Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

SEASON 02:
EPISODE 19

BY INSIDERMAN”

ILIKOISHIA:
Niliendesha gari kwa kasi sana na wakati nipo Vodacom HQ simu yangu ilianza kuita na ile kucheki ni wife alikuwa akipiga, ilibidi niingize gari pale Oryx kituo cha mafuta li tuongee maana nilijua atakuwa anauliza kama nimefika au laah!.

Muda huu simu ilikuwa imeita mpaka imekata na nilimpigia simu kwa haraka sana na haikuchukua muda alipokea,

“Nambie mke wangu unaendeleaje?”

“Hujanambia kama umefika salama.”

“Nimefika salama sema mambo mengi ila ningekuambia mke wangu.”

“Iryn amekuja home kutusalimia na yuko sebleni anacheza na Junior.”

Nilishtuka sana kupewa hizi taarifa na wife na nilijiuliza amekwenda kufanya nini home na lile tumbo lake?, kwanza sikuwa na wazo kwamba atakwenda home na nilianza kuingiwa na wasiwasi, na jasho lilianza kunitoka…”

Ni hivi….

Baada ya kutofautiana, Iryn aliondoka na kwenda Masaki “Samaki samaki” na baada ya kuwasili, alitafuta sehemu iliyotulia akakaa na aliagiza wine, japo hakuwa na plan za kutumia alcohol mpaka anajifungua.

Alitumia kama lisaa kuimaliza na alitaka kuongeza nyingine ila akaona italeta shida kwenye ujauzito wake maana anadai alikuwa kwenye hasira kali sana. Kipindi yuko maeneo haya kwa upande mwingine kuna mafisi walikuwa wanamsumbua wakimtongoza, kutokana na usumbufu anadai kuna mmoja alimtia kibao, sababu ya usumbufu na hapa akaona bora aondoke.

Kurudi hotelini asingeweza maana alikuwa hataki hata kuniona na alikuwa na hasira na mimi, kwenda kwa Claire hakutaka sababu hakumpa taarifa kuwa anakuja Dar, kwenda kwa mama Janeth pia aliona ngumu, sehem pekee ya kwenda na kuwa salama ni home kwa mama J.


Kipindi tunamtafuta mawazo yangu yalikuwa sahihi atakuwa amekwenda Masaki na kama ningeanza kwenda Samakisamaki, bhasi ningempata, kipindi napata wazo la kwenda Samakisamaki nilikuwa late tayari na tulipishana kidogo sana.

CONTINUE:

“Afu ni mjamzito kumbe ile siku nilikuwa sahihi.”

Nilikuwa kimya ghafla kama nimepigwa na ubaridi, nilisahau kama naongea na simu na muda huu wife alianza kuniita;

“Baba J mbona kimya, huongei?”

Niliwaza kwa haraka nikaona hakuna haja ya kuendelea kuongea na wife, chakufanya nimuage kwa kumpa ahadi ya kumcheki asubuhi, niliona kuendelea kuongea naye anaweza akawa ananichunguza.

“Swahiba kuna jambo nafanya hapa, nataka nikamilishe mapema ili ikiwezekana kesho nirudi Dar, tutaongea vizuri asubuhi maana hata mimi sielewi kitu, msalimie Iryn.”

Nilikuwa bado nawaza mambo mengi sana muda huu na ukizingatia sikuwa na ujanja wa kwenda home na wasiwasi mkubwa huenda Iryn ameamua kwenda kufunguka kwa mama J, kama mbwai iwe mbwai yaani tukose wote.

Nilichukua simu yangu kwenye drow na nilimpigia, lakini hakuwa online na nikachoma mafuta kwenda Mlimani city kumit na Bob maana alikuwa ameshanipa taarifa yuko around tayari.

Lengo la kwenda kuonana na Bob ilikuwa nimshirikishe kuhusu mimba ya Iryn, lakini baada ya kuwasili pale niliona nivunge tu, sikuona umuhimu wa kumshirikisha, kwani sio busara kumwambia kila mtu kuhusu hili jambo.

Kwa upande wake Bob alinifungukia kuwa wapo kwenye mahusiano na Lucy na wako serious, lakini Bob alilalamika kuwa Lucy anakaza sana kutoa tunda. Baada ya kusikia hizi taarifa niliishia kucheka sana mpaka Bob alihisi kuna shida maybe namla Lucy;

BOB: “Bro mbona unacheka kuna nini? Nisije kuwa nauziwa mbuzi kwenye gunia.”

MIMI: “Hahaha nimefurahi kusikia, anakuja geto na bado unashindwa kumuweka, niseme pole sana.”

BOB: “Kaka nina wasiwasi sana na wewe maana Lucy anakukubali kinoma, usije ukawa unafanya yako maana sikuamini kabisa.”

MIMI: “Kwanza kitendo cha kumtongoza bila kunishirikisha hapa ndo umezingua, mimi ni jamaa yako na umemjua manzi kupitia mimi, ulitakiwa unishirikishe, kama namla utajuaje?”

BOB: “Hapa kweli nilikosea bro, embu niambie kama kuna lolote linaendelea kati yenu.”

MIMI: “Hamna kaka usiwe na wasiwasi mimi sina historia nae zaidi ni mshikaji wangu wa maana na nina muheshimu, kama mpo kwenye mahusiano ni jambo jema, japo hata yeye bado hajanifungukia ila nilishaona dalili.”

BOB: “Hapa sasa nina amani, ila hana imani na mimi kabisa.”

MIMI: “Wewe ni mhuni tu, anaanzaje kukupa moyo wake wote?, ila kama mwanamke wa malengo umepata ni mpambanaji sana.”

Kwa upande mwingine message zangu nilizokuwa nimemtumia Iryn zilionesha tick 2 kuwa zimefika na palepale nilimtumia ujumbe kuwa aje Mlimani City ili tuongee ninamsubiri, lakini hakuwa anareply.

Mida ya saa 8 za usiku niliachana na Bob, Iryn alikuwa kama kawaida hajareply text zangu, nilihisi huenda atakuwa amerudi hotelini, hivyo sinabudi ya kuwahi kwenda.

Baada ya kuwasili hotelini alikuwa hajarudi, lakini sikuwa na wasiwasi juu ya afya yake sababu alikuwa home, ila wasiwasi wangu mkubwa ulikuwa ni kwa wife tu, pale ambapo Iryn atamfungukia ukweli. Niliwaza sana sababu ya Iryn kwenda home lakini sikuwa napata majibu na nilijiuliza ana mpango gani kufanya hivi? Iryn hafanyagi jambo kwa bahati mbaya, huwa anakuwa na target zake.

Muda huu simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni Claire akipiga, nilipokea simu yake kwa haraka sana na baada ya kupokea alikuwa anauliza kama nimempata Iryn, then akasema jioni atanicheki ili tuongee vizuri.

Asubuhi nilichelewa kuamka na nilijikuta napata wazo la kukagua bag la Iryn na bila kusita nilianza kulifungua ili nione kama kuna lolote. Nilianza kucheki mifuko ya pembeni kulikuwa na diary nikaanza kuipekua na kulikuwa na ratiba zake alizopanga kufanya soon ikiwemo Ufaransa, pia niliona kaandika tarehe ambayo anatarajia kujifungua na vitu vingine kibao.

Niliweka diary pembeni nikaendelea na upekuzi wangu wa kufungua upande mwingine wa bag, na nilitoa bunda 2 za pesa (euro & dollar) nikaweka pembeni. Nilitoa tena bahasha na ile kuifungua kulikuwa na picha, bhasi nikarudi kitandani kukaa kuziangalia vizuri.

