Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu


Kumbe kuna season 2 na sina habari uwiiiiiiiiiiii!!

Naanza na Season 2 episode 1
Naweka na siti kabisa sitaki kupitwaaaaa
🙇🙇🙇🙇🙇🙇🙇🙇🙇🙇🙇!


Cc Smart911
 

Attachments

  • Screenshot_20221003-150930~4.jpg
    22.1 KB · Views: 21
Season 1 Niliishia Iryn kaenda Sauzi kusoma, Jane were expecting a babyboy, Insaida anatarajia kuanza masomo kutokana nalile dili la kazi kutoka kwa yule mzee alifariki (Pama) kama sikosei, Iryn na jamaa walipata bebigelo then Jamaa na mama Junior were expecting to get married n lots of kutiana na kina Sumaiya sijui ni Asmah!


Naendelea na Season 2 sasa!

🙇


Cc Smart911
 
Insider wamekuteka au unaumwa?mbna kimya kaka kwema?
 
"Mke mwenza ameshaondoka??

Mke mwenza kivipi??"

khakhakhaaaa

Wee na mwenzio Iryn mlijifanya kumchozea mchezo mamaJ kumbe alikua anawachora tu akijua fika kinachoendelea !

Sijui kwanini nimecheka

Cc Smart911
 
Hilda Jf member alopatiwa kazi in the storeeee!👋👋


Naendelea epesode 2 chapter 2

🙇🙇

Cc Smart911
 
SEASON 02:
CHAPTER 14:

“BY INSIDER MAN.”

NYUMA:
Mida ya saa 9 mchana Iryn alinipigia simu na tuliongea kama lisaa hivi, alikuwa anajua kinachoendelea kuhusu mkesha wa mwaka mpya na yeye kwa upande wake alitamani sana angekuwepo pale.

IRYN: “Baby mama anaendeleaje?”

MIMI: “Yuko salama anaendelea vizuri.”

IRYN: “Na anaondoka lini?”

MIMI: “Baada ya mwaka mpya ataondoka.”

IRYN: “Baby nikuombe kitu, please.”

MIMI: “Niombe mummy na kuwa huru.”

IRYN: “Naomba niongee na mama nimsalimie, nisikie hata sauti yake tu. Naamini nitafunga mwaka vizuri sana nikisikia sauti yake.”

Nilinyamaza kwa sekunde na nilikuwa nikijifikiria jibu la kumpa maana niliona Iryn anataka kucheza faulo kwenye eneo la hatari.

ENDELEA:

Niliwaza sijui nimdanganye tu kuwa mama hayupo?

IRYN: “Baby, mbona kimya. Are you there?”

MIMI: “Nipo baby.”

IRYN: “Mbona hunijibu? Umekaa kimya.”

MIMI: “Nitakupa uongee naye but promise me hutafanya someting stupid.”

IRYN: “Usiwe na wasiwasi kwa hili, mimi ninamsalimia tu, inatosha.”

MIMI: “Ok.”

Nilitoka chumbani kwenda seblen, mama alikuwa pale na nikampa simu, lakini niliweka loud speaker maana niliona Iryn anaweza haribu mambo, sikuwa na imani naye kabisa.

MIMI: “Mama ongea na bossy wangu anataka kukusalimia.”

Mama alichukua simu na akaanza kuongea naye,

MAMA: “Aloooh.”

IRYN: “Mama shikamoo.”

MAMA: “Marahaba haujambo mwanangu.”

IRYN: “Sijambo mama yangu, unaendeleaje?”

MAMA: “Tunashukuru Mungu sana, sijui wewe huko unaendeleaje?”

IRYN: “Mimi ni mzima wa afya, samahani nilikupa ahadi ya kuja kukusalimia lakini mpaka sasa sijaonekana. Bado sijafanikiwa kurudi Dar mama.”

MAMA: “Usiwe na wasiwasi, tuendelee kuomba uzima tutaonana tu.”

IRYN: “Nikirudi Tanzania, nitakuja hukohuko mkoani kukusalimia hata kama Insider atakataa.”

Mama alianza kucheka pale,

MAMA: “Hahaha! Mwanangu usinifurahishe, wewe karibu nikupikie na mlenda.”

IRYN: “Ahsante mama, na unatarajia kuondoka lini?”

MAMA: “Siku zimeisha tayari kuendelea kubaki huku, nimecheza na mjukuu wangu mpaka nimeridhika.”

IRYN: “Na Junior alivyokuwa mtundu atakuwa amekuchosha sana.”

MAMA: “Hahahaa umejuaje?”

IRYN: “Naujua utundu wake.”

MAMA: “Amekopi kwa baba yake kila kitu, hivi vitu anavyofanya Junior na baba yake alikuwa hivihivi.”

Muda huu Iryn alianza kuangua kicheko,

IRYN: “Weeeh, mbona Insider ni mtulivu sana mama?, Junior is too much.”

MAMA: “Mimi ndo niliye mlea Insider mpaka anakua, tabia za Junior kama baba yake akiwa mtoto.”

IRYN: “Aisee, sawa mama leo nimefurahi sana.”

MAMA: “Junior akikua atabadilika ni utoto tu.”

IRYN: “Mama nitamtumia Insider Pesa ili ukafanye shopping kabla ya kuondoka, uwapelekee na wajukuu zawadi.”

MAMA: “Wee! Mwanangu nitashukuru sana na Mungu atakubariki.”

IRYN: “Ahsante mama nimefurahi kuongea na wewe na nikutakie mwakampya mwema.”

MAMA: “Ahsante mwanangu nimefurahi pia.”

