EPISODE 10
A TRUE STORY BY INSIDER
Niliamua kuzima simu kwasababu Mama J angeendelea kupiga afu sipokei hasira zingezidi kumpanda. Niliona kuzima simu ndo solution na inabidi nirudi home jion atlist hasira zitakua zimepungua hivyo itakua rahisi kuyajenga.
Niliwaza pale nje nitumie mbinu ipi kukiepuka hiki kikombe lakini sikuweza kupata majibu ya haraka maana kila mbinu niliona inakuwa ngumu kama inaleta ukakasi.
Nikawaza Mama J lazima mawazo yake mimi nilikua na mwanamke na kutokupokea simu zake na kujibu text ndo kunazidi kuniweka kwenye wakati mgumu. Nilijiona na hatia pia kwa jambo nililofanya.
Nilirudi ndani lakini this time nilikua nimenyong’onyea sana, Iryn akaniuliza “are you ok?” nakuona toka umetoka nje kama umebadilika ghafla sana. Nikamwambia niko sawa usingizi tu na uchovu.
Nilikaa na Iryn mpaka jion saa 10 na yeye alikua anakwenda kwa Grizmann, akanambia atarequest mimi nikapumzike tu. Na mimi nikatoka kuelekea home.
Nilivyofika Mwenge nikapata wazo nipitie sokoni nikanunue Kuku wa kienyeji, Tegeta ndo ilikua ni sehemu sahihi ya kupata kuku, hivyo nikachoma mafuta mpaka kule. Kweli nikapata jogoo mkubwa mzuri aliyenona kwa 25,000/=. Nikanunua nyanya sado moja, nikanunua vitunguu sado moja, nikanunua hoho sado moja, nikanunua na karoti sado moja, nikanunua na mahindi mabichi 10.
Ukiwa mwanaume inatakiwa uwe na mbinu sana, na mimi nilikua najua wife mawazo yake kichwani mimi nilikua na mwanamke, hivyo inabidi nimprove wrong. Nikarudi home na muda huo ilikua ni saa 11 jioni tayari, nilivyofika home nje ya geti kuna mti pale, nikapark gari pale.
Nikafungua boneti, nikavua t-shirt afu nikafutia engine, sikuishia hapo nikapaka na coolant si mnajua coolant ina wekundu?, bhasi nikachokonoa na oil ya kwenye engine nikapaka kwenye jeans na mikononi. Ile T-shirt nikaipaka na vumbi mgongoni, kilikua ni kitendo cha dakika tu. Niliamua kucheza kama Rambo anavyo move kwenye traps.
Nilifungua geti huyo mpka usawa wa kwetu nikapark gari, nikashuka afu nikakaa kwenye ngazi za kibaraza.
Sasa Mama J alivyoona siingii ndani akatoka nje, ile kumwangalia alikua ananitizama kwa macho makali sana, nikaona hasira zimeanza mpanda.
MIMI: Mke wangu Unaendeleaje, badala uje unipokee wewe unaniangalia tu.
MAMA J : Ningekua mimi ni mke wako hata usingethubutu kunifanyia mambo ya ajabu, umenizalisha sahivi unanichezea kama football.
MIMI : Mke wangu kaa chini tuongee, embu niangalie kwanza nilivyo hata hunionei huruma?, kaa chini tuongee nikwambie kilichonitokea.
MAMAJ : Ok nimekaa nakusikiliza
MIMI : Unajua mimi nakupenda sana hata haya yote nayofanya ni kwaajili yako na mwanangu, najua unahasira sana kwa mimi kutokurudi jana, ila naomba ufute hicho unachokiwaza kichwani
MAMA J: Hivi Baba J Are you insane?, umeondoka asubuhi jana unarudi leo jioni. Hakuna cha simu wala nini, hivi unaipenda familia yako?? Hivi ungekuta sisi tumepatwa na matatizo nani wa kulaumiwa?. Mwanaume gani unashindwa hata kujua maendeleo yetu pamoja na mtoto?. Nimekupigia simu zangu hutaki hata kupokea wala message hujibu, unataka mimi nikufikiriaje?. Maana nilishaanza kupata wasiwasi maybe wamekuteka maana matukio ya utekaji kwenye uber ni mengi.
“Haya maneno ya wife yalinichoma sana nilijiona ni mwenye hatia kwa upumbavu wangu.
MIMI: Ni kweli wife ulichosema nimekukosea sana ila kabla ya yote naomba unisamehe sana, ni kweli nimefanya kosa kubwa. Lakini naomba nikuelezee kilichotokea mke wangu.
MAMA J : Nakusikiliza, Go on
“Muda huu dada Junior akawa ametoka nje kunisalimia, nikamwambia atoe vitu kwenye gari.”
Mazungumzo yetu yakaendelea……….
MIMI : Jana nilikua Airport kuna mteja nilikua nimempeleka pale, sasa wakati nasubiri request na simu yangu ilikua chaji imekata nikampa mlinzi wa pale Airport anisaidie kuiboost. Ni mtu ambaye nafahamiana naye sasa wakati anarudi akanambia kuna wateja nimewapata wanaelekea Masaki wapeleke wanaulizia Tax. Alivyo waleta nikawaambia mpaka Masaki ni 50,000/= hawakukataa, ikabidi niwapeleke.
