Jeshi la polisi linafanya uchunguzi wa malalamiko ya mwananchi mmoja dhidi ya askari polisi wa kituo cha polisi Goba

Jeshi la polisi linafanya uchunguzi wa malalamiko ya mwananchi mmoja dhidi ya askari polisi wa kituo cha polisi Goba

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Taarifa kwa vyombo vya Habari.

Dar es salaam, 16/11/2021

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linafanya uchunguzi wa tukio la kijana anayefahamika kwa jina la Issa Kassim (20) mkazi wa Goba Wilaya Kinondoni kudaiwa kupigwa na askari wa Jeshi la Polisi na kusababishiwa maumivu makali.

Kijana huyo inadaiwa alikamatwa tarehe 10 Novemba 2021 kwa tuhuma za wizi wa TV na baadae kupigwa huku ikidaiwa ndugu zake walikuwa wakiombwa rushwa ili aachiwe. Malalamiko hayo ni mazito hivyo Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limeshafungua jalada la uchunguzi na mifumo ya kisheria itatumika ili kupata ukweli wa jambo hilo na ikibainika ni kweli hatua za kisheria na kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wahusika, Uchunguzi huo tayari ulikwisha anza.

MULIRO J. MULIRO– ACP

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.


Kuona malalamiko soma hapa>> Goba, Dar es Salaam: Polisi watuhumiwa kumpiga mtu mmoja na kumjeruhi
 
Kila mtu akileta malalamiko dhidi ya uonevu wa polisi yatafunguliwa majalada mengi sana, Kamanda Muliro ni vyema kuwapa mafunzo na semina mbalimbali za maelekezo juu ya namna ya polisi anavyopaswa kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria maana wengi weupe sana

Ukienda vituoni custumer care zero kabisa kazi yao kutishatisha watu tu. Kuna ndugu yangu amekamatwa toka last Thursday leo ana zaidi ya siku 10 kituoni mahakamani hawajampeleka ukiwauliza sababu mara mpelelezi wa case yake hayupo sasa kama hayupo si mumuachie mpk arudi, ukimpelekea nguo abadilishe hawataki yaani polisi ni wa ajabu sana

Hiki kigezo cha kuajiri kwa kutumia matokeo hafifu ni tatizo maana unapata watu ambao thinking capacity yao ni very low hata kwa jambo ambalo inahitajika akili ndogo tu kuling'amua kwao ni tatizo
 
Kwa hiyo mnategemea Murilo atakuja kuleta taarifa kuwa ni kweli.Yaani watende na wajichunguze wenyewe nawakiri kosa.

Iwepo idara ya Tume yakisheria ndio iwe inachunguza
 
Hili halikubaliki,tunaomba sheria zichukue mkondo,na siyo kwamba hao askari wapumbavu "WARISYA" tunashindwa kuwashughulikia,huwa muda mwingine ni uvumilivu na staha tu tunatumia,ila sasa nasema leo ya kwamba!!,Siku askari akija kunikamata mimi au ndugu yangu na akileta ubabe nafasi yake ajirini poti mwingine maana yeye atakuwa maiti!! @polisitanzania
Screenshot_20211116-181201.jpg
 
Hili halikubaliki,tunaomba sheria zichukue mkondo,na siyo kwamba hao askari wapumbavu "WARISYA" tunashindwa kuwashughulikia,huwa muda mwingine ni uvumilivu na staha tu tunatumia,ila sasa nasema leo ya kwamba!!,Siku askari akija kunikamata mimi au ndugu yangu na akileta ubabe nafasi yake ajirini poti mwingine maana yeye atakuwa maiti!! @polisitanzaniaView attachment 2013057

halafu ukisha muua unawapelekea polisi kisha unarudi zako home kuendelea na kazi nyingine,muue bana tumechoka sana.
 
Polisi hawaaminiki. Kungekuwa na mamlaka nyingine huru ya kuwachunguza polisi, kukusanya ushahidi na kuwapandisha kizimbani
 
Hivi Uganda nini kinaendelea?. Naona mzimu wa Hamza umefufukia kule. kwa nini lakini umeenda Uganda ukatuacha sisi?.
 
Back
Top Bottom