Baada ya kumaliza kuongea mama alinipa simu na mimi nikaagana na Iryn na niliendelea kuongea na mama yangu. Kwa upande wake mama alionekana kufurahi sana baada ya kupewa ahadi ya pesa.

MAMA: “Bossy wako anaonekana ni mtu mzuri sana.”

MIMI: “Ni kweli yuko poa sana, ana Roho nzuri.”

MAMA: “Kumbe anamjua Junior?”

MIMI: “Eeh mama anakujaga home, hata juzi alivyorudi Dar alikuja kutusalimia.”

Na nilichukua simu yangu nikamuonesha mama picha ya pamoja iliyowaonesha wife, Iryn na Junior.

MAMA: “Wewe! Kumbe ni chombo eeh? Na mlifahamianaje?”

MIMI: “Kupitia biashara ya Taxi ndo tulikutana ndo kunipa kazi kwenye kampuni yake.”

Mama mambo ya Uber yeye hajui, ni neno geni kwake zaidi anajua Taxi tu.

MAMA: “Kama bossy unaye, fanya kazi kwa uaminifu na kujituma utakula mema ya nchi.”

Muda huu message kutoka bank iliingia na ilionesha kiasi cha TZS 2,000,000 kimeingizwa kutoka kwa Iryn. Nilimuonesha mama ile message na yeye aliishia kufurahi sana maana ilikuwa ni surprise kwake ambayo hakutegemea.

Ukweli baada ya Iryn kuongea na mama yangu ni alifurahi sana kwakweli na alinishukuru sana kwa kumpa ruhusa ya kuongea na mama yangu.

Usiku mida ya saa 2 usiku niliondoka kwenda Masaki nyumbani kwa mama Janeth kwaajili ya mkesha. Tuliondoka wote pale home na nilianza kuwadrop akina mama J pale church Mbezi Beach na mimi nikaendelea na safari yangu.

Nilimpitia Lucy pale kituoni Mwenge ITV maana alikuwa akinisubiri ili twende wote kwa mama na tulitumia muda mfupi sana kuwasili Masaki.

Picha linaanza nje ya geti nakutana na magari kibao ya kifahari, nikamwambia Lucy hapa leo kuna ugeni wa kutosha. Lucy alikuwa akishangaa yale magari maana ni magari kwelikweli, hakukuwa na gari ya kawaida pale zaidi ya Subaru Forester tu. Mimi nilikuwa na ka-IST kangu na nilikuwa natafuta sehemu ili nikaweke, nikapata upenyo ili nikachomeke, bhasi Masai huyo kaja spidi kunizingua;

Nikajiuliza hivi hawa Masai mama kawatoa wapi? Maana jumla walikuwa watatu (3),

“Yellooo, usipark hapo.” Ilikuwa ni sauti ya Masai akinikataza nisipark gari.

“Masai nani kawaita hapa?”

“Kwani wewe nani unauliza hivyo.”

“Nimekuuliza tu nina maana yangu, pia nataka kujua kama kuna mtu kawaita hapa, sina taarifa zozote.”

“Sisi tumejiongeza tu.”

“Bhasi naomba mlinde haya magari vizuri, badae nitawacheki.”

“Sawa tajiri.”

Niliingia ndani nimeongozana na Lucy, kwa mbali tuliwaona Hilda na Rebecca wamekaa kwenye angle nzuri sana na sisi tukaenda kukaa meza yao. Kila meza ilikuwa na viti vitano (5), nikamwekea Asmah siti maana alikuwa kanitumia ujumbe nimuwekee siti ili akae karibu yangu.

Kwa upande mwingine walionekana wazungu na wageni mbalimbali ambao ni foreigners na wengi walikuwa ni wafanyakazi kutoka organization anayofanyia kazi mama Janeth. Sehemu ya event lilikuwa imepambwa na kupendeza sana muda huu na kwa haraka jumla ya watu ambao tulikuwepo kwenye eneo la tukio ni kama 50, japo wengine waliendelea kuja taratibu.

Baada ya dakika 10 Sumaiya aliwasili na alikuja tuliko kaa sisi na akakaa kwenye siti niliyokuwa nimemwekea Asmah,

MIMI: “Siti ina mtu usikae.”

SUMAIYA: “Ina mtu ni nani?”

MIMI: “We elewa hivyo, au Kiswahili kigumu?”

SUMAIYA: “Ooh ni Asmah, sasa hapa sitoki mpaka tunamaliza.”

MIMI: “Sometimes uwe mtu mzima, kwanza tumekaa kiofisi, wewe kakae na wenzio kule.”

SUMAIYA: “Nitakaa hapahapa na siondoki.”

Bhasi muda huu nikibishana na Sumaiya, kwa upande mwingine walikuwa makini sana wakiangalia movie inavyokwenda. Kwa upande wangu ilibidi niwe mpole tu maana huwezi kubishana na Sumaiya na ukamshinda, ni muongeaji na mbishi.

Asmah aliwasili na kwa mbali baada ya kuona meza yetu imejaa alitafuta sehem nyingine akakaa. Nilitamani sana niende kukaa naye lakini niliona italeta picha mbaya na maneno kwa kina Lucy, hivyo nikavunga. Ukweli Sumaiya alikuwa amenikatili sana na aliharibu mipango yangu, ukizingatia nilitaka kutumia hii chance kuendelea kumvuta Asmah.

Mama alikuja kwenye meza yetu kutusalimia na alifurahi sana kutuona, na alisema nimfuate ana maongezi kidogo na mimi.

