JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

Mwaka 1992. Taifa Stars dhidi ya Liberia. Beki asiyekuwa na masihara wakati huo akisalimiana na Nahodha wa Liberia, George Oppong WEAH. Namzungumzia David Mwakalebela "MP" wengine waliita Mwanza Patrol. Je unamkumbuka beki huyu wa nguvu enzi zake?.....hakuwa na mchezo hata kidogo!
Screenshot_20211226-085356.jpg
 
Mwaka 1992. Taifa Stars dhidi ya Liberia. Beki asiyekuwa na masihara wakati huo akisalimiana na Nahodha wa Liberia, George Oppong WEAH. Namzungumzia David Mwakalebela "MP" wengine waliita Mwanza Patrol. Je unamkumbuka beki huyu wa nguvu enzi zake?.....hakuwa na mchezo hata kidogo!View attachment 2057805
Mwakalebela David alikua beki wa kulia wa wana Kawekamo, wana TP Lindanda, Pamba FC ya Mwanza. Kikosi chao kilikua kama ifuatavyo;

Golikipa; Paul Rwechungura

Beki wa kulia(no 2): David Mwakalebela

Beki wa Kushoto (no.3): Abdallah Bori

Beki wa kati (no.4): George Magere Masatu

Beki wa kati(no. 5) James Washokera

Kiungo mkabaji(no.6): Nico Bambaga

Winga wa kulia(no. 7): Beya Simba

Kiungo Mshambuliaji(no. 8): Hussein Masha

Mshambuliaji wa Kati(no.9): Kitwana Sueleiman

Mshambuliaji Pembeni(no. 10): Ntenze John

Winga kushoto(no. 11): Fumo Felician Ferdinand
 
Mwakalebela David alikua beki wa kulia wa wana Kawekamo, wana TP Lindanda, Pamba FC ya Mwanza. Kikosi chao kilikua kama ifuatavyo;

Golikipa; Paul Rwechungura

Beki wa kulia(no 2): David Mwakalebela

Beki wa Kushoto (no.3): Abdallah Bori

Beki wa kati (no.4): George Magere Masatu

Beki wa kati(no. 5) James Washokera

Kiungo mkabaji(no.6): Nico Bambaga

Winga wa kulia(no. 7): Beya Simba

Kiungo Mshambuliaji(no. 8): Hussein Masha

Mshambuliaji wa Kati(no.9): Kitwana Sueleiman

Mshambuliaji Pembeni(no. 10): Ntenze John

Winga kushoto(no. 11): Fumo Felician Ferdinand
Duh..uko vizuri[emoji1545][emoji1545][emoji1534]
 
Mwakalebela David alikua beki wa kulia wa wana Kawekamo, wana TP Lindanda, Pamba FC ya Mwanza. Kikosi chao kilikua kama ifuatavyo;

Golikipa; Paul Rwechungura

Beki wa kulia(no 2): David Mwakalebela

Beki wa Kushoto (no.3): Abdallah Bori

Beki wa kati (no.4): George Magere Masatu

Beki wa kati(no. 5) James Washokera

Kiungo mkabaji(no.6): Nico Bambaga

Winga wa kulia(no. 7): Beya Simba

Kiungo Mshambuliaji(no. 8): Hussein Masha

Mshambuliaji wa Kati(no.9): Kitwana Sueleiman

Mshambuliaji Pembeni(no. 10): Ntenze John

Winga kushoto(no. 11): Fumo Felician Ferdinand
Hapo atangaze Dominic Chilambo.
Mpira ulikuwa burudani,siyo watangazaji wa Sasa.
 
Shivlingum found in Harwan area of #Kashmir during digging for a water reservoir for Harwan garden in 2017. It is believed to be of 6th century & is around 2.5 feet in height.
No one can deny the Sanatani Past of Kashmir

PC - Dr. Sushma Kaul
Screenshot_20211227-220259.jpg
 
Kama ulikua humjui vizuri King Majuto wacha nikufahamishe;-
Jina lake kamili anaitwa Amri Athuman alizaliwa mwaka 1948 jijini Tanga na kusoma shule ya msingi Msambweni iliyoko mkoani Tanga mwaka 1959 hadi 1965,
King majuto alianza sanaa ya kuigiza kwa mara ya kwanza mwaka 1958 akiwa kwenye majukwaa mbalimbali.
Katika enzi za uhai wake Mzee Majuto aliwahi kutumikia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Ruvu kwa kujitolea akiwa na umri wa miaka 17,
Ambapo alipata nafasi hiyo kwa kuteuliwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga enzi hizo marehemu Issa Mtambo.
Baada ya kufikisha miaka 18, Mzee Majuto alichaguliwa kwa mara nyingine kujiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kambi ya Twalipo iliyopo maeneo ya chuo cha Uhasibu jijini Dar es Salaam na ilipofika mwaka 1972 aliachana rasmi na masuala ya jeshi na kufanya kazi za kijamii.
Mzee Majuto ndio msanii wa kwanza nchini Tanzania kuandaa na kuuza kazi zake za sanaa kupitia mikanda iliyokuwa inafahamika kwa jina la 'VHS' enzi hizo, na hadi umauti unamfika (kifo) ameshiriki zaidi ya kazi 89.
Mbali na kipaji cha uigizaji, Mzee Majuto pia ni mtunzi, mwandishi pamoja na muongozaji filamu.
Marehemu Mzee Majuto ni miongoni mwa wasanii walioweza kufanikisha ndoto za vijana wengi waliokuwa na nia ya kutaka kufanya sanaa ya kuigiza,
Na kupitia yeye kwa namna moja ama nyingine waliweza kufahamika na kufanikiwa yale waliyokuwa wameyakusudia.
Septemba 24, mwaka 2015, Mzee Majuto alifanikiwa kuenda kufanya ibada ya 'Hija' kwenye mji wa Makka nchini Saudia Arabia na kunusurika kifo kufuatia ajali iliyotokea ya winchi kuanguka na kuua zaidi ya watu 109 na kujeruhi mahujaji 816.
Baada ya tukio hilo, Mzee Majuto ilipofika Mei 2 mwaka 2016 alitangaza rasmi kuachana na kazi ya uigizaji na kwamba anataka kumtumikia Mungu na kuomba asamehewe makosa kwa yale aliyotenda nyuma na kutangaza tena nia hiyo mwaka huu 2018 alipotoka nchini India kwa matibabu.
Jina la Mzee Majuto limeshindwa kupata thamani halisi ya kutokana na watu wengi walikuwa wanamtumia Mzee huyo kwa manufaa yao binafsi bila ya hata kumuangalia yeye namna ya kumuwezesha kiuchumi hususan katika sekta ya kilimo ambapo enzi za uhai wake alikuwa akipigania sana.
Itakumbukwa mnamo Oktoba 27, 2017, Waziri wa Habari, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe alikiri mbele ya umma kuwa Mzee Majuto amedhurumiwa pesa milioni 25 na kampuni ya filamu ambayo jina lake amelihifadhi na kudai atatumia hata mshahara wake kuhakikisha anawafunga watu hao.
Mwili wa marehemu Alhaji King majuto umezikwa kwao Tanga kwenye shamba lake.

Makala hii imeletwa kwenu na Dhulkad Madara kutoka morogoro
Screenshot_20211229-233115.jpg
 
Back
Top Bottom