JF True Life Stories: Unaikubali ipi kati ya hizi?

JF True Life Stories: Unaikubali ipi kati ya hizi?

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
4,805
Reaction score
17,850
Jf ni ulimwengu murua sana, una kila aina ya real life time experiencies, yani ukiwa humu unakuwa ni kama unaiona dunia na yanayoendelea ndani mwake.

Kuna true stories kadhaa zimeletwa na wadau humu jf, ni true stories zenye utamu na msisimuko wa hali ya juu. Ni stori ambazo zitakufurahisha na kukupa fundisho pia.

Baadhi ya simulizi kali ni hizi hapa:

1. Ya kwanza ni ya member anaitwa KigaKoyo, hii ni ya mapenzi, ilianzia kwenye uzi wa kula tunda kimasihara. Baada ya kuvutia wasomaji ikabidi iunganishwe itengenezewe uzi kabisa ambao ameupost JBourne59.

2. Ya pili ni ya member anaitwa jooohs. Hii ni ya mambo ya giza. Jamaa baada ya maisha kuwa magumu ilibidi ajaribu upande wa pili wa shilingi lakini alichokutana nacho......

3. Ya tatu na ambayo bado haijakamilika ni ya member anaitwa jerrybanks ambayo pia inahusu mambo ya nguvu za giza. Hii sasa ndio fungamwaka maana ni mkasa unaosisimua mnoo. Huu mkasa unapatikana kwenye uzi wa "kama ulishawahi kushuhudia nguvu za giza live". Kama bado hujaupitia kaupitie huu mkasa hutojutia muda wako.

4. Ya nne ni ya mtukutu Analyse. Huyu jamaa toka azaliwe ni mtukutu mnoo, toka kuangusha kondomu mbele ya darasa mpaka kufukuzwa seminari kwa kuiba nguruwe[emoji851]. Kaipitie hautojutia.

5. Ya tano ni ya mtu mzima Bossless. Jamaa aliyeshuhudia live vita ya kikabila ya Rwanda iloyosababisha mauaji ya halaiki. Inatisha lkn kuna mengi ya kujifunza


Najua hii mikasa imesomwa na watu wengi sana maana ni nyuzi zenye views 40K+ na comments 2K+. Je ipi kati ya hizo true life stories imetisha zaidi?
 
Jerrybank ni muongo hua anatunga visa, Mtoe kabisa. Kisa nachokipenda ni cha mkuu Analyse kina motivation kubwa.
Kwa mkuu kigakoyo stori yake ndani kama unasoma between lines utaona kuna Fasihi/utunzi pia.
Lakini pia stori ya mzee wa bao 23 Jbourne69 iko poa sana unahisi upo Enzi hizo za 70s.
 
Nimesoma ya joohs mpaka nikawa nahisi nimo kwenye story. Jamaa alisimulia mpaka watu wakawa wanaota usiku daahh.

Ila mkuu kuna story moja ya mzee bossless kuhusu vita vya wanyarwanda na yenyewe ni moto wa kuotea mbali.
 
Story zipo nyingi, fanya collection kwanza iliyokamilika

Kuna story ya Maisha ya Analyse n.k

Kama umeamua kuleta collection umiza kichwa na wewe, angalau uorodheshe hata Uzi/stories 15
Jf ni ulimwengu murua sana, una kila aina ya real life time experiencies, yani ukiwa humu unakuwa ni kama unaiona dunia na yanayoendelea ndani mwake.

Kuna true stories kadhaa zimeletwa na wadau humu jf, ni true stories zenye utamu na msisimuko wa hali ya juu. Ni stori ambazo zitakufurahisha na kukupa fundisho pia.

Mbili ni za mambo ya uchawi/nguvu za giza na moja ni ya mapenzi.

1. Ya kwanza ni ya member anaitwa KigaKoyo, hii ni ya mapenzi, ilianzia kwenye uzi wa kula tunda kimasihara. Baada ya kuvutia wasomaji ikabidi iunganishwe itengenezewe uzi kabisa ambao ameupost JBourne59.