Baada ya kuingia ndani seblen tulianza maongezi na kubwa aliuliza kwanini sijaja na wife? Ilibidi nimwambe wife amekwenda kanisani ila tutakuja siku nyingine.

Tuliendela na maongezi mengine na nilishtuka baada ya kuniambia kwamba Iryn hapokei simu zake,

MAMA: “Sijui huyu binti yangu anashida gani maana namtafuta sana hapokei na hanirudii.”

MIMI: “Hata mimi alikuwa hapokei simu zangu, lakini sio muda hapa tumetoka kuchati.”

MAMA: “Ndo nilitaka kukuuliza hili kama mna wasiliana, nitamtafuta badae tuongee.”

Niliwaza nikaona kama haimake sense, yaani Iryn asipokee simu za mama Janeth?, nilimuaga mama na nikarudi kukaa.

20:30 mama alianza kuongea kwa kutukaribisha na alikuwa ndo MC wa tukio,

Naomba nichukue fursa hii kuwakaribisha ndugu, jamaa na marafiki wote ambao mmekuja hapa nyumbani kwaajili ya kusherehekea na kuupokea mwakampya pamoja. Nina thamini uwepo wenu wa kuja hapa nyumbani, mnaowaona hapa ni ndugu na marafiki kutoka Organization X na balozi mbalimbali, pia kuna wafanyakazi kutoka kwenye kampuni yangu. Karibuni sana tuupokee mwaka mpya kwa pamoja na naomba mjisikie mko nyumbani, vinywaji vipo vya kila aina.”

Kulikuwa na nyama choma za kila aina ni wewe unachagua unataka ya nini, kama ni mbuzi, ng’ombe na kuku na zilikuwa zimechomwa kwa ufundi wa hali ya juu sana. Pale mezani nilikuwa nakimbiza JD na Lucy taratibu na story zilikuwa zimekolea sana, kasoro Asmah alikuwa ni mpweke maana hakuwa na mtu wa kuongea naye.

Mziki wa mbali na wa taratibu ulikuwa ukisikika na sauti za watu wakiongea chini chini nazo zilikuwa zikisikika. Baada ya nusu saa mama alisimama na kuanza kuongea tena na habari kubwa alisema anataja watu wa kwenda kutoa speech,

"Ladies and gentlemen, it’s now time to announce the people who will give us a brief speech about what happened in 2023. Our time is limited, so if you hear your name, please come forward to speak. The first person to give a speech is Insider. Please, you’re welcome."

Ukweli sikuwa na wazo kwamba nitaweza kuandikwa kwenda kutoa speech, ukizingatia hata sikujipanga, ilikuwa ni surprise. Muda huu kelele zilianza kusikika kutoka kwa team yangu maana walifurahi sana kusikia nakwenda kutoa speech.

Nilisimama kwenda mbele na mama Janeth alinikabidhi mic ili niongee, sasa baada ya kushika mike palepale nilipata kitu cha kuzungumza.

Kumbuka palikuwa na watu wa heshima na wenye status kubwa kutoka kwenye mabalozi na wengine kwenye taasisi anayofanyia mama Janeth. Confidence yangu ilikuwa ya hali ya juu sana muda huu na nilianza kutabasamu kwanza kabla ya kuongea,

“Good evening ladies and gentlemen.”

Baada ya kujibiwa nikaendelea kuongea,

“My name is Insider Man…..”

Mama alinikatiza na akasema niongee Kiswahili tu, na yeye atakuwa ana translate kwa wale ambao hawajui.

Na mimi nikaendelea,

“Kwanza napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai pamoja na uzima kufikia siku ya leo, pia nichukue nafasi hii kuwashukuru nyote mliokuja kusherehea pamoja katika siku hii ya kuaga mwaka 2022.

Kwa upande mwingine Asmah alionekana kutabasamu sana na alionesha hamu ya kutaka kusikia ni nini nachotaka kuzungumza muda huu.

……Mimi kama Insider mwaka huu wa 2022 ulikuwa mzuri sana kwangu na pia mwaka huu ulikuwa mbaya sana kwangu, kwani nilimpoteza mtu muhimu sana kwenye maisha yangu, Mungu amlaze mahali pema peponi, AMEN.

Attention ya watu ilizidi kuongezeka na kila mtu alionekana kutaka kusikia kutoka kwangu na mimi liliendelea,

….January mwanzoni katika harakati zangu za maisha nilikutana na moja ya mwanamke mrembo sana hapa duniani. Kipindi hicho nilikuwa dereva wa Uber, sasa nilikutana na huyu dada usiku na tulitokea Marina apartments kwenda Kijitonyama. Baada ya kumshusha dada aliomba business card yangu na alinipa ahadi ya kunitafuta tena kwaajili ya kufanya kazi zingine. Honestly sikumtake serious maana nilikuwa nakutana sana na wateja wa dizaini hii, anachukua business card lakini hatutafuti.

Watu walicheka sana na mimi nilinyamaza, baada ya kutulia nikaendelea,

Tarehe 12 January, siku ya sherehe za mapinduzi ya Zanzibar nilikuwa home nikifanya usafi wa gari, nina tabia ya kupenda kufanya usafi wa gari yangu atleast kwa mwezi mara 2. Sasa baada ya kurudi ndani nilikutana na missed call 2 za namba ngeni, niliamua kuzipotezea nikaenda kuoga. Baada ya kutoka bafuni ile namba ikapiga tena, nikapokea na aliweza kujitambulisha kuwa yeye ndo dada ambaye tulibadilishana namba siku ile usiku. Nilikuwa nimemsahau tayari, lakini baada ya kunikumbusha ndo kumkumbuka na aliomba tukutane pale Mlimani city.