Baada ya kuwapeleka Masaki, wakasema niwapeleke Morogoro muda huo ilikua jioni na mimi sikutaka kukataa lile dili nikawepeleka. Muda huo niko Masaki ndo nakumbuka nimeacha simu kule Airport kwa jamaa, lakini nilikua sina jinsi ikabidi niondoke hivyo hivyo. Tuliingia Morogoro Usiku, wakaomba niwasubiri tu ili turudi wote kesho na muda huo ilikua saa3 usiku ikabidi nikubali. Walinilipia hotel sasa baada ya kula nilisema nikirudi hotelini ningewapigia simu lakini nilivyofika room baada ya kuoga nikapitiwa na usingizi. Pia jana nimetoka hapa home na simu kubwa tu, simu ndogo nimeisahau mezani chumbani.
Leo tumefika Dar saa 9 mchana baada ya kuwapeleka wale wazungu Masaki, nikaenda Airport kuchukua simu yangu, lakini bahati mbaya sikuweza kumpata jamaa. Nimemwulizia kwa baadhi ya watu wamesema yuko off mpaka kesho na wameongea naye akasema simu anayo ila yuko mbali sana, tuonane kesho. Hayo ndo yaliyonikuta mke wangu.
“Nikaona wife kaanza kuingiwa na huruma huku ananiangalia”
MAMA J : Na mbona umechafuka hivo?
MIMI : Gari ilipata shida wakati tunarudi, nikapata fundi tukawa tunasaidiana kuiweka sawa ndomana unaona nimechafuka. Wakati niko Morogoro nikasema nikuchukulie na vitu vya home niliona bei rahisi tofauti na huku Dar.
MAMA J : Mimi nilishaanza kukuwazia vibaya ujue, hujui tu. Jitahidi uwe unafanya mawasiliano mapema. Utakuja kuniua kwa presha, nakupenda sana.
MIMI : Ni kweli mke wangu, ndomana nimekuomba msamaha kwa kilichotokea.
MAMA J : Na huyo mtu mwenye simu yako unamwamini atakurudishia?
MIMI: Sina shida naye maana ni mlinzi wa pale kesho nitaipata.
MAMA J : Mimi nimekusamehe, twende ukaoge. Hio Tshirt ya kutupa tu maana hata utumie jiki sidhani kama itarudi hali yake.
Wife akawa na amani kabisa like “Nothing happened” akaniogesha na akanipa na tunda tamu la Apple. Nikamwambia ajiandae na dada niwatoe out, niwapeleke KFC maana wife anapenda kuku wa KFC.
Tulikwenda pale Mikocheni Plaza, tulivyorudi home nikamwambia wife usifikiri mimi sina mipango, nikafungua droo aangalie “hii ni droo ambayo huwa naweka pesa zangu nazopata kwenye Uber, pesa zote zile nazopata kama dollar, Euro huwa nazitupia humo”. Baada ya wife kuona pesa zilikuwepo mle akajua kweli niko serious.
Siku ya jumapili iliisha hivo ndugu zangu nikawa nimeyamaliza na Mama J kwa amani kabisa. Lakini nikaplan kuwa na mikakati madhubuti ya kuhakikisha sirudii tena ujinga kama huu.
**********
VALENTINES DAY ya 2022 iliangukia jumatatu, nikapata wazo nimcheki Iryn lakini lengo langu mimi ni kumjua deep zaidi. Maana alikua anakutana na watu wakubwa sana yule jamaa yake Grizzmann alikua anafanyia kazi WIZARA YA UCHUMI NA FEDHA ya Ufaransa.
Ile asubuhi nikamtext “HAPPY VALENTINO THE BOSSY LADY” hili ni jina ambalo nilikuaga namwitaga. Ilipita kama 40mins akanijibu “Happy valentine Gentleman”.
“Leo una ratiba gani?”
“Leo nipo Insider vipi unataka nitoa out?”
“Umejuaje? Nataka leo nikusuprise Bossy wangu”
“Sawa nasubiri saprise yako then nina salamu zako kutoka kwa Grizz, badae utazipata”
Baada ya kuwa na uhakika wa appointment nikasema leo lazima nitumie kila mbinu ili nimchimbe deep zaidi. Iryn nilikua namuheshimu sana maana alikua na roho nzuri sana na pia alikua ananipa maisha. Honestly nimeingiza pesa nyingi sana kupitia yeye pia nimepata connection nyingi sana kupitia yeye.
Hii siku sikutoka kabisa home nilishinda nacheza na Junior, ilivyofika jioni nikamwaga wife naenda kufata simu Airport, sababu alikua anajua simu ipo huko hata hakua na shida.
17:00 nilikua nimeshawasili kwa Iryn pale getini. Sababu nilikua nimeshakuwa mwenyeji nilikua nafungua geti naingia ndani. Nikagonga mlango wa Iryn, nilivyoona kimya nikaingia ndani, nikakaa seblen nikasikia mtu anaoga.
