Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

uzi naona unanalibia ukingoni mana episode zinakuja kwa kuvizia sana . Ila mkuu insider Movie yyte sterling akifa au kuonesha uzembe mwishoni ina unmask uzur wote yan inaua mazuri yote .piga mashine ryne tena unanza na romance ndani kwake halafu zamisha mkunyenge wengi tutaona ww ni shujaa kijana mtafutaji na mpambanaji lakini pia rijali hupend uzembe .Nakuomba sana. lakin lia uzi wako nimejifunza vingini kama huyaojali inbox tuchat ya maisha sasa plz
 
“Insider thank you very much, I was wrong that day kusema kila mtu afocus na maisha yake, I’m sorry.”

Hapo ndo patamu kuliko hata denda lenyewe.
 
Shukrani mkuu..... pia uko sahihi hiii Ni JF Kila mtu ana uhuru wa kuwasilisha mawazo,mitazamo na maono yake.......MFANO Kuna I'd hapa jf inatambulika Kama BMX 6 ana story inaitwa 'hatima ya maisha yangu ipo kwa kijana wa buguruni'... something like that Kama sijakosea

Hivi mkuu ulishawahi kuipitia???.....vipi uandishi??? Mbona Kama ni same person......Acha niishie hapa

Eb nitag nikaisome mkuu
 
EPISODE 45


IN LOVING MEMORY OF MR. PAMA (2022).

CONTINUE….

Taarifa za Jane kuhusu kifo cha Mzee Pama nilihisi kama utani hivi, niliwaza huenda Jane atakuwa kachanganyikiwa huko. Ni taarifa ambazo zilinishtua sana kwa upande wangu, nilikuwa nahisi kutetemeka.

“Mzee Pama nimeongea naye juzi tu leo hii awe amekufa haiwezekani, acha nitoke niende Mbweni kwa Jane.”

Nilitoka chumbani na niliwakuta Mama J na Iryn wako seblen wakipiga story na baada ya kuniona niko kimtoko, Mama J alianza kuniuliza,

“Baba Junior unakwenda wapi usiku huu?”

“Nimepata taarifa za msiba wa Mzee wangu mwenye hiyo gari.”

Ni taarifa zilizowashtua pale na zilionekana kuwagusa muda huu.

“Insider tunakwenda wote ngoja nikavae sweta” ilikuwa ni sauti ya Iryn akitaka tuondoke wote na mimi sikutaka kumzuia.

Tuliondoka pale nyumbani na tulitumia muda mfupi sana kuwasili pale Mbweni na tulifunguliwa geti, nikaingiza gari ndani.

Muda huu nilikuwa nikisikia sauti za vilio kwa mbali na tuliingia ndani seblen. Tuliwakuta Jane akiwa ameegemea kwa mama yake akilia na mama yake akimbembeleza mwanae. Niliona huruma sana kwa Jane maana Mzee Pama amekufa bado Jane ana mimba ndogo, ukweli iliniuma sana.

Nilitumia nafasi hii kuanza kumbembeleza Jane na Iryn naye alisogea karibu lakini ilikuwa ngumu sana wakati huu kumtuliza akilia. Na muda huu ilibidi nimsogelee mama nianze kuongea naye wamezipataje taarifa.

“Mama mmezipataje taarifa?”

“Kuna mtu amepiga simu toka saa 3 usiku na akampa Jane hizi taarifa.”

Ilibidi nimwambie mama amtulize Jane ili tupange mipango mapema kabla watu hawajaanza kujaa. Tulipanga tuandae ma-tent pamoja na mziki kwa asubuhi kukicha pamoja na suala la chakula.

Jane alitransfer kiasi cha milioni 3 kwenye simu yangu kwaajili ya kukamilisha hayo masuala yote muhimu. Baada ya kumaliza mipango yetu ilibidi tumwache Jane akapumzike maana alikuwa amelia sana kwakweli.

Baada ya lisaa walikuja wageni wengine watano na vilio viliendelea ilikuwa ni huzuni sana pale Mbweni. Saa 7 usiku Iryn aliondoka na aliniacha mimi pale Mbweni, sikuwa na jinsi ya kuondoka pale ilibidi nilale tu.

Muda huu nilikuwa nakumbuka matukio yote ambayo nilikuwa na Mzee kwa vipindi tofauti. Nilikumbuka ile siku ambayo tuliongea na Mzee Pama na akanitumia milion 6, niliwaza huenda ilikuwa ni kama farewell Mzee alikuwa ameona kifo chake. Pia na suala la kunisisitiza sana kumwangalia Jane nilihisi Mzee alikiona kifo chake Mapema sana. Niliwaza pale Mzee alikuwa anasumbuliwa na nini? Maana alikwenda India mara mbili.

Usiku nilikesha tu pale seblen kwakweli maana nilikuwa nahisi kama niko Dunia nyingine kabisa nilikuwa siamini kama kweli Mzee Pama amekufa, nilikuwa naona kama utani.

Asubuhi mapema sana nilikwenda kutoa taarifa kwa Mjumbe wa nyumba 10 kuhusu msiba na aliweza kunipa connection ambapo nitaweza pata matents na viti. Baada ya kufanya mawasiliano na hao wanaokodisha matent nilikwenda Boko Magengeni kuonana na mhusika ndo alikuwa anapatikana maeneo yale. Nilifanikiwa kupata matent mawili na viti 50 na pia nilifanikiwa kupata mtu wa mziki kupitia jamaa wa matent.

Tuliondoka Boko na kwenda Mbweni na nilimwacha jamaa akiendelea kutengeneza na mimi nilikwenda kutafuta vitu vingine kama vinywaji na mahitaji mengine. Kuhusu mtu wa chakula nilimpata mama mmoja alikuwa anakaa kulekule Mbweni. Mpaka kufika saa 3 asubuhi kila kitu kilikuwa kipo sawa tayari na DJ alishakuwa ameanza kuplay nyimbo.

Nilipata wazo la kuwasiliana na Mary na nilimpa taarifa za msiba wa Mzee maana alikuwa anamjua. Kwa upande wa Mary taarifa hazikuwa nzuri kwakweli na aliishia kuhuzunika tu, na Mary alilsema ndani ya muda mfupi atakuwa amefika eneo la tukio hivyo nimtumie location tu.

Saa 4 asubuhi Mary alikuwa kawasili tayari pale Mbweni hivyo kidogo nikawa na mtu wa kunipa kampani. Baada ya Mary kuwasili pale alianza kulia pale nje na mimi niliishia kumkumbatia na kumfuta machozi.

