Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Mkuu wewe ni wale wa People Confuse Brain siyo 😂
 
kama ilivyo desturi ya Mtanzania. Ulipewa Uhuru na Mbotswana sasa unaenda kujipa na muungano kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh hpo kwenye miezi mitano straight bila kusex mkuu aisee ulijiweza big [emoji115][emoji851]
 
EPISODE 11

A TRUE STORY BY INSIDER:

Tunaendelea……

Niliendelea kukaa pale Whitesand mpaka nikamaliza heineken zangu mbili, mtu hatokei na muda ulikua umekwenda ilikua saa 8. Nikaamua kurudi kwenye gari nilale. Haikuchukua muda akawa amerudi akanambia nisogeze gari mpaka reception ili tuondoke. Kufika reception namwona yuko na mama mwenye mix ya Japan na uzungu, hao tukaondoka.

MIMI: Kumbe unahadi wateja wa kike

IRYN: Yeah kama huyo nilikua namfanyia Massaji, inabidi hata wewe siku nikufanyie stone massage inasaidia sana mgongo. Wewe muda wote upo kwenye gari itakufaa sana.

MIMI: Hizo dollar 2,000 mimi natolea wapi jamani?

IRYN: Wewe nitakupa offa, siku ukiwa tayari nambie.

MIMI : Sawa Bossy wangu kama ni offa mimi siwezi kukuangusha.

Nilimrudisha Iryn kwake na mimi nikarudi home kulala. Hii siku nakumbuka kulikua na dalili za mvua.

Asubuhi niliamka mapema nikaenda church mimi nasali KKKT. Hii siku nilitoa sadaka za shukrani na mafungu ya 10, niliingia misa ya asubuhi na mapema nikawa nimerudi home.

Baada ya kutoka church nikamwambia wife aandae mazingira mazuri kwani baadae tutaondoka kuna sehem tutaenda na tutakaa week nzima. Nikaingia kulala maana nilikua na usingizi balaa, ile niko kitandani Prisca akapiga simu alikua ananisalimia na pia kama na muda tutoke out. Lakini nikamwambia leo haiwezekani ratiba zangu haziko well organized maybe next time.

Nilikua najua kabisa Prisca anataka mahusiano, na mimi kwa upande wangu nilisema siwezi kudate naye kabisa sababu ya mke. Sometimes nilikua najilaumu kwa kuwa na mke mapema, maana nilikua nakutana na pisi kali nyingi sana.

Jioni sa12 tukaondoka pale nyumbani pamoja na dada wa kazi tukaelekea Masaki. Nilimwambia achukue nguo za kuvaa week na za mtoto pia. Tulifika masaki pale ilikua giza limeanza tayari, mlinzi alivyoliona gari langu akafungua geti. Wakati nikiwa napark gari, mlinzi alikuna kwangu chap, akanambia yule dada yako “Mbotwsana” alinipa hii noti, kuicheki ilikua ni €50. Nikamweleza thamani yake, akasema kama na cash nimpe yeye muda wa kwenda kubadilisha hana, bhasi nikampa 120,000/=.

Licha ya yote kuna maisha flani hivi ya kinyamwezi niliyaishi sana, kukutana na watu mbalimbali, kuingia maeneo ambayo sikuwai hata kutegemea nitakuja kuingia, ukweli sikujutia kazi yangu. Pia niliona ni bahati sana na bahati hairudii mara mbili.

Mama J aliipenda sana ile apartment na nikamwambia tutarudi home jumapili ijayo.

MAMA J : Hii apartment ume rent?

MIMI: Hapana kuna watu walikua wanakaa hapa wameondoka juzi.

MAMA J: Ni nani hao? na kwanini wakuachie?

MIMI: wale wazungu ambao nilikua nao Morogoro mpaka sikulala home, ndo niliwasaidia kutafuta hapa. Sasa wamendoka muda haujaisha ndo nimeamua tuje tubadili mazingira.

