Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Shujran sana mkuu INSIDER MAN unaupiga mwingi
Tunasubiri kinachoendelea maana nachungulia kila muda
huku sie tunachungulia kote Roma Roman na Insider Man....nyie watu hatari...insider anaongea real life yake na ubber...ila mwamba Roman utunzi wa hari ya juu...kuzunguka dunia SinganoJr. big up both.
 
Ongeza @kondamsafi
 
22:21
 
EPISODE 15

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

TUNAENDELEA

Jumanne asubuhi niliweza kuongea na Muajemi na kama kawaida alikua anauliza jambo lake limefikia wapi. Nikamwambia lipo pazuri na asiwe na haraka soon mambo yatakua mazuri.

Jumanne hii pia nilikua na miadi na Iryn kwaajili ya kumpeleka kwa Mama Janeth ambaye alisema kwake ni kama mama mlezi.

Niliwasili pale kwa Iryn na hii siku Iryn hakunitafuta kwenye simu kabisa, niligonga mlango na akafungua. Baada ya kunifungulia mlango na kunikaribisha alikimbilia jikoni, alionekana anapika wakati huo.

Mimi nilikua nimetulia pale seblen kama Baba mwenye nyumba sina hata habari. Baada ya dakika kadhaa Iryn alianza kuniita;

“Insider……”

MIMI: “Nambie Mummy”

IRYN : “Unaweza kupika ugali?.”

MIMI: “Yeah, kitu kidogo hicho, nije nikusaidie?

IRYN : “Nataka nile ugali leo nimepika samaki”

MIMI : “Mimi nisingekuwepo nani angekusongea?”

IRYN : “Ningepika wali, njoo bhasi na mimi nijifundishe.”

MIMI : “Mrembo kama wewe kuzungusha ule mwiko utaweza.?”

IRYN: “Shida yako unanichukuliaga poa sana”

Nilienda pale jikoni nikabandika maji kwaajili ya kupika ugali, na muda huo Iryn macho yake yote yalikua kwangu.

IRYN : “Insider upo vizuri sana ungekua Ulaya sahivi ungekua unafanyia kazi moja ya 5 - star hotel.”

MIMI: “Shida connection tu, angalia vizuri stage zote nazo fanya kesho sitokusaidia.”

Akanipiga na teke mguuni, lilikua teke la kichokozi flani hivi.

Nilisonga ule ugali vizuri mpka ukaiva na ulikuwa laini, bhasi Iryn alishangaa sana.

MIMI : “Na wewe unakulaga ugali?”

IRYN: “Na mwaka sijala ila naupenda sana. Nimeona stage zote kesho nitakusongea ugali wangu.”

Tulikula ule Ugali na Iryn alikwenda kujiandaa,
Baada ya hapo tuliondoka na kuelekea Masaki kwa Mama Janeth. Sikutaka kuuliza tunakwenda kufanya nini huko ila nilisubiri aniambie mwenyewe.

MIMI: “So mama Janeth ndo alikua rafiki wa Mama yako?”

IRYN: “Yeah, pia ndo alikua msaidizi wa Mama kazini kwa cheo, mama alikua coördinator yeye alikua kama Assistant. Nje na hapo walikua pia marafiki wakubwa sana.”

MIMI: “Leo hajakwenda kazini?”

IRYN: “Alikua safari karudi Jumapili nahisi watakua wamempa off”

Tulifika Masaki mapema na moja kwa moja tulikua getini kwa Mama Janeth yeye alikua anakaa karibu na zahanati ya IST, ukishavuka ukuta wa IST kuna kibarabara cha vumbi kinakata kushoto.(INTERNATIONAL SCHOOL OF TANGANYIKA).

Tulifunguliwa na Mlinzi na muda huo Mama Janeth alikua katoka nje kibarazani. Bhasi baada ya sisi kushuka kwenye gari, Mama Janeth alitoka kibarazani na Iryn naye alitembea kwa spidi wakakumbatiana.

“Waow my daughter I have missed you so much”

ili onekana ni watu ambao wamemisiana sana n hawajaonana kwa muda mrefu.

