Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

Hivi nyie watu mnasoma Bible ipi hadi leo mnasema Bikra Maria! Basi Mama ngu ni Bikra bado kwani alinizaa na ka endelea kuzaa , upo wapi Ubikra wa Maria wakati aliendelea kuzaa na Joseph kwa kawaida tu hamjui kuwa YESU anao Ndugu wa Damu kwa Maria?
uwe unatoka nje ya box. ulishaambiwa Yusufu alikuwa mgane wa watoto saba kabla ya kuoa. kwanini unakuwa mvivu wa kutafuta taarifa? Yesu ana kaka zake na dada zake toka kwa mama mwingine. lakioni kwa Maria yupo mwenyewe.
 
Alichomaanisha zekaria nabii na zekaria babaye yohane ni watu wawili tofauti.zekaria babaye yohane hakuwa nabii bali kuhani yaani mwongoza ibada madhabahuni
Hapo sawa nimekusoma mkuu.

Yes walikuwepo Zekaria tofauti kwa nyakati tofauti. Huyu aliyetajwa kwenye Bible kama Nabii ndiye mwenye chapter yake ya Zekaria kwenye Agano Jipya.

Hata huyu mwongozo ibada naye inasemwa alikuwa Nabii na ndio maana mrithi wake (yaani mwanae Yohana - Mbatizaji) alirithi kazi za baba yake.

Nadhani imekaa sawa sasa!
 
Wadau wa fikra,

Nafahamu kuwa muongozo wa Jukwaa hili unatutaka tuweke serious reports & discussions on Corruption, Politics na etc kwa ajili ya mijadala yakinifu. Tofauti na Jukwaa la Dini ambalo lengo lake kuu ni kuhamasishana kuhusu masuala ya kiimani na kufundishana yale yaliyo mema.

So, uzi huu hauna lengo la kuhamasishana kuhusu imani bali kujadiliana kwa kina kuhusu mambo ya kale (historical facts) yanayoingiliana kidogo na dini/imani. Naamini nimejaribu kuweka utofauti ili isionekane naleta mjadala wa kidini kwenye jukwaa hili makini.

Kupitia historia fupi ya Maria, nitaeleza mtihani wa Bikra Maria kwa Mkuu wa Kanisa/Hekalu alimolelewa, ambaye alikuwa ni Nabii Zakaria. Ni matarajio yangu tutaulizana maswali na kurekebishana kwa uungwana ili sote tuweze kuelimika na kufahamishana mambo mengi tusiyoyajua.

Hebu tuipitie historia hiyo kidogo..

Wazazi wake
Maria alizaliwa na Mzee Joachim na Bi. Anna ambao walikuwa ni wachamungu haswa. Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachamungu wa enzi hizo, Mungu aliwapa mtihani wa ugumba Mr. & Mrs Joachim kiasi cha kudharaulika katika jamii kabla ya kuwainua kwa kuwapatia msichana mtakatifu Maria, baada ya kuzidisha kwao ibada na maombI.

Malezi yake
Watakatifu zamani walikuwa wakiweka nia kwa watoto wao watakaowazaa. Familia hii ya mzee Joachim na mkewe waliweka nadhiri kwamba endapo Mungu atawajaalia mtoto, basi watamtoa wakfu - yaani atatumika kwenye kazi za Mungu (utumishi). Hivyo, baada ya uzao wa Maria na kufikisha umri wa miaka 2/3 baada ya kuacha ziwa, walitekeleza ahadi yao kwa kumpeleka hekaluni kulelewa na Kiongozi wa hekalu ambaye alikuwa ni mzee Zakaria, mume wa Elizabeth (mama yake Yohana Mbatizaji).

Hekaluni palikuwa pakilelewa mabinti bikra kwa kuwa walizingatiwa kuwa wasafi na watakatifu zaidi. Kwahiyo binti Maria aliishi humo pamoja na mabinti bikra wengine na kufundishwa maadili mema pamoja na sheria za Mungu. Wazazi wake walikuwa wakimtembelea mara kwa mara mpaka alipofikia umri wa miaka 10 wakafariki dunia.