MAMA J : Ni pazuri sana, hivi rent ni kias gani kwa mwezi?

MIMI: kama hapa si chini ya $3,000 kwa mwezi.

MAMA J: Mmh kuna watu wanahela sana. Hio hela si tunaanza ujenzi kwenye kiwanja chetu.

MIMI: Mostly wanaokaa huku ni foreigners wabongo ni wachache sana. Mkajiandae twende tukatembee kidogo.

MAMA J : Sisi tuko sawa ngoja nikamvalishe Junior.

Ile apartment ilikua na kila kitu ndani kama jiko lina vyombo, mashine ya kufulia yaani kila kitu na Ilikua imekamilika kila Idara. Ile apartment kulikua na kioo kikubwa kwa upande wa seblen kimetizama bahari na pembenj kulikua na mlango wa kwenda kwenye kibaraza cha seblen. Pale kibarazani ukikaa palikua na hewa flani amazing na kaupepo ka bahari kwa mbali.

Nilikua nimechili pale kibarazani, simu ikaanza kuita kucheki ni Iryn. Hii siku sikuwa na miadi na Iryn hakukua na kazi, nikapokea simu:

IRYN: Hi

MIMI : Nambie Bossy wangu, kama umelala hivi

IRYN: Hamna nimetulia tu seblen

MIMI: Leta habari

IRYN: Hivi Kidimbwi pazuri?

MIMI : Yeah naskia pazuri, sijawai ingia ndani ila huwa nawachukua wateja pale. Vipi unataka kwenda kwani?

IRYN : Yeah nilikua naangalia hapa kwenye instagram nimeona pazuri. Twende bhasi, maana niko home naona niko bored sana.

MIMI : Wewe wakujifungia ndani leo hii unaona pako bored?

IRYN: Afu leo nimeongea na majirani zangu wote nimechukua na namba zao.

MIMI: Umefanya jambo la busara sana, majirani ndo kila kitu.

IRYN : Unakuja sasa?

MIMI : Unajua niko Bunju kwa Mamdogo wangu, ungenambia mapema dear, twende next week bhasi. ( Sikutaka kubadilisha time table zangu kisa yeye japo nilitamani sana kwenda. Lakini nilikua na outing ya family).

IRYN : No problem, next week.

MIMI: Kama unajiskia bored unaweza kwenda,

IRYN: I can’t go alone there. Byeee!

Tulitoka out na family tukaenda Capetown pale kupoteza muda na tulikaa pale mpaka saa5 ndo tukarudi kwenye apartment. Wife alikuwa na furaha sana hii siku, mengine yaliyoendelea ni siri yetu.

******

Jumatatu nilimka mapema sana kama mnavyojua nilikua nakazi ya kuwachukua Mama wawili na Maggy. Ilibidi niamke mapema ili niende Mbezi kumchukua Mama 2 then ndo nimptie Maggy pale Mikocheni. Katika jambo ambalo nilikua serious bhasi ni pamoja na hili nashukuru Mungu sijawai hata siku moja kuzembea na ni mara chache sana kwa madogo kule Masaki ndo nilikua nazembea lakini nilikuwa na Backup plan.

Nilikuaga naanza na Mama wawili namdrop
Pale Azikiwe then namalizia na Maggy. Wakati tunatoka Azikiwe kuelekea Ohio Maggy akanambia leo tutafanya kazi ya siku nzima, akifika ofisn atanitumia root za kwenda afu nimpe na bei, nikamwambia sawa bossy wangu.

Baada ya kumdrop Maggy nikaenda kunywa chai na muda huo Maggy alikua kashanitumia timetable, ambapo root zilikua ni nyingi tu, kwanza naanzia na Airpot, narudi Posta, Kigamboni, Mbweni na Masaki. Nikampigia simu Maggy tukayajenga tukakubaliana 120,000/=, Maggy kampuni yao ina deal na mambo ya Real estate, kama kuuza nyumba, viwanja, kupanga nknk.

