Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

Maria hakufa mkuu,, alipalizwa Binguni...!

Sent using Jamii Forums mobile app

Kupalizwa kwa Maria ni Dogma ya Wakatoliki ila kuna maandiko na simulizi zinazosema kuwa alifariki pia tena kwa kufatwa na mwanaye na kupewa chaguo (kumbuka Maria hakuwa na dhambi ile yetu ya asili so hakuwa na ulazima wa kufa) akamjibu kuwa “Bwana, nataka kupitia kila ulichopitia” hivyo mwili na roho yake vikatengenishwa.

Kuna ushahidi wa sanda aliyozikiwa pia uko kwenye museum huko walipokuwepo. Ngoja nikutafutie hizo simulizi
 
Hapa si kweli. Yohana ambaye baba yake ni Zakaria na mama yake ni Elizabeth ndiye aliyekuja kumbatiza Yesu, yaani ni Yohana Mbatizaji, naye huyu aliuawa na Herode na kichwa chake kikatolewa kama zawadi kwa binti wa Herode siku ya birthday yake (Mathayo 14:1-12 na Marko 6:14-30). Kumbuka kuwa hata Yohana Mbatizaji alikuwa na wanafunzi wake (Luka 7:18-28) na hakuna popote katika Biblia ambako Yesu alimchukua Yohana Mbatizaji kama mwanafunzi wake.
Yohana aliyeandika Injili ya Yohana, zile nyaraka 3 na Ufunuo SIYO yule Yohana Mbatizaji mwana wa Zakaria na Elizabeth, kwani wakati hayo yanaandikwa Yohana Mbatizaji alishauawa na Herode. Yohana mwinjili na mwandishi wa nyaraka 3 na kitabu cha Ufunuo ni mwana wa Zebedayo (Luka 5:10). Yohana huyu alikuwa na nduguye aitwaye Yakobo. Vijana hawa wawili mama yao aliwaleta kwa Yesu akamwomba wakae mmoja kulia na mwingine kushoto kwa Yesu katika ufalme wake (Mathayo 20:20-28), na hawa walikuwa miongoni mwa mitume 12 wa Yesu kama walivyoorodheshwa katika Marko 3:13-18.
Tumsifu Yesu Kristo.
Madini haya jamani
 
Sipendi kuharibu hii mada nzuri ya muhusika pia najua lengo ni kuwa na uelewa mkubwa wa mambo kwa ujumla ikiwa pamoja na imani zetu

Lkn kwa sie ambao hatuamini hizi Hadith za Wayahudi na jamaa zao wa mashariki ya kati tunapita kimya hapa kwa huzuni kuu ya kwamba mtu mweusi itachukua muda sana kujisimamia

Kuna Mwanamalunde,Mkwawa , kinjekitile,Shaka , Nzinga mbandi, na kadhalika wanatakiwa kupewa heshima kubwa kuliko mtu mweupe mmoja eti ndo ‘muokozi’ wetu dah haya
Sisi weusi tunazidiwa na weupe kwa idadi.Nadhani tuko moja ya saba hivi.

Utropicana umetufanya tukawa na akili zubaifu,jiografia imetukinga sana na majanga kwa hivo Bongo ya mtu mweusi haitumiki ipasavyo.Halafu pia upatikanaji wa mahitaji ni abundantly, akili inazubaa!
Ila wakati umeshawasili na tutapanda upesi sn kwenye daraja la juu.

Kuhusu Mada ya Bikira Maria,its amazing....coming soon!
 
Sisi weusi tunazidiwa na weupe kwa idadi.Nadhani tuko moja ya saba hivi.

Utropicana umetufanya tukawa na akili zubaifu,jiografia imetukinga sana na majanga kwa hivo Bongo ya mtu mweusi haitumiki ipasavyo.Halafu pia upatikanaji wa mahitaji ni abundantly, akili inazubaa!
Ila wakati umeshawasili na tutapanda upesi sn kwenye daraja la juu.

Kuhusu Mada ya Bikira Maria,its amazing....coming soon!
Umeandika kitu kikubwa sana hizo sentensi za mwanzo mkuu
 
Kupalizwa kwa Maria ni Dogma ya Wakatoliki ila kuna maandiko na simulizi zinazosema kuwa alifariki pia tena kwa kufatwa na mwanaye na kupewa chaguo (kumbuka Maria hakuwa na dhambi ile yetu ya asili so hakuwa na ulazima wa kufa) akamjibu kuwa “Bwana, nataka kupitia kila ulichopitia” hivyo mwili na roho yake vikatengenishwa.

Kuna ushahidi wa sanda aliyozikiwa pia uko kwenye museum huko walipokuwepo. Ngoja nikutafutie hizo simulizi
Zurie kama Zurie
 
Wadau wa fikra,

Nafahamu kuwa muongozo wa Jukwaa hili unatutaka tuweke serious reports & discussions on Corruption, Politics na etc kwa ajili ya mijadala yakinifu. Tofauti na Jukwaa la Dini ambalo lengo lake kuu ni kuhamasishana kuhusu masuala ya kiimani na kufundishana yale yaliyo mema.