Picha zilikuwa zina maudhui tofauti zikiwemo za kipindi kile nimekwenda Ethiopia kwa ajili ya ukumbusho wa kifo cha mama yake, pia niliweza kuziona picha mbili ambazo tulipiga pamoja akiwemo na Jimmy. Picha nyingi alikuwa na mama yake ambazo walikuwa wamepiga maeneo tofauti ya Ulaya zilikuwa za miaka minne kurudi nyuma.

Zoezi langu la ukaguzi liliishia hapa baada ya simu yangu kuanza kuita na ile kucheki alikuwa ni Hilda akipiga, nilipokea na taarifa aliyonipa ni kuwa mama anahitaji ripoti na mimi ndo mhusika nayetakiwa kumtumia, niliona kuna haja ya kwenda ofisini kuzipitia ripoti zote na nilimwambia soon nitakuwa ofisini.

Niliingia kuoga ili niondoke maana muda ulikuwa unasoma ni saa 4 za asubuhi, kwa upande mwingine hakukuwa na taarifa yoyote kutoka kwa wife wala Iryn.

Niliondoka kwenda Masaki na baada ya kuwasili straight niliingia ofisini kuendelea na majukumu yangu sikutaka story. Mle ndani ofisini alikuwepo Hilda na baada ya kuniona aliishia kufurahi na story zingine zikaendelea huku tukiendelea na kazi.

HILDA: “Bossy nimekumiss sana, pia umepotea, sahivi sina mtu wa kupiga nae story.”

MIMI: “Mmhh acha unafiki Hilda, shoga yako Rebby hamna story sikuhizi?”

HILDA: “Si anakuwa busy na majukumu yake, ni ngumu kukaa na kupiga story kama hivi.”

MIMI: “Haya nimekuja leo nambie umemiss nini kutoka kwangu?”

HILDA: “Nilimiss kukuona kama hivi, atleast leo nina furaha.”

MIMI: “Ungekuwa ulinimiss ungekuwa ulipiga simu.”

HILDA: “Unapokea simu sikuhizi? Maana simu zangu kama huzionagi kabisa, hivi ni kwa wote au mimi tu?”

MIMI: “Hahahaa hamna utakuwa unapiga mida mibaya au niko busy, mbona leo nimepokea ontime?”

HILDA: “Sawa ila uwe unapokea simu, siku naweza kuwa kwenye trouble afu wewe ndo wa kunisaidia.”

MIMI: “Nisamehe bhasi mama, sifanyi kusudi.”

Saa 7 mchana Jane alinipigia simu na aliniomba niende Bahari Beach kwenye fremu ili nikakague kama fundi kamaliza na kafanya kazi nzuri before hajamlipa, sikuwa na nguvu ya kumkatalia na nilimwambia nitakwenda jioni.

Baada ya lisaa hivi, Hilda aliingia ofisini maana alikuwa ametoka kwaajili ya lunch na alianza kunipa hongera, lakini nilikuwa nashindwa kumuelewa hizi hongera zinatoka wapi na za nini?;

MIMI: “Hilda sikuelewi kuna nini?”

HILDA: “Naona unategemea kuwa baba soon.”

MIMI: “Baba tena? Niwe baba mara ngapi?”

HILDA: “Naona Iryn ana mimba usinidanganye kuwa sio yako.”

MIMI: “Wewe umejuaje kama ana mimba yangu?”

HILDA: “Iryn amekuja kutusuprise na yuko reception amekaa anaongea na kina Rebby ndo nimejua ni mjamzito.”

Of course sikujua kama Iryn kaja ofisini na ilibidi nishangae baada ya kupata hizi taarifa kutoka kwa Hilda na nilikuwa mpole,

MIMI: “Ahsante Hilda, nishakutumia hizo ripoti mtumie mama ziko sawa.”

HILDA: “Sio umtumie wewe?”

MIMI: “Kakuomba wewe ni busara ukamtumia wewe mwenyewe.”

HILDA: “Sawa bossy.”

Kwanza kitendo cha mama kumuomba ripoti Hilda kilinipa ukakasi sana na sikupenda maana alipaswa kuwasiliana direct na mimi, na sio Hilda.

Niliendelea kufanya kazi zangu na nilikuwa nategemea Iryn atakuja ofisini lakini ilikuwa tofauti na matarajio yangu na nilichukua simu nikamtext aje ofisini tuongee maana niliwaza kwenda reception naweza kuaibishwa na kupata aibu. Ilipita nusu saa kimya hajatokea wala kujibu ujumbe wangu japo ulikuwa umefika na hapa nikaona anazingua, nikapata wazo niondoke niende Bahari Beach.

Nilitoka ndani na nliwaona wamekaa nje kabisa kibarazani wakipiga story na mimi hata sikutaka shobo ya kuwasalimia, bali nilipita kama siwaoni na nilikwenda straight parking nikawasha gari na kuondoka maeneo haya.

Barabarani nilikuwa na spidi kali sana kuelekea Bahari Beach lengo nimalize mapema kisha nigeuke tena kurudi Masaki. Nilitumia muda mchache sana kuwasili eneo la tukio na baada ya kuiona kazi ya fundi niliridhika maana ilikuwa ni nzuri sana tena ya kuvitia.

Nilimpigia simu Jane kumpa taarifa na alisema anamtumia fundi pesa yake kwenye simu, kwa upande mwingine Jane aliomba niende Mbweni tukaonane kwaajili ya kupanga mipango ya biashara, sikuwa na namna ya kumkatalia, hivyo ilinibidi nianze safari ya kwenda kwake.

Nilitumia muda mfupi sana kuwasili pale kwake na niliambiwa yuko jikoni anapika na nilimfuata kumsalimia na tukaanza story, huku namsaidia kupika. Tulianza maongezi na msimamo wake ulikuwa ni uleule kuanza biashara mwezi wa pili maana kama fremu tumeshapata na kila kitu kimeshakamilika, kilichobaki ni kuanza biashara. Jane alikuwa serious sana, niliona ana shauku kubwa sana ya kuanza hii project, kwa upande mwingine alisema anatafuta dada mpya wa kukaa home na huyu wa sikuzote atampeleka dukani sababu anamuamini.

Kwa upande wangu nilimuunga mkono juu ya hili na nilimshauri afunge Cctv camera kwaajili ya usalama zaidi maana hatokuwa akishinda sana dukani sababu ya mtoto. Mwisho kabisa aliiomba kesho ambayo ni jumapili twende ukweni ili tukaonane na mama mkwe, niliishia kumkubalia licha ya ratiba zangu kuwa tight.

Nilishinda pale kwake mpaka giza lilikuwa limeshaanza kuingia na kabla ya kuondoka nilimpigia simu Hilda kumuuliza kama Iryn bado yupo ofisini na alinambia aliondoka muda mrefu sana, nilimuaga Jane nikaondoka, muda huu kichwani nilikuwa nawaza nitafute namna ya kuyajenga ili atulie maana alikuwa anakisirani sana.

Kipindi niko njiani nilipigiwa simu na Claire kubwa alikuwa ananipa taarifa ya kukutana Capetown fish market, sikutaka kumkatalia maana alikuwa ametoa ahadi ya kunicheki. Muda huu nilikuwa niko na Mwaikibaki road naifukuzia Palm village na kabla ya kufika Tanesco nilichepuka na barabara ya Msasani kuelekea eneo la tukio.

Baada ya kuwasili ilinibidi nipark gari upande wa pili, kisha nilitoa simu nikampigia kumpa taarifa kuwa nimefika na alinielekeza alikokaa na mimi nikazama ndani kuelekea usawa alionielekeza. Nilikuwa makini sana kuzungusha macho yangu maana palikuwa na watu wengi sana, si unajua mambo ya weekend?, kama warembo ndo walikuwa kibao wamekaa.

