ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,753
- 9,575
Habarini wadau wangu,
Natumai mko vyema na mnaendelea na majukumu yenu ya kutafuta ugali wa kila siku.
Ni bora leo tukaongelea jambo hususani lenye kuleta tija katika mstakabari wa maisha yetu. Je, kwanini unasema maisha yamekuwa magumu, vitu vimepanda kama ndege angani ilahali bado uko vilevile haujapanda kama hivyo bidhaa?
Angalia Je ni sehemu au ni mahali gani wewe upo kwa sasa na je hatua gani unaichukua ili kutoka hapo ulipo sasa? Je umeshafanikiwa kwa sehemu fulani katika yale malengo yako uliyopanga kwa mwaka huu? Je ulianzia wapi na unaendelea wapi? Je, umeweka jedwali au umelist yale malengo, miopango yako na je umeshajisemea moyoni kuwa nitaanza na hili na kumaliza na lile?
Je, umeshaona wengine walivyotoboa au toka mahali walipokuwa mwanzo na je umekwenda kujifunza kwao? au umeshachukua hatua gani kuwakabili ili ujifunze kwa yale ambayo wameshapitia wao? Bado muda ungalipo ni vyema kujifunza kwa wale waliiopanda juu sasa ili kuapnda juu pasipo kulalalma kuwa maisha magumu ilihali hatua haujachukua kutoka hapo?
Waweza kujiuliza ni sababu zipi zakufanya usitoboe? Au kutoka ama kuanzisha kitu ambacho kikapanda nawe ukaona nuru au mafanikio kwa hicho?
TUANGALIE SABABU ZA MKWAMO HUO
A) Kuchukualia mambo kiuwepesi ndiko kunafanya ubaki vilevile ulivyo na usipande juu
B) Kuona muda bado unakusubiri wewe
C) Kudhani kuwa uliumbwa kwenye hali hiyo bila wewe kuchukua hatua ya kutoka hapo ulipo
D) kuwa na mawazo mgando kila mara
E) Kuona kuwa yupo mtu atakutoa bila wewe kujisumbukia kung'ang'ana kutoka hapo
Ukiwaza vya juu na kutaka kujifunza kitu utatoboa ila ukitaka uwe mwenye usingizi na kulala na tu utaweza kuona mstakabali wako.
Mithali 19:15-29 " Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake; Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakuwa juu".
Ni vyema kujifunza kwa wengine waliotangulia nakwenda kujua walitokaje na kuwa juu katika kazi, biashara zao na utavuka tu.
ACHA NISEME KUWA PAMBANA, TAFUTA NA TIA BIDIII NA JUHUDI KWA YALE UYAFANYAYO UTAVUKA TU NA KUPANDA JUU.
Wasalaamu
LADYF
CC: Kilimbatzz , Half american , Demi , Mwifwa , Asprin , Bosco Henry, mpwayungu village
Karibuni wadau nipigieni kura sasa sijui ndo utaratibu huu hahaaa.
Natumai mko vyema na mnaendelea na majukumu yenu ya kutafuta ugali wa kila siku.
Ni bora leo tukaongelea jambo hususani lenye kuleta tija katika mstakabari wa maisha yetu. Je, kwanini unasema maisha yamekuwa magumu, vitu vimepanda kama ndege angani ilahali bado uko vilevile haujapanda kama hivyo bidhaa?
Angalia Je ni sehemu au ni mahali gani wewe upo kwa sasa na je hatua gani unaichukua ili kutoka hapo ulipo sasa? Je umeshafanikiwa kwa sehemu fulani katika yale malengo yako uliyopanga kwa mwaka huu? Je ulianzia wapi na unaendelea wapi? Je, umeweka jedwali au umelist yale malengo, miopango yako na je umeshajisemea moyoni kuwa nitaanza na hili na kumaliza na lile?
Je, umeshaona wengine walivyotoboa au toka mahali walipokuwa mwanzo na je umekwenda kujifunza kwao? au umeshachukua hatua gani kuwakabili ili ujifunze kwa yale ambayo wameshapitia wao? Bado muda ungalipo ni vyema kujifunza kwa wale waliiopanda juu sasa ili kuapnda juu pasipo kulalalma kuwa maisha magumu ilihali hatua haujachukua kutoka hapo?
Waweza kujiuliza ni sababu zipi zakufanya usitoboe? Au kutoka ama kuanzisha kitu ambacho kikapanda nawe ukaona nuru au mafanikio kwa hicho?
TUANGALIE SABABU ZA MKWAMO HUO
A) Kuchukualia mambo kiuwepesi ndiko kunafanya ubaki vilevile ulivyo na usipande juu
B) Kuona muda bado unakusubiri wewe
C) Kudhani kuwa uliumbwa kwenye hali hiyo bila wewe kuchukua hatua ya kutoka hapo ulipo
D) kuwa na mawazo mgando kila mara
E) Kuona kuwa yupo mtu atakutoa bila wewe kujisumbukia kung'ang'ana kutoka hapo
Ukiwaza vya juu na kutaka kujifunza kitu utatoboa ila ukitaka uwe mwenye usingizi na kulala na tu utaweza kuona mstakabali wako.
Mithali 19:15-29 " Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake; Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakuwa juu".
Ni vyema kujifunza kwa wengine waliotangulia nakwenda kujua walitokaje na kuwa juu katika kazi, biashara zao na utavuka tu.
ACHA NISEME KUWA PAMBANA, TAFUTA NA TIA BIDIII NA JUHUDI KWA YALE UYAFANYAYO UTAVUKA TU NA KUPANDA JUU.
Wasalaamu
LADYF
CC: Kilimbatzz , Half american , Demi , Mwifwa , Asprin , Bosco Henry, mpwayungu village
Karibuni wadau nipigieni kura sasa sijui ndo utaratibu huu hahaaa.