MARY: “Insider chanzo cha kifo ni nini?”

MIMI: “Kwakweli sijui mara ya mwisho kuongea na mzee ilikuwa jumatano na alisema anakwenda India. Nafikiri tutajua tu, nahisi mzee alikuwa anaumwa.”

MARY: “Yeah itakuwa hivyo, Mzee alikuwa ni mtu mzuri sana. Mungu amlaze mahali pema peponi.”

Mpaka muda huu nilikuwa sijui kifo cha Pama kimesababishwa na nini lakini Roho ilikuwa inaniambia ni ugonjwa. Kwa upande mwingine wageni walikuwa wakizidi kuingia taratibu na ilivyofika saa 5 Iryn alikuja pia.

Hii siku ukweli nilikuwa busy sana ni kama nilikuwa operation manager simu zote za wageni zilikuwa zinapigwa kwangu. Nilikuwa nakazi ya kuwalekeza wageni mpaka Mary akanipa wazo la kutengeneza mabango ya kuelekeza direction ya msiba ulipo.

Kwenye mida ya saa 6 mchana kuna wageni niliwapokea na walijitambulisha kwangu kama marafiki wa mzee Pama, na walisema wana mazungumzo private na Jane. Ukweli wote tulikuwa hatujui kilicho kuwa kinaendelea kuhusu taratibu zote za mazishi. Mipango na kila kitu vilikuwa vinafanyika Ununio kwa mke mkubwa, Jane alikuwa ni mchepuko tu.

Jioni nilikaa na Iryn akanambia kutokana na msiba hataondoka kwenda kwenye apartment yake mpya mpaka mambo ya msiba yaishe. Jioni Iryn aliomba kuondoka na mimi sikuona sababu ya yeye kuendelea kubaki maeneo haya hivyo nikafanya kurequest Uber impeleke home.

Mary alikuwa kampani yangu kubwa sana kipindi hiki na alikuwa akijituma sana asee, ungemwona usingekubali kama ni mtoto wa kishua. Mary alikuwa ananikosha sana mpaka nikaanza kujuta kwanini nilidate na Prisca?. Mary alikuwa kama wife material asee akiwa na khanga yake kiunoni.

Saa 4 usiku Mary aliniaga na akanambia asubuhi atakuja mapema, na mimi nikampa kampani ya usafiri mpaka kwao.

*******

Jumatano mwili wa marehem ulikuwa unatarajiwa kuwasili Dar es Salaam kutoka nje. Kwa upande mwingine ndugu wengi wa Mzee Pama walikuwa wanakuja kutoa pole kwa Jane.

Mzee Juma rafiki wa Pama alikuja Mbweni hii siku na tuliweza kuongea na kubwa alinambia ana maelekezo kutoka kwa Mzee Pama, hivyo taratibu zote za msiba zikikamilika tutaonana. Mzee Juma alinishukuru sana kwa jitihada zangu na jinsi navyojitolea pale msibani.

Jioni walitoka na Jane kwenda Airport kwaajili ya mapokezi ya Mwili wa marehem na ulikuwa unatarajiwa kuwasili usiku. Na taarifa nilizo zipata ni kwamba alhamis itakuwa ni siku ya kuaga mwili kwa hapa Dar na baada ya hapo utafirishwa mpaka Tabora na mazishi yatafanyika huko kwao.

Ile jioni nilimwambia Mary nitakwenda Tabora kwaajili ya mazishi na yeye akasema tutakwenda wote, na mimi sikuweza kumzuia. Niseme mimi na Mary tulikuwa bega kwa bega mpaka watu walikuwa wanafikiri sisi ni wenyeji wa pale.

Alhamis ndo ilikuwa siku maalumu ya kuaga mwili wa Mzee Pama pale kwake Ununio. Mwili ulikuwa unatarajiwa kuagwa saa 5 asubuhi na jioni ungesafirishwa kwenda Tabora.

Mimi na Mary tuliwasili mapema sana eneo la tukio tukitokea Mbweni. Hii siku kulikuwa na watu wenye hadhi, wakubwa na baadhi ya viongozi wa serikali hadi wastaafu. Mzee pama alikuwa ni mtu ambaye anajulikana sana na watu, hadi wazungu na foreigners walikuwepo hii siku.

Kwa upande mwingine Jane naye alikwenda mpaka Ununio kwaajili ya kuaga mwili na nilisikia kulikuwa na mke mwingine tena wa Mzee Pama alikuja pale.

Muda huu zilikuwa zinaonekana nyuso za huzuni sana, jinsi gani kifo cha Mzee Pama kilishika hisia za watu. Kila mtu alikuwa akimwongelea Mzee Pama kwa mazuri na pia aliwasaidia watu wengi sana enzi za uhai wake.

Mazingira yote ya pale kwa Pama zilionekana gari kali tu nazungumzia VX, V8, Range rovers, Jeeps, BMW, nknk. Gari zilijaa karibu mitaa yote ya karibu. Mzee Pama hakuwa mtu mdogo kabisa na eneo hili lilikuwa chini ya ulinzi mkali sana.

Mpaka saa 7 mchana zoezi la kuaga mwili lilikuwa limekamilika na mimi nilirudi Mbweni kwaajili ya kuweka mambo sawa kabla ya safari ya kwenda Tabora. Kwa upande mwingine Mary naye alikwenda home kujiandaa kwaajili ya safari ya baadae.

Ilibidi nirudi Mbweni ili kuweka mazingira vizuri kabla sijaondoka na lengo ilikuwa niwatambue watu ambao walikuwa wanabaki pale kwaajili ya usalama. Na watu waliobaki pale walikuwa ni ndugu wa Jane na baadhi ya rafiki zake. Na muda huu nilipata wazo nitafute Mlinzi wa kukaa pale getini kwaajili ya ulinzi.

Baada ya kuweka mambo sawa nilirudi home kubadilika na kuchukua baadhi ya nguo. Wakati naondoka nilimuaga Iryn naondoka kwenda Tabora na yeye alinitakia safari njema na akanikumbatia.

“Insider nawish nikupe kampani lakini itabidi nibaki kwaajili ya uangalizi wa biashara.”

“Usijali kuwa na amani mpaka sasa mchango wako umeonekana.”

Ilinibidi niache gari na nilirequest Uber ya Bajaji na wakati nasubiri pale kibarazani uliingia ujumbe wa TIGOPESA na kucheki Iryn alikuwa kaniingizia 500,000/=. Nilitabasamu ni kama alijua sina hela, ukweli ni kwamba nilikuwa nimetoboka sana hizi hela ndogo ndogo zilikuwa zinanitoka balaa pale msibani, hata ile Pesa aliyokuwa amenipa Mzee nilikuwa nishapunguza million 2 tayari kwenye masuala ya msiba.

