Jiji la Mbeya: Mfupa Mgumu kwa Makonda na CCM

Jiji la Mbeya: Mfupa Mgumu kwa Makonda na CCM

Mkuu tujadili hili suala kwa Hoja!

1. Njia ya barabara nne inajengwa wapi? na kwa maelezo yake ilitakiwa iwe ina pitika sasa. hata hivyo hiyo barabara ilianza kuboreshwa tangu makambako mpaka Igawa. mbeya hawakufika ila kulikuwa na mpango tangu enzi na enzi.. huyo dadako alisema akiingia tu ata anza ujenzi. sasa miaka minne. ujenzi umefika hatua gani.? 😂😂 Wana jua wabongo wengi vilaza, wana subiri waanze ujenzi mwaka 2025.?

2. Jengo la wazazi meta limeanza kijengwa kipindi cha sugu. hata hivyo si sugu wala dadako wote hawahusiki. hata chuo Cha UDSM kina jengwa Mbalizi. kwa taarifa yako kule ni jimbo la Mbeya Vijijini.. Dadako hagusi kule. hata mbunge wa kule haimuhusu hiyo. Hata hivyo hizo hazikuwa ahadi zake kipindi cha kampeni.
Lakini umeona majengo ya Muhimbili, Benjamin na CHATO.. huko kote unadhani ni wabunge wa maeneo hayo wamehusika.??

3. Unaishi mtaa gani na kuna kituo gani cha afya. Hivi unajua mtu akiwa uyole aka umwa ghafla ana lazimika kwenda Igawilo kule juu, anyway hivyo pia vimejengwa kwa hela za Covid. Hahusiki huyo dada enu.

4. stand ya Mkoa kuanza kujengwa baadaye.😂😂. dadako ni mbunge wa mkoa..? hata hizo barabara nne walia saini kwa mbwembwe pale kabwe zipo wapi? usiamini saaana story za baadaye.

5. Maji ya Mto kiwira .... mradi ulianza kipindi cha Sugu. ila hayajafika mpka leo. ila dadako ali jirecord kipindi ni naibu spika eti aliulizia bungeni.. basi hiyo clip akawa ana tereza nayo wakati wa kampeni.😂😂

6. Shule kila mtaa... 😂??. una changanya mtaa, kata, kitongoji na tarafa.. mtaa wa sokoni uyole kuna shule gani imejengwa, kata ya Ghana shule ipi ime jengwa.?

Hebu jaribu ku compare MBEYA Chato, mbeya na Dodoma, Mbeya Na Tanga.
hata Sumbawanga soon wata wazidi. wana barabara nne wale..

MBEYA WAKATI WA MVUA MATOPE, WAKATI WA KIANGAZI VUMBI.

Moja haikai mbili haikai.
Hivi unadhani kwa nini Bajaji Nyingi barabarani. sababu ni kuwa hakuna njia mbadala. hata barabara nyingi mbadala zilijengwa kipindi cha Sugu.

Kwa maslai mapana ya JiJi Letu.
Tupaze sauti , Maendeleo yaje. Kama Mama na Dada haziivi tujue moja.
Mtu akitoka Tukuyu na anataka kwenda Mjini, hana haja ya kupitia Uyole, kuwe na barabara ya mkato. mtu anaye ishi Veta na anafanya kazi Uhindini hana haja ya kupita Mwanjelwa.. Hiyo ndiyo MIZUNGUKO ...

Umeongea point tupu mkuu ila watakuja wanyakyusa wanaojua Mbeya ni Uyole tu watakupinga!

Jiji la Mbeya lingegawanywa katika halmashauri mbili ili kurahisisha maendeleo,jiji la Mbeya ni pana sana aisee kwa bahati Mbaya wafanya maamuzi wanaijua Mbeya barabarani tuu(TANZAM).
 
Tumeona ziara ya Comrade Makonda MNEC na mwenezi wa CCM Taifa maeneo mengi ya nchi.

Hata tuliokuwa tuna muona Makonda kama muhalifu (mwenye kudhulumu haki ya kuishi) sasa tuna muona shujaa.

Ukiachana na kuwa watu wengi wana angalia vi clip ambapo vinaonesha jinsi anavyo tatua migogoro kwa ufanisi papo kwa papo, lakini ukifuatilia mikutano yake uta baini ajenda zake hizi pia.