Niliikubali appointment yake na nilitoka home kwenda Mlimani city kuonana naye, lakini njiani mawazo yote nilijua dada anakwenda kunipa dili. Bhasi, baada ya kuwasili pale Mlimani city tulionana na tukaingia mkataba wa kufanya kazi pamoja.

Nilianza kufanya kazi ndogondogo kama kufanya delivery za mizigo, kumpa huduma ya usafiri na mambo mengine. Kwa kipindi chote nilikuwa niko smart sana na nilifanya kazi kwa bidii na uaminifu mkubwa, mpaka kupelekea kuniamini na kuanza kunipa majukumu makubwa.

Mpaka sasa mimi ni Manager wa kampuni yake na nina isimamia kwa weledi mkubwa sana na inafanya vizuri. Kwa ufupi niseme ni mtu ambaye amenikutanisha na watu wengi akiwemo mama Janeth, wafanyakazi wenzangu mnao waona hapa, na leo hii nipo hapa na nyinyi kwasababu yake.


Nachotaka kusema ni kwamba haya maisha yunayoishi kila mtu ambaye unakutana naye anaweza kuwa fursa au daraja la kufikia mafanikio. Tujifunze kuheshimu watu wote maskini kwa matajiri, tuishi na watu vizuri, tujitume na kufanya kazi kwa bidii, mafanikio tutapata. Uaminifu na uchapakazi wangu ndo ulifanya dada akaniamini mpaka sasa ana imani kubwa sana na mimi, hata mama hapa ana imani kubwa na mimi.”

Niliwapa na historia yangu na mzee Pama mpaka kufikia kifo chake na wakati nikisimulia kila mtu alionesha kuhuzunika sana, maana iliwagusa watu wengi sana muda ule.

Pia niliwaambia nitakuwa na charity ya kuwatembelea watu wenye uhitaji na ambaye ataguswa kwenda au kutoa mchango bhasi watamkabidhi mama Janeth na kwa wengine wataniona mimi.

Nilitumia kama dakika 20 kutoa speech yangu na baada ya kumaliza nilipigiwa makofi mengi sana kwa kutoa speech nzuri na nikarudi kukaa, lakini this time nilibadili meza nikaenda kukaa na Asmah.

"This is our Insider Manager, and he is very hardworking, honest, and a people person. Since he took the position of manager, our company has been doing very well. Let's applaud him for his good work. Mr. Ronald, welcome. Please give us your speech, I believe you have a lot to say."

Mr. Ronald ni mzungu na chap alisimama kwenda kutoa speech.

Muda huu nilikuwa busy na Asmah na alinipongeza kwa kutoa speech nzuri na alionesha kufurahi sana. Kwa upande mwingine Sumaiya alikuwa akituangalia sana, maana nilikuwa nimewakataa kwenye meza yao na nimekwenda kwa Asmah.

MIMI: “Mummy nafikiri leo ni siku nzuri ya kufikia muhafaka wa lile jambo letu, tuanze mwaka mpya na status mpya, kama ni wapenzi au laah.”

ASMAH: “Insider suala la kuwa kwenye mahusiano ni gumu sana kwangu, tuendelee kuwa washikaji.”

MIMI: “Huu ni uongo, ukweli mimi na wewe tuna hisia za mapenzi na unavyosema jambo kuwa gumu unamaanisha nini?”

ASMAH: “Una mke, bado unatoka na bossy wangu. Insider siku tukija gundulika msala utakuwa kwangu, nikwambie ukweli namuogopa sana Iryn, ataweza kunifanya kitu mbaya.”

MIMI: “Usinambie amekutisha tayari na wewe ukajaa.”

ASMAH: “Hapana hajanitisha lakini mimi namjua Iryn kabla yako, yule sio mtu wa kawaida hata marehem mama yake alikuwa ni mtu mkubwa sana.”

Nilianza kupata shauku ya kujua zaidi na maongezi yetu yalibadilika,

MIMI: “Ulimjuaje mama yake Iryn?”

ASMAH: “Before nilikuwa nafanyia kazi hotel “X” kama receptionist na hapa ndo kujuana na mama yake.”

Nilimkatisha maongezi yake,

MIMI: “Umefanya kazi kwenye ile hotel?”

ASMAH: “Ndo niliko kutana na mama Iryn, alitokea kunipenda na akanishawishi nije kwenye kampuni na atakuwa ananilipa mshahara mzuri ndo kumkumbalia na kuja huku mpaka leo.”

MIMI: “Ilikuwa ni mwaka gani wakati unaanza kazi?”

ASMAH: “Ilikuwa ni may 2020 wakati naanza kazi, na watu niliowakuta ni Rebby na Winny wale wameanza na kampuni kama sikosei.”

MIMI: “Sumaiya kumbe ni wa juzi tu.”

ASMAH: “Huyo kaja mwaka jana mwezi June na aliletwa na mama Janeth mwenyewe.”

MIMI: “How come alipewa umanager wakati wewe upo kitambo kwenye kampuni?”

ASMAH: “Hujui tu, Sumaiya ni rafiki mkubwa sana wa mama, pia nilishangaa sana Sumaiya kuhamishwa ofisi na hapa ndo niligundua Iryn ana nguvu kubwa sana kwenye hii kampuni.”

Asmah alinambia mambo mengi sana ambayo nilikuwa siyajui, pia nilimgusia kidogo kuhusu familia yake na alinambia mzee wake yuko Morocco.