Nilifanikiwa kumuona Iryn kwa mbali, ila yeye alikuwa hajaniona na walikuwa wakipiga story na Claire, na ile kuendelea kusogea ndo kuniona na tuliishia kupigana jicho. Ukweli sikujua kama Iryn angekuwa hapa na sikuwa na hili wazo kabisa, hivyo nilivuta kiti nikakaa na nilianza kumsalimia Claire, kisha nikahamia kwa Iryn, lakini alikuwa bado kanuna hata salamu yangu hakujibu.

Mhudumu alikuwa amekuja kunisikiliza na niliishia kuagiza juice tu, nilikuwa nimekula kwa Jane, hivyo nilikuwa niko full sikuwa na hamu ya kula. Claire kwa upande wake alishangaa sana kuona naagiza juice tu na alianza kuongea,

CLAIRE: “Shem only juice?”

MIMI: “Niko full ndomana, pia kule hotelini mama kijacho kafanya booking ya food, sioni haja ya kuchezea hela hapa, wakati hotelini chakula kimelipiwa.”

CLAIRE: “Wewe kweli mchumi kwahili nakupa salute.”

MIMI: “Kwanza nimekuja kuitikia wito wako, niambie unajambo gani unalotaka kushare?”

CLAIRE: “Nimewaita ili myamalize sijazoea kuwaona mmenuniana hivi, shida ni nini shem?.”

MIMI: “Acha kujifanya hujui kinachoendelea wakati unamkanda mzima umeambiwa, anyway hili suala hata lisikuumize kichwa sisi tutayajenga sawa?”

CLAIRE: “Mmh sawa naamini hivyo, she is pregnant huu ndo wasiwasi wangu.”

MIMI: “I can handle this so don’t worry, mambo mengine vipi?, sijakuona muda nimekumiss.”

Story zilichange tukaanza kuongea mambo mengine kabisa, lakini Iryn alikuwa kimya muda wote na alionesha kuwa busy na simu yake. Claire alimuita dada na akaniomba sana niagize chochote, kwani haitapendeza wao wanakula afu mimi siri, bhasi niliagiza seafood na tukaendelea na story zingine.

Mida ya saa 3 nilimpa taarifa Iryn tuondoke, lakini alisema anakwenda kulala kwa Claire, sikuwa na usemi zaidi nililipa bill zote nikawaaga pale. Sijui waliongea nini na wakati niko kwa gari nikijiandaa kuondoka, Claire alinipigia simu kunambia nimsubiri Iryn ili tuondoke wote.

Nilisubiri kwa dakika 10 ndo walikuja na tukaondoka na tulianza kumdrop Claire pale Marina, tukaendelea na safari ya kwenda Posta. Barabarani hatukuwa na maongezi yoyote zaidi ya yeye kuwa busy na simu yake na mimi niliamua kuvunja ukimya nikaanza kumhoji,

“Ulikuwa na lengo gani kwenda hivyo kwa mama J?”

Nilikuwa najibiwa bhasi, zaidi ya kuendelea kukaa kimya dizaini kama hanisikii, niliona huyu mwanamke analeta dharau, muda huu tulikuwa tunakaribia round about ya pale Aghakan hospital na nilielekea na barabara ya ocean road.

Baada ya kuona sijibiwi nilipark gari pembeni kwa mbele kidogo baada ya round about na nikalock milango, yeye alivyoona nimepark pembeni alianza kuongea;

IRYN: “Why stop here?”

MIMI: “Nahitaji majibu ya maswali nitakayo kuuliza naona unaleta dharau, sitaki kupata lawama zingine.”

IRYN: “Are you beating me again?”

MIMI: “Kilichokupeleka home ni nini? Unataka kuniletea matatizo kwa wife?”

IRYN: “Ningekuwa na nia ya kufanya hivo, toka jana ungekuwa ulishapigiwa simu na huenda sahivi mama J angekuwa kwao.”

MIMI: “Ausioo, hujajibu swali langu bado, I need answers.”

IRYN: “Siwezi kukujibu sababu ya kwenda kwa mama J, wewe ndo uliyeyasabisha haya yote.”

MIMI: “Laiti ungetoa ushirikiano hayo yote yasingetokea ila sababu ulileta dharau kwangu.”

IRYN: “Ulishindwa nini kusubiri niongee na simu then uulize naongea na nani? Zaidi umefika na kuanza kutumia force, bado ukanipiga na vibao juu, sijawahi kupigwa vibao kwenye historia ya maisha yangu, what you did was total torture..”

MIMI: “Kama simu ilikuwa haina shida kwanini uli switch lugha? Kuonesha hutaki nijue maongezi yenu, ni nini ulikuwa unahide?”

IRYN: “Insider unatakiwa uheshimu privacy ya mtu, kuswich lugha sio….”

Nilimkatisha maongezi yake maana niliona anazidi kunipa hasira,

MIMI: “Yaani unaongea na Ex wako afu unataka nikuamini? Hivi mfano wewe ungenikuta naongea na Asmah na nikafanya kama ulivyofanya wewe ungenielewa?.”

IRYN: “Mimi ningeheshimu privacy yako na sio kufanya kwa force kama wewe, ungesubiri nimalize kuongea na simu then uanze kuuliza, sio kunipora simu na kuanza kuniita malaya na kunipiga juu, hujui hata tulichokuwa tunaongea.”

MIMI: “Are you sure? ni mara ngapi umekuwa unanuna kwa maneno ya kuambiwa kuhusu Asmah na hayana proof?”

IRYN: “I know you had sex with her a couple of days ago.”

MIMI: “What?”

IRYN: “You heard me. Do you think I don’t know what is really going on between you guys?.”

MIMI: “Not really.”

IRYN: “Oohh nice.”

Niliendelea na safari ya kwenda hotelini, lakini niliingiwa na hofu kusikia maneno ya Iryn kuhusu Asmah na nilijiuliza kajuaje? Nilianza kuingiwa na wasiwasi maana alikuwa anaongea kama mtu ambaye ana ushahidi na anajua kinachoendelea.

Baada ya kufika hotelini aliingia kuoga then akalala hatukuwa na story zozote na mimi ilibidi nianze kufikiria amejuaje mimi nimesex na Asmah wakati tulifanya kwa siri sana?. Ni maswali ambayo nilikuwa ninajiuliza bila kuwa na majibu na nilijisemea kuna haja ya kuonana na Asmah, tukazungumza hili jambo.

****
Jumapili aliondoka kwenda South Africa na ile asubuhi mimi ndo nilikuwa wakwanza kuamka, nilimuamsha kumuuliza anaondoka muda gani?, alisema saa 6 ataondoka kwenda airport.

Nilijaribu kukaa nae chini ili tuyamalize, lakini hakuonesha dalili ya kutaka kuzungumza na kuyamaliza, kwani aliendelea kuninunia na sikutaka kuendelea kumbembeleza.

Kuna muda dada mhudumu alikuja room kutuhudumia na alikuwa akiongea na Iryn, ajabu ile simu ambayo ilipasuka sababu ya ugomvi alimpa yule dada kama mali yake, sikutaka kusema chochote na nilivunga.

Baada ya dada kuondoka nilishangaa kusikia akiniambia kuwa hakuna haja ya kumpeleka airport na atakwenda airport na gari ya hotel. Nilijisikia vibaya, lakini sikuwa nachakusema wala kubishana nae juu ya maamuzi yake na nilimuaga nikaondoka, sikuona haja ya kuendelea kupoteza muda.