1.Na yeye ni chawa wa mama, ana jitafutia nafasi ya juu zaidi. Anajikomba komba. Ila anawasema wenzake.

2. Ana jijenga yeye, muda wote ana jisifia yeye.. Kauli zake ni kama Makonda kaletwa na Mungu. bila makonda msingejua haya, walifanya makosa kunipa Uenezi, Watu wana taka kuniua, Watumishi wazembe wakisikia Makonda wana tetemeka.
Jamaa ni so grandiose

3. Anacheza ngoma ya wapinzani, kuwavuta kwenye mijadala yake, hasa Tundu Lisu. nawapongeza walivyo mpuuza. Muda mwingi ana tumia kuwapiga Vijembe.

4. Makonda ni yule yule, mwenye uadui na visasi. Mara zote analaumu kuwa ilikuwa ale shavu muda mrefu, ila kila jina lake likipelekwa kwa mama kuna watu wana fungua kesi kuwa eti kadhulumu nyumba (nadhani anamsema boss wa Yanga). "Nmekaa miaka mitatu nje ya mfumo, walikuwa na nafasi ya kunimaliza, sasa hawaniwezi"

TURUDI KWENYE MFUPA MGUMU JIJINI MBEYA
Kulikuwa na mambo kadhaa


Kwa sasa Jijini Mbeya kuna malalamiko ya kificho na bayana kuhusu utendaji Mbovu wa dada Spika. Miaka yake hana cha kujivunia zaidi ya matamasha na jogging.

Kwa kipindi chake cha miaka minne sijui ana jivunia nini, mi natamani nije nimsikilize. anasemaje?

Mitaani hata wale chawa wake maarufu wame ishiwa hoja. wana shindwa kumpamba tena.

Jiji la Mbeya lina asili ya kuongozwa na wapinzani kwa miaka mingi. huenda hii ilipelekea kutopewa kipaumbele. Daladala za kule zilikuwa zina itwa Mzunguko kwa maana ikianza stand kuu ni kuzunguka tu mpka igawilo, hakuna barabara za rami za mitaani tofauti na hizo barabara kuu (Moja ya kwenda dar, nyingine Malawi)

Alipoingia Sugu nadhani alikutana na Upepo wa Bank ya Dunia kujenga barabara za mitaani. kilometers nyingi Zika tandazwa akajipatia sifa.

Wakati wa shujaa mwenda zake, jiji likatengwa likawa ukiwa, hakukuwa na miradi mikubwa.. na mwenda zake akiwa uyole mahali ambapo alizomewa na kulazimishwa kuimba "mabadilikooo Lowasaaaa...." kipindi cha kampeni.

Sasa kawa Rais akawachana "Mlikosea na mnajua mlipo kosea, Mwaka 2020 msifanye tena makosa" Kwa hiyo hata kampeni za dada zika jikita hapo, Mbeya jini hamna Connection ndiyo maana hampewi maendeleo ikawa ni kuwa atakapo chaguliwa jiji lita pendeza tena, zita jengwa barabara nne (Hii ni plan ya kitambo sana, ila kwa kuwa wabongo wengi tuna utapia mlo wa kufikiri tuna ona kama ni kweli dada spika anaweza akajenga barabara nne kwa amri yake), pia waka aminisha watu kuwa mitaani barabara zitajengwa. Jiji litakuwa Evergreen

Intelligence ya CCM nadhani walijua kuwa Mbeya pagumu, Alipo fika makonda akabadilisha mtindo badala ya kusoma mabango, eti yeye ndiyo akawa ana msismamisha mtu na kuanza kumnaga.. akaamua kumtoa kafara meneja wa TARURA Mkoa.. ajieleze kwa nini barabara hazijengwi. " HILO SWALI ALIPASWA KUULIZWA MBUNGE, kwa sababu ndiye aliye ahidi.

Pamoja na promo kuubwa walio ifanya, bado hakukuwa na watu wengi. Wapinzani wakija kufanya maandamano yao pale wata pata watu wengi zaidi.

Amepita Mbeya bila kutatatua wala kuelezea Mambo magumu.. alikuwa na cheap Politics.