Baada ya dk 30 akatoka akanikuta seblen, “sikutegemea kama ningekuta mtu hapa”,
“wakati naingia ulikua naoga”
“Hata hivyo niliacha mlango wazi nilijua muda wowote unaingia ndomana nikaenda kuoga, vipi nimependeza?”
“Hiyo skin imekuaa sana mimi ndo nitakutia aibu leo”
“Ushaanza , so where are you taking me?”
“Saprise”
Hao tukatoka kuelekea parking ile tunatoka nje kuna dada alikua nje, alikua anatuangalia sana, tukamsalimia, Iryn akaenda fungua geti hao tukaondoka.
“Hawa majirani zako wananiangalia sana mpaka najishtukia, jana tu kuna kaka alikua ananiangalia sana”
“Unafikiri mimi na time nao? Humu ndani hatujuani kila mtu yuko busy na maisha yake”
“Majiran mnatakiwa mjuane kama umepatwa na shida usiku au umeumwa ghafla unafikiri nani wakukusaidia?”
“Leo Insider umeongea point sana, itabdi nifanye mchakato wa kuwajua majirani zangu niwe na namba zao”
Niliendesha gari mpaka Coral Beach hotel Masaki, hii ndo sehem niliyoona haitakuwa na watu wengi kwa siku ya valentine. Pia niliona ndo sehemu itakayomfaa Iryn kutokana na status yake.
Tulivyoingia beach tulikuta watu ila sio wengi kivile lakini macho yote yalikua kwa Iryn, alikua kavaa skin jeans ya blue, blauz nyekundu, raba za Airforce black na miwani mieusi but alikua kapendeza sana.
Nilikua nimemshika mkono kuonesha hata mimi na chombo kikali ila ukweli sio dem wangu ni bossy wangu na uzuri wa Iryn hakuaga mtu wa kujionyesha. Bhasi niliangaza macho nikapata sehemu ya kukaa ilikua mwishoni kwenye corner.
Dada alikuja pale kutusikiliza tukaagiza wine ya pamoja na chakula (wakati tunaingia tulikubaliana vinywaji ni juu yangu na chakula juu yake). Baada ya dakika kazaa wine ilifika tukaanza kuipeleka mdogo mdogo. Muda huu tulikua tunapiga story za kawaida tu!, huku tunacheka.
Baada ya dakika 15 chakula kikawasili tukaagiza wine nyingine binafsi huwa naipenda sana “Pearly Bay Sweet Rose wine” hii bhana ni tamu ila huwa inapanda taratibu ina 12% alcohol. Nawapa siri nyingine ya hii wine ni rahisi sana kuwanyegeza dada zetu.
MIMI: “Naona kila mtu anakuangalia Iryn, hata wazungu wanakushangaa jinsi ulivyo mzuri”
IRYN : “Unamwona yule dada kulia kwako?, bhasi yule ndo kafunika hapa”
MIMI : “Mhh kwanza hata robo hakufikii”
IRYN : “Insider hivi mimi unajua najiona wakawaida sana”
MIMI : Ungekua wakawaida hata watu wasingekua na habari na wewe, kwanza angalia yule Bro, yuko na dem wake ila anakuangalia sana”
IRYN : “Grizz anakusalimia na pia nina mzigo wako badae tukitoka nikumbushe nikupe” (Niliona kama Iryn anabadili gia)
Lengo langu mimi kubwa ilikua ni kumjua vizuri ila isingekua kazi rahisi kama anaakili zake, pombe atlist ingemfanya awe confident na kufunguka. Mbinu yangu ilifanikiwa kwani baada ya kuzipeleka wine kwa sana alianza kuongea sana hapo ratio ya glass ilikua ni 4:2 na yeye alikua anakunywa sana.
MIMI : So uliniambia baba yako ameishi Tanzania tangu 1995, yuko wapi now?
IRYN : Baba now yuko South Africa kule ndo home hapa Dar alikua na kampuni zake za Engineering, baada ya Magufuli kuingia Madarakani biashara zake zilianza kufisilika akaondoka kurudi South Africa hata kule pia ana kampuni zake. Hapa bongo kampuni iliyopo ni ya Electronics ndo najua bado ipo, pia anakampuni zingine Kenya zinafanya vizuri. But ukweli I hate my father Insider.
MIMI : Kwanini?
IRYN : My mother died because of my father. Siwezi msamehe kwa hili and he know that.
Alikua ameshika wine yake mkononi na ilikua robo glass akaimimina yote mdomoni, nikamwekea nyingine kwenye glass, Iryn akaanza kunipa mkanda mzima.
“Insider, Mimi nimezaliwa pekee kwa Mama yangu na ni mtoto wa pili kwa baba yangu. Mtoto wa kwanza wa Baba alizaaa mtaani hata mama yake simjui ila nina wadogo zangu watatu (3) kupitia kwa mama mwingine (mamdogo).
Baba yangu alikuja Tanzania mwaka 1995 na akafungua kampuni zake za Engineering. Alifungua Kampuni ya Construction na Electronics, kipindi kile anakuja kulikua na tenda nyingi sana za ujenzi wa barabara na Majengo.