Kipindi niko parking kichwani nilikuwa nawaza niende kwa Asmah ili tuongee, nilihisi litakuwa ni kosa la kiufundi lilifanyika bila yeye kujua. Nilimpigia simu na alinambia yuko Kigamboni ila atarudi badae, hiyo atanicheki akirudi ili tuoanane.

Nilikumbuka nina miadi na Cami binti ya Mzee Juma maana alikuwa ana maagizo yangu kutoka kwa mzee, nilimpigia simu na akanambia leo ni ngumu kuonana ila atanitafuta kesho na kunipa maelekezo yote kutoka kwa mzee. Baada ya kumalizana na Cami sikuwa na option nyingine zaidi ya kwenda home kupumzika na nilikanyaga mafuta mpaka home.

Baada ya kuwasili wife alikuwa hayupo na niliambiwa kaondoka kwenda church na atachelewa kurudi sababu kanisani kuna kongamano la vijana, hivyo nilikwenda straight room kulala.

Saa 10 jioni Jane alinipigia simu kunikumbusha kuonana na mama mkwe, kwa upande wangu nilikuwa nimeshasahau kama tuliongea kuhusu hili, ilibidi nimdanganye kuwa mama mkwe alisema akitoka kanisani atanicheki.

Baada ya kuongea na Jane nilimpigia simu mama mkwe kumuomba kama tunaweza kukutana kwa leo na alisema saa 12 jioni tuonane, ila alisema itabidi tutafute sehemu ya karibu ya kukaa kwaajili ya kufanyia maongezi sababu home kuna wageni.

Saa 12 jioni tulikutana pale Boko Basihaya- Fyattanga Bar na hii siku sikutaka kabisa kuingilia maongezi ya Jane na mama mkwe. Maongezi yao makubwa yalibase kwenye biashara kwa ujumla na alikuwa anapewa mbinu za jumla kuhusu hii biashara, pia alipewa connection ya suppliers mbalimbali wa kumletea bidhaa pale dukani.

Walitumia kama dk 45 na baada ya kumaliza mama mkwe aliniaga anaondoka kwenda home kuonana na wageni, nimshukuru sana kwa msaada wake na sisi tuliendelea na kupanga mipango mingine ya biashara.

Kwa upande wangu nilimshauri aanze biashara kwa umakini sana na asiingize capital kubwa mwanzoni, alisome kwanza soko then mengine atakuwa anafanya taratibu. Kuhusu masuala ya TRA na mamlaka zingine nilimwambia aniachie hizo kazi mimi nitamsaidia kufuatilia na nilimtaka ajitahidi kuandaa documents zote muhimu.

Mida ya saa 2 kasoro za usiku tuliagana ila kwa makubaliano ya kukutana tena kesho, tangu naachana na Jane nilikuwa nawaza kukutana na Asmah, ila sasa baada ya kuwasiliana nae alinambia bado yuko Kigamboni na hategemei kurudi leo, hivyo tutaonana kesho.

Baada ya kuongea na Asmah sikuwa na jinsi zaidi ya kuamua kurudi home tu, na nilipitia Pizza hut KFC nikanunua Pizza kama zawadi ya kupeleka home, mgahawa ulikuwa bado ni mpya toka uzinduliwe kwa branch ya Mbezi Beach.

Baada ya kurudi home kama kawaida Junior alitoka nje spidi kunipokea baba yake na ile kuingia ndani nawakuta akina wife wamekaa seblen wakipiga story, mama J alikuwa akiniangalia tu na hakusema neno lolote na alionesha kama hayupo sawa, na alianza kuongea;

“Baba J naomba tutoke nje kibarazani tuongee, nina maongezi muhimu sana ya kuongea wewe.”

TUKUTANE KESHO
Naaaaam.
The long wait is over....
 
SEASON 02
CHAPTER 20:


“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

PREVIOUS:
Baada ya kurudi home kama kawaida Junior alitoka nje spidi kunipokea baba yake na ile kuingia ndani nawakuta akina wife wamekaa seblen wakipiga story, mama J alikuwa akiniangalia tu na hakusema neno lolote na alionesha kama hayupo sawa, na alianza kuongea;

“Baba J naomba tutoke nje kibarazani tuongee, nina maongezi muhimu sana ya kuongea wewe.”

CONTINUE:

Ukweli sikutegemea kusikia hizi kauli kutoka kwa wife ukizingatia toka anipe taarifa za Iryn hatukuwa na mawasiliano tena, na mimi nilijua kila kitu kitakuwa shwari. Sasa kusikia anataka tuongee tena tukae kibarazani hapa nilianza kupata wasiwasi na nilianza kupoteza confidence, niliwaza huenda wife kajua kila kitu na alikuwa anasubiri mimi nirudi home.

Nilipiga hesabu za haraka nikaona ni bora nikaoge kwanza huku nafikiria majibu ya kumwambia endapo kama mambo yameharibika,

“Swahiba subiri kwanza nikaoge then nakuja tuongee.”

Niliingia chumbani chap na nilimpigia simu Iryn ili nijue kama kuna lolote waliongea na mama J, lakini kama kawaida yake alikuwa hapokei simu zangu licha ya kwamba alikuwa yuko online. Nilizidi kupatwa na hasira na nilimtumia ujumbe kuonesha sipendezwi na tabia zake maana anakuwa kama mtoto, ilibidi nimtumie ujumbe kumuuliza walichoongea na wife, lakini hakunijibu.

Niliona Iryn anataka kunigombanisha na mama J, kukaa kimya ana maanisha nini? Nilijua tu lazima kuna vitu waliongea, wife lazima atauliza ili kupima kama ni kweli au laah!. Kitendo cha kukaa kimya afu yuko online anasoma message zangu niliona ni dharau na alizidi kunipa hasira, nikaamua kwenda bafuni kuoga.

Bafuni nilikuwa naoga maji ya baridi lakini nilikuwa naona ya moto asee, haya mambo yanaumiza sana kichwa wewe yasikie tu, ila usiombe yakukute maana muda wote unakuwa na stress za kukamatwa.

Baada ya kumaliza kuoga na kujiandaa nilitoka seblen na wife alikuwa tayari yuko kibarazani akinisubiri na mimi nilichokifanya, nilichukua wine na glass 2 kisha nikamfata aliko.

MIMI: “Nambie mke wangu unazidi kuwa mzuri.”

WIFE: “Ningekuwa mzuri hata usingekuwa unahangaika na wanawake wengine.”

MIMI: “Sio kweli mimi nimetulia na wewe, embu niambie ni jambo gani unataka tuzungumze?”

WIFE: “Baba J naomba uwe honesty na mimi, ulikuwa unafahamu ujio wa Iryn Dar?”

MIMI: “Nimejua kupitia wewe ulivyonipigia simu, nje na hapa hapana.”

WIFE: “Una uhakika na unachoongea? Mbona yeye anasema unajua kila kitu?”

Nikajisemea hapa tayari nishaanza kulikoroga, nilijikuta naanza kumtukana Iryn;

MIMI: “Mhh hapana atakuwa alisema hivo ili kuondoa maswali, maana angesema mimi sijui sidhani hata wewe ungemwelewa ukizingatia hii nyumba ni yangu.”

WIFE: “Je ulikuwa unafahamu ni mjamzito?”

Hapa sasa nikawa hata sijui nijibu nini Yes or No maana jibu lolote lingekuwa na madhara,

MIMI: “Hapana labda nikuulize wewe ambaye mlionana kipindi kile, ulisema sio mjamzito.”

