Jifunze lugha za kigeni ndani ya JF

Jifunze lugha za kigeni ndani ya JF

Habari zenu wandugu. Basi kama kichwa cha habari kinavyojieleza, nimeamua kutaka kumwaga darasa humu jamvini kati ya lugha zifuatazo: KISOMALI, KIARABU, KIFARANSA na KITURUKI.

Hii naona itasaidia sana watanzania mana naona wengi wenu mnajua kiswahili tu na english ya kugongagonga. Hivyo basi inabidi wanajamvi mchague tuanze na lugha ipi? Lugha itakayopata kura nyingi ndiyo hiyo tutakayoanza nayo.

Karibuni wandugu.

Kifaransa tuanze nacho
 
Nafikiri tuanze na Kiswahili, coz bado kuna shida ya matamshi hapa
 
Sawa wandugu kesho jioni panapo majaaliwa nitaanza rasmi na lugha mbili, yani kifaransa na kituruki. Hivyo basi wale ambao wamechagua kifaransa watapata darasa lao na wale ambao wamechagua kituruki watapata darasa lao. ZINGATIO: kama ni kweli una nia ya kusoma moja kati ya kozi hizo mbili si vibaya ukawa na daftari maalum kwa ajili ya kozi hiyo. Karibuni wandugu.
 
Back
Top Bottom