Nilimpitia Mary pale kwao na alikuwa yuko tayari na alikuwa kavaa nguo full black kuanzia raba, T-shirt na miwani, kasoro skin jeans ilikuwa ya blue. Pia alikuwa kaninunulia miwani meusi na mimi kama zawadi.

Saa 9 alasiri tulikuwa pale Ununio kwajili ya kupata usafiri na tuliikuta costa moja tu imebaki na ilikuwa imejaa tayari. Wakati tukiendelea kushangaa pale na kuwaza namna ya kuondoka tulibahatika kupata gari landcruiser V8 ambayo ilikuwa inakwenda msibani na ilikuwa na seat 2 tu zimebaki.

Tuliondoka pale Ununio saa 10 jioni na Ilikuwa ni safari ya masaa 10 mpaka tunafika wilaya moja ya huko Tabora. Nakumbuka tulifika saa 8 usiku na baada ya kuwasili pale wilayani mjini tulikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Mzee Pama, uzuri hakuwa mbali na pale mjini.

Mzee alikuwa amejenga bonge la mjengo na lilikuwa ni eneo kubwa sana ambalo alikuwa anaishi mama yake na baadhi ya ndugu zake. Ndani ya mjengo kulikuwa na garden kubwa na mazingira mazuri sana na yenye kuvutia.

Tulivyofika pale tulikuta msiba unaendelea na watu wengi walikuwa wame wasili tayari na wengine walikuwa wakiwasili. Mary aliingia ndani kuonana na Jane na sisi tulikaa pale nje tukiendelea na mkesha.

Story zilizokuwa zinasikika hapa ni pamoja na utajiri wa Mzee Pama, nilijua Mzee Pama alikuwa ni mstaafu moja ya kampuni kubwa ya uchimbani madini. Pia Pama alikuwa ana miliki vitalu vya dhahabu, bado alikuwa na kampuni ya madini. Alikuwa na mali na Pesa chafu bado alikuwa anamiliki mahotel na nyumba kibao, ila sasa ungemwona Pama jinsi alivyokuwa, alikuwa anaonekana wa kawaida sana.

*******

Ijumaa ndo siku ambayo Mzee Pama alilazwa kwenye Jumba lake la milele na mazishi yalianza mapema sana. Watu wa Tabora waliaga maiti na hata wengine wa Dar ambao hawakufanikiwa kuaga nao waliaga na wale waliotaka kuaga kwa mara ya mwisho walipewa nafasi.

Muda huu kulikuwa na vilio kila kona yaani daah moja ya siku ambayo siji kuisahau ni hii, watu walilia sana huku Tabora vilikuwa ni vilio na huzuni.

Kwa upande mwingine Mzee alikuwa kaandika waraka ambao aliwatambulisha wake zake wote kuanzia mke mkubwa, Jane na alikuwepo mke mwingine ambaye alikuwa na watoto 2 ambao wote ni wa kike. Mzee pama alikuwa na bahati sana na watoto wa kike ni Jane pekee ambaye alikuwa na mimba ya mtoto wa kiume.

Mzee Pama aliandika mambo mengi sana na mwisho kabisa alisema ameandika barua kuhusu mirathi itakavyogawiwa kwa wake zake, watoto na ndugu. Pia aliwataja baadhi ya marafiki zake akiwemo Mzee Juma wawe waangalizi wa Familia yake na baada ya kumaliza kusoma ule waraka kila mtu alibaki na huzuni. Ulikuwa ni waraka mrefu ambao ulikuwa umegusa sana hisia na mioyo ya watu.

Baada ya sala na kila kitu Pama aliingizwa ndani ya Jumba lake la milele. Ni kaburi ambalo lilikuwa limejengwa ndani na likafunikwa kwa nzege juu.

Familia ya Pama ilikuwa na makaburi yao na yalikuwa palepale kwake kwa upande wa nyuma na yalikuwa ndani ya uzio/fense. Makaburi yalikuwa na uzio wake ambao umeungana na nyumba na gate la kuingilia makaburini lilikuwa kwa nyuma linajitegemea na upande wa nyumba.

Kwa upande wa Familia ya Pama walizaliwa watoto wa4 tu kwa Baba yao, Pama alikuwa wa kwanza kuzaliwa, aliefuatia ni dada yake, watatu alikufa na wa mwisho alikuwa ni mdogo wao wa kiume. Baba yao alikufa na walikuwa wamebakiwa na mama yao tu, mpaka kifo cha Pama walikuwa wamebaki watoto 2 na Mama yao.

Hii siku pia nilibahatika kuwaona watoto wote wa Mzee Pama mpaka yule Binti yake wa kwanza mkubwa wa Canada na yule anayesoma Australia.

Mpaka saa 8 mchana mazishi yalikuwa yamekwisha na taratibu zote zilikuwa zimekamilika. Baada ya hapo tulirudi nyumbani kwaajili ya chakula huku taratibu zingine zikiendelea.

Baada ya kumaliza mazishi ule usiku watu walikuwa wamekaa kwenye magrupu wakinywa bia. Kulikuwa na bia za kila aina na nyama choma za kutosha maana kuna gari ilileta vinywaji na nyama kwa wingi, mbuzi na ng’ombe. Kama mnavyojua wabongo wakisha maliza kuzika wanasahau wanaanza kunywa ili kupunguza stress.

Na mimi muda huu nilikuwa nimekaa na watu wazima tukipigia story mbalimbali. Kwenye group letu kulikuwa na wazee na wababa ni mimi pekee nilikuwa kijana. Story zilizokuwa zinapigwa hapa ni siasa na biashara ofcourse nilipata idea nyingi sana za biashara ila shida maokoto tu ndugu zangu.

Mary alikuja akaliunga na sisi pale na story zilikuwa zikiendelea na kila mtu alikuwa anaelezea jinsi alivyokutana na Mzee Pama mpaka kifo chake. Mary alionekana kuchoka sana na aliishia kulala kwenye mapaja yangu.

Huu usiku pia niliweza kuongea na Mzee Juma na tukaagana maana alisema kwa kesho tusingeweza kuonana atakuwa busy na kikao. Mzee Juma alisema ataendelea kubaki pale kwa siku mbili na tutaonana Dar akirudi kwa ajili ya mazungumzo zaidi. Alinipa pesa ya nauli kwaajili ya kurudia Dar na baadae kuja kuhesabu ilikuwa ni laki 3.