Kwa upande mwingine nilikuwa nikichati na Iryn na alisema yuko home anasubiri mwaka mpya. Habari nyingine aliyonipa ni kwamba mimba yake inazidi kukua, hivyo kuna umuhimu wa kutoa taarifa mapema Ethiopia. Nilimuuliza atatumia njia gani kutoa taarifa?, yeye kwa upande wake alisema atapiga simu kuongea na mama mkubwa wake.

Sherehe zilikuwa nzuri sana na baada ya kuukaribisha mwaka mpya, tulipongezana watu wote pamoja na kujuana. Bila kusahau picha nyingi sana zilipigwa hii siku kama ukumbusho na watu walianza kuondoka.

Niliweza kupata nafasi ya kuongea na wageni mbalimbali wa mama Janeth na wengi walisema watachangia hio charity na kuna ambao waliomba contacts zangu na taarifa za bank kwaajili ya kutuma michango.

Nilikwenda kumuaga mama ili niondoke, lakini alikuwa busy sana, hivyo nikaondoka bila kuagana naye. Asmah alikuwa anaoneka kuchoka sana maana alimaliza chupa 1 ya wine na tangu muda mrefu alikuwa akilalamika nimpeleke home akalale.

Niliondoka bila kuwaaga akina Lucy na kipindi
tunatoka getini kuelekea parking, nilisikia Sumaiya akiniita na sisi tukasimama.

SUMAIYA: “Insider mbona unaondoka na hatujaongea?”

MIMI: “Kuongea nini tena?”

SUMAIYA: “Kuhusu gari.”

MIMI: “Gari si tuliongea au umelewa? Nilikwambia maliza kwanza mafunzo mengine tutamalizia.”

SUMAIYA: “Sawa siku ile sikukuelewa, bhasi nimekuelewa.”

MIMI: “Jumatatu tutaongea vizuri, usiwaze.”

Wakati tumeingia kwa gari, Masai alikuja kudai pesa yao na nilimkabidhi tukaondoka.

Njiani Asmah alikuwa kalala mpaka tunawasili pale kwake, na nilimuamsha nikampa kampani mpaka ndani.

Alilala kwenye sofa na mimi nilienda jikoni kucheki kama nitapata soda ya coke ili nimpe anywe apunguze hangover. Kwa upande wangu hata mimi nilikuwa high sana maana tuliipiga chupa nzima ya JD na Lucy, na nilijisemea acha nipumzike kidogo then ndo niondoke kwenda home.

Nilikuja kushtuka saa 10 alfajiri na nikajisemea leo ndo leo, acha niondoke nirudi home kulala. Asmah alikuwa kalala vilevile kwenye sofa na sikutaka kumuamsha, huyo nikaondoka kurudi home.

Baada ya kuwasili home niliwakuta wife na Junior wanacheza kitandani na wife alinambia dogo hana usingizi anasumbua. Kwa upande mwingine hakuniuliza kwanini nimechelewa kurudi na tulifanya maongezi mengine kabisa.

****
Niliamka saa 6 mchana na nilikwenda kuoga kwanza kabla ya yote, then nikaenda kuonana na mama sebleni, ili nimuwish na heri ya mwaka mpya.

Hii siku kulikuwa na lunch ya pamoja kwa wafanyakazi wote pamoja na mama Janeth pale Serena hotel. Lakini kwa upande wangu nilisema sitokwenda na nitampigia simu mama kumpa udhuru.

Nilitoka kwenda kuonana na mama yangu, upande wake mama hakuwa na neno zaidi alionesha kuwa na furaha sana, bila kusahau alizikumbushia zile pesa zake alizopewa na Iryn. Tuliongea kuhusu safari yake ya kurudi mkoani na tulikubaliana aondoke jumatano na nilimuahidi kumkatia ticket ya ndege.

Wakati nikiongea na mama kwa upande mwingine Asmah alikuwa akinipigia simu, hivyo baada ya kuongea na mama nilitoka nje kuongea naye. Kwa upande wake alinambia anaendelea vizuri ila alihapa hatokunywa tena pombe maana imemsumbua sana, na mimi niliishia kucheka tu.

Kwa upande wake alishangaa sana mimi kumuacha salama maana kwa ile hali aliamini asingenusurika kwenye mdomo wa mamba. Nilimwambia siwezi kumla mwanamke ambaye kalewa na hajielewi, kwani ni sawa na kubaka na sio jadi yangu.

Asmah alisema anajiandaa kwenda hotelini kwaajili ya kwenda kupata chakula cha mchana na mimi nilimwambia sitokwenda na nilimpa sababu ya kutofanya hivo, nikamuomba aniwakilishe vizuri.

Baada ya kuagana na Asmah nilimpigia simu Iryn ili nimu-wish heri ya mwaka mpya, lakini hakupokea simu zangu na nikampigia simu Jane na Mzee Juma.

Saa 12 jioni tuliondoka familia yote kwenda Mlimani city kwaajili ya kupata chakula cha jioni pamoja na kufanya kikao chetu pamoja na mama.

Baada ya kuwasili tulikwenda kukaa pale Instanbul na kila mmoja aliagiza chakula anachotaka kula,

MAMA: “Angalau hapa naona chakula cha kuagiza, sio kule ulikonipeleka siku ile ni kwa kizungu.”

Tuliishia kucheka pale na story zingine zikaendelea taratibu huku tukipata chakula.

