JF Hard Talk "FaizaFoxy"

JF Hard Talk "FaizaFoxy"

Samahani sana jana kidogo mtandao kwetu ulikuwa unaingia na kutoka.

Tunaweza kuendelea leo kwani naona mtandao upo vizuri.
Asalaam aleykum FaizaFoxy karibu kwenye hard talk, ningependa kufahamu yafuatayo..
1. Wewe ni kabila gani?
2. Je umejaliwa kuwa na watoto? Ni wa ngapi kama wapo.
3. Umesoma hadi kiwango gani cha elimu

Asante!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm Nina hitaji msaada wako je naweza kuja pm utakua tayari?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mambo ya pm siyapendi. Kuna nyuzi nimefungua humu JF,, moja hii: Faidika na darsa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa - JamiiForums na nyingine hii: FaizaFoxy: Wanaonitongoza waje hapa - JamiiForums.. Nimefungua hizo nyuzi kwa kutokupenda kuwasiliana kwa pm.

Tafadhali pitia hizo nyuzi useme shida yako au sema hapa hapa tunahitaji msaada upi, kama kuna ufumbuzi kutoka kwangu au kwa mwana JF yeyote utasaidiwa. Usipende sana pm haps sote hatujuani.
 
Hilo ni kweli kabisa. Ilifikia mpaka Waislam kupunguziwa points zao wakati Ndalichako alipokuwa mkuu wa mitihani. Waislam mpaka wakaingia mitaani kuandamana mpaka Ndalichako akaachia ngazi.

Magufuli alipoingia madarakani akatuzaba Waislam kofi la kikelb kwa kumrudisha wizara hiyohiyo na kumfanya Ndalichako awe waziri wa elimu. Hatari.
@FaizaFoxy unaweza kuwa na uthibitisho wowote juu ya malalamiko yenu kuwa wanafunzi wa kiislam walikua wanapunguziwa alama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moja katika vitu ninavyohisi ni ubaguzi ni hilo la kuulizana umri. Unataka kunibagua kwa umri wangu?

Kwa ufupi, chukulia kuwa nilikuwepo kabla ya awamu ya kwanza. Alhamdulillah nimeziishi awamu zote tano baada ya Uhuru na Malkia wa Kiingereza alishakuwa Malkia wangu na nnamuheshimu.
duh inamaana kabla ya 1961 ulikuwepo!!!
 
Una mtazamo gani juu ya Raisi wetu mpendwa wa JMT ndugu JPM unafikiri ni chaguo lililokuja katika kwa wakati sahihi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Magufuli yupo vyema sana, sema wazee wenye diplomasia wangempiga msasa kidogo kwani kuna vitu anavyoweza kuongea vikatafsirika vibaya. Na watendaji wanamuiga style yake nadhani wangejielekeza zaidi kwenye usimamizi na uwezeshaji kama alivyofanya jana na juzi kuliko kuwa kwenye kudhibiti tu.

Kwa mikutano yake ya hivi karibuni, nahisi kama anaisoma JF na anafanyia kazi maoni yetu, soma huu uzi: Tahadhari kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya: Maigizo mnayofanya yatawagharimu... - JamiiForums
 
Kwa sasa elimu yangu haina umuhimu kwani nimejifunza kuwa kuelimika si kwenda shule pekee. Nimeona wengi wameenda shule kusomea ujinga.

Sijaolewa. Nimeoana na mume wangu. Mpaka sasa nafahamu ni mimi tu niliyeoana nae.
yani umemuoa na yeye amekuoa.
 
1- Ukipewa nafasi ya kua raisi wa jmt ni hatua gani za mwanzo kabisa utakazochukua kurekebisha unapoona hapako sawa?

2- Ni jambo gani kubwa utakalo anza ku deal nalo ili nchi ikue kiuchumi na ijitegemee na kuondokana na umasikini? (japo hii ni long plan)

3-Ni kweli bara la Africa watu ni "masikini" kwasababu ya westeners wanazinyonya nchi zao kwa njia mbalimbali kama mikopo,misaada fake n,k?
 
Hilo ni kweli kabisa. Ilifikia mpaka Waislam kupunguziwa points zao wakati Ndalichako alipokuwa mkuu wa mitihani. Waislam mpaka wakaingia mitaani kuandamana mpaka Ndalichako akaachia ngazi.

Magufuli alipoingia madarakani akatuzaba Waislam kofi la kikelb kwa kumrudisha wizara hiyohiyo na kumfanya Ndalichako awe waziri wa elimu. Hatari.
hapa umedanganya uma,mbona mimi nimesoma na rafiki zangu waislam na walikua wanapasua tu ,na waliokua wanafeli ni wale vilaza tunaowajua.sasa nyinyi wengi wenu mnakesha madrasa ,elimu ya darasani mnaiona ya kikafiri halafu mnataka mfaulu sawa na wakristo ambao shule ndio kipaumbele namba moja elimu ya biblia ni mpaka sunday school au kipindi cha dini .mpaka leo unguja na pemba ndio shule zinazoshika mkia kwenye mitihani ya kitaifa vp ndalichako bado anawafatilia huko ?punguza mihemko ya kidini mama
 
Unadhani nini sababu ya kuibuka kwa makundi ya kigaidi hasa yanayojificha katika mwavuli wa Dini Kiislamu, Je ni kweli mafundisho yenu yanawataka mfanye Ugaidi?
Gaidi kwa mmoja ni mpigania Uhuru kwa mwengine.