Mama yangu alikuja Tanzania kutoka Ethiopia mwaka 1992 na alikua anafanyia moja ya International organization hapa nchini. Mwaka 1996 ndo baba na mama yangu walikutana na kuanzishisha mahusiano. Mimi nimezaliwa mwaka 1998 pale hospital ya Muhimbili na tulikua tukiishi masaki.
Mwaka 2007 mama alirudishwa Ethiopia kuna kazi alikwenda ifanya, hivyo ikabidi turudi home wote, nikamalizia masomo yangu Ethiopia. Lakini nikiwa bado niko masomoni mama alirudi tena Tanzania 2010 moja kwa moja. Upande wa chuo nimesoma Ufaransa na nimemaliza 2020 ndomana unaona siku ile nilikua naongea kifaransa na Grizz nimekijulia kule, na huko ndo nilikokutana naye.
Wakati niko France nilijiongeza nikaanza kusomea shortcourse za “Body therapy” kama Massaji nk. Niliajiriwa na kampuni moja huko Ufaransa inadeal na masuala ya massaji na pia nilijuana na watu wengi.
November 2020 nilipata taarifa mama yangu anaumwa, ikabidi nirudi Tanzania ndo kujua mama anashida ya moyo na presha ya kupanda. December ndo alifariki hivyo tukazika Ethiopia nyumbani.
MIMI : Umesema mzee alihusika na kifo cha Mama kivipi?
IRYN : Kwa kipindi chote cha Mama kuishi na Baba hakuwai jua kama Baba ana Mtoto wa nje na ameoa mke mwingine. Hizi habari ndo zilimfanya mama apate mshtuko na kumsababishia shida kwenye moyo. Japo nilikuja kujua mama alikua anasumbuliwa na “High blood pressure” kwa muda mrefu, na hili ndo lilisababisha kifo chake.
“Insider order another wine please”
Nikamwita dada nikaagiza wine nyingine, kumbuka hii ilikua ni chupa ya 3 na Iryn alitokea kuipenda sana hii wine.
MIMI : Kwanini mliamua kuzika Ethiopia?
IRYN : Mama alitaka azikwe kule kwao, pia ndo utaratibu wa mila zetu. Hata mimi nikiamua nitazikwa kule.
MIMI : Baba yako alikuwepo kwenye msiba?
IRYN : Alikuwepo ila mimi toka nikutane na mama hospitaal anambie chanzo toka siku ile sikuwai ongea na Baba yangu, hata akinipigia simu sikuwai pokea simu zake mpaka sasa.
MIMI : Na ilikuaje ukaingia kwenye hii biashara?
IRYN : Nina best yangu anaitwa Isabella (code) ndo alinipa idea ya kujifunza “Body therapy” yeye pia ni wa Ethiopia. Sasa baada ya msiba ndo alianza kunitafutia wateja ni ana connection nchi nyingi sana duniani. Wateja wengi huwa ananipa connection, na pia kuna website ambayo huwa nalipia kila mwezi inanisaidia sana kupata wateja. Pia hata haya mahotel makubwa nafahamiana na watu ambao pia wananipa connection. Huwa nakuwa na kazi nyingi sana ujue, zingine huwa nazipiga chini kama hazina benefit, pia napendelea sana kufanya kazi na foreigners sababu ni waelewa, na ni wachache sana ambao nawavulia chupi yangu.
MIMI: Huo mtandao kuna baadhi ya wabongo wapo?
IRYN: Hahaaa Insider bhana, huu ni mtandao kwanza wanaojoin wanahela lazima ulipie dolla $4500. Wenye pesa wanaujua, Insider sahivi huna hela ila ukijapata pesa haya mambo utayajua na hutopata shida, I’m telling you. Ukitaka hata b*tch kutoka nchi yoyote mrembo, atakuja atakupa huduma zote unazotaka ni pesa yako tu. Na mwanamke anayejiunga na huu mtandao lazima awe mzuri au famous, kwa Tanzania namjua mmoja tu sinaga muda wa kufatilia maisha ya watu.
( Huyu alomtaja Iryn Ni moja ya warembo ambaye alihisiwa kutoka na Rozay).
MIMI: Nashindwa kujua jinsi unavyofanya kazi na kwanini uwe siri sana?
IRYN: Insider as I told you, kwanza kwa Mwanaume anayejiunga lazima aweke taarifa zake kila kitu, kama ni biashara au kazi anayofanya. Wakisharidhika na taarifa zake na akubaliana na sheria na taratibu zao ndo wanamfungulia Account. Inachukua almost siku 3 kuwa verified, kama taarifa zako zina walaakini kama criminal records, wanakupiga chini. Ukimeet requirements zao utalipia entrance fee sijajua kwa wanaume ni kiasi gani, ila kwa sisi wanawake kama nilivyokwambia ni $4500. Hizi bei zinatofautiana mimi wakati najoin nililipa hio ila kwa sasa itakua zaidi.