Baada ya kula mama alimuomba Elena atupishe ili tufanye maongezi. Mama aliongea na sisi kirafiki, siwezi taja vitu vyote ila nitawapa baadhi,

MAMA: “Wanangu nimekaa na nyinyi kwa mwezi mzima na jumatano nitaondoka kurudi nyumbani nitawaacha. Kipindi nilichokaa na nyinyi kuna mambo bado naona hayako sawa, hasa kwenye suala la kuaminiana, hapa kuna shida. Kama mtashindwa kuaminiana sasa, mkifunga ndoa mtaweza kubadilika? Eti mkamwana wangu.”

WIFE: “Mama kwasasa tumeyaweka sawa na hili ondoa wasiwasi kabisa.”

MAMA: “Sawa, jambo lingine naona wote mko busy, na mtoto muda wote yuko na dada. Naelewa mama J anasoma kwasasa na wewe upo busy kutafuta hela, lakini naombeni muwe mnatenga muda wa kukaa pamoja na mtoto hata kwenda kutembea kwa siku za jumapili ni muhimu.”

MIMI: “Mama hili ni kweli kabisa na sikupingi, lakini huwa tunatoka mara moja moja na mimi kama niko free huwa nashinda home na Junior.”

MAMA: “Junior amemzoea Elena kuliko mama yake, hajali hata kama ana mama, mshukuruni sana Mungu mmepata dada mzuri anayejali mtoto.”

MIMI: “Mama hili tulishaongea na mama J analifanyia kazi, ndomana sometimes huwa anakwenda na dogo dukani.”

MAMA: “Ndoa mtafunga lini? Naomba mniambie ni nini mlipanga?”

WIFE: “Mama tulikubaliana tufunge ndoa nikishamaliza chuo naona ni sawa tu, baada ya kumaliza chuo tutafunga ndoa.”

MAMA: “Kama mmekubaliana wote na kuafikiana hakuna shida mimi sina tatizo, nitaendelea kuwaombea na nyie mjiombee.”

WIFE: “Mama usijali.”

Baada ya kumaliza kikao chetu tuliondoka kurudi home kulala na sikuamini kama wife angeongea vile kuhusu suala la ndoa.

****
Jumatatu nilikuwa nina miadi ya kukutana na mama wa2 pale kwake maana aliomba tumpe kampani binti yake Pili kumrudisha shule.

Saa 4 asubuhi ontime nilikuwa kwake Madale, nilikaribishwa ndani na pale seblen alikuwepo binti yake Rachel. Nilikaribishwa chai dining na wakati nikiendelea kunywa Pili alikuja na tukawa tunaongea,

MIMI: “Mbona unawahi sana kurudi shule?”

PILI: “Mwaka wa mwisho huu ndomana.”

MIMI: “Aisee, mwaka huu tunaanza chuo kabisa, hongera zako.”

PILI: “Hahaa thank you, nimefurahi umekuja maana umetususa siku hizi.”

MIMI: “Wewe maliza shule tutaanza kula misele sawa?”

PILI: “Kwenye graduation yangu si utakuja?”

MIMI: “Kwanini nisije tena graduu ya mke wangu, lazima nije unafikiri mama mkwe atanielewa?”

Na muda huu mama wawili alikuja pale dining akiwa ameshikilia funguo za gari,

MAMA WA2: “Naona unampa mawaidha mke wako.”

MIMI: “Ningekuwa sijaoa, huyu ningeoa kabisa.”

PILI: “Naweza kuwa mke mdogo haina shida ili na mimi nipate mtoto mzuri kama Junior.”

Tuliishia kucheka pale dining na mama wa2 na alinirushia funguo za gari na akasema nikaitoe gari ili tuondoke kwenda Bagamoyo.

Wakati tuko njiani nilikuwa nikimsisitiza sana Pili asome kwa bidii na aachane na viboy kama anavyo, kwani wazee wa kula kimasikhara hawajawahi kufeli na nilikuwa serious wakati naongea naye.

Mapema sana tuliwasili Bagamoyo shuleni na baada ya kushuka tulipiga picha za pamoja kama ukumbusho. Mama wa2 alikwenda kumkabidhi binti yake na tukaondoka kurudi mjini, hatukutaka kupoteza muda kabisa.

Baada ya kuachana na mama wa2 nilikwenda ofisini lakini nilianza kwanza kupitia Mikocheni ili nionane na Lucy, ukizingatia ile siku ya mkesha tuliachana bila kuagana.

Nilimkuta Lucy anahudumia mteja hivyo nilikwenda ofisini kuangalia report kama zimetumwa, tulikuwa tunasubiri report zote za kufikia 31/12 ili tuanze kuandaa financial reports.

Nilitoa simu yangu na nilikuta Iryn kanipigia kama mara 3 hivi na nili-mcall back palepale na haikuchukua muda alipokea simu yangu,

MIMI: “Baby mambo unaendeleaje?”

IRYN: “I am good, toka tuachane juzi hujanitafuta tena na nikikutafuta simu zangu hupokei.”

MIMI: “Baby, jana nimekupigia hukupokea.”

IRYN: “Ulipiga tena?”

MIMI: “No”

Na palepale akakata simu, nikampigia tena ila hakupokea nikaamua kuachana naye.

Lucy alikuja ofisini, akakaa kwenye coach na ile kumtizama alikuwa akiniangalia, dizaini ya mtu ambaye anasikitika kwa kutikisa kichwa,

MIMI: “Mbona hivyo mumy kuna shida?”

LUCY: “Juzi ulikwenda mt*mba Asmah, afu mnaoneshaba mapenzi yenu hadharani mbele ya Sumaiya, mnaakili kweli nyie?”

MIMI: “Hapana sijafanya chochote na Asmah, afu mapenzi gani niliyaonesha kwa Asmah, mbona tulikuwa kawaida tu.”

