GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
1. Ni mabadiliko ya kuonyesha kumbe kulikuwa hakuna kabisa Maelewano kati ya aliyelala mazima na aliye Hai akiendelea na Kazi, bali ni Unafiki mtupu ndiyo ulikuwa Umeshamiri japo kuna Mtu kila katika Hafla alikuwa akionekana Kutabasamu na hata Kutuhutubia Watu kwa Kuunga mkono harakati zote za Kiutendaji za kuanzia 2015 mpakae tarehe 17 Machi, 2021.
2. Ni mabadiliko ya Kufyagia mazalia yote ya aliyelala mazima ili aliye Hai aweke anaowaamini na watakaomsujudia pia.
3. Ni mabadiliko ya Kimkakati hasa kwa Kumteua tena Mtu ambaye aliondoshwa mahala fulani mpaka Kutishiwa Bastola kwa Tukio baya la 'Gaidi na Fisadi Matege' mahala fulani Mikocheni hivyo amerudishwa hapo ili Kesi ya Tukio hilo sasa irejewe upya na hatimaye Mhusika akamatwe ili Chanzo cha Mashitaka mengine makubwa yanayomkabili kipatikane na hatimaye nae mwaka huu 2022 akione cha Moto ( Mtema Kuni ) kama alichokiona Mwenzake wa Hai Mkoani Kilimanjaro.
4. Ni mabadiliko ya Kuwafyagia waliokuwa Wanafiki wa Kipindi cha aliyelala mazima na Kuwakaribisha wapenda Uhalisia ila wasiopenda Kukosolewa wa aliyeko.
5. Ni mabadiliko ya Kuwathibitishia Watu kuwa kuishi Magogoni au Chamwino au Zanzibar hakuangalii sana Jinsia ya Mtu bali ni Kujiamini, Uwezo na kuwa Mwanadiplomasia mwenye Ubabe Moyoni kama si Rohoni.
6. Ni mabadiliko ya muendelezo wa Utamaduni wa Kiafrika kuwa Kipaumbele Kikuu ni Kuunda Safu yako ( Genge lako ) ili ule vyema na kwa Kujiamini kabisa Rasilimali Keki zilizopo kwa 95% na matatizo ( mahitaji ) ya Watu uyakabili kwa 5% tu ukiamini kuwa wanaokuja nao watayatatua.
7. Ni mabadiliko hasa ya Kutuonyesha wenye Akili Kubwa kuliko Wao kuwa si kweli kuwa kuna Watu wanakitaka Kiti cha Ufalme kama tulivyodanganywa kama si Kuaminishwa hapa Juzi kati Mkutanoni bali Lengo Kuu ni Kuua Makundi ( Magenge ) hasa Kuelekea Chaguzi ndani ya Nyumba Kuu ya Kitawala ( Kisiasa ) mwaka huu na kwamba japo Zanzibar inatuongoza Machoni mwetu ila uhalisia ni kwamba Pwani ( Bagamoyo na Chalinze ) ndiyo Usukani Kamili wa Tanzania kuanzia Machi 2021 mpaka 2025 na huenda hata 2025 hadi 2030.
Hongereni na Poleni kwa Mabadiliko.
2. Ni mabadiliko ya Kufyagia mazalia yote ya aliyelala mazima ili aliye Hai aweke anaowaamini na watakaomsujudia pia.
3. Ni mabadiliko ya Kimkakati hasa kwa Kumteua tena Mtu ambaye aliondoshwa mahala fulani mpaka Kutishiwa Bastola kwa Tukio baya la 'Gaidi na Fisadi Matege' mahala fulani Mikocheni hivyo amerudishwa hapo ili Kesi ya Tukio hilo sasa irejewe upya na hatimaye Mhusika akamatwe ili Chanzo cha Mashitaka mengine makubwa yanayomkabili kipatikane na hatimaye nae mwaka huu 2022 akione cha Moto ( Mtema Kuni ) kama alichokiona Mwenzake wa Hai Mkoani Kilimanjaro.
4. Ni mabadiliko ya Kuwafyagia waliokuwa Wanafiki wa Kipindi cha aliyelala mazima na Kuwakaribisha wapenda Uhalisia ila wasiopenda Kukosolewa wa aliyeko.
5. Ni mabadiliko ya Kuwathibitishia Watu kuwa kuishi Magogoni au Chamwino au Zanzibar hakuangalii sana Jinsia ya Mtu bali ni Kujiamini, Uwezo na kuwa Mwanadiplomasia mwenye Ubabe Moyoni kama si Rohoni.
6. Ni mabadiliko ya muendelezo wa Utamaduni wa Kiafrika kuwa Kipaumbele Kikuu ni Kuunda Safu yako ( Genge lako ) ili ule vyema na kwa Kujiamini kabisa Rasilimali Keki zilizopo kwa 95% na matatizo ( mahitaji ) ya Watu uyakabili kwa 5% tu ukiamini kuwa wanaokuja nao watayatatua.
7. Ni mabadiliko hasa ya Kutuonyesha wenye Akili Kubwa kuliko Wao kuwa si kweli kuwa kuna Watu wanakitaka Kiti cha Ufalme kama tulivyodanganywa kama si Kuaminishwa hapa Juzi kati Mkutanoni bali Lengo Kuu ni Kuua Makundi ( Magenge ) hasa Kuelekea Chaguzi ndani ya Nyumba Kuu ya Kitawala ( Kisiasa ) mwaka huu na kwamba japo Zanzibar inatuongoza Machoni mwetu ila uhalisia ni kwamba Pwani ( Bagamoyo na Chalinze ) ndiyo Usukani Kamili wa Tanzania kuanzia Machi 2021 mpaka 2025 na huenda hata 2025 hadi 2030.
Hongereni na Poleni kwa Mabadiliko.