Mwanaume anavyohitaji huduma kutokana na sehem anayokwenda anaingia kwenye web, ataspecify huduma anayotaka then atachagua Mwanamke aliyemwona anafaa kutokana na alichohitaji na sio zaidi ya hapo. Hii web iko very secured na salama sababu hawa jamaa wanapata taarifa za wateja wao kwa muda mfupi sana pale wanapojiunga. Letme show something:
“Palepale Iryn akasimama akaja upande wangu akakaa, akafungua hio website akaweka taarifa zake kwanza kuifungua tu lazima ajipige self then ikidetect kama ndo yeye inafunguka. Akanionesha jinsi ambavyo anabargain na wateja wake tofauti mle ndani”
IRYN : Si unaona kama hyu mshenzi anataka massaji na Sex nimemwambia $10,000, pia sijataka kufanya naye kazi, hii ndo njia ya kuwafukuza watu kama hawa. Ila sometimes inatokea mtu anakubali bhasi unafanya naye kazi kibishi. Nasisi tunalipa commission kutokana na idadi ya wateja tunaopata.
MIMI: Duuh aisee dunia ina mambo, sijawai sikiaga hii ndo wewe unaniambia. Hata kwa wanawake wengine ambao wana hio amount hawawezi kujiunga?
IRYN: Kama nilivyokwambia kwa mwanamke wa kawaida lazima uwe mzuri na uwe atlist unafikia 80% ya apperance yako ukishindwa fikisha hapo unakua disqualified, si mnasemaga “madem kisu” bhasi uwe kisu kweli kweli, sasa hapo ndo utakuta wanawake wanakimbilia uturuki kujitengeneza mwili. Pia lazima uwe na cheti cha mafunzo ya “Body therapy” nk, bila hivo huwezi kubaliwa. Ni wachache sana wanaomeet hizi requirements na wanawake utakaokutana nao huku ni visu kwelikweli. Wewe unaniona mimi kisu sasa uwe unatega pale Hyatt Hotel, siku mojamoja uwe unakwenda pale Level 8, utakuja kuonana na wanawake wazuri hata mimi utaniona takataka.
MIMI: Aisee hatari sana ila bado naamini kwa Tanzania unaingia “Top 3”.
IRYN: Leo nimekwambia mambo mengi sana kuhusu familia yangu, na mambo yangu binafsi. You and I we’ve got something in common, nimetokea kukuamini kwa muda mfupi sana. Anyway lets go I’m tired now, thanks for today.
Niseme tu Iryn alinifungukia sana ile siku alinambia mambo mengi sana, siwez weka yote kwakweli na pia sikutaka endelea muuliza maswali zaidi, ila nilisema nitaendelea kumuuliza taratibu. Maana nilitamani kujua kilichomrudisha Tanzania ni nikipi? na mambo mengine ila nikasema ntajua tu.
Tulitoka hapo tukaclear bill kama tulivyokubaliana awali na pia nikamchukulia mama watoto seafood kama zawadi. Muda huo ilikua ni tatu kasoro mama J alikua kashaanza piga simu.
Wakati tunatoka pale reception kuna dada wakizungu walikutana wakaanza kuongea sasa mimi sikutaka kumsubiri nikaamua kwenda kwenye gari, nikawaacha wakiongea pale reception.
Nilivyofika kwenye gari nikaanza kuongea na mama J nikamwambia niko njian nakuja, akanambia naomba niletee red wine Baba J, leo nimemiss vitu vichachu vichachu, nikamwambia sawa.
Wakati niko ndani ya gari nikasikia malumbano (“Just leave me alone…”, ….”Please..” ). Ilikua ni sauti ya Iryn bhasi nikatoka nje kuangalia nini kinaendelea. Kucheki alikua ni mwarabu dizaini kama anamzuia njia Iryn asipite “pass through” na mimi nikasogea pale. Jamaa alivyoniona nasogea akamruhusu njia, “Insider Just leave him, lets go”.
Mimi Nikasogea pale (tulikua tunatumia ngeli, kiswahili alikua pia anaongea)
MIMI: Bro! tatizo ni nini?
MWARABU: Wewe ndo boyfriend wake? Samahani bwana nilitokea kuvutiwa naye asee.
MIMI: Hapana sio girlfriend wangu ni Bossy wangu ila kwa ulichokuwa unafanya siku nyingine usifanye, kuna mbinu nyingi sana za kum-win mwanamke.
MWARABU: Kaka nisamehe niombee na msamaha pia kwake pia nahisi ni pombe nilitamani sana kupata namba yake ya simu.
MIMI: Kaka hapa ni hotelin mtu kama katoka kuonana na boyfriend wake utajuaje? Hivi hata wewe ukiona girlfriend wako anatoa namba za simu kwa mazingira kama haya utajiskiaje?
MWARABU: you’re right brother, I was going crazy that time. Nipe namba zako nitakucheki kesho.
Nikampa namba zangu jamaa akaingia kwenye Rangesport, sisi tuliondoka tulimwacha pale parking.
IRYN: Yaani yule Mwarabu kanivamia anaomba namba za simu. Kanikera sana kwakweli anataka kuharibu siku yangu.
MIMI: Pole atakua alipagawa na uzuri wako (nikampa viutani utani pale akaanza kucheka, akaongeza sauti ya music muda huo ngoma ya “Ayra starr-Bloody Samaritan ilikua ikiimba”). So, Yule dada mzungu ulokua unaongea nae ni nani? Maana nimemwelewa sana.