Kuanzia saa 4 asubuhi ndo muda tulioanza kazi , tukaenda Airpot kuna wageni wa kampuni alikua amekwenda wapokea. Tulipiga kazi tukaja kumaliza hizo ruti jion ilikua sa 12, nikampeleka Maggy Kwake na siku ikawa imeisha kihivyo.

Kwangu mimi niliendelea na kazi mpaka saa 4 usiku ndo nikarudi Masaki kwenye makazi mapya ya muda.

********

Ile jumanne kesho yake nilipigiwa simu na yule Mwarabu ambaye alikua anazinguana na Iryn kule Coral. Sababu nilikua kazini nikamwambia nitamcheki badae ili tuongee.

Niliendelea na kazi maana nilikua tayari naplan za kuanza ujenzi wa nyumba, maana niliwaza hizi pesa nazopata na sina pa kuzipeleka ni bora nikaanza ujenzi wa nyumba taratibu.

Kwenye saa11 jion Mwarabu alinipigia tena simu akaomba kama tutaweza onana itapendeza kwani itakua busara tukiongea face to face. Sikutaka kukataa ombi lake nikamwambia anipe muda na place, palepale akaomba niende CITY MALL atanirudishia cost zangu.

Saa 1 ndo muda tulionana na jamaa pale na tulikaa kwenye ki mgahawa kipo mle ndani. Bhasi pale tukaanza story akanambia pale ana biashara yake ya jewelry. Katika mazungumzo nikaja kufahamu kumbe jamaa sio Mwarabu ila ni mtu kutoka Iran ni Muajemi.

“Brother kwanza thanks for meeting me, na pia ni week tayari toka nichukue namba yako. Sikuweza kukucheki sababu nilikua Dubai na nimerudi jana”

“No problem, salama lakini? na biashara zinakwendaje”

“Alhamdulillah! Mwenyezi Mungu anajalia sijui kuhusu upande wako”

“Namshukuru Mungu pia cha muhimu ni uhai tu, mengine ni mipango yake, tunapambana”

“Kabisa hiko ndo cha muhimu Brother “

Muda huo dada alikua amekuja kutusikiliza mimi niliagiza coffee tu…

“Nafikiri ungeenda direct kwa ulichoniitia Bossy”

“Brother kwanza natanguliza samahani kwa kile kilichotokea siku ile, na hiki ndo kilichofanya leo nikuite tuongee”

“Ok yale yalishapita tayari, kuwa na amani”

“Nilichofanya kwa dada kilikuwa cha kijinga ni pombe zilikua afu sikutegemea kukutana na mrembo kama yule”

“Wewe umekutana na warembo wangapi mpakaa sasa”

“Brother kwa Tanzania yule dada ni mrembo nimeona wengi ila yule ni hatari. Nilichokuitia Bro naomba msaada wako nimpate yule Mrembo. Nakumbuka ulinambia ni Bossy wako ila mimi nimetokea kumpenda sana.”

“Brother umempenda au umemtamani?, you want to open her pants not more”

“Brother nikipata nafasi ya kuwa na mwanamke kama yule siwezi kumuumiza naweza mfanya akawa mke wangu na atafaidi maisha”

“Upo sahihi lakini kwa mwanamke kama yule ulimtamani. Ila anaboyfriend wake namjua kabisa, sidhani kama jambo lako litafanikiwa.”

“Natambua hilo kwa mrembo kama yule hawezi kukosa kuwa na mtu. Ila mimi nilichokuwa nataka ni kuonana naye tu, naomba nisaidie hili Brother”

“Kuhusu kuonana naye siwezi kukupa guarantee sana ila nitaongea naye, kama atakubali sawa na pia kumbuka yule ni Bossy wangu sitaki kuingilia mambo yake personal, but niachie ntalifanyia kazi….”

