Jiji la Dar es Salaam ndio nguzo kuu kwenye kufanikiwa, vijana kimbilieni huko

Miezi 3 TU umebadirika this is Dar, kikubwa uvumilivu km wewe mtoto wa mama usije baki na mama yako uendelee kunyonya
Hasa napendelea biashara
Hapa nilipo nafanya biashara ya duka nikipiga picha huko jinsi kulivyo na muingiliano mkubwa wa watu pesa itakuwepo nitatoboa bila kulima endapo mnayoyasema yana ukweli
 
Unapiga mishe gani
 
Umesema kwamba? Huoni Cha kufanya hakuna mashamba huko au unaogopa utazika pesa chini ya udongo tikiti zote zijae funza umekula hasara? usi-bet kwenye KILIMO utalia
Mashamba yapo sana, Lakini kilimo Cha mvua mtihani hiki.
 
Hongera sana mkuu, mapambano mema
 
Sehemu yoyote yenye watu, mchanganyiko wa jamii mbali mbali ni rahisi kufanya biashara.

Kwa Dar watu ni wengi kuliko majibu ya sensa, watu milioni 5 sio haba

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Ukweli, Lakini dar Kuna harakati ukifanya unapata Lakini harakati kama hizo ukizifanya mikoani hupati kitu.
 
Kama hzo biashara zinalipa, ni kwa nn uliziacha ukaingia kufanya kazi ya ualimu?
Sababu ni Nyingi mno, kubwa Lakini ni wazazi nadhani unaelewa wazazi wetu wa Kijijini, kama ningetia ugumu kwenda kwenye ajira ningetengwa na Kila mtu.
 
Sababu ni Nyingi mno, kubwa Lakini ni wazazi nadhani unaelewa wazazi wetu wa Kijijini, kama ningetia ugumu kwenda kwenye ajira ningetengwa na Kila mtu.
Jibu ni simple tu, hizo harakati ulizokuwa unazifanya ulikuwa unapata pesa ndogo sana zaidi ya mshahara wa mwalimu thus why wazazi wakaona ni kheri uende uwalimu tu, that's all acha kona kona.
 
Kauli mbiu ni tutabanana hapa hapa daslam
 
Jibu ni simple tu, hizo harakati ulizokuwa unazifanya ulikuwa unapata pesa ndogo sana zaidi ya mshahara wa mwalimu thus why wazazi wakaona ni kheri uende uwalimu tu, that's all acha kona kona.
Maana kama unaweza kuanza na laki 7 na progress unaiona...namaanisha kutoka kununua mzigo wa laki 5 mpaka kununua mzigo wa million 2 huoni progress?...utalinganisha na mtu anaepata pesa constant miaka yote?...
 
Sio kweli mkuu.
Kama kweli kwenye business yako ungekuwa unapata pesa ya kutosha kuzidi mshahara wa mwalimu i bealive wazazi wako wangekushauri ukomae na biashara tu badala ya kuajiriwa tena secta yenye mshahara finyu kama uwalimu, lakini kwa vile biashara ilikuendea mlama ukawa huna budi tu kwenda huko u-teacher so acha propaganda za kitoto.
 
Anachosema mleta mada namuelewa vizuri ila ustaarabu wa pesa lazima uwepo mimi nilianza kodogo kidogo tena nilianzia kwenye boda nikahamia kwenye genge na likakua na kua duka genge now nina harakati tofauti ila naamini ningekua mkoa wangu wa kilimanjaro mpka nione faida ya genge au duka inhekichukua mida sana kujitanua ki mtaji dar ni sehemu nziri sana zipo riziki usizotarajia imagine mzigo uko kwenye guta na mtu anaununua wote unajiuliza urudi sokoni au usepe home kwahyo dar kwa mtu anaetaka kutoka aje akiwa kajipanga na ajue anataka nini kwa wakati gani.
 
Sababu ni Nyingi mno, kubwa Lakini ni wazazi nadhani unaelewa wazazi wetu wa Kijijini, kama ningetia ugumu kwenda kwenye ajira ningetengwa na Kila mtu.
Japo umewafunua watu macho na nimekubali ulichoandika ila hapa umefeli kama kweli uliacha biashara iliokua inaingiza pesa vizuri na kwenda ualimu ambao kila mwezi wa tano wanasubiri kusikia mishahara imeongezwa au bado umekwama sana labda kama biashara ziligoma na kwa upambanaji ulioandika sidhani kama ingekua rahisi kuacha biashara hata kama ni ngumu
 
Soma uelewe, nimekwambia dar ni sehemu nzuri ya kuanza kwa mtu asiyekua na kitu, Kuliko huko mikoani. swala la kwenda kwenye ajira ilo ni swala kingine mkuu wengine wazazi wetu huko vijijini wanaona ajira ni Kila kitu kuliko hizo harakati zako, Niko na mtaji wa kutosha kwa Sasa wa kufanya harakati Lakini location nilipo ndio naona kama harakati sizisomi....Niko njiani kurudi huko mambo yakitiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…