IRYN : hahahaha! yule ni Manager upande wa Operation pale Coral, ni mtu mkubwa sana, usimwone vile.
MIMI: kwani Manager hana hisia? sema unanikazia tu.
IRYN: Insider umelewa wewe sio akili zako kabisa.
MIMI : Bhasi kesho nitakukumbusha ili ujue nilikua serious.
Tulivyofika kwake tukashuka maana alinambia kuna mzigo kutoka kwa Grizmann, nikaingia ndani akaja na kibahasha cheupe akanambia nitafungulia mbele ya safari.
Wakati narudi home niko njiani nikakumbuka Mama J kaniagiza wine, nilivyofika pale kwenye maduka ya pale karibu na “Massana Hospital” nikanunua wine, nikaelekea home.
Moja ya mipango mikakati niliyopanga ni pamoja nakuhakikisha kila navyo rudi home bhasi niwe na zawadi kwaajili yake pamoja na kumpigia simu mara kwa mara.
Baada ya kufika home nikamkuta seblen nikampa zawadi zake mimi nikaelekea chumbani kuoga. Nilikua sishiki mtoto mpaka niwe nimeoga si unajua kazi za Uber unakutana nawatu tofauti. Ile nimeingia chumbani nakuta wife kakipamba chumba na maua na cards afu taa ilikua nyekundu pale kitandani alikua kaandika “HAPPY VALENTINE BABA JUNIOR”.
Licha ya yote yanayotokeaga mimi na Mama J ila tunafanana kwa mambo mengi sana, inshort tunajuana yaani tunaweza gombana ile serious ila muda kidgo utafikiri hatugombana. Hata wazazi walishaachaga kutuingilia mambo yetu, Baba mkwe alishapata aibu akahapa hatokuja ingilia mambo yetu.
*******
Kwa upande wa yule dada Mbotswana nilikua naendelea kufanya naye kazi siku moja moja pale ambapo alikua akinihitaji kufanya kazi nilikua nakwenda. Nakumbuka hii siku alinipigia simu akanambia nimpeleke kwenye “Bureau De change” yoyote ambapo kuna usalama. Nikampeleka Mlimani city akafanya exchange, tukaingia pale Shoppers akafanya shopping then tukaelekea pale Palm village. Yeye aliingia ndani mimi nikawa namsubiri pale nje Parking.
Alivyorudi akanambia twende nipe kampani anataka kununua nguo, bhasi tukaingia pale WOOLWORTH. Akaniambia na mimi nichague nguo zangu aniachie kama ukumbusho. Nilichagua T-shirt ya “Form 6” na jeans ila sasa wakati nachagua nguo, zile Price tag ni hatari, Jeans bei ya chini kabisa ilikua ni 80k, T-shirt ya form 6 ilikua 60k nikasema hapa inatosha hata kama nimeambiwa nichague hapa enough. Akanambia zinatosha? tafuta na raba bhasi, nikapata raba moja kali sana ya Nike ila sasa bei yake ilikua 160k. (Hizi nguo na raba mpaka leo ninazo ni OG hazijawai kuonesha dalili ya kuchuja ni moja ya ukumbusho wa Dada Gorata from Botswana)
Gharama ambazo nilitumia mimi ilikua ni 310k bado yeye, alilipia jumla kama million 3 hivi hao tukaondoka. Akanambia Insider jumamosi hii mimi nitaondoka hapa Tanzania, nitakwenda Uganda. Nikamwuuliza mbona mapema hivi hata hujamaliza muda wako?, akanambia ni muhimu sana ila atakuja next time, ananamba yangu atakua ananicheki.
Jumamosi kabla ya kwenda Airport tulipitia pale Posta kuna watu alikua anaonana nao pale, hao ndo tukaelekea Airport. Hii ndo siku ambayo nilipata majanga pale Airport siji sahau hii siku.
Baada ya kushuka nilimkampani mpaka ndani huku nimeshika bag lake na yeye alikua anacheck-in saa 9 mchana, na alikuaa anategemea kuondoka sa11 jioni. Bhasi tukakaa mle ndani tukapiga story kiaina, nikamwaga mimi nasepa niendelee na majukumu mengine. Akanambia naomba nisaidie kuongea na dada pale kwenye zile apartments afanye usafi mle ndani maana alisahau kumwambia, nimeacha apartment ikiwa chafu sio busara. Akanipa 300,000/= this time alinipa kwa TZS, mimi huyo nikasepa zangu.
Nilikaa pale nje ya Terminal 3 kwenye vi ukuta vile nikiwa nasubiri request, nikaja kupata request lakini customer alikua Terminal 2, nikasema acha niende tu nikambebe niondoke mazingira haya. Wakati nafika kwenye gari yangu nakuta imefungwa krempu na kufuri juu. Ikabidi nitoke niende pale wanakolipia ushuru wa magari nijue kuna shida gani.
Wakati naelekea nikakutana na mlinzi nikamsimamisha nikamwuliza wewe ndo umefunga gari yangu?.
“Gari yako iko wapi?”
