Jezi mpya kwa timu mbalimbali kwa msimu ujao 2024/2025

Hizi jezi mpaka nimesimumuka ngoja tusubiri copy za kariakoo tuanze kuvimba nazo in fact jezi kali sana
Mimi nimeacha kuchukua za bongo coz nyingi feki wanaweka uzito wa kuzugia na Vitone tone kwa mbali, nikitaka Jezi now bora nikachukue zenyewe OG .Niliwahi ingia website ya Spurs nikakuta Jezi ni laki 4 Og ya chini yake kama laki mbili hivi hapo ndio nakujua huku tunapigwa .
 
OG gharama mkuu wacha tuishi na jezi zetu fake siku pochi ikinona tutaishi na OG
 
Mzee hizi za kariakoo Kuna zingine nzito inategemea uchaguzi wako ukienda kununua usimsikilize muuzaji angalia mzigo nakuhakikishia utapata nzito kama zinazouzwa kwenye maduka ya club
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…