Ile Jumamosi asubuhi watu wengu walianza kuondoka pale kwa Mzee Pama na mimi nilimwambia Mary tutaondoka na ileile V8 tuliyokuja nayo.

Saa 6 mchana tulitegemea kuanza safari ya kurudi Dar na kabla ya kuanza safari nilitumia kuongea na Jane. Jane alishukuru sana kwa kujitoa kwangu kwake na alisema yeye bado ataendelea kubaki mpaka vikao vya familia vitakapo kwisha.

Kwa upande mwingine aliniomba niendelee kumwangalizia nyumba yake maana kule alikuwa amebaki mama yake. Mnajua Jane alikuwa amelia mpaka sauti yake ilikauka na macho yalikuwa mekundu sana.

Saa 6 mchana mapema kabisa tulianza safari ya kurudi Dar na njiani tulikuwa hatujui vibao vya 50 ilikuwa ni spidi tu. Saa 4 usiku tuliwasilia Dar na walituacha pale Ubungo mataa wao walikuwa wanaelekea Tabata. Nilifanya kurequest usafiri kwaajili ya Mary na mimi nilichukua bajaji kwenda Changanyikeni kulala kwa Prisca.

Wiz khalifa ft Charlie Puth- See you Again. [emoji444]

CONTINUE

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Rest in peace mzee pama
 
EPISODE : 59

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

Ile kugeuka alikuwa ni Iryn na Lucy wakija usawa wetu na Prisca alionekana kuwa na wasiwasi sana.

CONTINUE:

Baada ya kufika pale kwenye meza yetu walitusalimia na Iryn alimwambia Lucy waende wakakae meza nyingine. Kwa upande wa Iryn hakuwa na story kabisa lakini Lucy alionekana kumind sana kwa kile alichokiona. Kwa upande wangu sikutaka kuonesha sign yoyote hata walivyokwenda kukaa sehemu nyingine nilifurahi sana kwakweli.

Kwa upande mwingine Prisca na Iryn walikuwa wakipigana sana macho na Prisca uvumilivu ulimshinda ikabidi aanze kuongea,

“Honey yule dada si ndo Bossy wako?”

“Ndio yeye kwani kuna tatizo?”

“Hapana ila sina imani naye.”

“Acha wasiwasi wako na wewe malizia kula tuondoke.”

Baada ya kumaliza kupata lunch ilibidi tuondoke hivyo nikaona itakuwa sio busara kuondoka bila kuwaaga na nilikwenda mpaka kwenye meza yao.

MIMI: “Kwahiyo mmeamua kukaa huku alone sindio?”

LUCY: “Insider hatujataka kuwaharibia maongezi yenu.”

MIMI: “Lucy umeanza lini hizi itikadi?”

Na muda huu Iryn alikuwa amekaa kimya yuko busy na chakula chake, na mimi ikabidi nianze kumzingua,

“Bossy hata wewe unaunga mkono maneno ya Lucy?”

IRYN: “Yuko sahihi sio busara kuingilia maongezi ya watu maana hatujui mna mipango gani.”

MIMI: “Lucy alipiga simu nikamwambia niko Lunch nilitegemea mnakuja kwaajili ya kampani, anyway mimi naondoka, Lucy tutaonana badae ofisini.”

LUCY: “Poa Insider msalimie shem kwa mara nyingine.”

Na mimi ilibidi nicheke tu muda huu.

Niliondoka na Prisca muda huu na baada ya dakika 3 Lucy alinitumia ujumbe uliosomeka

“Insider umezingua sana leo kwakweli na hauna bahati.”

Na mimi baada ya kuusoma ule ujumbe sikutaka kureply, hivyo niliplan badae nitakwenda kuonana naye pale ofisini.

Wakati tuko njiani story zangu na Prisca zilikuwa ni kuhusu suala lake la mimba na mimi niliendelea kumchimba zaidi kutokana na tatizo lake,

“Kwahiyo baby ulishika mimba ili uprove kama ni kweli au laah!?”

“Ndio honey ila kwa kilichotokea naamini nitapona.”

“Upo tayari kunizalia mtoto kama utapona?”

“Yes Honey natamani nikuzalie hata mapacha, pia Sorry kipindi hiki itabidi uvumilie maana nashindwa kukupa utamu, mpaka mwezi upite alisema Doctor.”

“Sasa utanisaidiaje? maana sitaki kuchepuka tena na mwanamke mwingine kwasasa.”

“Nitaangalia namna ya kukusaidia wewe twende home.”

Baada ya kuwasili home pale tulimkuta Mary yuko seblen na sisi tulipitiliza mpaka chumbani kwenda kuoga na baada ya hapo tuliishia kulala kitandani kwaajili ya uchovu.

Jioni niliwasiliana na Jane kubwa alinambia anarudi kesho ambayo ni Jumapili hivyo aliomba niende nikampokee Airport na mimi nilimuahidi kwenda kumchukua.

Baada ya kuwasiliana na Jane ilibidi niwasiliane na Lucy maana nilitaka akitoka ofisini tuonane pale Samakisamaki, Mlimani city.

Mimi nilitoka mapema sana Changanyikeni na niliwaaga akina Prisca naenda kutuma hela na sitokawia kurudi.

Saa 3 nilikuwa tayari niko pale Samakisamaki nikimsubiri Lucy na niliendelea kukimbiza chupa za heineken taratibu. Kwenye saa 4 kasoro Lucy ndo aliwasili maeneo haya na yeye kama kawaida aligiza chupa za Savanna, na story ziliendelea pale.

“Insider leo umezingua sana mshikaji wangu, yaan! niliona aibu sana muda ule na Iryn kanyong’onyea sana, baada ya kula aliondoka kwenda kwake hata chakula hakula vizuri.”

“Lucy wewe ndo uliyezingua wala sio mimi, kwanini ukaja na Iryn muda ule?.”

“Wewe ndo ulitakiwa unambie kama upo na demu mimi sikujua kabisa, wakati kaka anaingiza box kule ndani Iryn alimuuliza yule kaka na alisema umeondoka, muda ule nilikuwa na Iryn. Mimi ndo nikasema nikupigie simu ili nijue ulipo na ulivyosema upo Golden fork Iryn akasema twende wote.”

“Hapa tutaishia kulaumiana tu, kwa upande wangu sikujua ungekuja na Iryn na wewe ulijua niko peke yangu, lakini hakuna kilicho haribika, anasemaje Bossy.”

“Iryn anasema yule ni demu wako na anahisi unakula wote na dada yake, nikwambie kwa hii movie ya leo Iryn ushamkosa tayari.”