Mama Janeth alikua ni Mzungu na pia alikua anajua kuongea kiswahili vizuri kabisa. Tulikaribishwa ndani na muda ule ule zikaletwa popcorn kwenye vibakuli, Iryn akaanza maongezi na Mama Janeth. Na Iryn alichukua nafasi hiyo kunitambulisha kwa Mama Janeth kama mimi ni rafiki yake kwa hapa Dar.

Maongezi makubwa ambayo nilikua nikiyaskia ni pamoja na suala la nyumba alizoacha Mama Iryn. Mama Janeth alikua anamwambia Iryn haoni sababu ya kuendelea kuzisimamia zile nyumba wakati Iryn yupo.

Nyumba zilikua zimepangishwa na hivyo walikubaliana wale wapangaji watakapo maliza mikataba yao bhasi Iryn ataanza kuwa incharge. Pia walikubaliana kwenda kuzitembelea hizo nyumba zote siku ya alhamis.

Kwa upande wa biashara walizokuwa wanafanya na Mama yake, Mama Janeth alisema zinakwenda vizuri na akamwambia wakimaliza mazungumzo watakwenda kuitembelea Saloon.

Pia walizungumza suala la kubadilisha taarifa za kampuni ambapo Iryn angekua Director. Na sababu alikua na Bachelor ya Usimamizi wa Biashara kwake lisingekua shida, na Mama Janeth alifurahi maana aliamini Iryn angeenda kuwa msaada mkubwa kwenye biashara kutokana na elimu yake.

Iryn alikubali kuanza mchakato wa kubadilisha hizo taarifa za kampuni na wakawa wanaplan pale. Mama Janeth alimwambia Iryn kuhusu Mwanasheria watamtumia wa palepale ofisni, yeye atume TIN na documents zingine muhimu.

Baada ya hayo mazungumzo kuisha walikuja kudiscuss suala la mafao ambayo mama yake alikua anaweka kama kiinua mgongo.

Mama Janeth aliikwenda ndani na akarudi na bahasha mbili za (A4) ambapo bahasha moja nyeupe yenye nembo ya Blue ya organization, akatoa form moja pale na akaamwambia Iryn anatakiwa kuzijaza kwa makini sana.

“Hizi form utaondoka nazo Iryn kasome kwa makini sana angalia mshahara wa mama yako toka anajiliwa, total utakayopata uta times 30%. Nimekuwekea salary slips zote toka mama yako ameanza mkataba na Organization.”

Hio bahasha ya kaki ina taarifa za kampuni yetu na kila kitu kinachohusu kampuni. Pia kuna form za mikopo ipo humo ambayo mimi na mama yako tulikopa kupitia kampuni yetu, utapitia kwa makini ujue kiasi kilichokopwa na tulichorudisha. Kuna taarifa zote humo utaziona, kama kuna sehemu utakwama bhasi utanipigia simu mwanangu.

Mama Janeth alionekana kumpenda sana Iryn kweli kweli. Muda huo mimi nilikua kama mpenzi msikilizaji maana sikua nachokuzungumza pale, niliishia kula popcorn mpaka zikaisha.

Ni mazungumzo yaliyochukua masaa 2 na baada ya kumaliza walikubaliana alhamisi siku watakayo onana bhasi Iryn aende na zile form.

Muda huo Mama Janeth alikwenda ndani na akarudi na Camera aina ya Canon na akaomba niwapige picha na Iryn. Alinielekeza namna ya kupiga na mimi bila kukosea nikawapiga picha pale.

Tulitoka hapo tukaenda kwenye Saloon palepale Masaki na ilionekana kuwa busy sana. Mama Janeth akamtambulisha Iryn kwa wale wafanyakazi kama Bossy wao mpya akiwa kama mrithi wa Mama yake, hapo ndo wakajua Iryn alikua ni mtoto wa Marehemu. Ilikua ni Saloon kubwa tu ambayo inafanya mambo mengi sana mpaka kupamba maharusi.