So, uzi huu hauna lengo la kuhamasishana kuhusu imani bali kujadiliana kwa kina kuhusu mambo ya kale (historical facts) yanayoingiliana kidogo na dini/imani. Naamini nimejaribu kuweka utofauti ili isionekane naleta mjadala wa kidini kwenye jukwaa hili makini.

Kupitia historia fupi ya Maria, nitaeleza mtihani wa Bikra Maria kwa Mkuu wa Kanisa/Hekalu alimolelewa, ambaye alikuwa ni Nabii Zakaria. Ni matarajio yangu tutaulizana maswali na kurekebishana kwa uungwana ili sote tuweze kuelimika na kufahamishana mambo mengi tusiyoyajua.

Hebu tuipitie historia hiyo kidogo..

Wazazi wake
Maria alizaliwa na Mzee Joachim na Bi. Anna ambao walikuwa ni wachamungu haswa. Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachamungu wa enzi hizo, Mungu aliwapa mtihani wa ugumba Mr. & Mrs Joachim kiasi cha kudharaulika katika jamii kabla ya kuwainua kwa kuwapatia msichana mtakatifu Maria, baada ya kuzidisha kwao ibada na maombI.

Malezi yake
Watakatifu zamani walikuwa wakiweka nia kwa watoto wao watakaowazaa. Familia hii ya mzee Joachim na mkewe waliweka nadhiri kwamba endapo Mungu atawajaalia mtoto, basi watamtoa wakfu - yaani atatumika kwenye kazi za Mungu (utumishi). Hivyo, baada ya uzao wa Maria na kufikisha umri wa miaka 2/3 baada ya kuacha ziwa, walitekeleza ahadi yao kwa kumpeleka hekaluni kulelewa na Kiongozi wa hekalu ambaye alikuwa ni mzee Zakaria, mume wa Elizabeth (mama yake Yohana Mbatizaji).

Hekaluni palikuwa pakilelewa mabinti bikra kwa kuwa walizingatiwa kuwa wasafi na watakatifu zaidi. Kwahiyo binti Maria aliishi humo pamoja na mabinti bikra wengine na kufundishwa maadili mema pamoja na sheria za Mungu. Wazazi wake walikuwa wakimtembelea mara kwa mara mpaka alipofikia umri wa miaka 10 wakafariki dunia.

Ndoa
Alipofikisha umri wa miaka 13, yaani miaka mitatu baada ya wazazi wake kufariki, uongozi wa Kanisa uliamua Maria atoke hekaluni ili aweze kupata mume. Kwa mila na desturi za hekalu enzi hizo, binti akishavunja ungo anakuwa sio msafi tena hivyo hahitajiki kubaki hekaluni kwa sababu atalichafua. Hata hivyo, Maria alijenga hoja kwamba yeye wazazi wake waliamua kumtoa wakfu hivyo ameamua ataitunza bikra yake na kumtumikia Mungu maisha yake yote.

Jambo hili lilileta mtihani kidogo kwa mzee Zakaria kwa sababu ni unprecedented. Akalazimika kuitisha baraza la ushauri namna ya kudeal nalo ambapo uamuzi ulifikiwa kuwa aende altareni akiwa pekee aombe hekima ya Mungu. Usiku wake, alifanya hivyo na Malaika akamtokea na kumpa Muongozo kwamba aitishe mkutano wa wagane wachamungu ambapo mmojawapo atateuliwa na Mungu kwa ishara kwa kuwa bado Mungu ana kusudi maalum na Maria.

Basi, ndipo katika kusanyiko la wanaume hao wagane, alikuwemo mzee wa miaka takribani 80 aitwaye Joseph. Fundi seremala mchamungu haswa, ambaye mkewe Salome alifariki mwaka mmoja uliopita na alijaaliwa naye watoto 7.

Kufupisha story, mzee huyo alifanikiwa kuteuliwa kwa ishara ya mng'ao wa kitambaa. Naye binti Maria (13) hakuwa na pingamizi kwenye uamuzi wa Muumba. Akakubali kuolewa.

Na historia maarufu ya Bikra Maria sasa inaanzia hapo na kuendelea. Kuna haja ya kuisimulia zaidi?!
aksante sana mkuu
 
Mungu wangu umetoa wapi huo ujinga??wapi imeandikwa kuwa yaliyomo kwenye biblia ni summary tu?
Una Biblia? Kama ndiyo hukuwahi kusoma habari kwamba yangeandikwa yote aliyoyafanya Yesu hata ulimwengu wote usingetisha kukokokita Biblia?

Nenda pia kasome kitabu Cha Wafalme. Kila bada habari za Mfalme Moja Kuna maelezo mengine kuhusu Walafme yameandikwa katika vitabu vingine vya Wafalme HUSIKA. Au huwa hamsomi Biblia hadi NUKTA ya mwisho ya kitabu HUSIKA????
 
Back
Top Bottom