“Unajua Lucy kuna jambo bado hulijui kuhusu mimi, nimefahamiana na Iryn kupitia Uber hata hawa akina Prisca nimejuana nao huku na ni wateja zangu mpaka sasa, muda ambao nakuwa free kama wanataka huduma huwa sikatai.”

“Hukunambia hili, Iryn alikuwa anatamani sana kuongea na wewe leo ila ghafla furaha yake ikakata. Nikikuambia Iryn anakupenda huwa unazingua unataka mpaka akwambie nakupenda?. Nafahamu una familia labda unaheshimu hili, ila pia mimi siwezi kuingilia maamuzi yako wewe ni mtu mzima tayari.”

“Upo sahihi mtu wangu sasa kwa hili la leo unanishaurije?”

“Iryn alibadilika sana na alionekana kuumia ngoja kesho nimuone maana atakuja kutengeneza nywele, ila mtafute hata kama unamsalimia tu.”

“Mhh hapana bora kwenda kwake direct nafikiri itakuwa ina nguvu zaidi.”

“Vyote sawa ila usichezee hii bahati kwa mara ya pili tena, goodluck.”

Muda huu Prisca alianza kupiga simu kwa fujo na mimi sikutaka kuzipokea simu zake kabisa.

Tulitumia kama masaa 2 kukaa pale na Lucy na lingine alisisitiza sana niongee na Iryn kuhusu suala la SACCOS. Tuliondoka maeneo yale, yeye alitaka kurequest bodaboda lakini nikampa offa ya gari, Lucy ni bahili sana kwakweli.

Baada ya kurudi home Prisca alianza kufoka na kulalamika kuwa nilienda kwa mwanamke mwingine, hata Mary kwa upande wake ilibidi aanze kumshangaa mdogo wake anapata wapi nguvu ya kunifokea?. Kwa upande wangu sikutaka kuanza maneno naye niliamua kwenda chumbani.

Baada ya kuingia chumbani niliingia kuoga na baada ya kutoka bafuni nilikuta Prisca amekaa kitandani na alianza kujiongelesha pale,

“Baby sorry nimekukosea sana nilipatwa na wivu juu yako, najua unahamu lakini nashindwa kukupa sababu naumwa ila kama unataka chochote nambie mimi nikuridhishe.”

“Ok chezea mti wangu mpaka matawi yaanguke chini na hii ndo adhabu yako, siku nyingine usithubutu kufoka mbele ya dada yako na uwe na adabu.”

“Sawa baby haina shida.”

Na muda huu Prisca alianza kuchezea mti wangu taratibu kama nilivyomuelekeza na alikuwa ana uzamisha kwenye ndoo ya maji mpaka mti ulivyoangusha majani chini ndo tukalala.

Jumapili asubuhi niliwasiliana na Jane na alinambia anatarajia kuingia mapema sana JNIA hivyo saa 4 asubuhi niwe pale. Nilijiandaa haraka sana na nikaondoka kwenda kumpokea Jane na nilisubiri kwa nusu saa na alikuwa amewasili tayari.

Baada ya kumpokea tulikumbatiana pale kwa furaha, kwa upande mwingine tumbo lake lilikuwa kubwa sana kipindi hiki na alionekana kuanza kuchoka.

Wakati tuko njiani nikimpeleka Mbweni tulikuwa tunaongea yaliojiri Tabora hasa kwenye mirathi na Jane alisema Mzee amegawa urithi kwa kila mtu. Kwa upande wake alisema amepewa nyumba nyingine ambayo itakuwa ya mtoto wake atakaye zaliwa na iko Tabora mjini, ni mpya kabisa na alitoa simu akanionesha picha, ni bonge la mjengo.

Kwa upande wa pesa aliingiziwa pesa mingi sana, tuseme Jane alikuwa milionea tayari hata angelala ndani pesa zilikuwepo za kutosha.

Kwa ufupi kila mke wa Pama alipewa urithi na kila mtoto alipata urithi wake mpaka ndugu zake wa damu nao walipewa baadhi ya urithi na maelezo yote Mzee Pama ndo aliandika namna ya kugawa.

Baada ya kuwasili Mbweni tuliingia ndani na nilimsaidia kuingiza mabag yake ndani na muda huu mama yake alikuwa ametoka pale kibarazani kumpokea binti yake. Mdogo wake Vicky hakuwa mbali naye alitoka kumpokea dada yake na baada ya kuniona alinikonyeza.

Jane hakutaka kuingia ndani na tulikwenda kukaa garden kuendelea na mazungumzo yetu pale,

“Insider umeona gari yako nilivyo iharibu?”

“Nimeona zile bampa hazina shida usiwe na wasiwasi.”

“Nitakupa pesa ukanunue gari nyingine hii utaniachia.”

“Usiingie gharama shem tutanunua bampa tu tutabadilisha na gari itakuwa sawa.”

“Sawa utafanya hivo ila ngoja kwanza niendelee kujifunza.”

“Leo nilitaka nikuachie gari yako ujue.”

“Hapana acha niendelee kutumia hii ya kwako hiyo naiogopa eti, afu suala la mbwa vipi? mpaka leo hujanipa majibu, nataka nifuge mbwa wa kunisaidia ulinzi.”

“Nafikiri Rottweiler na Shepherd watakufaa sana na bajeti yake andaa si chini ya million 3 ili tupate mbwa wazuri.”

“Sawa nitakupa hii pesa leo ili uniletee hao mbwa.”

Muda huu Jane aliinuka kwenda ndani na alitoka na pesa kwenye bahasha akanikabishi pale na alinipa laki 2 kwaajili ya kujaza gari mafuta na mimi niliaga pale nikaondoka.

Safari yangu ilikuwa kurudi Changanyikeni na ilikuwa mchana muda huu, baada ya kuwasili pale nilikuta wanapika jikoni, mtu na dada yake na mimi niliishia kuwazingua muda huu.

Baada ya lunch niliwapeleka kwao Mbezi beach maana baba yao alikuwa anarudi hii siku na tulivyowasili pale kwao sikutaka kuingia ndani na niliondoka kwenda kwa mama wa2.

Niilipanga kwenda kuonana na mama wa2 kwa lengo la kumshukuru kwa kumsaidia ndugu yangu kupata kazi na suala la kupata mkopo mwingine ili nimalizie ujenzi kule Dodoma na kulipa deni la kiwanja.

Baada ya kuwasili pale kwake niliingia ndani na nilimkuta amekaa pale seblen anaangalia TV,

“Mama mkwe naona umetulia huna stress.”