Ni Wakat wa CCM mbeya kuji tafakari na kuchukua Hatua kama wana nia ya kuendelea kuliongoza. Kama Sugu atakuwa makini na uchaguzi ukawa siyo uchafuzi, Jimbo lipo wazi.

Mbeya ni mfupa Mgumu.
Kuna kazi za kuwapa wajinga na hao ndio wanaziweza ukimpa mwenye akili hawezi. Kazi anayofanya Makonda aniweza yeye ndio maana Samia hafanyi hiyo kazi.
 
Sawa wasalimie Mama John, Kabwe, Igowole, Mwanjelwa na Forest bila kusahau Block T na Mwakibete
 
Pumbavu,mijitu ya huko ni kipumbavu na ilimradi inishe ndio maana ujuaji umefanya limji lenu Lowe la kipumbavu sababu ya ubishi usio na Tija.
We Mp.mbavu jaribu kuficha Upum.bavu wako .
kumbe haupo Mbeya..?
yaani jiji liwe la kipumbavu sababu ya mijitu ya huko?! we upo wapi?!
Nani kakudanganya Mbeya jiji kuna ujenzi wa barabara Nne una endelea.?!
Kumbuka Mbalizi siyo Mbeya Jiji.
 
We Mp.mbavu jaribu kuficha Upum.bavu wako .
kumbe haupo Mbeya..?
yaani jiji liwe la kipumbavu sababu ya mijitu ya huko?! we upo wapi?!
Nani kakudanganya Mbeya jiji kuna ujenzi wa barabara Nne una endelea.?!
Kumbuka Mbalizi siyo Mbeya Jiji.
Anafikiri kila mtu ni mji.nga kama yeye
 
Unaandika vitu vya kufirika labda kwa mtu ambaye hayupo mbeya ndio atakuelewa. Ni kweli awamu ya kwanza ya kugombea kwa JPM watu wengi hawakuwa upande wake kutokana na hali ya ccm kwa kipindi hicho ila sio awamu ya 2020.

Unavyoona nyomi ya Makonda sasa ni kwasababu anatumia JPM style na nyie kama mnataka muwe na nyomi tumieni hiyo style japo wananchi hawawezi waelewa coz ndio mliyokuwa mkimpinga nayo. Mama alikuwa anawasare akawavutia pumzi kawapa tume huru kisha kawaletea JPM style ambayo ndio wananchi wengi wanaitaka sasa hivi mnatatapa tu na propaganda.

JPM style, kisha akaishia kupora uchaguzi. Nimecheka vibaya.
 
Si na wewe huwa unajinasibisha kama mtu wa Mbeya?
Kumbe huwa ni fix tu?!
Fala sana
Mpuuzi kabisa
Hufai kwa lolote.
We ni hasara kwa Taifa letu.
Kwetu ni Njombe,nawateteaga tuu Kwa sababu ndio Mkoa mkoa mkubwa Nyanda za Juu Kusini ila haiondoi ukweli kwamba huko kuna watu wajuaji wa upumbavu.
 
Kwetu ni Njombe,nawateteaga tuu Kwa sababu ndio Mkoa mkoa mkubwa Nyanda za Juu Kusini ila haiondoi ukweli kwamba huko kuna watu wajuaji wa upumbavu.
Kwa hiyo majibizano ya mtandaoni ndio yamekufanya ututukane wote?au u negativity wetu dhidi ya ccm ndio upumbavu kama ilivyo kwa mikoa mingine mikubwa?tutawaiga nyie wenye maendeleo hata kwa mtindo wa uchawa!
 
JPM style, kisha akaishia kupora uchaguzi. Nimecheka vibaya.
Hakuna uchaguzi ulioporwa hizo ni theory tu. Kila mkishindwa kwenye uchaguzi hamuishi visingizio, badala yakuangalia mlikosea wapi mnatafuta visingizio. Kwa style yenu ya kupinga kila kitu mnategemea mtamshinda nani kwenye uchaguzi. Mpaka sasa hata presisential canditade wenu kwenye uchaguzi wa mwakani haeleweki halafu mkija kugaragazwa kwenye uchaguzi mnadai mmeibiwa.
 
Back
Top Bottom