Ndoa
Alipofikisha umri wa miaka 13, yaani miaka mitatu baada ya wazazi wake kufariki, uongozi wa Kanisa uliamua Maria atoke hekaluni ili aweze kupata mume. Kwa mila na desturi za hekalu enzi hizo, binti akishavunja ungo anakuwa sio msafi tena hivyo hahitajiki kubaki hekaluni kwa sababu atalichafua. Hata hivyo, Maria alijenga hoja kwamba yeye wazazi wake waliamua kumtoa wakfu hivyo ameamua ataitunza bikra yake na kumtumikia Mungu maisha yake yote.

Jambo hili lilileta mtihani kidogo kwa mzee Zakaria kwa sababu ni unprecedented. Akalazimika kuitisha baraza la ushauri namna ya kudeal nalo ambapo uamuzi ulifikiwa kuwa aende altareni akiwa pekee aombe hekima ya Mungu. Usiku wake, alifanya hivyo na Malaika akamtokea na kumpa Muongozo kwamba aitishe mkutano wa wagane wachamungu ambapo mmojawapo atateuliwa na Mungu kwa ishara kwa kuwa bado Mungu ana kusudi maalum na Maria.

Basi, ndipo katika kusanyiko la wanaume hao wagane, alikuwemo mzee wa miaka takribani 80 aitwaye Joseph. Fundi seremala mchamungu haswa, ambaye mkewe Salome alifariki mwaka mmoja uliopita na alijaaliwa naye watoto 7.

Kufupisha story, mzee huyo alifanikiwa kuteuliwa kwa ishara ya mng'ao wa kitambaa. Naye binti Maria (13) hakuwa na pingamizi kwenye uamuzi wa Muumba. Akakubali kuolewa.

Na historia maarufu ya Bikra Maria sasa inaanzia hapo na kuendelea. Kuna haja ya kuisimulia zaidi?!
Kwa maelezo yako uliyoandika unatuambia kwamba kumbe watu walikua wakiabudu kanisani kabla ya MARIA kupata mtoto?.
 
Kwa maelezo yako uliyoandika unatuambia kwamba kumbe watu walikua wakiabudu kanisani kabla ya MARIA kupata mtoto?.
Naona neno kanisa linaleta utata. Kimsingi nimelitumia kwa sababu za kimuktadha tu. Ni tafsiri ya kiistilahi wala isikubabaishe.

Halafu mbona nimefafanua vizuri hata kwenye matini ya uzi wenyewe? Au umesoma title tu?
 
Hapa inahitajika busara kubwa kukuelimisha mkuu.
as long as hakijaandikwa kwenye biblia na kinamuhusu Mungu is't Rubbish hata shetani anaweza kuandika vyakwake akasema ni vya Mungu .kwakuwa huna ujuzi wa maandiko ndiomaana unategemea maandiko nje ya biblia
 
Sipendi kuharibu hii mada nzuri ya muhusika pia najua lengo ni kuwa na uelewa mkubwa wa mambo kwa ujumla ikiwa pamoja na imani zetu

Lkn kwa sie ambao hatuamini hizi Hadith za Wayahudi na jamaa zao wa mashariki ya kati tunapita kimya hapa kwa huzuni kuu ya kwamba mtu mweusi itachukua muda sana kujisimamia

Kuna Mwanamalunde,Mkwawa , kinjekitile,Shaka , Nzinga mbandi, na kadhalika wanatakiwa kupewa heshima kubwa kuliko mtu mweupe mmoja eti ndo ‘muokozi’ wetu dah haya
 
as long as hakijaandikwa kwenye biblia na kinamuhusu Mungu is't Rubbish hata shetani anaweza kuandika vyakwake akasema ni vya Mungu .kwakuwa huna ujuzi wa maandiko ndiomaana unategemea maandiko nje ya biblia
Sawa mkuu. Uko sahihi!
 
