JF new members only

Umeongea ukweli kabisa Evelyn, mimi mara ya kwanza kabisa kujua jf mi 2010-2012.
Nilifungua account hio 2012 kwa msukumo wa hoja zilizokuwa zinawasilishwa wakati huo, ukweli hoja nyingine zilikua juu ya upeo wangu lakini niliona kabisa Jf ni sehemu ninayoza kupata nilicho kikosa kwenye mfumo rasmi wa elimu, na kweli nilipata.
Mimi binafsi kwa asili sio muongeaji sana au wa kujichanganya sana ila ni mpenzi sana wa kusoma, hii platform ilikua ni ndani ya mapendeleo yangu ya kusoma, hivyo ikanijengea uraibu mpaka kesho siwezi kua nje ya jf.

Shida ilianzia pale 2015, siasa za majitaka kupondana , u chadema na u ccm mapenzi na mahusiano ilizalisha wanachama wengi ambao ndio tulio ingia naao 2020 kuja huku tulipo ambapo tuweza kusema kumeharibika sana au kuhitimisha kusema jana ni nzuri kulio leo.
 
Changamoto nyingine ninayo iona kulingana hoja yako hii ni wale wanachama wa zamani kufungua I'd mpya na kujitoa ufahamu, sambamba na wapya ambao utashi wao ni mdogo kulingana na aina ya wanachama wa mtandao huu.
 
Unamtag vipi mtu na nawezaje kum-ignore member ni hayo tu mhenga wa jf
Kum tag member anza na @ kisha andika jina lake
Kumu ignore my bofya profile yake kisha chagua option ya ignore
 
Iko kwenye kiwango bora zaidi kwasasa naweza kukiri hilo
Kweli kabisa ndugu yangu, japo jana hatuwezi kuilinganisha na leo , kuna ya jana yalikua bora kuliko ya leo pia kuna ya leo ni bora kuliko ya jana.

Wakati huu jf inaelekea kutimiza miaka 20 mara kadhaa nimeomba uongozi wa jf ufanye namna ya kuwatambua na kuwashukuru wanachama waanzilishi kwa I'd name zao ambao mpaka leo wengi wao wapo, kusema tu asante inaleta furaha sana .
 
Changamoto nyingine ninayo iona kulingana hoja yako hii ni wale wanachama wa zamani kufungua I'd mpya na kujitoa ufahamu, sambamba na wapya ambao utashi wao ni mdogo kulingana na aina ya wanachama wa mtandao huu.
Nadhani hili lilikuja kudhibitiwa.. Ukimshinda mtu kwenye hoja moja anakurudia kwa ID mpya.. Ama ID moja ni mwanao sana halafu anafungua ID nyingine ya kukunanga
 
Kwa ukubwa wao sasa wao JF na kipindi ilichopitia bado nadhani inastahili pongezi hasa hasa kwakuwa chanzo cha habari za kuaminika na kuaminiwa na hata mataifa rafiki
Kwasasa tayari kuna mataifa ya Afrika yameshaomba kuwa na JF kwenye mataifa yao.. Hili kwangu ni kubwa sana
Kuna miradi mingi kwasasa kwa manufaa ya Jamii ambayo hapo mwanzoni haikuwepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…