LUCY: “Insider unakera sana sometimes, sasa unajiachiaje vile mbele za watu, hata kama unafanya bhasi kwa akili.”

MIMI: “Lucy taratibu naona umepaniki, hamna sign yoyote niliyoonesha kwa Asmah, kama ulimind nilivyowaacha pale labda useme.”

LUCY: “Nope hata sijamind kwa hilo but becareful una maadui wengi sana.”

MIMI: “I know, kama kuna something fishy kinaendelea kati yetu hata nisingeenda kukaa naye pale. Na wewe unajua fika Asmah ni mtu wangu karibu sana toka naanza kwenda Masaki, ndo yeye mtu wa kwanza kumjua.”

LUCY: “Ukaribu kwa mwanamke uliyemla? You can’t be serious Nigga.”

MIMI: “Tuachane na hayo, naomba nitumie ripoti zangu za wiki iliyoisha ili tuanze kuandaa hesabu.”

LUCY: “Sawa bossy nitakutumia badae.”

Niliagana na Lucy, lakini alionekana kumind na kwa mara ya kwanza Lucy alionesha kuchukia waziwazi na kutopenda mienendo yangu. Niliwaza kama Lucy kafikia hii stage nitakuwa salama kweli? Nilichoma mafuta kwenda Masaki.

Baada ya kuwasili Masaki niliingia ndani na nilikwenda straight reception kumsalimia Hilda na baada ya kuniona alionesha tabasamu na tukaendelea kupiga story. Kubwa alilamika niliondoka bila kumuaga pale kwa mama Janeth maana alitegemea ningempa lift. Niliamua kupoteza mada kwa kumuuliza kama Asmah yupo na akanambia yupo ndani ofisini.

Kipindi niko njiani kuingia ofisini dada wa clearing alinipigia simu na habari kubwa alinambia kuna haja ya kwenda Zanzibar ili akaweke mambo sawa ili mzigo usichelewe kutoka na kuna kampuni atashirikiana nayo. Mpaka naingia ndani ofisini tulikuwa tukiongea kuhusu hili jambo na niliona wazo lake ni zuri, hivyo niliinga mkono yeye kwenda huko.

Baada ya kumaliza kuongea na dada nilimsalimia Asmah na yeye alionesha tabasamu kali sana mpaka nikawa naziona dimpoz zake,

MIMI: “Kuniona tu umefurahi, niambie za toka juzi.”

ASMAH: “Fresh tu, nimefurahi kukuona, na mbona umechelewa kuja ofisini?”

MIMI: “Nimetoka Bagamoyo ndo nimepiliza huku.”

ASMAH: “Iryn kapiga simu kanifokea sana anataka ripoti zake.”

MIMI: “Anakufokeaje wakati wewe huhusiki na ripoti?.”

ASMAH: “Sasa mimi ningefanya nini? Nimemwambia ripoti unazo wewe na haujafika ofisini bado, alinichonijibu eti tunafanya kazi kwa mazoea.”

MIMI: “Achana nae watakuwa wamemtibua huko, afu hasira zake anataka kuzimalizia kwako. Na wewe acha unyonge, kuwa kama Sumaiya alivyokuwa anamvimbia.”

ASMAH: “Sumaiya alikuwa na jeuri ya mama Janeth, mimi natolea wapi hio jeuri?”

MIMI: “Siku utakayo kubali nislide hizo legs, utapata jeuri ya kumvimbia.”

ASMAH: “Bhana, andaa hizo reports mtumie mapema asije akapiga tena simu.”

Nilipata wazo la kwenda Zanzibar pamoja na dada Agent, lakini niliona ni vema nikaenda na mtu mmoja kule Zanzibar, kati ya Asmah na Hilda. Kwenda na Asmah Zanzibar niliona ni msala maana tukienda kule tunaweza fanya maafa makubwa, niliona bora niende na Hilda.

Nilishinda ofisini mpaka usiku na niliondoka na Hilda kurudi home na kipindi tuko njiani nilimwambia ajiandae ijumaa tutakwenda wote Zanzibar.

Baada ya kuachana na Hilda nilielekea na uelekeo wa Mwakibaki road na nilimpigia simu Iryn kumpa taarifa ya kwenda Zanzibar, na yeye kwa upande wake alisema ni wazo zuri.

Kwa upande mwingine alifurahi sana kuisikia speech yangu na alinambia mama Janeth kamtumia clip ambayo nilikuwa nazungumza. Iryn alifurahi sana kumpaisha mbele za watu na akanipa ahadi ya kuja Dar week ijayo kwaajili yangu, kwani kanimiss.
****
Jumatano mama alikuwa anaondoka kwenda mkoani na nilimkatia ticket ya ndege kama nilivyokuwa nimempa ahadi. Mama kwa upande wake alikuwa na furaha sana maana ndo alikuwa anapanda ndege kwa mara ya kwanza katika historia ya maisha yake.

Saa 4 asubuhi tuliondoka familia nzima kwenda Airport JNIA na baada ya kuwasili maeneo yale tuliweza kuonana na dada TYNA. Sikumwambia mama wala Tyna kama nitawakutanisha kwani nilitaka iwe surprise.

Mama baada ya kumuona Tyna walikumbatiana kwa bashasha ukizingatia ni kama binti yake, afu mama yake na mama yangu ni marafiki pia. Waliongea mambo mengi sana na tukaishia kupiga picha ya pamoja. Pia, Tyna alishangaa sana kuona Junior anakua kwa kasi maana mara ya mwisho kumuona alikuwa ni mdogo sana.

