Jiji la Dar es Salaam limekauka, hakuna maji

Limekau kabisa....watu hawana maji, ardhi ni kavu Sana...miti na maua inakauka, ndege nao wamepotea siwaoni....

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Ndege Gani unawaowaongelea hapa ? Au kunguru ,
Maana miaka yote niliyoishi dar ndege ninaowaona kwa wingi ni kunguru tu na Bado wanatia vurugu kama kawa
 
Wacha niendelee kukaa huku huku porini...
 
28 October 2022
Dar es Salaam, Tanzania

Regional Commissioner Amos Makala - "Ahadi ni deni, nitakuja jumanne kuona kama mradi umekamilika "

RC Amos Makala akiwa ameongozana na viongozi wa CCM mkoa wakiwemo bi. Kate Kamba, mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bw. Amos Makala amesema amelivalia njuga suala la maji hivyo Kigamboni atapiga kambi mpaka kieleweke ili maji yaanze kuwafikia wana wa Darisalama...
Source : Dar es Salaam RS Digital
 
Kwani hao Viongozi hawawezi kuzindua huo mradi wa Maji bila kumwaga maji chini?
 
RC Amos Makala akiwa ameongozana na viongozi wa CCM mkoa wakiwemo bi. Kate Kamba, mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bw. Amos Makala amesema amelivalia njuga suala la maji hivyo Kigamboni atapiga kambi mpaka kieleweke ili maji yaanze kuwafikia wana wa Darisalama...
Source : Dar es Salaam RS Digital[emoji23]

Huu mradi uko njia ya Kwenda Mwasonga Kilometer mbili hivi kutoka Kibada, tank limeshakamilika na sasa kazi iliyopo ni ya kutandaza mabomba kuelekea maeneo tofauti

Kwasasa mabomba yalikokwisha kamilika kwa asilimia miamoja mwisho wake ni kibada, yaani yameshatandikwa, yameshachomewa na kufukiwa, kuna line pia inaelekea Ferry kupitia Mjimwema hiyo baadhi ya maeneo nayo imeshakamilika lakini haijakatiza mjimwema
Laini nyingine inatoka Kibada kuelekea daraja la Nyerere hii bado kabida haijafika popote
Kuwapa matumaini ya maji ya kigamboni watu wa dar ni kuwapa matumaini hewa kwakuwa kama yatawahi kufika basi the earliest ni January 2023
 
Kuwapa matumaini ya maji ya kigamboni watu wa dar ni kuwapa matumaini hewa kwakuwa kama yatawahi kufika basi the earliest ni January 2023

Viongozi wa serikali ya CCM hawataki kuwaambia ukweli wana wa Darisalama, matokeo yake wanaibua mjadala mpana kuwa kweli ndani ya wiki hii ya kuanzia tarehe 7 November - 14 November 2022 kuwa tatizo la maji mji mzima wa Dar es Salaam litakuwa limeisha kabisa na kubakia kuwa ni historia.
 
Hapa kigamboni hata sina habari ...kila siku namwagilizia miti yangu...mnawasikiliza wanasiasa sio...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…