Baada ya kilakitu na mazungumzo yao kukamilika waliagana na Mama Janeth aliendelea kubaki pale saloon. Baada ya kutoka hapo Iryn akasema twende Coco beach nikale mihogo, nimeimiss.

Muda mfupi tulikuwa tumewasili pale Coco na wakati tunaingia walionekana watu wakiifukuzia gari, si mnajua pale Coco ukienda jinsi watu wanavyo gombania mteja?.

Tulipark gari yetu vizuri na baada ya kushuka kwenye gari, Iryn alinambia nimfuate. Alionekana mtu ambaye anayajua mazingira vizuri ya pale. Tulikwenda na tukaa sehemu moja ipo na mwishoni huku, tukatulia pale huku tukipulizwa na upepo mzuri wa Bahari.

Kuna Kaka alikuja pale na alioneka kufahamiana na Iryn vizuri tu.

“Sister karibuni sana, karibuni jamani”

IRYN : “Nataka mihogo mizuri laini na mishikaki. Utaleta mihogo 4 na mishikaki 20.”

MIMI: “Mbona unaagiza mishikaki mingi sana hivyo?”

IRYN : “Kaka pia niitie yule wa madafu. Insider akileta ndo utajua kwanini nimeagiza mingi hivo.”

MIMI : “Sawa Bossy wangu mimi siwezi kupinga.”

IRYN: “Afu hilo jina silipendi, hujui tu.”

MIMI : “Sasa unataka nikuite nani? Kwani wewe sio Bossy wangu.?

IRYN: “Niite jina langu, simple tu.”

Na muda huo jamaa wa dafu alikua kafika wakati tukiwa kwenye mazungumzo, jamaa akatukatia madafu 2 pale na Iryn akamwambia jamaa amkatie mengine 2 ya kuondoka nayo.

IRYN: “kaka kama mabaya sikulipi, kama unajua ya leo sio mazuri bora usikate”

“Dada mimi ndo mtaalamu wa madafu hapa umefika hata usiwe na wasiwasi.”

Jamaa baada ya kutukatia madafu na kuondoka story ziliendelea pale taratibu huku tukifurahia utamu wa dafu.

IRYN : “Insider unapaona pale?”

MIMI: “Pale ndo ilikua siku yangu ya mwisho kumpiga mama picha”

Na muda huo Iryn alitoa simu kwenye mkoba na alinionesha picha alokuwa kampiga mama yake eneo lile. Alinionesha picha zingine za Mama yake nyingi tu ambazo walikua pamoja na zile ambazo na mama yake alikua peke yake.

Nikaomba anioneshe na picha za Baba yake, bhasi akanionesha picha ambazo walikuwa pamoja yaani yeye, baba na Mama yake. Pia akanionesha picha ambazo alikua na Baba yake.

Baba yake Iryn alikua ni Mzungu ila alikua ni M-South Africa, Iryn alinambia origin ya Baba yake ni Uholanzi.

Mama yake Iryn alikua mzuri sana alikua na ule urangi wa ki-Ethiopia nafikiri sote tunajua Waethiopia walivyobarikiwa kwa uzuri. Na Iryn alifanana na sana na mama yake na alichukua kidogo kwa Baba yake kutokana na picha nilivyoziona na yeye alikiri hivo kafanana sana kwa mama.

Muda huo jamaa alikua kaleta mihogo na mishikaki na hapo ndo nikagundua kwanini Iryn aliagiza mishikaki mingi.

IRYN : “Insider umeelewa sasa kwanini niliagiza mishikaki mingi?”

MIMI : “Nimeelewa ni vidogo sana asee. Ila ni vitamu sana.”

IRYN : “Mimi na mama tulikuaga tunakuja hapa tunakula mihogo na mishikaki na tulikua tunakaa hapa.”

MIMI: “Nashangaa kuona hata wewe unakula mihogo.”

IRYN : “Shida yako Insider unanichukulia mimi kama slay queens, pole yako.”