“Hahaa mkwe una vituko sana, afu mbona ijumaa hukuja na uliahidi utakuja, nikapika na chakula kabisa kwaajili yako.”

“Nisamehe kwakweli kwanza nimekuja kukushukuru kwa kumsaidia ndugu yangu, pia nahitaji mkopo mwingine.”

“Usijali mkwe hilo ni jambo dogo sana na ameanza training tayari, suala la mkopo ulitaka kiasi gani?”

“Million 20 tu, nataka nikamilishe ujenzi wa nyumba kule ili watu waingie nianze kupata kodi.”

“Sawa niachie nilifanyie kazi afu tutawasiliana.”

“Ahsante mama mkwe maana huwa unaniokoa sana, embu niambie nikufanyie jambo gani kama shukrani yangu kwako.”

“Kamsalimie Pili shuleni Jumapili Ijayo please.”

“Hili usijali mama mkwe nitakwenda kumsalimia mke wangu.”

Nilikaa pale na mama wa2 tukipiga story mbalimbali za maisha mpaka nikapata dinna, na jambo lingine aliniambia mwisho wa mwezi atahamia kwenye nyumba yake Madale.

Baada ya kutoka pale kwa mama wa2 niliamua kwenda Kidimbwi kupoteza muda maana home ningekuwa peke yangu tu. Wakati niko Kidimbwi nikiendelea kukimbiza chupa kwa upande mwingine Muajemi alinitafuta na tulikuwa tukichat kwa whatsapp.

Muajemi alikuwa anaulizia progress ya lile jambo la Iryn na mimi nilimwambia bado nalifanyia kazi ila Iryn bado mgumu sana. Kwa upande wake Muajemi alionekana kukata tamaa lakini nilikuwa nampa moyo ila kwa upande wangu nilikuwa nafurahi sana kuona anakata tamaa.

Nakumbuka hii siku nilikaa mpaka majogoo ndo nikarudi kulala na nilirudi saa10 usiku home. Kwa upande mwingine nilikuwa bado na stress na lile suala la Prisca, ukweli sikuwa sawa ila nilikuwa najikaza tu kiume.

Nililala kidogo tu na alarm ndo iliyoniamsha hivyo ilibidi nijiandae haraka ili nikamchukue mama wa2 kwenda Posta, kama nilivyosema hii kazi ilianza kuwa kero kwangu lakini sikuwa na jinsi maana maji nilikuwa nisha yavulia nguo.

Baada ya kumpeleka Posta mama wa2 niliendelea na ratiba zangu zingine kama kawaida. Wakati niko Mikocheni Mzee Juma alinipigia simu akanambia kesho atarajia kuondoka Dar kwenda nje. Mzee alisema saa 5 asubuhi niwe pale kwake ili tuongee suala langu kabla hajaondoka.

*****
Ile jumanne mapema sana nilikwenda Mikocheni kwa Mzee Juma lakini sikwenda na gari, niliiacha ofisini na mimi nilitumia bodaboda.

Baada ya kuwasili pale kwake nilikaribishwa ndani seblen na Camilla alikuwa seblen pale amekaa, nilimsalimia na mimi kama kawaida nikala buyu hata sikuwa na habari naye.

Camilla alikuwa na uzungu mwingi sana maana hata kuongea na baba yake alikuwa anadekadeka sana, alikuwa ni mtoto pekee wa kike wa Mzee Juma.

Haikuchukua muda sana Mzee juma kutoka ndani na tulianza maongezi pale seblen kuhusu suala langu la kwenda shule.

Kwa upande wangu nilimwambia kwa mwaka huu itakuwa ngumu kwenda shule maana sikuwa nimejipanga bado, kwani nina mambo mengi ya kuyaweka sawa hivyo tulikubaliana nitaanza masters mwaka huu 2023.

Mzee Juma alilikubali pendekezo langu na akasema yeye hana shida ukifika muda huo atanisapoti na pia alinitoa wasiwasi kwa hili. Kwa upande mwingine mzee Juma alikuwa na safari ya kwenda nje na alisema tuondoke wote na tuliongozana na binti yake.

Tuliondoka pale kuelekea Airport lakini tulipitia kwanza Serena Hotel na tulipata lunch, pia mzee alikuwa ana appointment zake. Baada ya hapo tuliendelea na safari yetu na ndani ya muda mfupi tulikuwa tumewasili pale JNIA Terminal 3.

Tulikaa na mzee Juma pale kwa dakika 45 hivi na yeye alituaga pale kubwa alisema tutaendelea kuwasiliana na kama ninakwama kifedha au nina tatizo lolote niwe namjulisha nisiogope.

Baada ya kurudi parking tulikokuwa tumepark gari Camilla alinza kuongea na mimi,

“Can you drive?”

“Hapana siwezi kwakweli itabidi unifundishe kuendesha gari.”

“Mhh really?”

“Nipe card nikalipie parking.”

Njiani tulikuwa tunapiga story mbalimbali na mimi nilimjaribu kumdokezea kutoka out siku moja na Camilla kwa upande wake alisema yeye hapendelei kwenda sehemu zenye kelele, lakini alikubali ombi langu.

“Na kudrop wapi?”

“Utanidrop hata pale Zantel sio mbaya.”

“Kwani wewe una elekea wapi?”

“Naelekea Mikocheni karibu na Palm Village.”

“Twende nikupeleke.”

Bhasi tuliongozana na Cammy mpaka pale ofisini lakini aliishia nje getini na tuliishia kubadilishana namba za simu na yeye aliondoka maeneo yale.
Kwa upande wangu pia sikutaka kuendelea kupoteza muda pale ofisini bali niliondoka kwenda Agha khan hospital kumchukua Prisca na nilimkuta mama yake akimsubiri.

Tulikaa pale na mama tukiongea mambo mengi na kubwa alitaka kujua najishughulisha na nini, kwa upande wangu nilimwambia nimejiriwa kwenye kampuni kama C.O.O (Chief Operating Officer). Mama upande wake hakuwa na maswali sana ila alionekana kunikubali sana.

Baada ya Prisca kutoka mama yake aliongea na daktari kama dakika 10 na alitoa pesa akampa binti yake na akatuaga.

“Prisca honey wako amekuja nafikiri ataku-takecare acha mimi niwahi ofisini na wageni.”

“Sawa mama byee.”

Inshort mama yao akina Prisca ni pini balaa na kafanana sana binti zake. Mama yake aliondoka na sisi tulikaa kidogo tukisubiri dawa na baada ya hapo tukaondoka, lakini tulikwenda Changanyikeni.