2. Ya pili ni ya member anaitwa jooohs. Hii ni ya mambo ya giza. Jamaa baada ya maisha kuwa magumu ilibidi ajaribu upande wa pili wa shilingi lakini alichokutana nacho......

3. Ya tatu na ambayo bado haijakamilika ni ya member anaitwa jerrybanks ambayo pia inahusu mambo ya nguvu za giza. Hii sasa ndio fungamwaka maana ni mkasa unaosisimua mnoo. Huu mkasa unapatikana kwenye uzi wa "kama ulishawahi kushuhudia nguvu za giza live". Kama bado hujaupitia kaupitie huu mkasa hutojutia muda wako.


Najua hii mikasa imesomwa na watu wengi sana maana ni nyuzi zenye views 40K+ na comments 2K+. Je ipi kati ya hizo true life stories imetisha zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
dah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.

ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.

Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.

Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.

Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.


Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.

lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama


picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoja niiongeze hapo juu.
Nimesoma ya joohs mpaka nikawa nahisi nimo kwenye story. Jamaa alisimulia mpaka watu wakawa wanaota usiku daahh.

Ila mkuu kuna story moja ya mzee bossless kuhusu vita vya wanyarwanda na yenyewe ni moto wa kuotea mbali.
 
Jf ni ulimwengu murua sana, una kila aina ya real life time experiencies, yani ukiwa humu unakuwa ni kama unaiona dunia na yanayoendelea ndani mwake.

Kuna true stories kadhaa zimeletwa na wadau humu jf, ni true stories zenye utamu na msisimuko wa hali ya juu. Ni stori ambazo zitakufurahisha na kukupa fundisho pia.

Baadhi ya simulizi kali ni hizi hapa:

1. Ya kwanza ni ya member anaitwa KigaKoyo, hii ni ya mapenzi, ilianzia kwenye uzi wa kula tunda kimasihara. Baada ya kuvutia wasomaji ikabidi iunganishwe itengenezewe uzi kabisa ambao ameupost JBourne59.

2. Ya pili ni ya member anaitwa jooohs. Hii ni ya mambo ya giza. Jamaa baada ya maisha kuwa magumu ilibidi ajaribu upande wa pili wa shilingi lakini alichokutana nacho......

3. Ya tatu na ambayo bado haijakamilika ni ya member anaitwa jerrybanks ambayo pia inahusu mambo ya nguvu za giza. Hii sasa ndio fungamwaka maana ni mkasa unaosisimua mnoo. Huu mkasa unapatikana kwenye uzi wa "kama ulishawahi kushuhudia nguvu za giza live". Kama bado hujaupitia kaupitie huu mkasa hutojutia muda wako.

4. Ya nne ni ya mtukutu Analyse. Huyu jamaa toka azaliwe ni mtukutu mnoo, toka kuangusha kondomu mbele ya darasa mpaka kufukuzwa seminari kwa kuiba nguruwe[emoji851]. Kaipitie hautojutia.

5. Ya tano ni ya mtu mzima Bossless. Jamaa aliyeshuhudia live vita ya kikabila ya Rwanda iloyosababisha mauaji ya halaiki. Inatisha lkn kuna mengi ya kujifunza


Najua hii mikasa imesomwa na watu wengi sana maana ni nyuzi zenye views 40K+ na comments 2K+. Je ipi kati ya hizo true life stories imetisha zaidi?
Pia nyingine ni hizi "ulishawahi kusaidiwa/kumsaidia mtu usiyemfahamu?",hii ina simulizi nzuri sana,pia kuna hii "kwa tuliowahi kufungwa gerezani...."
 
Sijasoma hizo zingine lakin ile simulizi wa mauaji ya Rwanda ilinivutia, maana alisimulia ambayo hatukuwahi kuyasikia. Wacha nizitafte na hzo zingine ambazo zinasifiwa
 
Back
Top Bottom