WIFE: “Baba J unauhakika? Yeye anadai mimba inamiezi 4 kasoro, how hujui kwamba ni mjamzito afu ni bossy wako?.”

MIMI: “Kuwa bossy wangu sio kigezo cha kujua private life yake, hayo ni mambo yake binafsi mimi hayanihusu, haya maswali yote unayouliza unamaana gani? Sikuelewi ujue, tunaongelea maisha ya mtu ambayo hayatuhusu.”

WIFE: “Baba J wewe ni muongo sana, Iryn anasema unajua yeye ni mjamzito na hukutaka kuniambia, pia umenidanganya kuhusu yeye kuja Dar wakati ulikuwa unajua.”

MIMI: “Hivi kwaakili ya kawaida tu, ningekubali kwenda Zanzibar wakati najua Iryn anakuja Dar?. Suala la ujauzito wake mimi sikumbuki kama alishawahi kunambia, huenda yuko sahihi lakini mimi sikumbuki.”

WIFE: “Unakumbuka zile picha nilizozikuta kwenye gari? Nikipiga hesabu ya umri wa mimba yake ni sawa kabisa.”

MIMI: “Mimi ningejuaje kama ni za Iryn? sababu ile gari inatumiwa na mama yake pia, hayo mimi siwezi kukujibu maana sielewi kitu, unanichanganya tu hapa, what’s your point?”

WIFE: “Najaribu kuunganisha tringle nahisi hio mimba ni yako 100%.”

MIMI: “What? Mama J tutakorofishana hapa sasa hivi, hivi una matatizo gani?”

WIFE: “Baba J mimi ni mwanamke kama Iryn, nikimwangalia namuona kabisa anakitu moyoni ila hawezi kuongea, namuona kabisa anakupenda, mnasiri kubwa sana mnaificha.”

MIMI: “Hivi tungekuwa na mahusiano angekuwa na uthubutu wa kuja hapa home? Kwa confidence gani?, Na ujue anakuja hapa home kwaajili yako na sio mimi.”

WIFE: “Iryn anampenda sana Junior mpaka nashindwa kuelewa huu upendo unatoka wapi? Hivi unajua Junior alikuwa anamshika tumbo na anafuraha zote.”

MIMI: “Sasa Junior kumshika tumbo kuna shida gani? Unawaza ujinga tu.”

WIFE: “Ipo siku nitajua kinachoendelea kati yenu.”

MIMI: “Afu wewe ni mnafiki sana, Iryn akija unacheka naye, akiondoka lawama zote zinakuja kwangu, sasa nisikilize kwa makini, naomba umpige marufuku asije hapa, kama kuonana muwe mnatafuta sehemu ya kuonana ila sio kwangu naomba tuelewane kwa hili.”

WIFE: “Sidhani kama hiyo ni busara, mimi siwezi kumfukuza wala kumwambia asije nyumbani na dini hainifundishi hivo, hata kama ni adui yangu mimi siwezi kumchukia nitakublame wewe.”

Ni maongezi yaliyochukua karibu lisaa maana tuliongea mambo mengi sana ikiwemo ya Elena kwenda shule.

Wife aliingia ndani kuangalia JUAKALI na mimi nilikwenda chumbani na ile kushika simu nakutana na missed call 2 za Asmah, nikazipotezea na nilikutana na ujumbe wa Sumaiya akihitaji gari yake.

Nilipanda kitandani kulala lakini nilikuwa nafikiri suala la Iryn kuhusu ujauzito wake, pia niliwaza sana nikaona huu msala kutoboa ni ngumu sana, hili jambo likija kujulikana nihesabu maumivu. Kwa upande mwingine nilifikiri kwa stage niliyofikia kuna haja ya kumshirikisha sister yangu, ila sasa ni busara nikamfata Arusha kuliko kuongea kwa simu.

Kipindi naendelea kutafakari haya mambo simu yangu ilianza kuita na ile kucheki ilikuwa ni namba ngeni ikipiga, nilijifikiria kwa sekunde kadhaa nikaipokea na alikuwa ni Pili binti ya mama wa2.

Nilishangaa sana kuona Pili akinipigia simu usiku na nilihisi huenda ana matatizo na yeye alisema anaomba nimtumie hela kwani mama yake amemgomea. Nilimuuliza kivipi mama amgomea wakati kila mwezi anamtumia pesa ya matumizi? Alilijitetea kuwa pesa alizopewa amenunulia simu, hapa sasa ikabidi nianze kumpiga maswali;

MIMI: “Mama anajua unatumia simu shuleni? Si alisema ukimaliza atakununulia au umesahau?”

PILI: “Uncle naomba tuchati siko sehemu nzuri.”

Ndani ya muda mfupi alinirudia na tukaanza kuchati;

“Uncle wenzangu wote wanasimu kasoro mimi tu.”

MIMI: “Simu ya nini? Una matumizi gani na hio simu? Kwanini usingevumilia mama akununulie? huoni utakuwa umemkosea sana?”

PILI: “I know but mimi namaliza shule soon, simu ni muhimu kuwa nayo.”

MIMI: “Pili listen to me carefully, umefanya mistake kubwa sana bora hata ungenishirikisha kabla ya kufanya maamuzi, mama akijua mtagombana sana ukizingatia wewe ndo binti yake wa kwanza na anakutegemea.”

PILI: “Promise me hutamwambia mama kama nina simu.”

MIMI: “Mimi siwezi kumwambia lakini huoni ni risk hata kwako kwa huko shuleni?”

PILI: “Hapana niko makini sana, kama hivi weekend ndo nakuwa natumia.”

MIMI: “Ok, nakutumiaje hio pesa?”

PILI: “0688xxxxxx Jina xxxx xxxxx.”

MIMI: “Soon nitakutumia ila naomba uwe makini sana na shule, mama yako akifahamu hii siri tutagombana sana.”

Nilimtumia elfu 55 pamoja na ya kutolea lakini nilikuwa na wasiwasi mkubwa sana, mpaka kufikia maamuzi ya kununua simu nilihisi huenda kuna sababu, japo alikuwa ana approach 18 years. Sikutaka kufikiri sana sababu hata mimi haya maisha nilikuwa nimeyapitia enzi hizo niko ordinary na advance level.
*****

Jumatatu nilikuwa na ratiba mbili muhimu ya kwanza ni kwenda site Bahari beach na ya pili kuonana na Jane, nilipiga hesabu nikaona ni bora nikaanza na site then nikamalizana na Jane maana alikuwa hatabiriki. Nilimpigia simu Cami ile asubuhi na tukakubaliana tuonane saa 5 asubuhi na atanipitia ili twende wote huko site.

Saa 5 kasoro alinipigia simu kunipa taarifa kuwa yuko njiani anakuja kunipitia na mimi nilimwambia aje home kunichukua sababu nilikuwa na Junior afu dada yake amekwenda sokoni.

Baada ya muda mfupi Cami aliwasili home na nilimkaribisha ndani tukaendelea na story zingine na kubwa kuhusu maelekezo ya site. Baada ya nusu saa Elena alirudi na sisi tukaanza safari ya kwenda Bahari beach na njiani tulikuwa tunapiga story nyingi sana;

CAMI: “Tunachotakiwa kufanya sisi ni kuwa tunafanya ukaguzi wa kushtukiza tusiwe tunatabirika inshort.”

MIMI: “Ni hilo tu au kuna maagizo mengine?”

CAMI: “Inatakiwa tukija tunakaa muda mrefu tunaangalia progress kama kuna sehemu hatuelewi tunamuuliza constructor.”

MIMI: “Sawa bossy mtoto, ningekuwa sijaoa ningeongea na mzee nifanye kweli.”