MIMI : “Jinsi ulivyo ni ngumu mtu kukuelewa, mrembo kama wewe kula mihogo ni ajabu sana, hii waachie akina Mwajuma”

IRYN: “Napenda sana traditional foods”

Muda huu pia nilikua nawaza namna ya kumuingia kuendeleza mada ya Muajemi, maana ile pesa yake nilikua naipigia malengo sana.

MIMI: “Afu unakumbuka kule Kidimbwi ulisema tutadiscuss ishu ya Muajemi, nasubiri jibu lako ili nimpe kirungu chake.”

Muda huu Iryn alikua akiniangalia….

IRYN: “Si anataka tuonane? Haina shida, nikigundua ni Important person nitamkip close.

MIMI : “Hayo ni wewe ila nahisi atakua ni Potential sana, hata kwangu pia.”

IRYN : “Kwani wewe Insider una mipango gani ?”

MIMI: “Na mpango wa kufungua biashara ya Lubricants, atlist nina experince nayo.”

IRYN : “Good, I love your hustles. Sitaki kukuuliza maswali but you promised utaniambia kuhusu wewe.”

MIMI: “Usijali hata home nitakupeleka, ukale ugali wa mlenda.”

IRYN: “I will be waiting for that day”

MIMI: “Muajemi tunameet naye lini?

IRYN: “Alhamis tukimaliza mizunguko tunaonana naye, you said he can be trusted but I trust you”

MIMI: “Nipe tano bhasi”

Ile kunipa tano nikampa tano ya nguvu akaanza kulalamika pale… “Au au… ndo nini hivi Insider…”

Nikamwambia inuka bhana inuka bhana nataka nikusaprize.

Nikamwinua nikampeleka pale aliponionesha alimpiga picha mama yake. Nikamwambia anipe simu yake nimpige picha, bhasi akaweka mapozi nikampiga picha za kutosha.

Licha ya yote kuna mambo ambayo nilikua namfanyia Iryn sababu nilijua anaya miss kutoka kwa mwanaume. Jamaa yake Grizz alikua Ufaransa ambapo nilikua najua lazima atakua na demu kule, hakuna mapenzi ya mbali kwnye Dunia hii. Na yale mambo nilokua namfanyia alikua akiyafurahia sana tena sana, hata kitendo cha kumpiga picha alifurahi sana.

Tukalipia ile Bill kwa jamaa na sisi tukaondoka pale Coco, sasa wakati tuko kwenye gari Prisca alikua anapiga simu, nikakumbuka nilimuahidi nitakwenda kumuona chuo na sikwenda lazima atakua kamind. Muda huo na mimi sikusita palepale nikapokea simu yake, tukaongea na nikamwambia nitakwenda kwao kumwona.

Tulikwenda na Haile selassie Road na tulikuja kutokea pale Kanisani “St peters”, sasa wakati tuko pale mataa tunasubiri folen, ile mitaa huwa wanauzaga sana maua. Nilipata wazo nimnunulie Ua Iryn kama zawadi nifanye kumsaprize na ua, nikamwita dogo mmoja akaja chap na maua.

“Dogo maua unauzaje?

“Bro park gari pale tuongee vizuri.”

Muda huu Iryn alikua akiniangalia ni kama alikua anajiuliza Insider ananua ua kwa ajili ya nani? Na alikua akitizama kinachoendelea kwa makini, na mimi nilimsoma akili yake.

“Dogo kwani hapa huwezi fanyia biashara? Pale mataa hatutoki sahivi si unaona kuna traffic pale?.”

“Bro haya utanipa elfu 20 na haya elfu 30”

Nilipiga jicho kali na nikalipenda Ua moja lilikua jekundu afu ni zuri sana,

“Nimelipenda hili, dogo bei za maua nazijua vizuri nipe bei za jioni mimi nilipie.”

“Bro hilo top nipe 25 hata wewe si unaliona lilivyo zuri?”

Japo nilikua najua bei yake ni 20k bhasi sikutaka kubargain naye sana na nikatoa pesa nikampa kiroho safi na palepale nikapandisha kioo cha gari.

Sikutaka kumpa Iryn nafasi ya kuongea hata kidogo na nikamkabidhi lile ua palepale.

