Jinsi Eric Shigongo alivyojiunga Chuo Kikuu akiwa na elimu ya msingi

Jinsi Eric Shigongo alivyojiunga Chuo Kikuu akiwa na elimu ya msingi

Anaogopa au? Chuoni unaweza Fanya chochote ukiwa na fedha ila o'level inaugumu sio kidogo
Akafanye mtihani wa O LEVEL ndipo matokeo yakitoka atamwamkia Shikamoo Profesa Ndalichako

Na GPA YAKE FAKE YA 4.8 anaenda ibuka na division zero

O level mtihani wa NECTA sio wa kitoto

ARUDI AKAFANYE KAMA YEYE KIDUME
 
Huu utaratibu hata Ulaya upo, mradi uwe na miaka 21 na unajua kusoma na kuandika. Lakini kuna course unaifanya kwa mwaka mmoja kupata credits za kuingia chuo. Katika hiyo course unafundishwa jinsi ya kuandika essay, kupeleka assignments, hesabu na Lugha ya kufundishia katika nchi uliyopo.
Mbona huku haupo kwa watu wote ,kwa mara ya kwanza umesikika kwa Tajiri!!!!!
 
Wabongo roho mbaya zimetujaa kumama*make!!dah!!hii nchii hii!!kila mtu anajikuta wazir wa elimu!!kwani shgongo akifanikiwa udsm wewe ku*ma itasababsha cheti chako kabatini kipotee??dah!!
 
Mnayafanya maisha kuwa magumu sana

Necta ndio kitu gani ?!
Mtihani wa Form Four....unamaana gani hasa katika maisha ya Mtanzania?!

Acheni uchawi wa mchana nyie

Tusaidie kuficha ujinga wako japo kidogo Mkuu. Unauliza mtihani wa kidato cha nne una faida gani kwenye maisha ya mtanzania?.
 
Fikiria unampeleka mwanao shule unakutana na Head Master mwenye Digrii Shigongo [emoji23][emoji23][emoji23]

Au umetafuta pesa ukanunua kiwanja ukasema sasa nitafute injinia aje kunidondoshea kagorofa kakitozi, pita pita zako unaunganishwa na Injinia mwenye Digrii Shigongo

Achana na yote sasa unaenda hospitali kwenye maongezi maongezi unasikia daktari au mfamasia ana Digrii Shigongo [emoji15][emoji15]

Acheni utani wakuu tuiwaze vizuri hii "Digrii Shigongo"
 
Tusaidie kuficha ujinga wako japo kidogo Mkuu. Unauliza mtihani wa kidato cha nne una faida gani kwenye maisha ya mtanzania?.
Ovyo kabisa
Tatizo akili ipo ndani ya Chupa....
Tembea Duniani ....uone maisha ya Watu na elimu zao

Mnang'ang'ania mifumo isiyokuwa na tija katika ustawi wa maendeleo......!!!!

Sasa
Jilinganishe wewe na form four yako na Shigongo......
Utakuja kupasuka msamba....
 
Nmebahatika kumsikiliza huyu jamaa. by the time alikuja chuoni kwetu so event ilikuwa ya kingereza.

Ana english nzuri kuliko pHD holders wengi ninaowafahamu.
Hivi hapa kwetu ukijua kuongea ki-inglishi tayari ni msomi! Mie nadhani inglishi ni lugha tu kama kisukuma au kinyalukolo tu. Kuwa msomi ni kitu kingine kabisa.
 
kwani ajali ina mwenyewe.! Kwanza si mpaka itokee

Tena jamaa ni mstaarabu sana ikitegemea na pesa alizonazo na status aliyonayo kijamii

Wala isingemuwia ugumu kudanganya hivyo vicertificate vyenu vya o'level na advance wala visingekua issue kwake

Ila sema kajitoa kuwapa moyo watu waliojikatia tamaa ya elimu kwa mifumo yenu yakifarisayo
Angepeleka wapi vyeti vya kufoji.Hujui siku hizi kuna mfumo wa kuhakiki.Ataumbuka vibaya kuliko sasa.
 