*******
Tangu sakata la Iryn kunikuta na Prisca pale Restaurant hatukuwai kuwa na mawasiliano yoyote wala kuonana, na mimi niliona nimtafute Iryn ili tuyajenge pia nimshirikishe suala la kuanzisha SACOSS ya kampuni.

Ile asubuhi baada ya kumaliza majukumu yangu niliamua kwenda Changanyikeni kupumzika na nilikuwa peke yangu pale maana Prisca alikuwa amekwenda kazini.

Niliamua kumpigia simu Iryn ili niombe appointment ya kukutana naye badae, baada ya kupiga simu alipokea na tukaanza kuongea,

“Hi Bossy habari yako?”

“I’m fine familia haijambo?”

“Iko salama, sasa naomba badae tuonane kama utakuwa na nafasi ili tuzungumze maana nilikuwa na jambo nataka kukushirikisha kuhusu kampuni.”

“Insider huwezi kuongea kwenye simu?”

“Ninaweza kama ukitaka ila kwa umuhimu wa hili jambo itapendeza sana tukizungumza face to face, kama ratiba zimekubana tunaweza fanya siku nyingine.”

“Okay nimekuelewa nitakupigia simu badae kukupa feedback.”

Baada ya kufanya mazungumzo na mimi niliingia jikoni kupika chakula na baada ya lisaa Prisca alirudi kutoka kazini.

Toka sakata la mtoto litokee upendo kwa Prisca ulikuwa umeongezeka sana yaani nilikuwa tayari kumfanya awe mke wangu wa pili.

Jioni tulikuwa tumelala seblen kwenye coach moja na yeye alikuwa ameegesha kichwa chake usawa wa kifua changu na mimi muda huu nilikuwa namchezea nywele zake kichwani. Na muda huu simu yangu ilianza kuita na nilimuomba Prisa anisaidie kunipa na baada ya kuichukua aliangalia ni nani anapiga, na aliishia kukunja sura,

“Bossy Lady again, huyu mwanamke hata simuamini haiwezekani na uzuri wote ule hushawishiki na kwanini anakupigia sana simu?”

“Hutaki Bossy anipigie simu?”

Baada ya kupokea simu ya Iryn, alinambia saa 2 usiku nikamchukue kwake na alipendekeza twende Mikocheni Plaza. Kwa upande mwingine Iryn alionekana kuwa na furaha wakati tukiongea, kwani muda ule asubuhi wakati nimempigia alionekana mtu ambaye anajilazimisha kuongea na mimi.

“Baby hakuna kwenda huko kwa uyo b*tch, kama vipi tunakwenda wote.”

“Bossy wangu unamuita b*tch are you serious?, Prisca kuwa na mipaka utani tibua tafadhali.”

Na mimi nilikwenda chumbani kubadilika ili niondoke maeneo haya mapema, mpaka naoga na kujiandaa ilikuwa saa1 usiku tayari na nilikuwa nataka kuwai nipitie kwanza pale Mlimani city ili nimchukulie zawadi Iryn.

Nilimkuta Prisca amelala palepale kwenye coach na alikuwa ameninunia sana na mimi hata sikujali nilimuaga pale na aliishia kuninunia. Kwa upande mwingine nilikuwa siioni key ya gari pale seblen, Prisca alikuwa kaificha.

Na mimi sikutaka kubishana wala kugombana naye maana alikuwa bado kwenye dozi ilibidi niwe mpole tu muda huu. Licha ya kutumia upole wangu na kumbembeleza anipe key alikuwa bado hataki kutoa funguo, nikaona Prisca ananiona mimi kama toy lake la kuchezea.

Ilibidi nianze kuwa mkali muda huu na tulianza purukushani pale na key alikuwa kaibana kwenye mapaja yake na alikuwa kavaa dela. Prisca alikuwa amenikera sana kwakweli lakini niliamua kuwa mjinga na mimi niliondoka.

“Nitamwambia Mama Junior kuhusu huyu b*tch wako maana huridhiki na wanawake ulio nao.”

“Tena usithubutu kabisa kufanya huo ujinga maana hunijui vizuri.”

Niliondoka lakini nilipitia kwanza pale Mlimani city na nilikuwa nimekwenda kununua zawadi ya Ua kwaajili ya Iryn. Niliwasili pale kwake na kwa upande wake alikuwa amejiandaa tayari, sasa wakati anakuja kuingia kwenye gari na mimi nilishuka nikamfungulia mlango ili aingie,

“Insider nani kakuambia anataka kukaa na wewe mbele?”

“Najua unapenda sana ila unataka kukaza, leo umependeza sana asee.”

“Sitaki sifa zako.”

Na muda huu tulikuwa tumeshaingia kwenye gari na mimi nilitumia kama dakika 1 kumuangalia usoni huku nikitoa tabasamu.

“Insider stop that tuondoke bwana.”

Baada ya kuwasili pale Mikocheni plaza tulikwenda moja kwa moja mpaka Pizza Hut na tulikaa pale nje kwenye meza. Mimi niliinuka kwenda kuweka odda na niliagiza Large pizza na nilirudi kukaa, muda huu nilikuwa namuangalia sana Iryn usoni.

“Insider nambie ulikuwa una jambo gani kwanza?”

“Nilimiss sana kukaa na wewe hivi, unakumbuka mara ya mwisho kuja hapa kuna jamaa alikuwa anakusumbua ukaamua kumkera?”

Iryn muda huu alianza kucheka,

“Acha utani wako niambie una ishu gani?”

“Nilikuwa nawazo tuanzishe SACCOSS ya kampuni lengo tuwasadie wafanyakazi pale wanapo pata shida bhasi iwe rahisi kupata mkopo kupitia kampuni. Kwanza hii itapelekea hata wafanyakazi wadumu muda mrefu na itaweza kuwasaidia kiuchumi, tutaweka riba za kawaida ambapo zile faida zitasaidia hata masuala mengine kama kuwapa motisha nk.”

“Idea ni nzuri sana pia suala la bima Mama Janeth amekamilisha tayari kwa kila mtu, sasa hili nakuachia wewe lifanyie kazi na mimi pia kwa upande wangu nitaliangalia hili kwa undani zaidi.”

Na muda huu jamaa alileta Pizza pale mezani

“Queen eeh.”

“Ndio bossy hujakosea na Queen mwenyewe ndo huyu hapa, kwanza tupige na picha kabisa kabla hujafata juice.”

Jamaa alitupiga picha ya pamoja na Iryn na maoengezi yakaendelea.

