Pengine muda utasema.Kutokana na taarifa ya Polisi inaonesha kuwa, ama:-
√ Mbowe, hakuanguka nyumbani kwake ila kwa Joyce Nkya, hawara yake wa muda mrefu. Angeanguka nyumbani kwake James, mwanae angechukua hatua stahiki, ikiwa ni pamoja na kuamsha majirani; au
√ Alivamiwa na wahuni waliotumwa na wabaya wake Joyce Nkya, wakitoka kwenye ulevi. Yawezekana ndiyo sababu hakuwa na walinzi.
Lilian alidai talaka siku nyingi kutokana na tabia za jamaa
Kuna mwanamama ni jirani yeke Mbowe na ni mbunge, anasema hakusikia lolote hadi asubuhi na alishangaa kusikia Mbowe kashmabuliwa na anasema siku hiyo alilala saa saba
View attachment 1476358View attachment 1476359
USHAHIDI wa awali wa Jeshi la Polisi nchini kuhusu madai ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe umeonesh kuwa siku hiyo ya tukio Mbowe alikuwa amelewa chakali na alizunguka kwenye kumbi mbalimbali za starehe zinazouza vileo ikiwemo ya Royal Village.
Pia ushahidi huo unaonesha mbali ya kuwa kwenye maeneo hayo ya starehe alikuwa nyumbani kwa mzazi mwenzake Joyce Nkya ambaye ni Mbunge wa Viti Maaluma Chadema na kwamba hata taarifa za kwamba ameshambuliwa zinatia shaka kwani mashahidi wote ambao wameojiwa hakuna anayethibitisha uwepo wa tukio hilo zaidi ya Mbowe mwenyewe na dereva wake.
Taarifa ya Jeshi la Polisi nchini iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari na Msemaji wa Jeshi hilo David Misime amesema Juni 9 mwaka huu walitoa taarifa ya awali kupitia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Gilles Mroto kuhusu tukio la lililoripotiwa kuwa Mbowe amelezwa jijini Dodoma kwa kile kilichodaiwa kushambuliwa wakati anaingia nyumbani kwake .
Misime amesema baada ya kutolewa kwa taarifa hiyo ya awali wamekuwa wakipokea simu nyingi kutoka kwa waandishi wa habari wakitaka kufahamu matokeo ya uchunguzi kuhusu taarifa iliyofikishwa Kituo cha Polisi Kati Dodoma.
"Napenda kujulisha kuwa Jeshi la Polisi limeendelea kufanya upelelezi wa kina kuanzia kwa mhanga mwenyewe wa tukio ambaye alidai kuwa muda wa saa saba hivi usiku akiwa kwenye ngazi ya kuingia nyumbani kwake akiwa na anatoka kwa mzazi mwenzake aitwaye Joyce Nkya ambaye ni Mbunge wa Viti Maaluma Chadema anayeishi eneo la Medeli Mjini Ddoma alishambuliwa na kuumia kwenye mguu wa kulia.
"Mhanga wa tukio hilo alidai wakati anashambuliwa alipiga kelele nyingi kuomba msaada ambao aliupata kutoka kwa dereva wake ambaye naye alipiga simu kwa Joyce Nkya kisha hospitali iliyoko takribani umbali wa kilometa tano nje ya Jiji la Dodoma pasipo umuhimu wa kutoa taarifa Polisi kabla ya kwenda kwa Joyce Nkya na Hospitali,"amesema Misime.
Ameongeza upelelezi wao umepata ushahidi kutoka kwenye eneo la tukio unaonesha kulikuwa na watu kwa namna yoyote wangeweza kusikia makelele yaliyopigwa na Mbowe kuomba msaada na wengine walikuwa na uwezo wa kuona bila kizuizi kitendo cha kushambuliwa .
"Hata hivyo kwa mujibu wa wa mashahidi hawa hakuna hata mmoja aliyeweza kusikia kelele hizo au kuona mbowe akishambuliwa. Kwa mantikini hiyo ushahidi pekee unaozumngumzia kushambuliwa ni maelezo ya mhanga wa tukio(Mbowe) pamoja na dereva wake.
"Ambayo kwa hali ilivyo sasa yanatia shaka kuhusu ukweli wa tukio hili.Mashaka hayo yanaongezeka zaidi pale tulipobaini kuwa nyumbani kwa Mbowe alikuwepo kijana wake aitwaje James Mbowe ambaye hawakuona umuhimu wa kumjulisha kuhusu tukio lililotokea hapo nyumbani badala yake waliona umuhimu wa kumjulisha Jocye Nkya aliyekuwa mbali na eneo la tukio,"amesema.
Pia amesema uchunguzi wa Jeshi la Polisi nchini umethibitisha kuwa siku ya Juni 8 mwaka huu Mbowe alitembelea sehemu kadhaa za starehe zinazouza vileo ikiwepo ya Royal Village na kupata kinywaji.
"Hata hivyo alipofika hospitali alioneana akiwa katika hali ya ulevi chakari kiasi cha kushindwa kutamka maneno sawa sawa.Tunaendelea na uchunguzi kutafuta ukweli wa tukio hili, hivyo tunaomba wananchi wenye taarifa zinazoweza kusaidia upelelezi huo wazilete kwetu. Tutaendelea kutoa taarifa kwenu kadri ushahidi utakavyopatikana,"amesema Misime kupitia taarifa ya jeshi hilo kwa vyombo vya habari.
Pia soma
> News Alert: - Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana
> Freeman Mbowe na Joyce Mukya wamtumia Mjomba wa Mtoto kupata cheti cha kuzaliwa
> Mhe. Mbowe na Mhe. Joyce Mukya mtafanya hili suala kuwa siri mpaka lini?
