Jimbo la kigamboni halina uwakilishi tangu Dr.Ndugulile afariki

Jimbo la kigamboni halina uwakilishi tangu Dr.Ndugulile afariki

Kwa ufahamu wangu, Kwa sheria za tume ya uchaguzi, hilo jimbo uchaguzi unapaswa kufanyika, na kwa sasa michakato ya uchaguzi ilipaswa iwe imekamilika.
Vyama vya siasa havina interest au vimekata tamaa au vimesusa?

Vyama vya suasa ndio wadau wa chaguzi hizo, sisi wananchi hatuwezi kuishinikiza tume ifuate sheria, ila vyenyewe vinaweza, lakini sijasikia hata vyombo vya habari kuandika au kuuliza.

Vilipaswa viwe vimeanza heka heka za kampeni na uchaguzi, hata mbunge akidumu wiki mbili, chama kitapata ruzuku, na mbunge atalipwa kiinua mgonho cha milioni 500.

Sielewi kwanini havichangamki.
 
Mbunge ww ccm hata asipokuwepo hakuna madhara, maana michango ya wabunge wa ccm hudhibitiwa na party caucus ya chama, hivyo awepo asiwepo ni sawa tu. Na uchaguzi ukifanyika ni kupoteza muda, kwani mbunge wa atatangazwa kimabavu. Na pia ni kutoa fursa kwa vyama vya upinzani kuamsha hisia za watu dhidi ya ulegelege wa ccm, na wizi wao wa kura.
Kwa maana hiyo vyama vingine ndio vinaogopa uchaguzi kwasababu vinajua havita shinda?

Sasa itakuwaje October 2025?
 
Majimbo yenye uwakilishi yana nini Cha ajabu?
wabunge wanalipwa milioni 500 za kiinua mgongo.

Pesa za mfuko wa jimbo zinamsimamizi ambaye ni mbunge.

Jimbo lina muwakilishi bungeni.
 
Kwa maana hiyo vyama vingine ndio vinaogopa uchaguzi kwasababu vinajua havita shinda?

Sasa itakuwaje October 2025?
Vyama vingine ndio vinapanga uchaguzi usiwepo? Na kwa taarifa yako Tanzania hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
wabunge wanalipwa milioni 500 za kiinua mgongo.

Pesa za mfuko wa jimbo zinamsimamizi ambaye ni mbunge.

Jimbo lina muwakilishi bungeni.
Unajua utaratibu wa kuzitoa pesa za mfuko wa jimbo, au ukisikia msimamizi ni mbunge basi unadhani ndio mwenya maamuzi yote?
 
Hiyo no reform no election ilipitishwa na vikao halali vya cdm Freeman Mbowe akiwa bado mwenyekiti. Ila sasa Lisu ndio anaipazia sauti sana.
Kwa hiyo ndio kusema chadema haina interest na jimbo la kigamboni au hiyo no reform no election ina pinga uchaguzi?
Vipi vyama vingine, na tume inasemaje inakubali no reform no election?
 
Hii ina uhusiano gani ma huu ubunge wa kigamboni kaka? Nimeoma kwa haraka sikuona uhusiano wowote, naweza kuwa sikuelewa au nime ruka maana.
Kuna watu wana kitu kinachoitwa inquisitive, the urge to know, wewe umeuliza swali, ukajibiwa na link, ungekuwa inquisitive, ungefungua hiyo link, ukishindwa ku connect ndipo unauliza.
P
 
Kuna watu wana kitu kinachoitwa inquisitive, the urge to know, wewe umeuliza swali, ukajibiwa na link, ungekuwa inquisitive, ungefungua hiyo link, ukishindwa ku connect ndipo unauliza.
P
Nimefungua nikaisoma, ndio maana nikakuuliza kaka.
 
Kwa hiyo ndio kusema chadema haina interest na jimbo la kigamboni au hiyo no reform no election ina pinga uchaguzi?
Vipi vyama vingine, na tume inasemaje inakubali no reform no election?
Hakuna msemaji wa hivyo vyama hapa, sisi ni members wa jf, sio wasemaji wa chama chochote cha siasa.
 
Hakuna msemaji wa hivyo vyama hapa, sisi ni members wa jf, sio wasemaji wa chama chochote cha siasa.
Nimeuliza general sikumaanisha wewe ni msemaji wavyo, au tume.
 
Nimefungua nikaisoma, ndio maana nikakuuliza kaka.
Then tatizo ni uelewa!. Umeuliza
Sasa wananchi wanawakilishwaje muda huu, au wanaadhibiwa kwa mbunge wao kufariki kipindi kibaya?
Nitakujibu kwa link Ushauri wa bure: CHADEMA iachane na issue ya Wabunge wake 19, iwasamehe waendelee na Ubunge wao. Kwa muda uliobakia kuwatengua hakuna maslahi yoyote!
Ukiifungua unakutana na jibu la swali lako.
Wanabodi

Ibara ya 49 (5) ya Sheria Mpya ya Uchaguzi inasema (5) Endapo uchaguzi mdogo unatakiwakufanyika na tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge imetangazwa au imejulikana kwa mujibu wa matukio yaliyo ainishwa katika Ibara ya 90(3) ya Katiba, uchaguzi mdogo hautafanyika katika muda wowote wakati wa kipindi cha miezi kumi na mbili mara tu baada ya tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge.

Hivyo nashauri Chadema iachane na hili jambo, kwa muda huu uliobakia kabla ya kuvunjwa kwa bunge, hakuna tena uchaguzi mdogo wowote,
P
 
Yes
Kwa mujibu wa Ibara ya 49 (5) ya Sheria Mpya ya Uchaguzi inasema (5) Endapo uchaguzi mdogo unatakiwakufanyika na tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge imetangazwa au imejulikana kwa mujibu wa matukio yaliyo ainishwa katika Ibara ya 90(3) ya Katiba, uchaguzi mdogo hautafanyika katika muda wowote wakati wa kipindi cha miezi kumi na mbili mara tu baada ya tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge
P
Hili nimelielewa, kumbe sheria zimefunga mlango.
 
Back
Top Bottom