“Twende nikuonyeshe”
“Gari yako imefungwa sababu umepaki vibaya, ndo upakiji gani wa gari huu?”
Ukweli wakati nimemshusha dada Gorata hata sikuzingatia parking, tulishuka na kuanza kuondoka kuelekea ndani.
“Sawa mzee kweli ni kosa hata mimi naona ila makosa kama haya mnatoa elimu na sio kufunga gari”
“Mbona mabango yapo kila kona na yanatoa tahadhari ya kupaki gari vizuri”
“Nani anahusika sasa hapa maana naona muda unakwenda”
Muda huo mteja alikua kashaanza kupiga simu kama naenda maana anaona sitokei na ana haraka.
“Dada naomba nisamehe sana mimi niko hapa Terminal 3 ila nimekuta gari yangu imefungiwa na sijui itafunguliwa muda gani. Naomba ni cancel ili ufanye kurequest nyingine ili uwai”
“Sawa kaka haina shida pole sana” [emoji3513]
Tulikwenda mpaka pale ofisini wanakolipia watu ushuru wa parking nikaonana na Bossy wao ndo incharge kama sikosei. Tukawa tunazungumza na palepale akawa amekuja Mlinzi ambaye alifungia gari yangu.
ASKARI: Bossy huyu jamaa mimi nahisi ni Uber.
MIMI: Kwanini unasema mimi ni Uber?”
ASKARI: Sababu nimekuona umekaa pale nje muda mrefu, usingekua Uber ungekua umeondoka, ulikua unasubiri request.
MIMI: Kitendo cha kukaa pale na kupumzika mimi ni Uber unajua nimetokea wapi?
INCHARGE: Nipe simu yako niikague kama wewe kweli sio Uber.
MIMI: Samahani sana siwezi kukupa simu yangu bila utaratibu kama unataka simu yangu fata utaratibu unavyotaka hapo ndo nitakupa simu yangu.
INCHARGE: Kama hutaki tutakuandikia fine ya Uber wanaotumia vibao vya njano na ni kosa kubwa sana kwa hapa AirPort.”
MIMI: Mkuu mbona siwaelewi mara mseme Wrong parking, mara mseme mimi ni Uber. Which is which?” Mnanipotezea muda ujue.
INCHARGE: Una makosa yote mawili nayote utaandikiwa”
MIMI: Hahahahaha nyie watu bwana, fine ni kiasi gani?
INCHARGE: Kwa kutumia vibao vya njano ni 100,000 na wrong parking ni 30,000. Utalipia 130,000/= then tutakufungulia gari yako.
MIMI: Mkuu hapo mimi nitalipia 30,000 tu, sababu ndo kosa langu ila hilo lingine ni lako mimi sihusiki.
INCHARGE: Gari yako itaendelea kukaa hapo hapo parking.
Baada ya kuona jamaa wananikazia nilijua wanatengeneza mazingira ya kunipiga hela, nikakumbuka pale Airport nina ndugu zangu, acha niwacheki nione watanisaidiaje.
Nikaamua kumpigia jamaa mmoja ambaye tulimaliza chuo mwaka mmoja, yeye alipata kazi pale JNIA.
MIMI: Mzee vipi Insider hapa, niko Airport hapa upo pande zipi?
JAMAA : “Bro! nimetoka hapo jioni niko mbali sana kwa sasa, mbona hukunambia kama unakuja?”
MIMI : “Sikia nimepatwa na majanga hapa sasa unanisaidiaje?”
JAMAA : “Nini tena kimetokea?”
“Ikabidi nimwelezee jamaa kilichotokea pale”
JAMAA : Sasa kaka huyo jamaa nishamjua ila hapo itakua rahisi kwa kesho kutoa gari, sidhani kama atakwepo muda ambao mimi nitakua narudi. Wewe njoo asubuhi tutoe gari maana hata sasa muda umeenda kutoa itakua ngumu.
MIMI : Mzee niache gari tena?, si bora nilipie fine tu niondoke zangu, kumbuka parking inaendelea kusoma.
JAMAA : Nitawapigia simu wanaohusika na tolls ili wazuie gari isiendelee kusoma parking. Nitumie namba za gari chap. Sitaki utoe pesa yoyote kaka, vumilia kesho mapema tunatoa gari.
Baada ya kuona jamaa analeta story ambazo sijazipenda nikasema acha niende na Plan B, hapo tayari ilikua saa 1 usiku na madakika. Pale Airport nina ndugu yangu ambaye ni rafiki na dada yangu kindakindaki, sasa nilikua sina namba yake ikabidi nimpigie simu sister yangu.
“Nambie mdogo wangu”
“Dada naomba namba za dada Tyna ninashida nazo haraka”
“Mmmh kuna nini teena unanitisha”
“Dada wewe nitumie nitakuelezea badae”
Dada chap akanitumia namba za Tina, palepale nikapiga ikawa inaita ….. akapokea;
“Habari nani mwenzangu”
“Dada Tyna ni mimi Insider uko poa?”
“Kumbe ni wewe aisee za siku?”
“Salama, niko Airport hapa dada yangu nimepatwa na majanga”
Ikabidi nimwelezeee chote kilichotokea mpaka gari kuzuiwa.
