Jeshi la Polisi lasema askari aliyejinyonga alikuwa peke yake mahabusu

Jeshi la Polisi lasema askari aliyejinyonga alikuwa peke yake mahabusu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi kuelezea tukio la Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Grayson Mahembe kujinyonga katika mahabusu alipokuwa anashikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya mfanyabiashara Mussa Hamisi, mkoani Mtwara.

Wamesema askari huyo baada ya kutoa maelezo alifungiwa mahabusu peke yake na askari wengine ambao ni watuhumiwa wenzake waliwekwa mahabusu nyingine za mikoani ili wasiharibu Ushahidi, ndipo alipochukua hatua ya kujinyonga.

Kwa suala la mazishi ya kijeshi polisi wamesema askari aliyejitoa uhai hazikiwi kijeshi kwa kuwa anahesabiwa hajafa kishujaa na hastahili heshima ya gwaride la mazishi linalochezwa na risasi na mabomu ya kishindo kupigwa.


1.jpg
2.jpg

 
Kwa hiyo afande anakosa gwaride linalochezwa kwa risasi na mabomu ya kishindo? (Rejea aya ya mwisho)
😂😂😂😂
Bila shaka hii taarifa imeandikwa na mzee wa kipigo cha 🐕 koko
 
Ipi pathologist report?na why haraka ya mazishi wakati bado uchunguzi haujafanyika,kwanza police tuelezeni nini kinafanyika kwa suspect kabla ya kuwekwa mahabusu?
 
Back
Top Bottom