Mama alicheck-in kwaajili ya kuanza safari na sisi tukaondoka maeneo yale, lakini mimi nilikuwa na ratiba za kwenda ofisini, hivyo nilimwambia mama J afanye kurequest usafiri wa kuwarudisha home.

Baada ya kuwasili ofisini nilimkuta Asmah hana furaha na nilistaajabu kumuona akiwa vile na sio kawaida yake kabisa, nilihisi huenda anaumwa au kuna jambo linamsumbua.

Nilisogea mpaka usawa wake kumuuliza tatizo ni nini mbona yuko vile?

ASMAH: “Insider kwahiyo umeona bora kwenda Zanzibar na Hilda na sio mimi?”

Ofcourse ni maamuzi ambayo hayakuwa fair, ukweli nilipaswa kwenda Zanzibar na Asmah, lakini sasa niliona ni msala kwenda naye kule. Niliwaza nampa jibu gani huyu mrembo, ili anielewe?

MIMI: “No sio hivyo, na wala usinifikirie vibaya, nimefanya hivi ili kuepusha maneno yasiyo na maana na wangesema nakupendelea sana. Pia, hii ofisi nani wa kumwachia kwa kipindi hiki kama wote hatupo? Wewe tulia kuna safari kibao zinakuja huko mbeleni, uta enjoy.”

ASMAH: “Nilitamani kwenda Zanzibar ni muda sijakwenda, nikapumzishe na akili yangu.”

MIMI: “Nikirudi kutoka huko, tutapanga tena siku ya kwenda Zanzibar wote hii unaonaje?”

Asmah aliishia kuniangalia bila kusema kitu na muda huu simu yangu ilianza kuita na ile kucheki ni Ghati alikuwa akipiga, nilitoka kwenda kupokelea simu yake mbali.

Ghati alinipa taarifa kuwa anaumwa na mtoto wake na wako home Mbweni. Zilikuwa ni taarifa mbaya kwangu na nikampa ahadi ya kuonana naye badae maana nilikuwa nina ratiba za kwenda kwa Jane hii siku.

Jioni nilitoka kwenda Mbweni kuonana na Jane na baada ya kuwasili pale kwake niliweza kuonana na mdogo wake Vicky.

Vicky alinikaribisha ndani na kwa mara ya kwanza toka Jane ajifungue nakuta pale sebleni hakuna watu. Tulikaa tukiendelea kupiga story za hapa na pale kwani ilikuwa ni muda umepita bila kuonana.

Jane alitoka chumbani akiwa na mtoto na niliomba nimshike tukaendelea na maongezi yetu. Maongezi yetu makubwa yalibase kwenye sakata la kufungua biashara na nilimwambia mama mkwe wangu ameridhia, hivyo tutafute siku ya kukutana naye.

Jane alifurahi sana kusikia hizi taarifa na akanambia ni arrange siku then twende, na nilimwambia nikisha confirm kwa mama mkwe nitampa taarifa. Tuliendelea kupiga story na alikumbushia tena kuhusu zawadi nayotaka kutoka kwake na nikamwambia siku ambayo tutakutana na mama mkwe, nitamwambia.

Mida ya saa 12 niliwaaga na mpango wangu kichwani kwenda kwa Ghati. Nilianza kwanza kupitia supermarket nikanunua mazaga ya kutosha, then nilikwenda straight kwa Ghati.

Baada ya kufika kwenye apartment yake, niligonga mlango, dada wa kazi ndo alitoka kunifungulia na kunikaribisha ndani.

Ghati alitoka ndani na baada ya kuniona alionesha kufurahi sana, lakini alikuwa kavaa kipant kifupi kinachoishia mapajani na shepu yake ilikuwa ikionekana barabara.

Nilijikuta na concentrate kumtizama na muda huu mtoto wake alitoka ndani nikambeba. Dogo alionekana kuumwa kweli na niliaambiwa ni homa zinawasumbua ila kwasasa wanaendelea vizuri.

Nilishinda na Ghati mpaka usiku nikapata dinna kabisa ndo nikaondoka kurudi home.
***
Ijumaa ilikuwa ndo safari ya kwenda Zanzibar na tulitarajia kuondoka na boti ya saa 6 mchana. Kwa upande mwingine dada agent alikuwa kawasili muda sana Zanzibar na alinambia anaendelea na process.

Nilimpa taarifa wife nakwenda Zanzibar na nilifanya kurequest uber ya kutupeleka Posta. Nilimpitia Hilda home Morocco na alitoka akiwa amependeza sana na niliishia kumwagia masifa kedekede, na tukaendelea na safari yetu ya kwenda Posta.

Tulianza safari ya kwenda Zanzibar na Baada ya kuwasili Zanzibar tulikwenda moja kwa moja hotelini kupumzika maana nilikuwa nishafanya booking ya room mapema sana.

CHAPTER 15.
 
.
Mary kumponda mdogo wake Priska kwamba ndio alikua na makosa ni kujikosha tu kwahuyo Insaida anasahau damu nzito kuliko Maji na katu mwanaume sio ndugu yako ptyuuuuu!

Naendelea nilipoishia

🙇🙇

Cc Smart911
 
Badae nitawataja washindi zangu. Nilipata msiba mkoani, nimerudi jana usiku.
Aisee pole , watu walipaniki mno wakataka kuja kukusweka rumande kuwa hujawapa episode
Anajishtukia tu aone reaction ya jamaa anaonekana anamtaka leolesho

Cc Smart911
Sema mkiringa na mwanaume Kama anakupenda anafurahi kukubembeleza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…