Sipendi kuharibu hii mada nzuri ya muhusika pia najua lengo ni kuwa na uelewa mkubwa wa mambo kwa ujumla ikiwa pamoja na imani zetu

Lkn kwa sie ambao hatuamini hizi Hadith za Wayahudi na jamaa zao wa mashariki ya kati tunapita kimya hapa kwa huzuni kuu ya kwamba mtu mweusi itachukua muda sana kujisimamia

Kuna Mwanamalunde,Mkwawa , kinjekitile,Shaka , Nzinga mbandi, na kadhalika wanatakiwa kupewa heshima kubwa kuliko mtu mweupe mmoja eti ndo ‘muokozi’ wetu dah haya
Hawa jamaa uliowataja hapo mwishoni kuna vitabu vyao? Natamani kuwasoma vizuri wote, hasa falsafa zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ni kweli mbona unashindwa kutoa sura na mstari husika kusapoti habari uliyotuletea? Usilete UTANI kwenye maandiko matakatifu. Toa ushaidi sura ipi na mstari upi kwenye Biblia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu wanataka kila kitu kiwe na reference kibiblia utafikiri ni kitabu cha historia na hata kingekuwa kitabu cha historia kisingeweza kubeba yote. Mafundisho yanarithishwa kwa maneno na maandishi. Kanisa limetunza hayo divinely hata sasa kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio maana mi nilikuwa najiulizaga kwa hapo.huyo yusuph anaishia kula kwa macho2 toka kwa mary mpaka anakufa.angekuwa kijana hii leo tungekuwa tunaongea mengine huenda angesha tembezaga miti bila kuangalia huyu ni mama wa roman catholic.
 
Basi ndiye huyo huyo. Baba yake alikuwa Zakaria na mama ni Elizabeth mkuu wangu.
Hapa si kweli. Yohana ambaye baba yake ni Zakaria na mama yake ni Elizabeth ndiye aliyekuja kumbatiza Yesu, yaani ni Yohana Mbatizaji, naye huyu aliuawa na Herode na kichwa chake kikatolewa kama zawadi kwa binti wa Herode siku ya birthday yake (Mathayo 14:1-12 na Marko 6:14-30). Kumbuka kuwa hata Yohana Mbatizaji alikuwa na wanafunzi wake (Luka 7:18-28) na hakuna popote katika Biblia ambako Yesu alimchukua Yohana Mbatizaji kama mwanafunzi wake.
Yohana aliyeandika Injili ya Yohana, zile nyaraka 3 na Ufunuo SIYO yule Yohana Mbatizaji mwana wa Zakaria na Elizabeth, kwani wakati hayo yanaandikwa Yohana Mbatizaji alishauawa na Herode. Yohana mwinjili na mwandishi wa nyaraka 3 na kitabu cha Ufunuo ni mwana wa Zebedayo (Luka 5:10). Yohana huyu alikuwa na nduguye aitwaye Yakobo. Vijana hawa wawili mama yao aliwaleta kwa Yesu akamwomba wakae mmoja kulia na mwingine kushoto kwa Yesu katika ufalme wake (Mathayo 20:20-28), na hawa walikuwa miongoni mwa mitume 12 wa Yesu kama walivyoorodheshwa katika Marko 3:13-18.
Tumsifu Yesu Kristo.
 