Kama mtu yeyote akijiunga na chuo kikuu anaweza kusoma na kufaulu, mpaka akahitimu, kwa nini pawepo na ubaguzi wa nani adahiliwe na nani asidahiliwe. Waseme, wewe tu na ada yako. Kama nafasi ipo njoo, jilipie, usome.

Ndio maana mpaka leo Chuo Kikuu Huria kinawekewa mikingamo kuishi kama dhima yake inavyotaka: Huria; kila anayetaka kusoma aje. Siyo kwamba hizo digrii zinatolewa kama sandakarawe.
Elimu ya juu huwa naona ni magumashi sana(sababu inanunulika). Kuna mtu anaweza asiwepo darasani zaidi ya mwezi na CA zikasoma poa kuliko mliokaa kitako na kufanya (physically kabisa). Final exams ikija tayari mtu yuko na coverage ya wapi pa kusoma, jiulize amepataje?
 
Elimu ya juu huwa naona ni magumashi sana(sababu inanunulika). Kuna mtu anaweza asiwepo darasani zaidi ya mwezi na CA zikasoma poa kuliko mliokaa kitako na kufanya (physically kabisa). Final exams ikija tayari mtu yuko na coverage ya wapi pa kusoma, jiulize amepataje?
Kama kweli iko hivyo inanunulika hiyo ni hatari.

Lakini kwenye uzi huu watu wamekuwa wapinzani wa mfumo wa RPL. Hapo unazungumzia digrii moja tu. Nchi za Ulaya (Uholanzi ikiwa mojawapo), ukitimiza masharti fulanifulani, unatunukiwa shahada ya Uzamivu (PhD), pasipo kujali madarasa yapi uliwahi kufikia.

Shigongo ndie muasisi au mmojawapo wa waasisi wa aina fulani ya magazeti. Aina hiyo ya magazeti imefanya vizuri sokoni, na kuyashinda magazeti yenye majina makubwa. Hadithi za Shigongo nazo zililenga wasomaji fulani, na zikapata hadhira kubwa. Amekuwapo kwenye tasnia katika vipindi mbalimbali. Bado pana watu roho zinawauma kwamba kapewa admission kwenda kusoma Mass Communication degree? Baada ya kupewa admission kama uwezo wake kielimu ungekuwa mdogo, angedakwa sup na hatimaye kudisko kabisa.

Mawazo mgando ya kwamba lazima apitie vidato ndio apokelewe chuo.

University inatokana na neno universal... mahali ambapo kila mtu anakaribishwa. Sasa mbona roho zinatuuma kiasi hiki kuona na wengine wanajiunga?

Pana mtu aliwahi kusema, Tanzania ikianzisha digrii ya soka, Messi na Ronaldo watakosa admission.
 
Hongera kwake Erick Shigongo.

Hata hivyo, kuna jambo haliko sawasawa, kupata GPA ya 4.8 siyo kitu cha kawaida. Ni wanafunzi wenye uwezo mkubwa sana darasani ndiyo wanafaulu kwa kiwango hicho, Shigongo anasema alikuwa anapata si zaidi ya 25% akiwa shule ya msingi, yeye ni mwanafunzi wa kawaida. Na hii inakinzana sana na matokeo yake ya shahada.
Tupo pamoja, nami nimehisi kuna magumashi yamefanyika.
 
Hivi hapa kwetu ukijua kuongea ki-inglishi tayari ni msomi! Mie nadhani inglishi ni lugha tu kama kisukuma au kinyalukolo tu. Kuwa msomi ni kitu kingine kabisa.
Mimi sijazungumza habari za usomi. Hivi mbona watu mnakuza mambo?
 
Na wewe ni muamini wa English mkuu. Yaani iyo ni lugha tu Kama lugha zingine sio kuwa msomi pekee ndiye anayeiongea.

Ungezaliwa uingereza ama kameruni ya kaskazini unaakiongea bila ya kujua kusoma abcd so na hapo tutakuita kuwa wewe ni msomi ama inakuwaje kisa unaongea English.
English sio kuwa wewe ni msomi mkuu.usomi ni kuwa na maarifa fulani ama ujuzi
Mimi kuna sehemu nmezunguzia usomi?


You are missing a point.
 
Back
Top Bottom