CAMI: “Sidhani kama angehafiki hili jambo.”

MIMI: “Kwanini?”

CAMI: “Mzee anasemaga wewe ni mpambanaji afu mimi mvivu, so nisingekufaa.”

MIMI: “Mimi sihitaji upambanaji wako, nachohitaji ni mapenzi tu.”

CAMI: “Hahahaa! Insider unavituko sana, sasa kama mimi sio mpambanaji afu ikatokea wewe umekufa watoto watakula nini?”

MIMI: “Kama baba nitahakikisha naweka pesa za kutumia familia hata miaka 30 ijayo, mimi nachotaka kutoka kwako yaani nikirudi usiku nikukute upo uchi kitandani.”

CAMI: “Hahahahaa, acha me nicheke.”

MIMI: “Au na kwenye hii sekta bado huiwezi?”

CAMI: “Mungu hakunyimi vyote kuna kitu atakupa unique.”

MIMI: “Upo sahihi kama hivi amekupa familia ya kitajiri, bado ni mzuri kipi kingine unahitaji?”

CAMI: “Hamna Insider sisi ni wa kawaida tu, hatupo kama unavyofikiria.”

Ndani ya muda mfupi tulikuwa tumewasili eneo la tukio na palionekana kuwa busy sana maana ujenzi ndo ulikuwa unaanza na kipindi hiki walikuwa wanachimba kwaajili ya foundation.

Tulitumia masaa 2 pale na kabla ya kuondoka nilifanya mawasiliano na Jane akanambia tuoanane kesho kwaajili ya kufanya manunuzi ya vitendea kazi vya dukani, na tulikubaliana tuwahi ili twende na Kariakoo.

Tuliondoka na tulianza kupitia Juliana kwaajili ya kupata lunch na tuliagiza ugali kwa Kitimoto, na alitokea kukipenda sana Kitimoto cha pale Juliana akatoa ahadi ya kuwa tunakwenda pale kula kitimoto.

Tulitumia kama lisaa hivi kisha tukaondoka na alinidrop home akaendelea na safari zake, lengo la kurudi home nichukue gari ili niende Masaki. Kipindi niko home Lucy alinipigia simu kunipa taarifa kwamba Landlord kamtafuta kuulizia mrejesho kama tulovyokuwa tumemuahidi, nilimjibu nakwenda ofisini tuzungumze.

Kumbuka hii ishu nilipaswa kuongea na Iryn lakini tulishindwa kuongea na kupanga mipango sababu tulikuwa tumetofautiana, hivyo niliona ni bora niongee na Lucy ili awasiliane na Iryn direct.

Niliondoka kwa spidi kali kwenda Mikocheni kuonana na Lucy na tulikaa nje kibarazani tukiongea na kubwa alitaka kujua kama nimeongea na Iryn au laah!

LUCY: “Natumaini umeongea na Iryn anasemaje?”

MIMI: “Huwezi amini sijafanikiwa kuongea naye zaidi tumeishia kugombana.”

LUCY: “What? Tatizo ni nini tena?”

MIMI: “Iryn alikuja Ijumaa sasa aliniletea dharau na niliishia kumtia vibao.”

LUCY: “Unazingua ujue, hivi unafahamu yule ni mjamzito? Hivyo vitu ni kawaida kwa wajawazito, inategemea na mood aliyonayo, wewe hivo vitu vidogo unapaniki?”

MIMI: “Too much alinitia hasira, achana na hizi ishu yalishapita.”

LUCY: “Sasa tunafanyaje? Maana wewe ndo ulikuwa wa kuongea na Iryn akauelewa.”

MIMI: “Sikia, mimi kaninunia kabisa hana hata hamu ya kuniona wala kuongea na mimi, chakufanya ongea nae kuhusu hili.”

LUCY: “Sawa, ila next time usifanye hivyo, kumbuka ni mjamzito hapa ndo unakofeli, wajawazito wanavitimbi sana unatakiwa kuwa mvumilivu, nitaongea nae myamalize.”

MIMI: “Usithubutu kuongea nae zaidi ya hili nililokwambia, afu utanipa mrejesho.”

LUCY: “Mhhh okay no problem.”

MIMI: “Hongera kwa kumpata mwenza, tunakula pilau lini?”

LUCY: “Hahahaa Insider tulia kwanza, naona unawaza mbali sana.”

Tuliishia kucheka pale na mimi nikaondoka kwenda Masaki na nilianza kupitia pale Morocco kwa Jamaa ili nicheki gari ya kununua ambayo haina mambo mengi.

Nilifanikiwa kuonana na jamaa pamoja na kuziangalia gari alizo kuwa nazo, ila sasa nilikuwa nakosa choice nichukue gari gani na nilimwambia anipe muda kesho nitamcheki, nikaondoka kwenda Masaki.

Baada ya kufika ofisini nilianza kuzinguana na Rebby maana alikuwa pale nje kibarazani na kubwa alikuwa ananipa hongera ya mimi kuwa baba, pamoja na kunipa sifa kedekede za kumtia mimba mwanamke mrembo.

Niliendelea kutaniana na Rebby na habari nyingine aliyoniambia ni kwamba kitendo nilichofanya jana cha kuondoka bila kuwasalimia, Iryn alimind na alimwambia Rebby kuwa mimi na dharau, ilibidi nicheke maana Rebby alikuwa hajui kinachoendelea.

Niliingia ndani ofisini na niliwakuta Hilda na Nolie wakipiga story huku wanacheka, sasa ile mimi kuingia ghafla walinyamaza na Nolie alisimama ili aondoke, nikampa ishara akae;

MIMI: “Kwahiyo mmeniona mmenyamaza kama sio umbeya ni nini?”

HILDA: “Tulikuwa tunacheka mambo yetu tu.”

MIMI: “Kumbe Nollie ni muongeaji? Maana namuonaga yuko serious sana hataki story.”

HILDA: “Hamna lolote, hajakuzoea anakuogopa sana.”

NOLLIE: “Hilda acha zako, unazingua.”

MIMI: “Next time tutakwenda wote Zanzibar ili unizoee vizuri.”

HILDA: “Mhhh! Bossy ukisema mimi siwezi kupinga, kwanza hii jeuri natolea wapi? afu Asmah alikuja kutusabahi alisema atakuja badae.”

MIMI: “Ngoja nimcheki, nina shida nae sana.”

HILDA: “Mama pia amerudi, mmepishana kidogo tu.”

MIMI: “Mama karudi? Hajamind kunikosa hapa?”

HILDA: “Anaanzaje kukumind wakati wewe ni mkwe wake?”

Niliishia kucheka na nikatoa simu kumpigia Asmah ili tuonane na alinambia yuko ofisini ameanza kazi rasmi leo, hivyo atanicheki badae kidogo ili tuonane.

Saa 12 jioni Asmah alinicheki ili tuonane na tulikubaliana tukutane Salt restaurant na nilimwambia atangulie nitamkuta, yeye baada ya kufika alinipa taarifa na ilinichukua dakika 20 kufika eneo la tukio.

MIMI: “Kigamboni unamishe gani sikuhizi mpaka unalala huko?”

ASMAH: “Kuna ndugu zangu kule.”

MIMI: “Mmh hujawahi kunambia kuhusu hili, kubali ulikuwa kwa bwana wako.”

ASMAH: “Kweli Insider nilikuwa na sister why should I lie to you?”

MIMI: “Sawa tuachane na haya, weekend hii nilikuwa na Iryn, moja ya kauli alizoziongea na zimenipa utata ni kwamba mimi na wewe had sex, kajuaje?”

ASMAH: “How? Labda wewe uwe umetoa siri au ameona chats zetu, kwangu mimi sijaonana na mtu yoyote mwenye mawasiliano ya karibu na Iryn zaidi yako.”

MIMI: “Hata mimi sielewi maana ameongea kuonesha anajua kinachoendelea na anasema yeye sio mjinga.”

ASMAH: “Labda anafanya guessing hana uhakika wa hili.”

MIMI: “Inawezekana ikawa kweli au ripota zake wanamdanganya na yeye anajaa.”

ASMAH: “Hapo sasa nakuunga mkono, nilisahau ana CIA wake wanampa taarifa.”

MIMI: “Tuachane na haya, naona unazidi kuwa mrembo sana, naomba nizalie mtoto.”

ASMAH: “Mhh kukuzalia ni ngumu hata Dini hainiruhusu kuzaa bila ndoa.”

MIMI: “Ila inakuruhusu kusex na mimi?”

ASMAH: “Insider suala la mapenzi kila mtu ni mdhaifu na tumetofautiana, kwani wewe Dini inakuruhusu?”

MIMI: “Hapana hainiruhusu kufanya hivi.”

ASMAH: “The same applies to me.”

MIMI: “Kwahiyo mtoto unanizalia au hutaki?”

ASMAH: “Achana na hizi mada bhana, please.”

MIMI: “Sound like yes, vipi kuhusu ofisi mpya mshahara wanakulipaje?”

ASMAH: “Not bad kama 2.5M na point something.”

MIMI: “Wow atleast kuna excess kubwa ukicompare na zamani.”

ASMAH: “Shida ya huku nitaishi kwa kutegemea mshahara tofauti na Salon ambako mishemishe zilikuwa ni nyingi.”

Muda huu simu yangu ilianza kuita na ile kucheki alikuwa ni Sumaiya akipiga, moja kwa moja nilijua anataka gari yake maana tulikuwa tumekubaliana kumrudishia leo. Kwa upande wangu nilishia kumtia kiswahili na nilimwambia nitampa kesho, lengo langu nimuwekee android TV kama ahsante.

Niliendelea kuongea na Asmah mpaka saa 1 usiku ndo kuagana na nikaondoka kurudi home.

Baada ya kuwasili home zilipita kama dakika 10 simu ya Jimmy ilianza kuita na ilibidi nipokee kwa haraka sana kumsikikiza maana nilihisi kuna jambo anataka kunambia,

JIMMY: “WhatsApp brother, how are you doing?”

MIMI: “Niko salama bro, ni kitambo kidogo.”

JIMMY: “Yeah, sio sana vipi lakini mambo yanakwendaje?”

MIMI: “Namshukuru Mungu bro, binti yako mdogo anasemaje?”

JIMMY: “Hahaha she’s really fine, maendeleo yako kwa ujumla?”

MIMI: “Salama kaka, leta habari.”

JIMMY: “Kuna jambo nataka kushare na wewe kama mwanaume mwezangu, leo nimewasiliana na Iryn, ila habari mbaya amesema anataka ku-abort ujauzito wake sababu kubwa anadai haoni future yoyote na wewe, anaweza jikuta anaingia kwenye matatizo na familia bila manufaa yoyote.”

MIMI: “Sidhani kama hio ndo sababu najua anahasira na mimi nafiri amekwambia kilichojiri.”

JIMMY: “I don’t know anything bro, please tell me.”

Ilibidi nimpe mkanda mzima kuhusu kilochotokea na Iryn kule hotelini,

JIMMY: “Ndomana anataka kufanya maamuzi ya ajabu kumbe tatizo limeanzia hapa.”

MIMI: “Ndio hivo bro sijui unanisaidiaje juu ya hili maana mimi niko upande wake na siwezi kumuacha alone kwenye hili, na wewe ni kama shem wangu nakwambia ukweli.”

JIMMY: “I will try to talk to her again, pia na wewe ukae nae chini myamalize kabla hajafanya maamuzi ya ajabu.”

MIMI: “Hili ondoa shaka, tutayamaliza soon.”

JIMMY: “Jitahidi bro, namjua Iryn vizuri hasa kwenye kufanya maamuzi magumu kama haya.”

Baada ya kumalizana na Jimmy nilijikuta niko katika wakati mgumu sana afu ndo kwanza mimba ina miezi 4, ila sioni future ya huyu mtoto. Niliwaza kama nitamkosa na huyu mtoto bhasi nitajiweka kwenye kundi la wanaume ambao hawana bahati hapa duniani, kwa Prisca mtoto alipotea kizembe na Iryn tena?.

Nilipata wazo nimpigie simu kwa mara nyingine na kama hatapokea bhasi nimuandikie ujumbe mzuri wa kumuomba msamaha na kumkumbusha tulikotokea, niliona ni bora nikajifanya mjinga kuliko kukosa vyote. Sasa ile nafungua whatsapp ili nimpigie nakutana na tofali ilibidi nianze kucheka tu maana sikuwa na jinsi, nilijisemea huyu mwanamke kazi ipo.
*****

Asubuhi nilifanya mawasiliano na Jane ili tupange ratiba mapema za kuonana na kwenda Kariakoo, nilitaka haya mambo yafanyike mapema ili nipate muda wa kwenda ofisini, mama Janeth alikuwa karudi na muda wowote angekuja ofisini na asiponikuta haitapendeza. Baada ya kuwasiliana na Jane tulikubaliana tuoanane kuanzia saa 3 na nilimwambia anipitie Rainbow pale filling station ya Oilcom.

Saa 3 na madakika ontime alinipitia pale Oilcom na tulianza safari ya kwenda Kariakoo na alisema tuanze kwanza kutafuta fridge yale yakuwekea ice cream, then tutaendelea na kutafuta vitu vingine. Habari njema kwa pale Kariakoo nina watu wangu, hivyo haikuwa tabu kwangu kuwapigia simu na kuwapanga mapema.

Kwa ufupi zoezi letu lilikamilika mapema sana na lilikwenda kama tulivyopanga maana kufikia saa 6 mchana tulikuwa tumekamilisha kila kitu kwa kule Kariakoo. Baada ya hapo tulipeleka mazaga yote dukani, kwa upande mwingine kuna baadhi ya suppliers walikuwa washaanza kushusha mizigo, mambo yalikuwa ni moto.

Nilishinda na Jane mpaka saa 9 mchana pale dukani na nikamuaga huyo nikaondoka kwenda Masaki ofisini, ila nilianza kwanza kupitia Mikocheni ili nionane na Lucy anipe feedback ya jambo ambalo tulikuwa tumeongea.

Baada ya kuonana na Lucy majibu aliyonipa ni kwamba bado hawajapata solution yoyote, afu dizaini kama Iryn hayuko serious na hili jambo, aliniendelea kunisisitiza mimi ndo niongee na Iryn maana ndo atanielewa vizuri kuliko yeye.

MIMI: “Iryn kaniblock labda umpigie niongee nae kupitia simu yako, kidogo anaweza kunisikiliza.”

LUCY: “Aisee! Mmegombana kwenye kipindi kibaya, nipe simu nimpigie.”

Lucy alimpigia simu lakini hakupokea na alipiga mara mbili bila majibu yoyote,

MIMI: “Achana nae, mama amerudi acha nikaongee nae kuhusu hii ishu.”

LUCY: “Hapo sawa atleast inaweza kusaidia.”

Niliondoka kwenda Masaki na baada ya kuwasili nilikwenda straight ndani na jambo la kwanza nilimuuliza Hilda kama mama alikuja ofisini na akanijibu hakuja, hapa kidogo nikawa na amani, ukweli nilikuwa nazingua.

Niliwaza nimpigie simu mama ili tuoanane tuzungumze kuhusu suala la landlord, hata baada ya kumpigia simu hakupokea nikahisi atakuwa busy na atanirudia.

Mida ya saa 11 nilitoka kwenda kuonana na Allen na nilimuaga Hilda, kwa masharti ya kunipa taarifa pindi mama akija ofisini, uzuri ofisi ya Allen ipo Masaki hapahapa na sio mbali.

Nilitakiwa kuonana na Allen ili anipe ushauri kuhusu sakata la Iryn maana nilikuwa njia panda afu nakosa maamuzi ya kufanya. Nilitumia muda mchache sana kuwasili pale ofisi kwake, nilikuwa nimeshampa taarifa ya uzuru wangu na ndo ilikuwa siku ya kwanza naingia ofisi kwake.

Baada ya kuwasili pale reception nilikaa nikimsubiri na hakuchukua muda alikuja kunipokea na akanikaribisha ndani kwenye ofisi yake.

ALLEN: “Insider mdogo wangu karibu sana.”

MIMI: “Ahsante sana bro, nimekaribia kwa wakaguzi.”

Pembeni alikuwepo dada na alinitambulisha pale kwa mbwembwe zote!

ALLEN: “Winny huyu unayemuona anaitwa Insider ndo kijana pekee hapa mjini anayemiliki Audi Q7 new model, usimwone hivyo ukamdharau.”

Yule dada aliishia kutabasamu na kunikaribisha kisha akaondoka,

MIMI: “Kaka ndo unafanya nini hivo?.”

ALLEN: “Nilikuwa nakukaribisha ondoa wasiwasi, jisikie upo nyumbani muda wowote karibu tupige story.”

MIMI: “Kaka mimi sijaja kupoteza muda hapa na kilichonileta ni jambo ambalo linanisumbua sana sana, kutokana na profession uliyonayo naamini unaweza kunisaidia kimawazo kuhusu hilo jambo.”

ALLEN: “Sawa dogo, shida ni ipi hiyo.”

Na alivaa miwani kuonesha yuko serious,

MIMI: “Kaka mimi nilishakosea lakini sio wakwanza kukosea, mistake ilishatokea na sina jinsi….”

Alinikatisha maongezi yangu;

ALLEN: “Mdogo wangu be free just talk kama litakuwa chini ya uwezo wangu litaisha kama litakuwa beyond, hatutakosa solution.”

Nilianza kumpa mkasa mzima kuhusu Iryn na jinsi tulivyokutana mpaka anapata mimba na jinsi mambo yanavyokwenda kwasasa. Kipindi namsimulia kwa upande wake alikuwa makini sana kunisikiliza na baada ya kumaliza kumsimulia alianza kuongea;

ALLEN: “Mdogo wangu hili jambo hata lisikuumize kichwa ni dogo sana, mimi hapa unavyoniona nina mke na watoto wawili lakini nina mtoto wa nje, vivyohivyo ilitokea bahati mbaya. Na nikupe siri moja kama huijui, asilimia kubwa ya wanaume wana watoto nje ila ni ngumu kumjua mtu wa dizaini hii, ila ni wengi.”

MIMI: “Wasiwasi wangu ni wife akija kujua naona kabisa tunaachana na mimi sitaki kuona dogo akilelewa na mama mwingine.”

ALLEN: “Mdogo wangu hili ondoa shaka, kwanza hawa wanawake wote inaonesha wanakupenda na huu ndo udhaifu wao, mama J anakupenda kukuacha ni ngumu sana, hii ni advantage kwako, tuachane na haya masuala tuanze kuongelea suala la Iryn maana ana mtoto wetu.”

MIMI: “Upo sahihi nafikiri hapa ndo muhimu kwanza mengine tutadiscuss badae.”

ALLEN: “Nisikilize kwa makini mdogo wangu, yule mtoto ni wetu na hakikisha hufanyi mistake yoyote, ukimkosa uyo mtoto hata wazazi hawatokuelewa maana ni ukoo, wazazi hawawezi kumkataa mtoto eti sababu umezaa na mwanamke mwingine nje, hakuna kitu kama hicho. Hili jambo halihitaji kutumia nguvu ni akili, wazazi wake wanataka uende Ethiopia ili uwape assurance ya ndoa, kama nilivyokwambia before kwa tamaduni za kiafrica hakuna mzazi ambaye atafurahi kuona mtoto wake ametiwa mimba bila ndoa, hakuna.”

MIMI: “Uko sahihi bro kwa hili nakubali, hata kwa mama J ilikuwa hivihivi, baada ya kumvalisha pete mambo yakatulia.”

ALLEN: “Exactly ndo ilivyo na wazazi walitulia sababu umewapa assurance ya kumuoa binti yao, mdogo wangu haya mambo kama tunacheza na auditing za financial statements.”

MIMI: “Hahahaa bro unazingua, mimi na Auditing wapi na wapi?”

ALLEN: “Si utasoma masters au CPA utayajua tu, sasa nini tufanye kwenye hili jambo ni simple, kwanza onesha upo side yao, na hakikisha haufanyi jambo ambalo litawapa mashaka, kwasasa hakuna haja ya kwenda Ethiopia zaidi utakwenda kujiwekea kamba shingoni, tusubiri kwanza ajifungue hapo sasa tutakuwa na jeuri ya kwenda Ethiopia.”

MIMI: “Kaka hivi unafikiri wanaelewa? Ndo kwanza mimba ina miezi minne”

ALLEN: “Nisikilize mdogo wangu, haya yote atakayetusaidia ni Iryn mwenyewe, yeye sasa ndo awe kifua mbele kuhakikisha anakusafisha na kukuwekea mazingira mazuri huko kwao. Hata usipaniki kwa hili sababu dada anakupenda, pia amebeba mimba kwa interest yake tena bila kumlazimisha, hawezi kwenda against na wewe.”

MIMI: “Jana nimetoka kuongea na kaka yake amenipa taarifa anataka kufanya abortion na amenisisitiza sana juu ya hili.”

ALLEN: “Mdogo wangu anakutisha tu hawezi kufanya hicho kitu, kutokana na historia uliyonipa na mazingira aliyokulia si rahisi kutoa hio mimba kwanza ina miezi 4, hawezi hizo ni hasira tu, ila atakaa sawa na atakutafuta akikumiss, kama huniamini wewe acha kumtafuta nampa siku 3 atakuwa amekutafuta mwenyewe.”

Wakati tukiendelea na maongezi Hilda alinipigia simu na nilikumbuka nilimwambia mama akija anijulishe, bhasi baada ya kupokea alinipa taarifa mama yuko ofisini, hivyo ilibidi nimuage Allen kwa kumwambia nakwenda kuonana na Bossy na nitarudi soon.

Ilikuwa ni saa 12 jioni wakati natoka pale ofisini kwa Allen na nilitoka kwa spidi kurudi ofisini na ndani ya dakika 5 nilikuwa nje getini na ile naingiza gari ndani namuona mama amesimama kibarazani anaongea na Hilda.

Nilishuka kwenye gari nikaenda straight mpaka usawa wao na nikamsalimia pale kwa adabu zote, matokeo yake alinijibu kama mtu ambaye hataki salamu yangu na aliingia ndani.

Kwa lile tukio hata Hilda alibaki anashangaa maana hakutegemea kuona mama akinifanyia vile, ukizingatia mimi ni mtu ambaye ananikubali na kuniamini, ukweli nilijisikia vibaya sana baada ya hili tukio…..

CHAPTER 21
 
Back
Top Bottom