  • Thanks
Reactions: IoT
Hapa si kweli. Yohana ambaye baba yake ni Zakaria na mama yake ni Elizabeth ndiye aliyekuja kumbatiza Yesu, yaani ni Yohana Mbatizaji, naye huyu aliuawa na Herode na kichwa chake kikatolewa kama zawadi kwa binti wa Herode siku ya birthday yake (Mathayo 14:1-12 na Marko 6:14-30). Kumbuka kuwa hata Yohana Mbatizaji alikuwa na wanafunzi wake (Luka 7:18-28) na hakuna popote katika Biblia ambako Yesu alimchukua Yohana Mbatizaji kama mwanafunzi wake.
Yohana aliyeandika Injili ya Yohana, zile nyaraka 3 na Ufunuo SIYO yule Yohana Mbatizaji mwana wa Zakaria na Elizabeth, kwani wakati hayo yanaandikwa Yohana Mbatizaji alishauawa na Herode. Yohana mwinjili na mwandishi wa nyaraka 3 na kitabu cha Ufunuo ni mwana wa Zebedayo (Luka 5:10). Yohana huyu alikuwa na nduguye aitwaye Yakobo. Vijana hawa wawili mama yao aliwaleta kwa Yesu akamwomba wakae mmoja kulia na mwingine kushoto kwa Yesu katika ufalme wake (Mathayo 20:20-28), na hawa walikuwa miongoni mwa mitume 12 wa Yesu kama walivyoorodheshwa katika Marko 3:13-18.
Tumsifu Yesu Kristo.
Milele Amina.

Nilisahihisha mkuu. Awali wakati naandika nilishindwa kuwatofautisha.

Yanayobaki yapo kama yalivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh
Kwahiyo Yusuph (Joseph) aliye mposa Maria alikuwa ni mzee mwenye watoto 7? Kisha akataka kumuacha kwa siri ili asimtie aibu baada ya kugundua kuwa Maria ni mja"mwepesi"?
Aloo, Tunaomba na kitabu cha rejea (reference book) ya hii maandiko yako
Hii itakuwa ni Injili mpya sana kwangu
Eeh kwakweli, I wonder

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu Yosefu kuna uwezekano mkubwa alikuwa marehemu. Nasema kuna uwezekano kwa sababu hakuongelewa so hakuna uhakika kutoka biblia(kabla sijaombwa mstari wa kifo chake) lakini kuna viashiria.

Yesu akiwa msalabani alimkabidhi Mama yake kwa Yohana (Yohana 19: 26-27) ikimaanisha kuwa Yosefu alikuwa marehemu hivyo mama yake angebaki mpweke. Sababu hii ya kifo cha Yosefu ndiyo hupelekea dhana ya kuwa Yosefu alikuwa mzee hivyo alikufa kutokana na uzee.

Kingine ni kuwa Maria anaaminika kubaki bikra hadi kufa kwake. Hii inaweza kuaminika endapo tu Yosefu alikuwa mzee wa makamo hivyo hakuwa na shauku na mwali wake.

Vilevile Yesu alikuwa na kaka zake kama inavyoelezwa kwenye injili ya Mathayo 13:55-56 wakitajwa kwa majina Yakobo, Yusufu, Simoni na Yuda. Hawa wanaaminika walikuwa watoto wa Yosefu aliwapata kabla ya kuwa na Maria. Hitimisho ni kuwa maandiko japo hayajasema ila yanaashiria Yosefu alikuwa mzee wa makamo.
Maria hakufa mkuu,, alipalizwa Binguni...!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau wa fikra,

Nafahamu kuwa muongozo wa Jukwaa hili unatutaka tuweke serious reports & discussions on Corruption, Politics na etc kwa ajili ya mijadala yakinifu. Tofauti na Jukwaa la Dini ambalo lengo lake kuu ni kuhamasishana kuhusu masuala ya kiimani na kufundishana yale yaliyo mema.

So, uzi huu hauna lengo la kuhamasishana kuhusu imani bali kujadiliana kwa kina kuhusu mambo ya kale (historical facts) yanayoingiliana kidogo na dini/imani. Naamini nimejaribu kuweka utofauti ili isionekane naleta mjadala wa kidini kwenye jukwaa hili makini.

