Pre GE2025 Jeshi msipotambua umuhimu wenu, mtatumika vibaya kwa maslahi ya wanasiasa na wala siyo kwa maslahi ya Taifa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ila hali ya Sasa hivi ni ukapitalisti mtupu usoshalisti upo kwenye makaratasi tu.
 
Nawatakia kila la kheri nyombo vya ulinzi na usalama nchini kwa uimara, bidii na weledi katika kudhibiti uharibifu, uporaji na uhalifu mathalani wa mapanyarodi, nyumbu na maandamanaji haramu πŸ’

Wanainchi wengi hususani mimi mwenyewe nawapongeza sana kwa ubunifu mlokuja nao. Suala la usafi wa mazingira jijini Dar es Salaam ni muhimu sana hususani kipindi hiki hatarishi kwa mlipuko wa kipindupindu....

Yeyote atakae jitokeze kuchafua mliposafisha huyo ni takataka tembeeni nae bila mbambamba mwendo wa ngiri, ili iwe fundisho kwa wakaidi na wachafua mazingira wengine....

Tunategemea Amani na utulivu wa kiwango cha lami January 23 na 24...πŸ’

Mungu Ibariki Tanzania..
 
Alafu Kuna mtu anasema waliozaliwa tisini 90s ndio wanasabanisha matatizo Kwa Taifa eti kisa wanamambo ya laana wakati inajulikana Taifa lipo kwenye mikono ya kizazi gani
 
Unaongelea jeshi ambalo linawapiga raia hovyo hovyo mitaani?
 
Jeshi la kwanza kabisa baada ya ya la wakoloni kutimuliwa na nyerere lilijengwa na vijana was UVCCM!

Tusishangae Kwa haya!!

La kujiuliza he jwtz watakubali!!?
 
Wanajeshi wanapaswa kuheshimu mamlaka ndio maana wakuu wa mkoa na wilaya wanapigiwa salute na hao wanajeshi ,wakipewa agizo ni utii ,nawasifia sana ni watiifu
 
Alafu Kuna mtu anasema waliozaliwa tisini 90s ndio wanasabanisha matatizo Kwa Taifa eti kisa wanamambo ya laana wakati inajulikana Taifa lipo kwenye mikono ya kizazi gani
Nilishaandika kabisa uzi hapa JF kuhusiana na kizazi hiki kinachotuongoza Mkuu. Nadhani mambo yatakaa sawa tukifanya kama walivyofanya Burkina Fasso. Tuweke vijana wadogo lakini wazalendo kwa Taifa Lao.
 
Hoja yako imekaa kisiasa mno. Kwani Usafi hauwezi kufanyika siku nyingine isipokuwa siku hiyo ambayo hao jamaa walishapanga maandamano?
Tukumbuke na kuzingatia kwamba endapo yatatokea maafa (kama maandamano yatafanyika) mm na ww tutahusika kwa namna moja au nyingine e.g. Kuzika/rambirambi, kukosa amani siku hiyo - maduka/fremu na shughuli /huduma zitatatizika, huenda wakahusika Ndg au Jamaa zetu humo.
Mchuma janga hula na wakwao.
 
Jeshi la kwanza kabisa baada ya ya la wakoloni kutimuliwa na nyerere lilijengwa na vijana was UVCCM!

Tusishangae Kwa haya!!

La kujiuliza he jwtz watakubali!!?
Kwa nini wasikubali Mkuu?!
Mi nafikiri kuna mambo huwa si ya kuomba bali ni kutekeleza tu kwa vitendo ikiwemo mabadiliko.
 
Ni wizi mtupu mkuu.
Wengi wanaumia, wanafaidi wachache
Yeah. Na hao wachache ndo wamelewa kiasi cha kutaka kuwaamuru hata Wanajeshi wetu watukufu eti wainame washike mfagio kufagia barabara ili VX 9 zilizonunuliwa kwa kodi zetu ambazo ndizo wanazotumia wao zipite vizuri. Ni AIBU. AIBU mno.
 
Yeah. Na hao wachache ndo wamelewa kiasi cha kutaka kuwaamuru hata Wanajeshi wetu watukufu eti wainame washike mfagio kufagia barabara ili VX 9 zilizonunuliwa kwa kodi zetu ambazo ndizo wanazotumia wao zipite vizuri. Ni AIBU. AIBU mno.
Hili halikubaliki
 
Umenena vyema Mkuu.
Jasho jingi wakati wa amani, damu chache wakati wa vita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…