Jina lipi la utani mlimbatiza baba yako kutokana na ukali wake?

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Katika familia nyingi za kiafrika ukali kutoka kwa mzazi mmoja au wawili, hasa baba imekuwa kama desturi kwa baadhi ya familia.

Hali hiyo inaweza kusababisha watoto kuwa na hofu na wasiwasi badala ya upendo na usalama kutoka kwa wazazi.

Mfano mzuri ni pale baba anaporudi nyumbani kutokana na ukali wake, watoto wanakimbilia chumbani au nje.

Tuandikie katika familia yenu mlimbatiza baba jina gani? Na kwanini?

Si kwetu tulikuwa tunamuita Osama
 
Kuna mzee mmoja hapa jirani yangu watoto wake wanamuita Mtalebani. Nilikuwa sielewi ila sasa kama nawaelewa wale vijana.
 
Tutakuwa na baba mmoja nini Mkuu? Na kwetu alikuwa na jina hilo, na ndvu alizokua nazo ni mule mule!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…