> Joyce Mukya ni nani? Pamoja na kutokuwa active kwenye Siasa bado anapeta ubunge CHADEMA zaidi ya miaka 10
Tangu juzi tumepata nakala ya uchunguzi wa polisi ambao umeandikwa bungeni , kila mtu mwema amelidharau kabisa jeshi la polisi .Mbona ndugu yangu umekuwa mpole baada ya haya majibu? Nakutakia usiku mwema.
Hii video inamaana gani mshana.
Alipigwa na dreva wake bila yeye kujua! Siku akienda polisi na huyo dreva wake sote tutajua kama hivi kwa Mbowe.Hata Tundu Lissu alikuwa amelewa chakariii akajipiga marisasi.
Zamani balozi hizo zikitoa statement unajua fika zimefanyiwa utafiti zikathitishwa independently na mashirika Yao ya kijasusi nk ndipo watoe statement Sasa hivi hamna kitu wakipitia jamii forums wakiona Kuna jungu wanalitolea tamko no verification no what?Hata Balozi za USA, UK, na EU walipokimbilia kutoa matamko kumbe tatizo ni ulevi na ufusika. Sasa sijui wataficha wapi sura zao. Shame on them!!
Kwanini hukuweka hapa mapema?Tangu juzi tumepata nakala ya uchunguzi wa polisi ambao umeandikwa bungeni , kila mtu mwema amelidharau kabisa jeshi la polisi .
Watoe na ya Lissu.Jeshi la Polisi litoe hadharani foot prints za CCTV Camera zilizopo eneo lote la Nyumba za Serikali ambapo Mh. Mbowe alivamiwa zioneshe hayo wanataka kuaminisha Umma. Ninyi ni Jeshi sio Idara ya Propaganda ya CCM.
Polisi Sikilizeni, Mbowe alishakuwa ni "taasisi" na fikra zake za "Changes" zipo kwa mamilioni ya Watanzania, kamwe hamwezi kummaliza Mbowe, ambaye yupo kila Kitongoji, Kijiji, Mtaa, Kata, Taraafa, Wilaya na Mkoa. Mbowe yupo kwenye mioya na vichwa vya Watanzania!
Mr mkiki.
Alikataa...!!!!..😂😂😂😂Mbowe alikataa cctv camera nyumbani kwake
Hahajha... Sawa, lakini mwambie Mbowe aache ulevi na usanii oktoba inakaribiaEndeleeni na sherehe za kichawi.
Aibu kubwa sana kwa IGPYaani jeshi la Polisi hata kutunga hadithi nako ni shida.
1. Ukisoma utaona kuna majina mawili tofauti ya habari moja, Joyce Mukya na Joyce Nkya. Maana yake ni kuwa huu haukuwa uchunguzi bali utunzi
2. Jeshi la Polisi linasema Mbowe alipita sehemu zenye vileo. Kuonekana Bar hakuna maana mtu amekunywa.
Ulevi unaweza kupatikana katika restaurants, je ukionekana huko ina maana umelewa.
3. Aibu kubwa kwa jeshi ni pale inaposema Mbowe alilewa chakari. Jeshi la polisi halifanyi kazi kwa hisia. ''Ulevi chakari ni kitu gani katika vipimo''? Hakuna kitu kama hicho na huwezi kukitumia makalamani.
Jeshi la Polisi lilipaswa kutoa takwimu za vipimo kama hawana wakae kimya , wasijipake zaidi
4. Kwamba mtu hawezi kutamka maneno ni dalili ya ulevi. Well, nani aliyesema hayo kutoka Hospitali?
Kwanini hawakutaja jina la Dk akliyethibitisha kutotamka vema maneno
Ukisoma habari yote ni aibu tu. Eti mashahidi hawakusikia, hivi Tundu Lisu aliposhambuliwa kulikuwa na mashahidi gani,. Mbona Jeshi la Polisi halielezi kwanini waliondolewa walinzi na kamera, eti leo limefanya uchunguzi
Jeshi la Polisim, kukaa kimya ni busara maana taarifa kama hii kwa wenye akili wanabaki wakicheka.
Hii tamthilia ni tamu sana, well done Police Tanzania
Pascal Mayalla Mag3 JokaKuu
Unaandika huku unaona aibu kwa jeshi la polisi kutia aibuHata siku mlipoambiwa Joyce kazalishwa na mwenyekiti mlichachamaa na kupanik
Sasa inakuwaje polisi nao wasingesema kabisa kwamba hakudondoka nyumbani kwake?Kutokana na taarifa ya Polisi inaonesha kuwa, ama:-
√ Mbowe, hakuanguka nyumbani kwake ila kwa Joyce Nkya, hawara yake wa muda mrefu. Angeanguka nyumbani kwake James, mwanae angechukua hatua stahiki, ikiwa ni pamoja na kuamsha majirani; au
√ Alivamiwa na wahuni waliotumwa na wabaya wake Joyce Nkya, wakitoka kwenye ulevi. Yawezekana ndiyo sababu hakuwa na walinzi.
Jeshi livunjwe tuanze upya kabisa.Hivi kumbe Polis huwa wanatoa report? Basi kama wameanza kutoa ripoti tunaomba tupate na ripoti za Lissu, Saanane na wengine wote waliopotea.
Yaani vipimo vya hospitali navyo visiaminike? Ni suala la kuchukuliwa vipimo upya kuthibitisha, maana majeraha, km kuvunjika mguu, hayafutiki siku moja.