“Vipi za Dodoma huko?”

“Salama najua unaelewa tayari kilichoendelea best yako atakuwa alikwambia hapa unanichora tu, labda wewe unambie habari za Ethiopia, uliifanikisha?”

“Nilifanikiwa Insider, nashukuru Mungu kwa hili maana tulitaka kuifunga lakini mama alikuwa anasaidia watoto wengi sana kupitia hii organization, Japo alikuwa anatumia majina ya ndugu zake maana wao hawaruhusiwi kuwa na hizi organization.”

“Oohh kumbe nilikuwaga sijui hili.”

“Haitakiwi na mama alikuwa anatumia jina la mamkubwa, ila naye umri umeenda ndomana ameamua kuikabidhi kwangu na Jimmy atakuwa Director.”

“Vipi Jimmy hawezi kukusumbua?”

“Hapana hawezi, Jimmy ni smart sana ukiacha madem, na hizi ni tabia za kila mwanaume even you una mke ila bado huridhiki.”

“Hahahaa mimi nimeridhika sana hujui tu.”

“Mmh I don’t trust you, Insider wewe ni mhuni sana hata Lucy nishaanza kuwa na mashaka naye.”

“Lucy ni mtani wangu sana afu nampenda sababu yuko real sana.”

“Remember that Man and Woman can’t be friends”

Tulikaa kwa muda mrefu pale tukipiga story na kubwa tulionekana kumisiana sana maana tulikuwa tunaongea mambo mengi sana na Iryn alionekana kufurahi sana. Tuliamua kuondoka maeneo yale na mimi nilimpeleka Iryn pale kwake na baada ya kuingiza gari ndani alishuka akasema anakuja nimsubiri.

Baada ya dakika 5 alikuja kwenye gari na alikuwa ameshikilia mfuko mkononi na akanipa pale.

“Insider hizi ni zawadi za kutoka Ufaransa.”

“Wow Ahsante sana mummy, afu nilisahau kukuuliza habari za Ufaransa.”

“Insider haya tutaongea siku ingine sawa? Acha mimi nikalale.”

Alifungua mlango akaanza kuondoka na mimi nikakumbuka nina zawadi yake ya Ua, nilishuka na nikamuita

“Iryn….” I have your gift

Nilitoa Ua kwenye gari maana lilikuwa kwenye bahasha na muda huu Iryn alikuwa amesha sogea kwangu, na mimi bila kuchelewa nilifungua bahasha na nikatoa lile Ua na lilikuwa ni zuri sana jekundu.

Baada ya kumpa zawadi Iryn aliniangalia na alionesha kuifurahia zawadi yangu,

“Insider thank you very much, I was wrong that day kusema kila mtu afocus na maisha yake, I’m sorry.”

Na Iryn alianza kuondoka na mimi nilimshika mkono nikamvuta kwangu nikamkumbatia, na palepale alinivuta tukaanza kunyonyana mate, ni gari iliyotuharibia pozi muda huu maana ilitumulika na ilikuwa ikija usawa wetu.

Iryn hakuongea chochote bali aliondoka kwa haraka na mimi niliingia kwenye gari nikaondoka maeneo haya.

Nilikuwa narudi changanyikeni kama kawaida na wakati nimekaribia na chuo cha EASTC Mary alipiga simu na mimi nilipokea simu yake,

“Hi shem.”

“Insider kwa kipindi chote kumbe una mke na mtoto na bado ukataka kuzaa na mdogo wangu Prisca?, kwanini umemficha Prisca mpaka anazama kwenye mapenzi na wewe?. I really hate you for that, poor Prisca”

Na mimi sikutaka ongea lolote muda huu bali nilinyamaza kimya na yeye alikata simu.

Baada ya kufika kwa Prisca nilifungua geti nikaingiza gari ndani. Mlango ulikuwa umefungwa wa seblen hivyo ikabidi nigonge lakini alikuwa hafungui, nikapiga na simu lakini hakupokea simu zangu. Niliamua kumtumia text Prisca kuwa kama hafungui mimi naondoka na sitokuja tena kwake.

Nilikaa pale nje kama dakika 20 hivi sasa kuna jamaa alitoka ambaye ni jirani tukaanza kupiga story pale nje, na story zilinoga sana baada ya kujuana tunatoka mkoa mmoja afu ni kabila moja ,hivyo alikuwa ni home boy.

Tuliagana na jamaa pale baada ya kuona Prisca hafungui mlango na wakati nawasha gari ili niondoke ndo alifungua mlango.

Baada ya kuingia ndani alianza kufoka kwamba nimetoka kuchepuka na Bossy na alikuwa akilalamika kuwa namtesa sana. Kwa upande wangu niliona Prisca ameanza kuvuka mipaka, anasahau yeye ni mchepuko tu kwangu hata kama nampenda sio kuvuka mipaka namna hii.

Niliamua kumuacha pale akiendelea kulalamika na mimi nilikwenda jikoni kupakua chakula, tangu anaanza kufoka mimi sikuongea neno lolote.

Muda huu simu yangu ilianza kuita maana ilikuwa seblen nimeiweka chaji, na Prisca alikimbilia kuichukua simu yangu,

“Ona malaya wako anapiga simu.”

Na mimi baada ya kuona anayepiga simu ni mama Junior niliumia kwakweli kuona mke wangu akiitwa malaya, kwakweli uvumilivu ulinishinda muda huu maana niliona Prisca kavuka red line.

“Mke wangu unamuita malaya, mama watoto wangu?”

Nilipatwa na hasira na niliishia kumchapa vibao viwili vya nguvu na alianza kulia pale,

TUTAENDELEA
🙆🙆🙆
 
Eeh! Mr. InsiderMan, mwisho wa yote, naona kwa mbaali kama Iryn ndiye atakuwa mama J. Utabiri wa mama utatabiri upya hivyo, hasa kazi ya MZEE JUMA utafanyia/Master's Degree utajasomea Ufaransa! Wee twende tu, shauri yako
 
Rottweiler
IMG_3020.jpeg


German Shepherd
IMG_3017.jpeg


Rottweiler & Shepherd
IMG_3019.jpeg
 
Rottweiler ni mbwa mwenye nguvu sana za miguu ana anauwezo wa kutembea muda mrefu bila kuchoka, ni mstaarabu hana mambo mengi ila hanaga masikhara kama wewe ni adui.

Comb ya Rottweiler & shepherd sidhani kama kuna kibaka atakatiza kwa Jane. Na sasa ni wakubwa balaa sio poa [emoji1544][emoji1544]
 
Back
Top Bottom