Hii noti inanikumbusha Mzee mmoja alikuwaga mfanyakazi katika mgodi wa Mwadui, enzi hizo wavuta tumbaku walikuwaga wanatumia maganda ya mahindi kusokota sigara. Sasa huyu Mzee alikuwaga analima mahindi kwa wingi Sana akivuna anayatundika nje kwenye 'NSHIGITE' msiojua kisukuma mnisamehe Bure. Ukipita kwake ukamkuta yeye halafu ukaomba ganda la mahindi anaingia ndani anakuja na hiyo noti anakuambia ganda hili hapa.
Kijijini kwetu tuliibatiza tukawa tunaiita jina la huyo Mzee.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.