The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Badala ya kubana matumizi/ kuondoa matumizi mabaya wakati huu ambao misaada imesitishwa mathalani sekta ya afya kutoka USAID fedha kama hizi zingesaidia kuziba gaps zinanunuliwa CCTV camera ambazo ukitokea uhalifu hazitoi msaada wowote na kukaa kama mapambo tu... mfano tukio la Lissu 2017, Camera zilikuwepo lakini siku hiyo hazikufanya kazi sasa hizi nazo zinaenda kusaidia nini kama kukiwa na matukio zinachakachuliwa?
======
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema Jiji la Dodoma kwa mwaka huu wa 2025 limetenga bajeti ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuweka kamera za ulinzi (CCTV Camera) katika barabara za jiji hilo.
Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Anwani za Makazi katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete Jijini Dodoma, Senyamule amesema hatua hiyo ni tafsiri ya kuendelea kuunga mkono operesheni iliyofanyika ya anwani za makazi kwani kupitia camera hizo usalama na utulivu utaongezeka na kuimarika.
Senyamule amebainisha kuwa kamera hizo zitalinda miundombinu ya mawasiliano, kwani kumekuwa na changamoto ya wizi wa nguzo za anwani za makazi, hivyo wizi huo utadhibitiwa.
======
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema Jiji la Dodoma kwa mwaka huu wa 2025 limetenga bajeti ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuweka kamera za ulinzi (CCTV Camera) katika barabara za jiji hilo.
Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Anwani za Makazi katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete Jijini Dodoma, Senyamule amesema hatua hiyo ni tafsiri ya kuendelea kuunga mkono operesheni iliyofanyika ya anwani za makazi kwani kupitia camera hizo usalama na utulivu utaongezeka na kuimarika.
Senyamule amebainisha kuwa kamera hizo zitalinda miundombinu ya mawasiliano, kwani kumekuwa na changamoto ya wizi wa nguzo za anwani za makazi, hivyo wizi huo utadhibitiwa.