Wanabodi,
... a quick assessment yangu yangu kwa watia nia 5 wa urais wa JMT kwa tiketi ya Chadema kwa kutumia logical progression.
Kuna uwezekano ugombea wa Lissu ni just a "Pacemaker" tuu, ndio maana Freeman nae kagombea, hivyo sasa mgombea wa ukweli wa urais wa Chadema could be ni Freeman Mbowe!.
Lazarus Nyalandu ni very serious contender, ila he is too gentlemanly kwa kushindana na Magufuli.
Mchungaji Msigwa anatania tuu!.
Dr. Mayrose Majinge - Mwanamke ajitokeza kuwania Urais kupitia CHADEMA. Ni Msomi, Mwanamke wa Shoka, Ana uwezo na Jembe Kweli, ila...
NB. Sio lazima kila kitu kwenye critical thinking na logical progression za any predictions kama hii ya Jicho la Tatu ni lazima kitokee au litimie!, hivyo ikitokea other wise msije kunishukia!
Nawatakia mchakato mwema.
Paskali.
Maelezo mengi kuhusu nani mgombea Urais CHADEMA kwa kutumia nadharia yako ya "Critical Thinking & Logical Progression" siyo tu inafikirisha, haitoi picha ni mtia nia gani atasimamishwa kugombea.
Hata vile, kutokana na matukio ya hivi karibuni, yanayohusu tabia na mwenendo wa Mbowe, M/Kiti wa CHADEMA, nadharia yako inaweza kutumika. Matukio hayo ni kama yafuatayo:
1) Mbowe, bila kumng'unya maneno, anahusika kwa 100% kuamuru Wabunge wake kususia kikao cha Bunge cha bajeti na cha mwisho, kwa sababu dhaifu kujikinga dhidi ya maambukizi ya COVID-19. Kama wabunge, na waheshimiwa, hawakuwa na uwezo binafsi kukataa, ni dhahiri maamuzi ya mwisho ya nani asimamishwe kama mgombea wa Urais, yatakuwa ni yake Mbowe. Iwapo kama kweli ana nia ya kugombea, hao wengine wapo tu kama bendera na kuidanganya jamii kuwa CHADEMA kuna demokrasia. Na tayari wafuasi wake wameanza kuishambulia CCM ati ina fomu za mgombea mmoja tu ambaye ni Rais Magufuli.
2) Kwamba anatuhumiwa kulewa chakali hadi kuteguka mguu, kunatoa picha ya mtu asiyestahili kuwa kiongozi wa ngazi ya Urais wa nchi. Na kama tuhuma hiyo ni kweli, inathibitisha kuwa Msigwa ni mchungaji mwongo maana ndiye, akiwa na Esther Bukaya, aliyetoa taarifa ya Mbowe kushambuliwa ati kwa sababu ya kisiasa. Awali Msigwa alikwisha kukiri kusema uwongo kuhusu Kinana, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, na akaomba radhi. Je, ni tabia ya viongozi wa CHADEMA kusema uwongo!
3) Kufukuzwa kwa Wabunge waliokiuka amri ya kususia bunge, kunaweza kuweka doa kwenye nia ya Mbowe kuwa mgombea wa Urais kwa tiketi ya CHADEMA. Atakuwa na wakati mgumu katika kampeni, iwapo vyama vya upinzani, ikiwemo CCM, vikiamua kuwatumia kumbomoa Mbowe.
3) Wabunge 5 wanawake wamekihama chama, wawili wao wakituhumu kuwepo kwa rushwa ya ngono katika uteuzi ndani ya chama na unyanyasaji. Ni kwa kiasi gani hao waliotia nia ya kugombea Urais wanahusika, ni suala la kusubiri hao watazungumza nini zaidi ya waliyokwisha kusema.
4) Wimbi la kukihama chama kwa viongozi waliokuwa wamechaguliwa, kwenda vyama vingine, kunatoa mwanya wa kuvuja kwa siri za chama kuhusu tabia na mienendo ya hao waliotia nia ya kugombea Urais kwa tiketi ya chama. Yetu macho na masikio kwa kuwa hakuna binadamu asiye na makandokando.
5) Kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kunawaweka katika wakati mgumu watia nia kujieleza kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu.
Nawasilisha.