“This gift is for you mummy”

Ni kama Iryn alipigwa na shock hakuamini kama lile ua lilikua ni kwaajili yake ni ilikua saprizi moja ya kutotegemea. Kama ni point bhasi pale nilibeba point 10, na muda huo Iryn alikua anafuraha sana.

Nikamwambia Iryn hii ni zawadi yangu kwako kwa yote unayonifanyia, sina uwezo wa kukunulia saa ya gharama, sina uwezo wa kununulia necklace ya gharama, lakini kwa hiki kidogo naomba ukipokee kwa mikono miwili.

“No Insider It’s means alot to me, Ahsante sana kwa hii zawadi hujui to what do I feel right now. Nashukuru sana hii ni zawadi kubwa sana kwangu hujui tu.”

Wakati tuko njiani Iryn aliendelea kulitizama lile ua kwa furaha sana.

Tulifika kwake nikapark gari pale getini nje, nikamfungulia geti nikamsindikiza mpaka kwake na nikamfungulia mlango. Nikamuaga nawai tutawasiliana badae bhasi na palepale akanihug kwa nguvu, aisee nililifeel lile joto lake na lilikua amazing [emoji2956] afu lile OG.

Tukaachana pale na mimi uelekeo ulikua ni kwenda kuonana na Prisca, sasa wakati niko njiani nilikua nawaza zawadi ya kumpeleka Prisca. Ua ndo ilikua zawadi nzuri kwake lakini mazingira yalikua magumu kurudi tena pale namanga. Niliwaza sana lakini sikuona zawadi ya kumchukulia, nikasema nitaingia pale Shoppers hapohapo nitajua cha kumpelekea.

Hatimae nilifika pale Shoppers Mbezi Beach na nikazama ndani lakini huwezi amini hata sikuona cha kumnunulia. Nilizunguka mle ndani kama mtalii na nikaishia kununua popcorn na bubblegum “Mentos” zinakuwaga kwenye vikopo vidogo hivi.

Na muda mfupi nilikua getini kwao, nikampigia simu akanambia niingie ndani daah “what the fvck” nilijisemea moyoni. Sikutegemea angenambia niingie ndani, na muda huo mlinzi alikua kafungua geti tayari.

Muda huo nikijifikilia jamaa akaja akanambia amesema uingie ndani,

“Prisca ameanza ujinga gani huu…..”. Nilishindwa kataa nikaingia nikapark gari na yeye alikua katoka tayari kunipokea.

Nikampa ule mfuko nilokuja nao akanambia niingie ndani, sikuweza kukataa maana wanasema maji ukishayavulia nguo sharti uyaoge.

Nikaingia ndani nikamkuta Mary yuko seblen, lakini pia pale seblen palikua na dada mkubwa mmoja na madogo wawili wa kike.

Mary alivyoniona akanisalimia pia akanikaribisha kwa tabasamu.

MARY: “Insider leo umeamua uingie ndani”

MIMI: “Nimeingia sababu ya mgonjwa lasivyo nisingethubutu”

MARY: “Hakuna anachoumwa huyo anakusumbua tu.”

Prisca alinitambulisha kwa ndugu zake na alinza na yule dada mkubwa ambaye alinitambulisha kama Mamdogo wake, hakuishia hapo akawatambulisha wale madogo wa2 wakike ni wadogo zao. Hapo nikajua kumbe familia yao wako watoto wa4 lakini wote ni wa kike.

Na muda huo dada alikua kaniletea juice na mimi nikaanza ikaifakamia palepale. Ofcourse sikuwa confident sana mle ndani ukizingatia Mwanaume nilikua peke yangu naye koroma mle ndani.

MARY : “Insider leo utanipa namba yako ya simu, sometimes huwa nahitaji huduma ila nashindwa kukupata.”

Wakati anaongea hivyo, alipigwa jiko kali sana na Prisca

MIMI: “Haina shida, Prisca ameshindwa kukupa?”

MARY : “Insider Prisca hawezi kunipa namba yako, na sijui kwanini hataki niwe na namba yako.”