Mandela alifungwa miaka 27 kwa ugaidi, alihukumiwa maisha!

Tunaamini Mandela ni gaidi?

Picha ya ugaidi, Uislam unakataza hata kudhuru mdudu. Uislam ni mwema sana.

Kwanini hautumii fursa ya teknolojia na kujisomea Qur'an mtandaoni ili uelewe Waislam wanafundishwa nini.

Hii index nzuri kabisa ina cover kila neno liliomo ndani ya Qur'an: QuranIndex.Net ipitie.
 
Unakwepa point unazoulizwa. Watu wanataka kujua elimu yako.
Kutoka na michango yako humu ndani, wangependa kujua.. umefika university, su level gan ya elimu?
Kwa sasa elimu yangu haina umuhimu kwani nimejifunza kuwa kuelimika si kwenda shule pekee. Nimeona wengi wameenda shule kusomea ujinga.

Sijaolewa. Nimeoana na mume wangu. Mpaka sasa nafahamu ni mimi tu niliyeoana nae.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kote. Msimu wa baridi Canada nnakuwa Tanzania na likiwa joto kule nnakuwa huko.
Sawa Mkuu,Vipi Maisha ya kutafuta huko kwa tunaotaka kuja kutafuta,vipi kuna uwezekano wa kutusua kifedha? Kazi za aina gani kwa watu wasio na degree(DEIWAKA) ambazo zinalipa kwa huko na wanalipa Tsh ngapi per 1hr,week ,month?
 
Ugaidi kwa mmoja ni mpigania Uhuru kwa mwengine.

Mandela alifungwa miaka 27 kwa ugaidi, alihukumiwa maisha!

Tunaamini Mandela ni gaidi?
Nazungumzia hawa wanaobeba mwavuli wa kidini km Boko Haram, Al-Shabab, ISIS nk. kama ulivyosema Ugaidi ni mpigania Uhuru kwa mwingine na hawa wote wanadai wanapigania Uhuru wa kidini ili kuweka Islamic Law (Sharia). Swali langu ni kwamba ni kweli mafundisho yenu yanawataka mfanye Ugaidi?
 
Nazungumzia hawa wanaobeba mwavuli wa kidini km Boko Haram, Al-Shabab, ISIS nk. kama ulivyosema Ugaidi ni mpigania Uhuru kwa mwingine na hawa wote wanadai wanapigania Uhuru wa kidini ili kuweka Islamic Law (Sharia). Swali langu ni kwamba ni kweli mafundisho yenu yanawataka mfanye Ugaidi?
Ndiyo hao ninaosema mimi. Gaidi kwa mmoja mpigania Uhuru kwa mwengine.

Ukiwasoma boko haram wanasema wao wanapigania haki lakini ukiwasoma wanaowapinga wanaweka hawa ni magaidi.

Ukiwasoma Alshaabab wansema wao wanipigania Somalia kwa kuvamiwa na majeshi ya nje. Lakini wengine wanasema ni magaidi.

Hayo hayakuanza leo wala jana. Ndiyo maana nikakupa mfano wa Mandela.

Ukipitia mitandaoni na kutaka kujifunza, utakuta kuna Red Brigades Walikuwa Italy, nao ni hivyo hivyo.

Ireland utawasoma kina Sinn Fein na kundi lake la IRA nao waliitwa magaidi.

Hakuna dini yenye amani kama Uislam. Uislam ungekuwa na ugaidi hapa Tanzania kungekuwa hakuna dini nyingine kwani Uislam ulikuwepo hapa zaidi ya miaka 1000 kabla ya Ukristo.
 
Unakwepa point unazoulizwa. Watu wanataka kujua elimu yako.
Kutoka na michango yako humu ndani, wangependa kujua.. umefika university, su level gan ya elimu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Elimu yangu mimi wewe inakusaidia nini kuijuwa?

Siku za nyuma nilikuwa najibu hilo swali kwa kujisifu elimu yangu ( pitia uzi huu wa zamani utakuta jibu la hilo swali: Faidika na darsa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa - JamiiForums ) lakini nimejifunza kuwa hata leo hii mimi ni mwanafunzi.
 
Afrika bongo zenu zimebunguliwa yaani watu wakae wawafelishe wakati nyie mnakesha madrasa!! Tena somo lenyewe mnalosemea Islamic Knowledge.

Nimelelewa na ndugu mwislamu huku mm nikiwa mkristo toka lakwanza hadi la saba, wakati mm nilikua narudi masomo ya jioni watoto wao walikua wanalazimishwa kwenda Madrasatul jioni (wao wanaita Chuo) mwisho wa siku walibaki kua mbulula peke angu ndo nikatoboa lasaba.

Waislamu mnapenda Public Sympathy mno mnataka muishi kwa kuonewa huruma na watu ati mnaonewa.. But kwanini nyie tu?? Si mabudha, Indu, Etc??
Badirikeni ni wakati wa Survive to the fittest
 
Back
Top Bottom