“Kaka nitashukuru sana kuhusu pesa hakuna shida”

“Money only impresses lazy girls. Bossy wangu hana shida na hela, pesa anazo ni wanawake wachache sana ambao wanaweza kuajiri dereva kama mimi. Cha kukushauri acha aamue mwenyewe kukutana na wewe na sio kutumia pesa. Mnajua nyinyi matajiri mnatumia pesa kupata mwanamke lakini wengi wao wanafake love.”

Kwa ufupi tuliongea sana na yule Muajemi na akaniahidi kunipa million 3 kama nitafanikiwa kumkutanisha na Iryn. Sababu nilikua nashida na pesa niliona hiyo kazi sio ngumu kwangu lakini pia nilikua nawaza jinsi ya kumuingia Iryn. Pia nilijua Muajemi sio mtu wa kitoto kwani huko Iran
anabiashara zake za mafuta anauza jumla, anafanya biashara za Lubricants na pia alinambia ana fanya biashara za kuuza pumps za mafuta kwenye filling stations.

Tuliagana pale tukaelekea kwenye gari lake akanipa bahasha ya kaki, akanambia hio sio rushwa bali ni muda wako. Kwenda kwenye gari kuifungua ilikua ni million1 afu zilikua noti za 5,000 mpya, zile ambazo zimetoka bank. Muda ule nilitulia pale parking nikifikiri njia ya kumshawishi Iryn akubali kumeet na Muajemi na pia nilikua nikiitamani ile million 3. Muajemi mwenyewe alikiri itakua kazi ngumu sana kwangu kumshawishi Iryn ndomana kaniwekea lile dau.

Nilirudi nyumbani mapema sababu nilikua na kikao na Mama J na dhumuni kubwa ilikua ni suala lake la kurudi shule. Mwezi wa 3 ilitakiwa arudi chuo akamalizie semester ya 2 na pia kupanga mipango ya biashara atakayofanya. Niliona ni busara nikamfungulia biashara ambayo itakua inampatia pesa za mahitaji yake binafsi.

Pia tulipanga suala la kuanza ujenzi wa nyumba hiki ni kile kiwanja nilichonunua na kilikua Dodoma. Sababu mzee wangu ni engineer nilisema nitawasiliana naye anipe ushauri na plan nzuri ya kuanza ujenzi.

Upande mwingine mama wawili alinipa taarifa kwamba ataanza likizo wiki ijayo mwezi March, lakini akasisitiza niwe nakwenda kumchukua bint yake asubuhi. Pia mama wawili akanambia akianza likizo itabidi nimepeleke vacation Bagamoyo.

Week ileile Iryn alinicheki akanambia kuna mzigo nikamsaidie kuuchukua bandarini lakini this time nitafute gari kubwa ni mwingi sana. Niliwasiliana na yule Agent yake wa Posta akanambia tutafute canter zaizi ya kati inatosha na tutapata kulekule.

Niliwasili Posta tukatafuta hiyo canter ambayo tuliipatia pale Gerezani. Tukaelekea Kurasini kupakia mzigo, jamaa alinikabidhi documents zote za mzigo. Jamaa akanambia angalia gharama za huo mzigo na kodi zake, huyo Bossy wako anapesa sana sijui nani anamuhonga, nilikua na mpango wa kumtongoza lakini siwezi pale.

Gharama za ule mzigo mpaka kodi ilikua ni 189 million na point kazaa, na mzigo wenyewe ulikua ni mawigi sio yale ya kichina ni OG,nazungumzia Peruvian hair, Brazillian hair natakataka zingine kibao kama makeups, yale mambo ya saloon mimi sina elimu juu ya haya mambo. According to Iryna anakwambia wigi zake yabei ya chini ni 300,000/= kwa retail.

Nilipeleka ule mzigo pale home, baadhi tukaingiza ndani kwake na mwingine kuna dada wa Saloon alikua amekuja pale ndo alisupply sehem zingine. Iryn akanambia pia wanauzaga na jumla kwa baadhi ya bidhaa.

Lakini nilikua bado na maswali kichwani hizo biashara alizianza lini? Hata nikipeleka mzigo kwenye saloon zake ni zina wateja sana. Niligundua Iryn sio mtu wa kujionyesha, pia yuko serious na biashara zake na pia ana pesa.

*******
Jumapili ndio siku ambayo nilirudi na familia home baada ya kukaa kwa week nzima pale Masaki. Tulirudi home jioni na hii siku baada ya kuirudisha familia home nilikwenda kuonana na Prisca nilikua na miadi naye maana alikua ananisumbua sana.

Mawazo ya kifisi yalikua yakinijia kichwani kuhusu kumla Prisca, niliona nashawishika kumla yule mtoto. Pia niliwaza kama nitasema nimle, bhasi nitakua nimempa Greenlight ya kuendelea kunisumbua sana, niliwaza hata nikimwambia na mke kwa yule mwanamke asingeweza kataa.

Prisca ni mwanamke ambaye alikua ananitafuta sana, Ofcoz nilikua najua anachotaka ni mahusiano lakini kwa upande wangu niliona hapo ni sawa na kutembea na bom mfukoni ambalo muda wowote litalipuka. Pia nilimwona Prisca kama mwanamke king’ang’anizi atakuja niletea shida kwenye ndoa yangu.

Wife nilimwaga nakwenda kuangalia mpira sitaki kuwasumbua wakiwa wanaangalia tamthilia zao. Hata yeye hakua na shida na mimi kabisa aliniruhusu kiroho safi.

Saa 2 ndo tulionana na Prisca niliamua tuonane pale “EB 25 Lounge” iko Makonde. Tulikaa na Prisca pale mpaka saa5 usiku, nikaamua kumpeka kwao. Sasa wakati nimefika kwao si akanipa mdomo asee kilikua ni kitendo cha haraka, kiukweli sikuweza kuzuia na ndani ya muda mfupi tulikua tumebadilishana lita kadhaa.

Lakini ilibidi nimzuie maana tulikua kwao getin hata angetoka mtu tungeonekana, ikabidi nimwambie hii sio sehem sahihi. Lakini alionekana ni mtu ambaye alikua anataka zaidi, baada ya kuingia ndani na mimi nikarudi home kulala.

**********

Jumatatu nilizungumza na mzee kuhusu suala la mimi kuanza ujenzi na yeye kwa upande wake alifurahi sana kusikia zile habari. Nikamwambia mzee kiwanja kipo Makulu-Oysterbay na ukubwa wa kiwanja ilikua ni (20x20)

Mzee akanishauri kwa mazingira niliyomwelekeza kwa Makulu kuna project ya kujenga mahakama kuu sio muda mrefu, hivyo alinishauri nijenge nyumba ya kupangisha, Mzee pia alinishauri nijenge nyumba ambayo itakua ni moja ila itakua na wapangaji sehemu 2 tofauti na kila partition iwe na jiko na stoo, sebule, masta, room ya kawaida na public toilet. Mzee akanambia atanitumia ramani nzuri pamoja na uzio wake.

Tulikua tuko week ya kwanza kabisa ya mwezi March ilikua ni alhamis nakumbuka ile siku. Hii siku nilikua nimetoka kuonana na jamaa yangu ambaye ni Architect, nilimpa pia kazi anichoree ramani ya nyumba ya vyumba viwili, nilimpa maelezo na ukubwa wa uwanja.

Saa 1 mapema nilirudi home kumpuzika, kama kawaida yangu mimi huwa nikirudi kabla ya yote lazima nioge kwanza ndo mambo mengi yafuate.
Baada ya kuoga niliicha simu kwenye chaji mara nyingi mimi sio mtu wa kuzima data, hii ilikua inatokana pia na kazi nayofanya muda wote data zinakua ON. Sasa inaonekana kumbe prisca alinicheki kwenye whatsapp na muda huo wife alikua chumbani. Mama J kuona text ya Prisca ndo akafungua simu, password zangu alikua anazifaham na mimi nilikuaga namwachia simu yangu sababu hakuna ujinga nilokuaga naufanya.

Mama J alikuja seblen muda huo nilikua nacheza na Junior. Nilikua namuendesha kwenye kibaskeli cha miguu 4 na muda huo Junior alikua na miez 8. Mama J akaniita “Baba J”

“Prisca ni nani?”

“Prisca yupi unamzungumzia?”

“Uliyemsave Prisca- mbezi”

“Ni customer wangu huyo, vipi kuna shida?”

Muda huo ikabidi niache kucheza na Junior nigeuke naona kashika simu yangu, nilihisi moyo kupasuka.

“Ni customer wako au mpenzi wako?, hivi unaniona mimi kama mtoto hivi. Customer gani ambaye mnapelekana Beach, mnapigana picha, mnatumiana picha, chats zenu ninaonesha nyinyi wapenzi ni customer gani huyo?? Na inaonekana mmeanza mahusiano toka muda mrefu sana, kumbe unarudi usiku unanambia upo kazini kumbe uko na malaya wako. Hata ile lipstick ilikua ni ya Prisca ila ukanidanganya leo nimejua ukweli sasa, hata jumapili uliniaga kumbe umeenda kuonana naye. Baba J naomba nirudi home tu ili nikuache ufanye mambo yako kwa uhuru, utakapomaliza njoo home nichukue. Nikiendelea kukaa hapa nitakufa kwa presha, mpaka unatafuta mwanamke mwingine maana yake umenichoka.”

Baada ya kuona mama J anaongea sana, sikutaka kuongea chochote ilibidi niondoke maeneo yale ili hasira zake zipungue. Nilijua baadae nikirudi hasira zake zitakua zimeisha hapo tutaweza kuongea vizuri.

Nikatoka home pale nikaenda barabarani kuna liquor store moja ambayo unaweza kaa na kunywa, bhasi nikaagiza wine pale ili kupunguza stress. Kwa upande mwingine nilijiona ni mpumbavu sana palepale nikaanza jilaumu kwanini nilikua sifuti zile chats?? Hapo pia nilikua nawaza namna ya kuyamaliza na mama J, nilijua haitakua kazi rahisi.

Kwenye saa 5 hivi nilirudi home, nikamkuta dada seblen, nikaenda moja kwa moja chumbani. Nikamkuta kalala kama mtu mwenye mawazo, nikamwambia mama J naomba tuongee sasa. Nakumbuka alinambia hakuna cha kuongea kwa sasa niache nilale, ila mimi kesho nitaondoka. Jumatatu naanza masomo sitaki stress kwa sasa bora nikae mbali na wewe, mimi sikutaka kuendelea mwongelesha sababu namjua ni mtu wa aina gani nikasema kesho tutaongea asubuhi…

EXTRA EPISODE 02[emoji116]

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
 
Swali la kizushi
Hivi story kama hii huwa unakuwa unaandika kwa diary kila siku au maana inakuwa ngumu sana kukumbuka hadi conversation za kila siku na ukizingatia story ina mda mrefu

Kuna baadhi ya matukio muhimu huwezi kuyasahau kwenye maisha yako atlist uwe una shida kwenye kumbukumbu. Mambo yenyewe ya mwakajana.
 
Mkuu kwanza nikupongeze utafutaji wako umenikumbusha kitu ambacho nilianza kujisahau kuwa serious na kazi kuna muda km nilianza kujisahau lakn sahz nimekuwa serious mambo yanaenda....ila mkuu nimenotice kitu nahisi unahisi kuwa mkeo ni member wa jf! So yale matukio ya wanawake ambayo ni marachache mwanaume kutoingia dhambini unayapunguza kdg ili hata mama jay hata akisoma asikuhisi kuwa ni ww baba jay...
 
Asante Kwa leo
 
Bro umekula maisha sn, ila wew ni wa kishua from the ground, kitendo cha mzee wako kuwa engineer at the first place changamoto hukuwa nazo nying sn big up
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…