TYNA: Mpe simu mtu ambaye yuko hapo ofisni niongee naye.
“Nikampa jamaa mmoja hivi alikua anaringaringa sana, nikampa simu akakataa kuongea”
MIMI : Sister jamaa amekataa
TYNA: Ok haina shida naomba nivumilie kidogo, ndani ya nusu saa nitakuaa hapo, kuna kazi namalizia.
Nilisubiri pale kama dakika 45 Dada Tyna ndo akaja pale, alivyoniona akaja akani hug.
TYNA : Nambie mdogo wangu unazidi kuwa HB
MIMI : Hata wewe naona Tyako linazidi kukua afu umenawiri kweli Airport kuzuri.(Tyna ni mtani wangu sana)
TYNA: Twende kwa huyo mshenzi ambaye hataki kupokea simu zangu. Nikamwonesha Tyna yule dogo
TYNA: Wewe ndo ulikua hutaki kuongea na mimi?
DOGO : Hamna dada sikujua kama ni wewe.
TYNA: Hivi kama angekua ni Mkurugenzi mkuu? Ambaye alikua anataka kuongea na wewe?. Kwanini mnamwonea customer? Mnambambikia makosa ushahidi mnao?
DOGO : Sio mimi ni Incharge ndo kazuia hiyo gari amesema isitoke mpaka kesho.
“Palepale Tyna akapiga simu kwa Incharge lakini haikupokelewa”
TYNA: Na Askari aliyefungia gari yuko wapi?
DOGO : Ni fulani atakua kashaondoka maana alikua anamaliza lindo saa 12.
TYNA : Naomba funguo za ile krempu. Palepale akamwita mlinzi twende ukafungue gari, afu mwambie uyo Askari Jumatatu tuonane.
Jamaa akafungua gari pale huku mimi na Tyna tukiendelea na story. Wakati jamaa anataka kuondoka Tyna akampa noti ya 10,000 akalipie parking maana kadi walikua wameichukua. Tukaendelea na story pale mpaka jamaa alivyorudi tukaagana nikasepa.
Muda huo ilikua tatu kasoro tayari ikabidi nimpigie simu Iryn nakumwambia nilipata majanga nikifika nitakusimulia nayeye hakua na shida kabisa.
Nilivyotoka pale Airpot nilikimbiza sana gari kuelekea Kijitonyama. Nilitumia dakika 30 kuwasili pale kwa Iryn, nilivyofika nikaingia ndani nikaingia jikoni kuangalia kama kuna chochote maana nilikua na ubao hatari. Nilibatika kupata cupcakes na juice, nikawa nakula huku naelekea seblen, nikamkuta Iryn amekaa huku ananicheka.
IRYN : Sasa kama hujala si ungesema muda ule?
MIMI : Acha inauma hatari ila hapa freshy nitapunguza njaaa, anyway you look great mummy.
IRYN: Mmh fanya chap tuondoke bhana au unataka tukeshe leo? Tunaanza na Mbweni.
MIMI : Twende mimi niko ok hapa nitakua nakula huku nadrive
IRYN : Mhh wewe nawe, tuondoke maana tushachelewa afu nipe story za huyo dem wako wa kibotswana.
Wakati tunatoka nje ili tuondoke tukoanana na yule dada wa sikuzote ambaye anakaa karibu na apartment ya Iryn.
JIRAN : Nawaona mnatoka out, mmependeza
MIMI : Ahsante Jiran karibu cake.
IRYN : Ahsante jirani badae.
Wakati tuko njiani tulikua tunapiga story huku tunacheka.
IRYN : eeh nipe story za Mbotswana, nilivyoona unachelewa sikutaka kukuharibia kumbe ulikua na majanga pole.
MIMI : Si unaona hizi pamba kuanzia juu mpaka chini ni zawadi za Mbotswana.
IRYN: Hata mimi naona leo umependeza sana kwakweli, hongera kwa Mbotswana amekuacha salama kweli?
MIMI : Hata hivyo sijaingia hata robo ya kupendeza kwako.
IRYN : Insider bhana, mbona mimi najiona wa kawaida tu. Afu kimbiza gari tunachelewa ujue.
Tuliwasili Mbweni saa4 kasoro, mlinzi akafungua geti nikapark gari Iryn akaingia ndani, mimi nikaelekea kupiga story na mlinzi. Tulipiga sana story na mlinzi pale baada ya masaa 2, Iryn akanipigia simu kuwa hanioni kwenye gari niende. Bhasi nilivyofika pale akanitambulisha kwa tajir yake hao tukasepa.
Safari yetu ilikua ni kwenda White sand hotel, hatukuchukua muda tukawa tumewasili pale. Mimi nikaamua kununua heineken 2 nikaenda zangu kupoa upande wa chini karibu na beach.
Maeneo yale walionekena watu wakipenzika sana na wapenzi wao palepale nikapata wazo Mbotswana ameondoka na muda bado upo kama siku 9 ndo kodi yake iishe kwenye ile apartment. Nikapata wazo kwanini nisiende na Mama watoto tukachili kwenye ile apartment? Kidogo tubadilishe mazingira?
TO BE CONTINUED
Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu