Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,072
Wadau wa fikra,

Nafahamu kuwa muongozo wa Jukwaa hili unatutaka tuweke serious reports & discussions on Corruption, Politics na etc kwa ajili ya mijadala yakinifu. Tofauti na Jukwaa la Dini ambalo lengo lake kuu ni kuhamasishana kuhusu masuala ya kiimani na kufundishana yale yaliyo mema.

So, uzi huu hauna lengo la kuhamasishana kuhusu imani bali kujadiliana kwa kina kuhusu mambo ya kale (historical facts) yanayoingiliana kidogo na dini/imani. Naamini nimejaribu kuweka utofauti ili isionekane naleta mjadala wa kidini kwenye jukwaa hili makini.

Kupitia historia fupi ya Maria, nitaeleza mtihani wa Bikra Maria kwa Mkuu wa Kanisa/Hekalu alimolelewa, ambaye alikuwa ni Nabii Zakaria. Ni matarajio yangu tutaulizana maswali na kurekebishana kwa uungwana ili sote tuweze kuelimika na kufahamishana mambo mengi tusiyoyajua.

Hebu tuipitie historia hiyo kidogo..

Wazazi wake
Maria alizaliwa na Mzee Joachim na Bi. Anna ambao walikuwa ni wachamungu haswa. Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachamungu wa enzi hizo, Mungu aliwapa mtihani wa ugumba Mr. & Mrs Joachim kiasi cha kudharaulika katika jamii kabla ya kuwainua kwa kuwapatia msichana mtakatifu Maria, baada ya kuzidisha kwao ibada na maombI.

Malezi yake
Watakatifu zamani walikuwa wakiweka nia kwa watoto wao watakaowazaa. Familia hii ya mzee Joachim na mkewe waliweka nadhiri kwamba endapo Mungu atawajaalia mtoto, basi watamtoa wakfu - yaani atatumika kwenye kazi za Mungu (utumishi). Hivyo, baada ya uzao wa Maria na kufikisha umri wa miaka 2/3 baada ya kuacha ziwa, walitekeleza ahadi yao kwa kumpeleka hekaluni kulelewa na Kiongozi wa hekalu ambaye alikuwa ni mzee Zakaria, mume wa Elizabeth (mama yake Yohana Mbatizaji).

Hekaluni palikuwa pakilelewa mabinti bikra kwa kuwa walizingatiwa kuwa wasafi na watakatifu zaidi. Kwahiyo binti Maria aliishi humo pamoja na mabinti bikra wengine na kufundishwa maadili mema pamoja na sheria za Mungu. Wazazi wake walikuwa wakimtembelea mara kwa mara mpaka alipofikia umri wa miaka 10 wakafariki dunia.

Ndoa
Alipofikisha umri wa miaka 13, yaani miaka mitatu baada ya wazazi wake kufariki, uongozi wa Kanisa uliamua Maria atoke hekaluni ili aweze kupata mume. Kwa mila na desturi za hekalu enzi hizo, binti akishavunja ungo anakuwa sio msafi tena hivyo hahitajiki kubaki hekaluni kwa sababu atalichafua. Hata hivyo, Maria alijenga hoja kwamba yeye wazazi wake waliamua kumtoa wakfu hivyo ameamua ataitunza bikra yake na kumtumikia Mungu maisha yake yote.

Jambo hili lilileta mtihani kidogo kwa mzee Zakaria kwa sababu ni unprecedented. Akalazimika kuitisha baraza la ushauri namna ya kudeal nalo ambapo uamuzi ulifikiwa kuwa aende altareni akiwa pekee aombe hekima ya Mungu. Usiku wake, alifanya hivyo na Malaika akamtokea na kumpa Muongozo kwamba aitishe mkutano wa wagane wachamungu ambapo mmojawapo atateuliwa na Mungu kwa ishara kwa kuwa bado Mungu ana kusudi maalum na Maria.

Basi, ndipo katika kusanyiko la wanaume hao wagane, alikuwemo mzee wa miaka takribani 80 aitwaye Joseph. Fundi seremala mchamungu haswa, ambaye mkewe Salome alifariki mwaka mmoja uliopita na alijaaliwa naye watoto 7.

Kufupisha story, mzee huyo alifanikiwa kuteuliwa kwa ishara ya mng'ao wa kitambaa. Naye binti Maria (13) hakuwa na pingamizi kwenye uamuzi wa Muumba. Akakubali kuolewa.

Na historia maarufu ya Bikra Maria sasa inaanzia hapo na kuendelea. Kuna haja ya kuisimulia zaidi?!
 
Duh
Kwahiyo Yusuph (Joseph) aliye mposa Maria alikuwa ni mzee mwenye watoto 7? Kisha akataka kumuacha kwa siri ili asimtie aibu baada ya kugundua kuwa Maria ni mja"mwepesi"?
Aloo, Tunaomba na kitabu cha rejea (reference book) ya hii maandiko yako
Hii itakuwa ni Injili mpya sana kwangu
 
Duh
Kwahiyo Yusuph (Joseph) aliye mposa Maria alikuwa ni mzee mwenye watoto 7? Kisha akataka kumuacha kwa siri ili asimtie aibu baada ya kugundua kuwa Maria ni mja"mwepesi"?
Aloo, Tunaomba na kitabu cha rejea (reference book) ya hii maandiko yako
Hii itakuwa ni Injili mpya sana kwangu

Sahihi kabisa mkuu. Ukiisoma vizuri Injili ya Luka utakutana na simulizi. Ama ukitafuta agano la kale na baadhi ya vitabu vinavyofafanua zaidi mambo ya nyakati utakutana nayo. Nilichofanya ni ku-compile tu ili iwe kwenye mtiririko mzuri.
 
Wadau wa fikra,

Nafahamu kuwa muongozo wa Jukwaa hili unatutaka tuweke serious reports & discussions on Corruption, Politics na etc kwa ajili ya mijadala yakinifu. Tofauti na Jukwaa la Dini ambalo lengo lake kuu ni kuhamasishana kuhusu masuala ya kiimani na kufundishana yale yaliyo mema.

So, uzi huu hauna lengo la kuhamasishana kuhusu imani bali kujadiliana kwa kina kuhusu mambo ya kale (historical facts) yanayoingiliana kidogo na dini/imani. Naamini nimejaribu kuweka utofauti ili isionekane naleta mjadala wa kidini kwenye jukwaa hili makini.

Kupitia historia fupi ya Maria, nitaeleza mtihani wa Bikra Maria kwa Mkuu wa Kanisa/Hekalu alimolelewa, ambaye alikuwa ni Nabii Zakaria. Ni matarajio yangu tutaulizana maswali na kurekebishana kwa uungwana ili sote tuweze kuelimika na kufahamishana mambo mengi tusiyoyajua.

Hebu tuipitie historia hiyo kidogo..

Wazazi wake
Maria alizaliwa na Mzee Joachim na Bi. Anna ambao walikuwa ni wachamungu haswa. Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachamungu wa enzi hizo, Mungu aliwapa mtihani wa ugumba Mr. & Mrs Joachim kiasi cha kudharaulika katika jamii kabla ya kuwainua kwa kuwapatia msichana mtakatifu Maria, baada ya kuzidisha kwao ibada na maombI.

Malezi yake
Watakatifu zamani walikuwa wakiweka nia kwa watoto wao watakaowazaa. Familia hii ya mzee Joachim na mkewe waliweka nadhiri kwamba endapo Mungu atawajaalia mtoto, basi watamtoa wakfu - yaani atatumika kwenye kazi za Mungu (utumishi). Hivyo, baada ya uzao wa Maria na kufikisha umri wa miaka 2/3 baada ya kuacha ziwa, walitekeleza ahadi yao kwa kumpeleka hekaluni kulelewa na Kiongozi wa hekalu ambaye alikuwa ni mzee Zakaria, mume wa Elizabeth (mama yake Yohana Mbatizaji).

Hekaluni palikuwa pakilelewa mabinti bikra kwa kuwa walizingatiwa kuwa wasafi na watakatifu zaidi. Kwahiyo binti Maria aliishi humo pamoja na mabinti bikra wengine na kufundishwa maadili mema pamoja na sheria za Mungu. Wazazi wake walikuwa wakimtembelea mara kwa mara mpaka alipofikia umri wa miaka 10 wakafariki dunia.

Ndoa
Alipofikisha umri wa miaka 13, yaani miaka mitatu baada ya wazazi wake kufariki, uongozi wa Kanisa uliamua Maria atoke hekaluni ili aweze kupata mume. Kwa mila na desturi za hekalu enzi hizo, binti akishavunja ungo anakuwa sio msafi tena hivyo hahitajiki kubaki hekaluni kwa sababu atalichafua. Hata hivyo, Maria alijenga hoja kwamba yeye wazazi wake waliamua kumtoa wakfu hivyo ameamua ataitunza bikra yake na kumtumikia Mungu maisha yake yote.

Jambo hili lilileta mtihani kidogo kwa mzee Zakaria kwa sababu ni unprecedented. Akalazimika kuitisha baraza la ushauri namna ya kudeal nalo ambapo uamuzi ulifikiwa kuwa aende altareni akiwa pekee aombe hekima ya Mungu. Usiku wake, alifanya hivyo na Malaika akamtokea na kumpa Muongozo kwamba aitishe mkutano wa wajane wachamungu ambapo mmojawapo atateuliwa na Mungu kwa ishara kwa kuwa bado Mungu ana kusudi maalum na Maria.

Basi, ndipo katika kusanyiko la wanaume hao wajane, alikuwemo mzee wa miaka takribani 80 aitwaye Joseph. Fundi seremala mchamungu haswa, ambaye mkewe Salome alifariki mwaka mmoja uliopita na alijaaliwa naye watoto 7.

Kufupisha story, mzee huyo alifanikiwa kuteuliwa kwa ishara ya mng'ao wa kitambaa. Naye binti Maria (13) hakuwa na pingamizi kwenye uamuzi wa Muumba. Akakubali kuolewa.

Na historia maarufu ya Bikra Maria sasa inaanzia hapo na kuendelea. Kuna haja ya kuisimulia zaidi?!
chanzo cha hii taarifa (reference) ipo wapi au ni mawazo yako???
 
so Joseph ALIKUWA MZEE WA MIAKA 70!
MJANE!
ANA WATOTO SABA?
duh!
aloooh!
mbon mi huwa nahisiga alikuwa junki tu namuaimagine kuwa bonge la handiiiii(AHAHAHAHHA)
my bad!

Hakuwa kijana. Alikuwa mzee mchamungu sana na mwenye hekima.

Yes alikuwa mjane na alibarikiwa watoto 7; Wanne wa kiume na watatu wa kike. Marehemu mkewe alikuwa akiitwa Salome.

Licha ya uzee, inawezekana alikuwa handiiiiii kama JK.. Si ajabu!
 
chanzo cha hii taarifa (reference) ipo wapi au ni mawazo yako???

Hili swali nimeshalijibu mara mbili hapo juu. Soma vizuri Injili ya Luka na Isaiah kidogo.. Pita pita kwenye maandiko yahusuyo nyakari na vizazi kisha unganisha dots..

Mimi nimechukua muda kukusanya na kuweka pamoja tu, sio mawazo yangu binafsi.
 
Kwahiyo uko serious hautaendelea?
Mkuu hiyo stori naweza kuiendeleza lakini haitokuwa na jipya kivile.. Ni yale yale ya Malaika Gabriel kuleta ujumbe kuhusu Maria kupata mtoto kwa uwezo wa roho mtakatifu n.k.

Badala yake, nafikiria kuleta simulizi yenye topiki tofauti though bado najiuliza nilete simulizi ipi.. Zipo nyingi lakini ambayo niko nayo tayari ni ile ya Maria Magdalena na maisha yake ya ukahaba kabla hajakutana na Yesu na kutubu..

Zipo nyingi sana mkuu..
 
Mkuu hiyo stori naweza kuiendeleza lakini haitokuwa na jipya kivile.. Ni yale yale ya Malaika Gabriel kuleta ujumbe kuhusu Maria kupata mtoto kwa uwezo wa roho mtakatifu n.k.

Badala yake, nafikiria kuleta simulizi yenye topiki tofauti though bado najiuliza nilete simulizi ipi.. Zipo nyingi lakini ambayo niko nayo tayari ni ile ya Maria Magdalena na maisha yake ya ukahaba kabla hajakutana na Yesu na kutubu..

Zipo nyingi sana mkuu..
Leta yoyote utakayowiwa mkuu! Barikiwa
 
Aseee duh,
Sina facts za kupinga hii hoja,ntauliza mapadri tu.
Never imagined this,old man married virgin mary,
It sounds funny and ridiculous BUT it might be true
 
Back
Top Bottom