MIMI: “Lete simu nikuandikie hapahapa.”

Na muda uleule Mary alikuja akaa pembeni yangu, nikamwandikia namba na akabaki palepale hakuondoka.

Muda huu Mamdogo wao alikua akiniangalia kwa macho ya kiwizi wizi, nikama mtu ambaye alikua anasikia story zangu ila alikua hajapata bahati ya kukutana na mimi. Prisca naye muda wote alikua kimya hakusema neno lolote.

PRISCA: “Insider can we talk private?”

MIMI: “Yeah,sure”

Tulitoka pale tukakaa kibarazani lakini nilikua sijiamini kabisa maana nimeingilia Himaya ya watu. Prisca japo alinitoa wasiwas kwamba wazazi wake sio minder hawana shida kabisa.

Pale kibarazani kulikua na coach vidogo flani hivi vi-nne na meza ndogo duara ya kioo.

MIMI: “Nambie unaendeleaje Mummy”, nilikua ninamshika mashavu.

PRISCA : “Safi tu”

MIMI: “Mbona kinyonge sana? Umepooza sana, shida nini?.”

PRISCA : “Insider you fvcked me hard that day, but now am okay”

MIMI: “Ooh sorry, seems like unataka tena.”

Prisca kama alipata na ka-aibu fulani ila aliishia kutabamu na akachange mada. Lakini mimi nilielewa anachohitaji.

PRISCA : “Nimefurahi umeingia ndani leo.”

MIMI : “Nimeingia leo sababu unaumwa ila hutoniona tena humu ndani.”

PRISCA : “Usijali hata mimi nitakuja kwenu.”

Nikaona huyu mwanamke ameanza kuleta mambo ya kichawi, aje kwangu kufanya nini?

MIMI: “Mimi nasepa hata hivyo muda umekwenda, na muda huo ilikua saa1 usiku na madakika tayari”

Na muda huo Mary alikua amekuja pale kibarazani na akakaa.

MARY : “Insider unavyoondoka nishtue nataka unipe lift.”

MIMI: “Mimi ndo naondoka hapa, nilikua na mpango wa kuja kuwaaga huko ndani.”

Tukaondoka pale na Mary tukaingia kwenye gari hao tukaondoka.

MIMI: “Unaelekea wapi.?”

MARY : “Nataka kwenda stationery na kazi ya kufanya nataka nimpe mtu kazi. Insider wewe unakaa wapi?”

MIMI: “Mimi nakaa Massana kule.”

MARY : “Pale si pana stationery nzuri”?

MIMI : “Yeah ipo”

MARY : “Twende hapo.”

MIMI: “Ila sitokurudisha utarequest”

MARY : “Sawa”

Wakati tuko njiani tulikua tunapiga story mbalimbali na Mary akili yake ilionekana kukomaa sana. Tulifika pale Massana nikamdrop kwenye stationery mimi nikaondoka, nikamwambia ukirudi home utanijulisha.

Mimi nilivyorudi kama kawaida niliingia bafuni, baada ya hapo nikachukua laptop yangu nikaanza kuangalia mipango yangu. Pia mimi nilikua nimeandaa Excel sheet ambayo nilikua naweka taarifa za biashara kila siku kwa nilichoingiza na kutoa. Kama mafuta nilikua nachukua risiti kila napo jaza ili zinisaidie katika mahesabu, mwisho wa mwezi ndo nilikua napiga accounting za mwezi husika hasa kwenye mapato na matumizi na faida iliyopatikana.

Baadae kidogo Iryn alinipigia simu na tuliongea sana hii siku kwenye simu kuliko zote. Na zaidi aliifurahia sana ile zawadi ya UA akanambia mtu wa mwisho kumpa zawadi ya Ua alikua ni mama yake. Na mimi ndo nimekua mtu wa kwanza kumpa zawadi hio baada ya kifo cha mama yake. Tuliongea sana na simu na akaomba kesho niende kwake nikamsaidie kuzipitia zile form pamoja.

TO BE CONTINUED.

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
 
Kwahyo leadermoe mwamba alishavuta?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…