Jina la mdudu huyu kwa viluga please: Nina shuhuli nayo

Jina la mdudu huyu kwa viluga please: Nina shuhuli nayo

kwetu hawapo kwa hiyo hana jina. Labda la kiswahili la kobe.
 
Inkuru-Kikurya

Nilikuwa tarime muda si mrefu. Nilifurai sana nilipokuta babu anaitwa Sokulu. Kama kwetu kabisa. Au sikusikia vizuri?

Ningedhani hata huyu tutafanana.

Sisi kwetu Kobe anaitwa = In'gobe. Lakini haziwi kubwa kama huyu. Vinakuwa vidogooo.
 
mmh...uyu naye. kobe si kiswaili icho. nimesema naomba viluga.

Kwa hiyo kiswahili sio kiluga?
Viluga ni nini?
Huelewi kuwa kiswahili ni luga ya waswahili?
Kimakonde ni lug(h)a ya wamakonde.
Kinyamwezi ni kiluga ka wananyamwezi. Kihehe, kichaga ...

Kiswahili kimepewa hadhi ya kuwa kiluga/lugha ya Taifa vilevile lakini haiondoi kuwa kenyewe ni kiluga pia.
 
Kwa hiyo kiswahili sio kiluga?
Viluga ni nini?
Huelewi kuwa kiswahili ni luga ya waswahili?
Kimakonde ni lug(h)a ya wamakonde.
Kinyamwezi ni kiluga ka wananyamwezi. Kihehe, kichaga ...

Kiswahili kimepewa hadhi ya kuwa kiluga/lugha ya Taifa vilevile lakini haiondoi kuwa kenyewe ni kiluga pia.


aah bwana ondoka hapo unanchanganya mie!
 
Cameroun anaitwa Etoo'

ya kweli hayo mwaya? basi mwenzio 1985 nilishiriki mkutano fulani wa kimataifa pale Kinshasa. Tukawa tumepelekwa eneo fulani linaitwa Something a' Nsele; kitu kama hicho. Pama mjengo mkubwa sana wa mikutano mali ya Mobutu Sese Seko walisema. Pana mto mkubwa sana unapita kwa nyumba ya jengo.

Basi alitokea mama mmoja kabeba uyu mdudu kwenye kapu la kusuka (yale makapu ya vipande vya matete ambayo karibu kila kabila la kibantu wanajua kusuka). Si watu walianza kunyang'anyiana wanataka kununua---eti chakula! Aise.....nilishangaa?!
 
Nilifikiri unapata shule...haya bana usijichanganye.
Kiswahili si kiluga bali ni liluga!

ha ha ha...haya bwana Nonda. Sijui bwana? sijui bibi utajazaga mwenywe ukouko. Usiku mwema.
 
....
Basi alitokea mama mmoja kabeba uyu mdudu kwenye kapu la kusuka (yale makapu ya vipande vya matete ambayo karibu kila kabila la kibantu wanajua kusuka). Si watu walianza kunyang'anyiana wanataka kununua---eti chakula! Aise.....nilishangaa?!

Unashangaa watu kula uyo mdudu?
Umeshaona watu wa Tanzania wanaokula wo,wo,woh(mbuzi wa Mbeya)? https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/273150-nimekula-nyama-ya-mbwa-5.html
Wanaokula nyoka je? Wanaokula panya?. mamba? mende? vyura? utumbo wa ng'ombe, mbuzi.kuku? wanaokula nguruwe?

Kuna mdudu ambaye haliwi ulimwengu huu? usifungue links kama una moyo!
Binadamu analiwa link Some Thailand Cannibals 'Eating' A Human (Gruesome Pictures - Viewers Discretion Advised!) - Ethnic, Racial, Or Sectarian Politics - Nairaland

link Thai Cannibal Kills And Eats Sons Thought They Were Pigs - Wazaap!


Kama "watu" wanakula the mother of all dudus, kuna ambacho hakitaliwa?
Kuna dugu yetu hapa jf anatoa dawa ya kunywa mkojo....nguluwe anakula ile kitu inatoka kwa mata.ko na ipo mtu inapenda hii kitimoto kuliko nyama ingine yoyote!! Utashagaa ,mwisho utashindwa kushangaa.
 
Unashangaa watu kula uyo mdudu?
Umeshaona watu wa Tanzania wanaokula wo,wo,woh(mbuzi wa Mbeya)? https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/273150-nimekula-nyama-ya-mbwa-5.html
Wanaokula nyoka je? Wanaokula panya?. mamba? mende? vyura? utumbo wa ng'ombe, mbuzi.kuku? wanaokula nguruwe?

Kuna mdudu ambaye haliwi ulimwengu huu? usifungue links kama una moyo!
Binadamu analiwa link Some Thailand Cannibals 'Eating' A Human (Gruesome Pictures - Viewers Discretion Advised!) - Ethnic, Racial, Or Sectarian Politics - Nairaland

link Thai Cannibal Kills And Eats Sons Thought They Were Pigs - Wazaap!

Aise mineogopa kufungua izo links nina kikombe cha kahawa hapa mezani.

Ila nikupe hii: kule kwetu panya ni chakula muhimu sana jamaa yangu. na mimi hii leo ukinipatia panyapori, namuoka vizuri, namnyunyizia chumvi na pilipili halaf namla wakati ukiangalia. Wala sitakuwa na chembe moja ya aibu! Wale panyapori ni watamu aise. Miaka ya 1960 wakati nakua kijijini moja ya stadi za maisha ilikuwa kujua mitego mbalimbali. Kabila langu tuna historia ya uwindaji, ufugaji na kilimo. Mimi nilikuwa fundi wa mitego ya panya, ndege njiwa na kware. Bibi yangu mzaa baba alikuwa fundi sana wa mitego ya ndege kwa ulimbo. Alinifundisha ufundi ule. Sema sasa nimeishajichanganya sana hapa dar ufundi ule unapotea sasa.
 
Aise mineogopa kufungua izo links nina kikombe cha kahawa hapa mezani.

Ila nikupe hii: kule kwetu panya ni chakula muhimu sana jamaa yangu. na mimi hii leo ukinipatia panyapori, namuoka vizuri, namnyunyizia chumvi na pilipili halaf namla wakati ukiangalia. Wala sitakuwa na chembe moja ya aibu! Wale panyapori ni watamu aise. Miaka ya 1960 wakati nakua kijijini moja ya stadi za maisha ilikuwa kujua mitego mbalimbali. Kabila langu tuna historia ya uwindaji, ufugaji na kilimo. Mimi nilikuwa fundi wa mitego ya panya, ndege njiwa na kware. Bibi yangu mzaa baba alikuwa fundi sana wa mitego ya ndege kwa ulimbo. Alinifundisha ufundi ule. Sema sasa nimeishajichanganya sana hapa dar ufundi ule unapotea sasa.

Sasa mkuu
Kama unakula panya pori, kwa nini ulishangaa watu wanaotaka kununua kobe kama mboga/kitoweo(nyamachoma)? Soma post #32 .

Mimi hapa ninapoishi niko karibu na pori na panya wanakuja hapa nyumbani kunitembelea. Nitakualika uje utege mitego yako ili tutengeneze nyamachoma(kuoka msosi wa nguvu).
 
Sasa mkuu
Kama unakula panya pori, kwa nini ulishangaa watu wanaotaka kununua kobe kama mboga/kitoweo(nyamachoma)? Soma post #32 .

Mimi hapa ninapoishi niko karibu na pori na panya wanakuja hapa nyumbani kunitembelea. Nitakualika uje utege mitego yako ili tutengeneze nyamachoma(kuoka msosi wa nguvu).


hilo nalo neno mkuu wangu.
Mboga mbili naweza kula na ugali mkubwa nikaumaliza pasipo shida
ni Mlenda, au panyapori. Itabidi tu uniPM nijue unaishi karibu na pori gani.
 
hilo nalo neno mkuu wangu.
Mboga mbili naweza kula na ugali mkubwa nikaumaliza pasipo shida
ni Mlenda, au panyapori. Itabidi tu uniPM nijue unaishi karibu na pori gani.

Nimejaribu mara sita kuku-PM, napata ujumbe kuwa the ID of the member has been changed. Lakini naishi karibu na pori la Mabwepande. Ukifika kwenye mbuyu karibu na mamantilie/mamalishe uliza tu,kwa Nonda wapi watakuleta nyumbani.
 
Back
Top Bottom