mara ya kwanza. Kipindi kile walipoona vita imekuwa ni nzito, hasa mizinga iliyokuwa inapigwa na JWTZ wakaamua waachie Goma, hasa ule mlima waliougeuza kuwa ngome yao. Hawapendi kufa, wanapoona wamezidiwa huwa wanakimbia, idadi ya vifo kwao sio kubwa sana, hawataki kufa sababu wakifa wanajua wanatia hasara kwa serikal ya kwao Rwanda.
 
drc ni wapuuzi kabisa. wana raia zaidi ya 80mil, rwanda in 6mil ni ni kubwa kama mkoa wa Tanga (26,000sqkm). wangeacha kuconcentrate na kujibizana na M23 wakajigawa kundi kubwa likaanzisha vita ya nguvu ya kushtukiza rwanda na wasisikilize cha mmarekani wala UN wala AU wala ye yote..
Mambo hayapo rahisi hivyo mkuu. Labda wajikusanye wanunue MRLS za maana, watenge mabilioni kadhaa wanunue missiles nzito nzito kisha wakinukishe ila kuingia kwa mguu wakongo hawawezi, ni jeshi lililojaa genge la wahuni, tena walau kidoogo miaka ya hivi karibuni.
 
Ningekuwa Rais wa Congo, ninge vamia Rwanda kwanza ili kuleta amani ya kudumu Congo! Ila kwa kuwa Wakongo wenyewe hawajaluona hilo watateseka sana
 
Mambo hayapo rahisi hivyo mkuu. Labda wajikusanye wanunue MRLS za maana, watenge mabilioni kadhaa wanunue missiles nzito nzito kisha wakinukishe ila kuingia kwa mguu wakongo hawawezi, ni jeshi lililojaa genge la wahuni, tena walau kidoogo miaka ya hivi karibuni.
Uko sahihi. lakini kwa hali ilivyofikia, hata wakiingia rwanda na smg au AK47 wakafanya asault ya hata saa moja na wakaitangazia dunia kuwa ni kwa sababu ya uovu wa rwanda kupitia m23, watakuwa wamemfikishia ujumbe kagame. Baada ya hata waanze kulipua rwanda kwa makombora ya masafa.

kumbuka rwanda ni ndogo sana. milipuko miwili tu kanchi kote katatetemeka, watu hawatalala
 
Congo haiwezi kuwa na amani bila PAKA kufa.
 
Uko sahihi. lakini kwa hali ilivyofikia, hata wakiingia rwanda na smg au AK47 wakafanya asault ya hata saa moja na wakaitangazia dunia kuwa ni kwa sababu ya uovu wa rwanda kupitia m23, watakuwa wamemfikishia ujumbe kagame. Baada ya hata waanze kulipua rwanda kwa makombora ya masafa.

kumbuka rwand ani ndogo sana. milipuko miwili tu kanchi kote katatetemeka, watu hawatalala
Dawa ni kuponda kichwa na walamba asali na sio Kuuwa watu Wasio na hati
 
Watumie drones kuponda vichwa vya nyoka mchezo utakwisha haraka sana kuliko kupoteza risasi kuponda mkia.
 
Ningekuwa Rais wa Congo, ninge vamia Rwanda kwanza ili kuleta amani ya kudumu Congo! Ila kwa kuwa Wakongo wenyewe hawajaluona hilo watateseka sana
Kila nchi ina mabaya yake. Mbona hapa TZ watu wamewahi chota fedha kwenye viroba? Ufisadi ni wa kutisha. Hata sisi tunateseka sana na huu ufisadi.
 
Back
Top Bottom