Kupitia historia fupi ya Maria, nitaeleza mtihani wa Bikra Maria kwa Mkuu wa Kanisa/Hekalu alimolelewa, ambaye alikuwa ni Nabii Zakaria. Ni matarajio yangu tutaulizana maswali na kurekebishana kwa uungwana ili sote tuweze kuelimika na kufahamishana mambo mengi tusiyoyajua.

Hebu tuipitie historia hiyo kidogo..

Wazazi wake
Maria alizaliwa na Mzee Joachim na Bi. Anna ambao walikuwa ni wachamungu haswa. Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachamungu wa enzi hizo, Mungu aliwapa mtihani wa ugumba Mr. & Mrs Joachim kiasi cha kudharaulika katika jamii kabla ya kuwainua kwa kuwapatia msichana mtakatifu Maria, baada ya kuzidisha kwao ibada na maombI.

Malezi yake
Watakatifu zamani walikuwa wakiweka nia kwa watoto wao watakaowazaa. Familia hii ya mzee Joachim na mkewe waliweka nadhiri kwamba endapo Mungu atawajaalia mtoto, basi watamtoa wakfu - yaani atatumika kwenye kazi za Mungu (utumishi). Hivyo, baada ya uzao wa Maria na kufikisha umri wa miaka 2/3 baada ya kuacha ziwa, walitekeleza ahadi yao kwa kumpeleka hekaluni kulelewa na Kiongozi wa hekalu ambaye alikuwa ni mzee Zakaria, mume wa Elizabeth (mama yake Yohana Mbatizaji).

Hekaluni palikuwa pakilelewa mabinti bikra kwa kuwa walizingatiwa kuwa wasafi na watakatifu zaidi. Kwahiyo binti Maria aliishi humo pamoja na mabinti bikra wengine na kufundishwa maadili mema pamoja na sheria za Mungu. Wazazi wake walikuwa wakimtembelea mara kwa mara mpaka alipofikia umri wa miaka 10 wakafariki dunia.

Ndoa
Alipofikisha umri wa miaka 13, yaani miaka mitatu baada ya wazazi wake kufariki, uongozi wa Kanisa uliamua Maria atoke hekaluni ili aweze kupata mume. Kwa mila na desturi za hekalu enzi hizo, binti akishavunja ungo anakuwa sio msafi tena hivyo hahitajiki kubaki hekaluni kwa sababu atalichafua. Hata hivyo, Maria alijenga hoja kwamba yeye wazazi wake waliamua kumtoa wakfu hivyo ameamua ataitunza bikra yake na kumtumikia Mungu maisha yake yote.

Jambo hili lilileta mtihani kidogo kwa mzee Zakaria kwa sababu ni unprecedented. Akalazimika kuitisha baraza la ushauri namna ya kudeal nalo ambapo uamuzi ulifikiwa kuwa aende altareni akiwa pekee aombe hekima ya Mungu. Usiku wake, alifanya hivyo na Malaika akamtokea na kumpa Muongozo kwamba aitishe mkutano wa wagane wachamungu ambapo mmojawapo atateuliwa na Mungu kwa ishara kwa kuwa bado Mungu ana kusudi maalum na Maria.

Basi, ndipo katika kusanyiko la wanaume hao wagane, alikuwemo mzee wa miaka takribani 80 aitwaye Joseph. Fundi seremala mchamungu haswa, ambaye mkewe Salome alifariki mwaka mmoja uliopita na alijaaliwa naye watoto 7.

Kufupisha story, mzee huyo alifanikiwa kuteuliwa kwa ishara ya mng'ao wa kitambaa. Naye binti Maria (13) hakuwa na pingamizi kwenye uamuzi wa Muumba. Akakubali kuolewa.

Na historia maarufu ya Bikra Maria sasa inaanzia hapo na kuendelea. Kuna haja ya kuisimulia zaidi?!
Ni mara ya kwanza kusikia simulizi kama hili. Linahitaji sources ili kujiridhisha zaidi na kuamini uhalisiwake.
 
Back
Top Bottom